Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Bila ya shaka hakuna ubishi kuwa nchi yetu sasa inaugua maradhi makubwa, pengine ni maradhi makubwa zaidi ya ukimwi. Ufisadi, mfumuko wa bei za vyakula unakua kila siku wakati wenzetu wanaojiita ndio watawala wa nchi hii wanakula kuku kwa mrija. wiki hii nimepata bahati ya kufika katika kijiji kinachoitwa Kubi ambacho kipo mpakani mwa Kondoa na Singida kwa upande wa kusini magharibi mwa Kondoa, kwa ukwli hali ni mbaya sana huko. lakini kuna watu wanaishi, wanaishi kama wanayama wa porini.Serikali nayo ipo ikiwatazama kwa dharau kama tembo amtizamavyo sisimizi. tupeni macho yenu huko Libya, Tunisia na Misri, lakini hatutaki kufika huko. nchi yetu ya amani. je, mnataka kuivuruga?