Tanzania Isishiriki London Olympiki 2012?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Kwa vile tunategemea neema ya Mungu kufanya vizuri, nashauri Tanzania isishiriki mashindano hayo. Tusishikiri kwa sababu hatutaki kushinda bali tunataka tuwepo kwenye orodha ya nchi zitakazopita mbele kwenye gwaride la wanamichezo wote. Kwa vile Waziri wetu wa Michezo ameshindwa kabisa kuandaa timu kwa karibu miaka 4 sasa tangu Olimpiki ya China 2008 ni wazi kuwa hatuna uwezo, vifaa, mbinu wala lengo la kufanya vizuri.

Na hatuna watu wenye uwezo wa kufikiria namna ya kujiandaa na mashindano haya hasa ukiangalia kuwa karibu mashindano yote ya kimataifa ya mwaka huu ambapo nchi mbalimbali zimekuwa zikifudhu katika riadha Tanzania imefanya vibaya na mara zote ni kwa sababu ya "kukosa maandalizi ya kutosha".

Sasa kwanini tusiamue kutoshiriki hadi pale tutakapokuwa na uongozi wa kisiasa wenye lengo la kuhakikisha timu zetu zinafanya vizuri na kutenga fedha na muda wa kutosha kwa maandalizi.
 
naafiki wazo 100% siyo tu olympika,tusishiriki michezo yoyote ya kimataifa tunaenda kutia aibu tu, tungejiwekea mkakati wa kama miaka miwili ama mitatu tujijenge haswa kisha ndiyo tuende,viongozi wengi waliopo kwenye michezo siyo wenyewe kabisa, unawaona siku ya kukabidhi bendera ya taifa tu, wanamichezo wakoje hakuna anaejali.
 
But you know tutashiriki. na tutafikia lengo letu asilimia 100% "kushiriki"
 
Kwa vile tunategemea neema ya Mungu kufanya vizuri, nashauri Tanzania isishiriki mashindano hayo. Tusishikiri kwa sababu hatutaki kushinda bali tunataka tuwepo kwenye orodha ya nchi zitakazopita mbele kwenye gwaride la wanamichezo wote. Kwa vile Waziri wetu wa Michezo ameshindwa kabisa kuandaa timu kwa karibu miaka 4 sasa tangu Olimpiki ya China 2008 ni wazi kuwa hatuna uwezo, vifaa, mbinu wala lengo la kufanya vizuri.

Na hatuna watu wenye uwezo wa kufikiria namna ya kujiandaa na mashindano haya hasa ukiangalia kuwa karibu mashindano yote ya kimataifa ya mwaka huu ambapo nchi mbalimbali zimekuwa zikifudhu katika riadha Tanzania imefanya vibaya na mara zote ni kwa sababu ya "kukosa maandalizi ya kutosha".

Sasa kwanini tusiamue kutoshiriki hadi pale tutakapokuwa na uongozi wa kisiasa wenye lengo la kuhakikisha timu zetu zinafanya vizuri na kutenga fedha na muda wa kutosha kwa maandalizi.

Hapo kwenye red who decides? The principle of the IOC is that participation in the Olympics of nations must be independent of government.
 
Hapo kwenye red who decides? The principle of the IOC is that participation in the Olympics of nations must be independent of government.

well.. kama wao OIC watatoa fedha za mafunzo, na kugharimia wanamichezo wetu tushiriki; lakini kama fedha zitatoka kwa serikali yetu well huwezi kuwa independent of the government. Serikali ikisema haina fedha itakuwaje?
 
Wabaki tu hapa nchini wale ugali wao. Huko London waende kufanya nini labda kwa hela zao na si hela za walipa kodi kwani mwisho ni ku enjoy kupanda ndege na kununua mashati tu!
 
Wewe Mgonjwa kweli Kenya Riadha wanajituma na sio Viongozi wa kisiasa waiaowafanya wanariadha wao kukimbia na kushinda Medali

This topic is bogus hapa haifai kuwa hapa kwenye Siasa... yaani watanzania hatuna siasa yaani tumechoka; bogus bugus complaints...
 
well.. kama wao OIC watatoa fedha za mafunzo, na kugharimia wanamichezo wetu tushiriki; lakini kama fedha zitatoka kwa serikali yetu well huwezi kuwa independent of the government. Serikali ikisema haina fedha itakuwaje?

Serikali itasemaje haina fedha wakati juzi tuu wizara husika imemwaga fedha kwenye sherehe isiyokuwa na mpango huko Butiamna? Kwenye Olympic hatupeleki athletes kwa maana ya kushindania medali. Ndio maana unakuta msafara una viongozi wengi zaidi ya wachezaji.
 
Mzee Mwanakijiji,
Ndugu yangu maji haya hatuyawezi hata kama tutasema tusipeleke utaonekana una wivu tu watu wanaenda kutanua roho inakuuma. Hivyo fanya ni wajibu wao kama vile wanakwenda kanisani au msikitini kufanya ibada za wanamichezo..utaumiza kichwa sana mkuu wangu Tanzania yetu ndio inakwisha hivyo! ukiwauliza wao watakwambia wee ndio hujui maanake siku hizi tuna vijana wanakimbia metre elfu 1.5 na 3 kwa kazi zaidi kuliko Filbert Bay, Juma Ikangaa na Nyambui ingawa hawashindi, hivyo tuna maendeleo ya michezo kuliko enzi za Nyerere.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom