Tanzania inaongoza Duniani kwa miundombinu mibovu

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,294
16,983
Tanzania ni moja ya nchi 10 masikini zaidi Duniani, hii ni rekodi ambayo Tanzania tumeishikilia kwa miaka mingi na wala hatuna mpango wa kuachia nafasi yetu hii adhimu kwa sababu kwa miaka yote tumekua tukifabya kila jitihada ili tuendelee kubakia pale pale au angalau kwenye 10 bora.

Kwenye miundombinu tunashika nafasi ya kwanza kua na miundombinu mibovu Afrika hasa kwenye miji mikubwa, ukianza na Dar es salaam, miunndombinu ni mibovu hakuna mfano, hadi unajiuliza hii nchi ina watu walioenda shule kweli? Nenda Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma, kila mahali miundombinu ni mibovu, hakuna mpango miji, hii nchi ni kama haina serikali ya kusimamia hilo. Viongozi wetu wametembea sana ulaya, hawajifunzi? Yaani hata kupanga miji kwenye ardhi yetu tunahitaji misaada ya wanaoitwa mabeberu?

Kitu pekee tunaweza kujivunia ni amani kwenye dimbwi la umasikini.
 
Wizara ya Ardhi, nyumba na Maendeleo wakae Chini kuupanga huu mji

Huko chanika na sehem nyingine watu wanauziwa Viwanja vimekaa hovyo kabisa kama kashata za Mia Mia, Hakuna Hata plan

Miaka 10 badae sehem inakua kama Tandale Au Manzese Hapo Hapo wanakuja na wataingia gharama kubwa kuwalipa watu kupisha Miradi Barabara, Soko nk Hali ya Kuwa mipango ingefanyika mapema tena kwa gharama Ndogo Sana

Sidhan kama hilo Swala linawashinda ni vile tuu mpaka wajiskie
 
Next kaoneka,
Incompetent culture is very strong in the government institutions .. ..yaani kuanzia mawaziri hadi watumishi wa ngazi za chini wote wamerelax , ukiwauliza wanakuambia 'nifanye kazi nisifanye mshahara wangu upo pale pale.
 
Hakimu Mfawidhi,

Nikweli tunawachukia hawa wanao tuongoza

Ila sio kwa kiwango cha kusema uwongo huu plus kukashifu inch yako kwa kiasi hicho...

Kwa taarifa yako tu kwa miundo mbinu ilio imara na ya kisasa kumi bora africa hatukosi...
 
Nikweli tunawachukia hawa wanao tuongoza

Ila sio kwa kiwango cha kusema uwongo huu plus kukashifu inch yako kwa kiasi hicho...

Kwa taarifa yako tu kwa miundo mbinu ilio imara na ya kisasa kumi bora africa hatukosi...
Jamaa ana fikir anawadanganya watoto anaowafundisha vidudu huko...upuuzi tu😈😕😒
 
Uko sahihi kabisa, Barabara zetu hazijengwi katika ubora unaostahili hivyo kupelekea kuharibika ndani ya muda mfupi na haya ni matokeo ya rushwa na incomptence ya mainjinia wetu..tunapiga kelele tunajenga miundombinu kwa hela nyingi ambayo haidumu.

Twende kwa jirani zetu waKenya , wapo seriousy sana ktika sekta ya barabara..unapita kwenye brabara hadi.unasema YES hapa.kuna wasomi walisimamia ujenzi bora wa barabara..

Serikali yetu bado inaendeshwa kizamani..Rais amejitahidi kuwaengage vijana katika sehem mbalimbali ambapo wao walitakiwa kuwa chachu ya mabadiliko kwa kuleta mawazo mapya na chanya kutokana na mabadiliko ya kasi dunia inayopitia but still wameonekana kupwaya na kutoonyesha tofauti yoyote..

Mara nyingi.tumekuwa tukijitapa kwamba sisi.Tanzania ni sleeping Giant..hivi tutaendelea kulala mpaka lini?? Majirani zetu kama Rwanda speed wanayokwenda nayo in 20 years to come vijana wetu watagombania Visa ya kuingia huko kutafuta maisha mazuri.

Mabadiliko makubwa sana yanatakiwa kufanywa kuanzia kwenye mitaala yetu ya Elimu, We have to mordenify our education curicullum so that it can suit the current technological changes..Majirani zetu wakenya naona wao wameliona hili na wapo kwenye mchakato huo.

WE HAVE TO CHANGE otherwise tutaendelea kuwa wasindikizaji..
 
Uko sahihi kabisa, Barabara zetu hazijengwi katika ubora unaostahili hivyo kupelekea kuharibika ndani ya muda mfupi na haya ni matokeo ya rushwa na incomptence ya mainjinia wetu..tunapiga kelele tunajenga miundombinu kwa hela nyingi ambayo haidumu.

Twende kwa jirani zetu waKenya , wapo seriousy sana ktika sekta ya barabara..unapita kwenye brabara hadi.unasema YES hapa.kuna wasomi walisimamia ujenzi bora wa barabara..

Serikali yetu bado inaendeshwa kizamani..Rais amejitahidi kuwaengage vijana katika sehem mbalimbali ambapo wao walitakiwa kuwa chachu ya mabadiliko kwa kuleta mawazo mapya na chanya kutokana na mabadiliko ya kasi dunia inayopitia but still wameonekana kupwaya na kutoonyesha tofauti yoyote..

Mara nyingi.tumekuwa tukijitapa kwamba sisi.Tanzania ni sleeping Giant..hivi tutaendelea kulala mpaka lini?? Majirani zetu kama Rwanda speed wanayokwenda nayo in 20 years to come vijana wetu watagombania Visa ya kuingia huko kutafuta maisha mazuri.

Mabadiliko makubwa sana yanatakiwa kufanywa kuanzia kwenye mitaala yetu ya Elimu, We have to mordenify our education curicullum so that it can suit the current technological changes..Majirani zetu wakenya naona wao wameliona hili na wapo kwenye mchakato huo.

WE HAVE TO CHANGE otherwise tutaendelea kuwa wasindikizaji..
Uliyoyaandika mengine yana mashiko ila kusema kwamba Kenya wana barabara nzuri ni upotoshaji wa wazi kabisa.
Aidha hujawahi kwenda Kenya au wewe ni mkenya unajitutumua hapa.

Kati ya nchi zenye barabara mbaya Afrika mashariki Kenya inashika namba.
 
Kwa vifo na mateso tunayopata vipindi vya mvua, hatuna budi kuongeza.
 
Kwenye miundombinu tunashika nafasi ya kwanza kua na miundombinu mibovu Afrika hasa kwenye miji mikubwa, ukianza na Dar es salaam, miunndombinu ni mibovu hakuna mfano, hadi unajiuliza hii nchi ina watu walioenda shule kweli?


Habari inanoga ikiwa na sampuli
 
Ni kweli kwamba nchi kama Sudan kusini ama Somalia wanatushinda kwa miundombinu? Wamejenga lini ilihali kila siku wanavurumishiana mijibomu tu? Vipi kuhusu DR Congo?
Tanzania ni moja ya nchi 10 masikini zaidi Duniani, hii ni rekodi ambayo Tanzania tumeishikilia kwa miaka mingi na wala hatuna mpango wa kuachia nafasi yetu hii adhimu kwa sababu kwa miaka yote tumekua tukifabya kila jitihada ili tuendelee kubakia pale pale au angalau kwenye 10 bora.

Kwenye miundombinu tunashika nafasi ya kwanza kua na miundombinu mibovu Afrika hasa kwenye miji mikubwa, ukianza na Dar es salaam, miunndombinu ni mibovu hakuna mfano, hadi unajiuliza hii nchi ina watu walioenda shule kweli? Nenda Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma, kila mahali miundombinu ni mibovu, hakuna mpango miji, hii nchi ni kama haina serikali ya kusimamia hilo. Viongozi wetu wametembea sana ulaya, hawajifunzi? Yaani hata kupanga miji kwenye ardhi yetu tunahitaji misaada ya wanaoitwa mabeberu?

Kitu pekee tunaweza kujivunia ni amani kwenye dimbwi la umasikini.
 
Tanzania ni moja ya nchi 10 masikini zaidi Duniani, hii ni rekodi ambayo Tanzania tumeishikilia kwa miaka mingi na wala hatuna mpango wa kuachia nafasi yetu hii adhimu kwa sababu kwa miaka yote tumekua tukifabya kila jitihada ili tuendelee kubakia pale pale au angalau kwenye 10 bora.

Kwenye miundombinu tunashika nafasi ya kwanza kua na miundombinu mibovu Afrika hasa kwenye miji mikubwa, ukianza na Dar es salaam, miunndombinu ni mibovu hakuna mfano, hadi unajiuliza hii nchi ina watu walioenda shule kweli? Nenda Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma, kila mahali miundombinu ni mibovu, hakuna mpango miji, hii nchi ni kama haina serikali ya kusimamia hilo. Viongozi wetu wametembea sana ulaya, hawajifunzi? Yaani hata kupanga miji kwenye ardhi yetu tunahitaji misaada ya wanaoitwa mabeberu?

Kitu pekee tunaweza kujivunia ni amani kwenye dimbwi la umasikini.
Uliona wapi taifa la wajinga lina miundombinu bora

Taifa limejaa wajinga kuanzia juu mpaka chini
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom