Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Mapema mwaka huu wakati suala la Libya limeanza nilitoa pendekezo la serikali yetu kusitisha uhusiano wake na Libya kwa sababu ya uamuzi wa Gaddafi kutumia silaha kushambulia wananchi wake mwenyewe na hivyo kuinuka dhidi ya watu wake. Nilitoa pendekezo wakati ule kuwa Tanzania kama taifa ambalo kuundwa kwake kulitokana na uelewa wa utu wa binadamu basi tungesitisha uhusiano na Libya mara moja in protest. Of course, haikutokea na tukachagua na tumeendelea kuchagua upande mbaya wa historia. Lakini zaidi nilishangazwa - kama wengine - jinsi serikali yetu ilivyokuwa na haraka ya kukataa 'bendera ya waasi' na hata kurudia kutotambua NTC huko Zanzibar na kuomboleza wazi kuondolewa na hatimaye kifo cha Gaddafi na kuwalaumu wananchi wa Libya.
Wakati huo huo tumeona kule Syria mambo yakiendelea na Assad akiwashambulia wananchi wake na kuwaua kama mtu anavyotungua ndege mtini. Yote ni kwa sababu wananchi wake wamechoshwa na utawala wake. Bahati mbaya sana kinachofanywa siyo operesheni ya kipolisi tena - kurudisha amani - bali ni operesheni ya kijeshi ambapo watu wengi wameuawa wanaume kwa wanawake, wazee kwa vijana ambao wamejaribu kuandamana kushinikiza mabadiliko ya kisiasa.
Arab League taasisi ambayo nayo ni kama AU ya Africa imejikuta ikijaribu kuingilia kati na kumbembeleza Assad kukubali 'road map' na Assad inaonekana hataki kabisa kwani licha ya kukubali bado jeshi lake linaendelea kushambulia wananchi. Hatimaye AL imeamua kuisimamisha Syria kutoka kwenye jumuiya hiyo na bila ya shaka kujaribu kui-isolate Syria.
Tanzania iko upande gani na kwanini?
Hadi hivi sasa hatujasikia kauli yoyote ya maana ya kuonesha kutofurahishwa kwetu kama taifa (kupitia serikali yetu) na mauaji ambayo utawala wa Assad unayafanya. Je, Tanzania haijali hilo au tunasubiri wengine waoneshe njia na sisi tufuate? Ni mantiki gani ambayo inatufanya tuendelee kuwa na uhusiano na serikali ambayo imeinuka dhidi ya wananchi wake, kuwaua kama kuku na kukataa kabisa kutafuta suluhisho la kisasa isipokuwa mpaka wananchi wapigishwe magoti kwanza?
Lakini taarifa za leo kuwa balozi mbalimbali zimeshambuliwa huko Syria kingetufanya hata kumuita balozi wa Syria nchini "for consultation" lakini tulikuwa na haraka ya kumuita aliyepandisha bendera kusherehekea ukombozi wa watu wake badala ya hawa wanauua wananchi wao. Tumekasirishwa na bendera zaidi kuliko utu! Je, ni mpaka nani aseme kuwa kinachoendelea Syria ni kinyume na utu na haki za msingi za binadamu?
Je yawezekana serikali yetu inashindwa kuchukua msimamo mkali dhidi ya serikali inayoua wananchi wake ya Assad kwa vile sisi wenyewe tayari tumeanza kuwa na serikali ya aina hiyo hiyo na yawezekana huko mbeleni tukaona vikosi vyetu vikishambulia mamia ya wananchi wetu wanaoandamana kama wale wa Syria dhidi ya serikali yao? Yawezekana hiki ndicho kinachotufanya tushindwe kuchukua msimamo. Je kama wale watu zaidi ya 3000 wangeuawa na vikosi vya NATO kule Syria ni kweli tungekaa kimya? Yawezekana kuna imani iliyopotoka kwamba kuuliwa na NATO ni kubaya zaidi kuliko kuuliwa na serikali yako?
Wakati huo huo tumeona kule Syria mambo yakiendelea na Assad akiwashambulia wananchi wake na kuwaua kama mtu anavyotungua ndege mtini. Yote ni kwa sababu wananchi wake wamechoshwa na utawala wake. Bahati mbaya sana kinachofanywa siyo operesheni ya kipolisi tena - kurudisha amani - bali ni operesheni ya kijeshi ambapo watu wengi wameuawa wanaume kwa wanawake, wazee kwa vijana ambao wamejaribu kuandamana kushinikiza mabadiliko ya kisiasa.
Arab League taasisi ambayo nayo ni kama AU ya Africa imejikuta ikijaribu kuingilia kati na kumbembeleza Assad kukubali 'road map' na Assad inaonekana hataki kabisa kwani licha ya kukubali bado jeshi lake linaendelea kushambulia wananchi. Hatimaye AL imeamua kuisimamisha Syria kutoka kwenye jumuiya hiyo na bila ya shaka kujaribu kui-isolate Syria.
Tanzania iko upande gani na kwanini?
Hadi hivi sasa hatujasikia kauli yoyote ya maana ya kuonesha kutofurahishwa kwetu kama taifa (kupitia serikali yetu) na mauaji ambayo utawala wa Assad unayafanya. Je, Tanzania haijali hilo au tunasubiri wengine waoneshe njia na sisi tufuate? Ni mantiki gani ambayo inatufanya tuendelee kuwa na uhusiano na serikali ambayo imeinuka dhidi ya wananchi wake, kuwaua kama kuku na kukataa kabisa kutafuta suluhisho la kisasa isipokuwa mpaka wananchi wapigishwe magoti kwanza?
Lakini taarifa za leo kuwa balozi mbalimbali zimeshambuliwa huko Syria kingetufanya hata kumuita balozi wa Syria nchini "for consultation" lakini tulikuwa na haraka ya kumuita aliyepandisha bendera kusherehekea ukombozi wa watu wake badala ya hawa wanauua wananchi wao. Tumekasirishwa na bendera zaidi kuliko utu! Je, ni mpaka nani aseme kuwa kinachoendelea Syria ni kinyume na utu na haki za msingi za binadamu?
Je yawezekana serikali yetu inashindwa kuchukua msimamo mkali dhidi ya serikali inayoua wananchi wake ya Assad kwa vile sisi wenyewe tayari tumeanza kuwa na serikali ya aina hiyo hiyo na yawezekana huko mbeleni tukaona vikosi vyetu vikishambulia mamia ya wananchi wetu wanaoandamana kama wale wa Syria dhidi ya serikali yao? Yawezekana hiki ndicho kinachotufanya tushindwe kuchukua msimamo. Je kama wale watu zaidi ya 3000 wangeuawa na vikosi vya NATO kule Syria ni kweli tungekaa kimya? Yawezekana kuna imani iliyopotoka kwamba kuuliwa na NATO ni kubaya zaidi kuliko kuuliwa na serikali yako?