Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kwa vile tunategemea neema ya Mungu kufanya vizuri, nashauri Tanzania isishiriki mashindano hayo. Tusishikiri kwa sababu hatutaki kushinda bali tunataka tuwepo kwenye orodha ya nchi zitakazopita mbele kwenye gwaride la wanamichezo wote. Kwa vile Waziri wetu wa Michezo ameshindwa kabisa kuandaa timu kwa karibu miaka 4 sasa tangu Olimpiki ya China 2008 ni wazi kuwa hatuna uwezo, vifaa, mbinu wala lengo la kufanya vizuri.
Na hatuna watu wenye uwezo wa kufikiria namna ya kujiandaa na mashindano haya hasa ukiangalia kuwa karibu mashindano yote ya kimataifa ya mwaka huu ambapo nchi mbalimbali zimekuwa zikifudhu katika riadha Tanzania imefanya vibaya na mara zote ni kwa sababu ya "kukosa maandalizi ya kutosha".
Sasa kwanini tusiamue kutoshiriki hadi pale tutakapokuwa na uongozi wa kisiasa wenye lengo la kuhakikisha timu zetu zinafanya vizuri na kutenga fedha na muda wa kutosha kwa maandalizi.
Na hatuna watu wenye uwezo wa kufikiria namna ya kujiandaa na mashindano haya hasa ukiangalia kuwa karibu mashindano yote ya kimataifa ya mwaka huu ambapo nchi mbalimbali zimekuwa zikifudhu katika riadha Tanzania imefanya vibaya na mara zote ni kwa sababu ya "kukosa maandalizi ya kutosha".
Sasa kwanini tusiamue kutoshiriki hadi pale tutakapokuwa na uongozi wa kisiasa wenye lengo la kuhakikisha timu zetu zinafanya vizuri na kutenga fedha na muda wa kutosha kwa maandalizi.