Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,887
- 143,983
Huu ndio ukweli japo ni mchungu kwa baadhi ya watu.
Mawazo mazuri ya namna ya kujenga nchii hii hutolewa na wapinzani kupitia vikao mbalimbali vya Bungeni,kupitia mitandao ya kijamii,vyombo vya habari,mikutano ya kisiasa,n.k..
Kwa mfano,kunapotokea matatizo wapinzani hutoa ushauri wa nini kifanyike lakini hawa wenzetu kazi yao ya kwanza huwa ni moja tu nayo ni kukejeli na kubeza mawazo ya wapinzani.
Hata hivyo,mambo yanapoharibika, hawa jamaa wana tabia ya kujirudi na kuchukukua ushauri wa upinzani kimya kimya na kuufanyia kazi tena bila hata shukrani.
Cha ajabu na kushangaza,mambo yakikaa sawa hawa jamaa wanaanza tena kukodolea macho na kisha wanharibu kwa kugawana kilicho cha wote utazani ni chao peke yao.
Wakishaharibu wanabaki kukodoleana macho na kulindana huku hawajui wafanyaje.Hapo tena wapinzani kwa uzalendo wao wanajitosa na kuingilia kati na kutoa mawazo mbadala ya namna ya kurekebisha hali hiyo.Kama kawaida yao, watawakejeli na kuwabeza wapinzani alafu kimya kimya tena wanachukua ushauri wao na wao kuongeza mawazo yao kidogo then wanarekebisha hali ya mambo inakaa sawa.
Mambo yakitengemea wanaanza tena kuvuna na kujigawia(si huwa mnamsikia mh. analalamika kila mahali ni dili tu,ukigeuka ni dili tu?) na mchezo unakuwa ni ule ule as a result katika maeneo mengi kama Taifa tunajikuta tunapiga "mark time" tu huku miaka inaenda.
Angalieni hata wanavyoiba sera za upinzani ingawa wanashindwa kuzitekeleza vizuri mpaka tuwasaidie mawazo.
Fanya utafiti kidogo utakubaliana na mimi na kwa kuanza fuatilia hili sakata la mdororo wa uchumi hapa nchini uone mawazo /solution zinatolewa na watu gani na hali ikitengemaa ni kina nani watakuwa wa kwanza kuharibu.
Mawazo mazuri ya namna ya kujenga nchii hii hutolewa na wapinzani kupitia vikao mbalimbali vya Bungeni,kupitia mitandao ya kijamii,vyombo vya habari,mikutano ya kisiasa,n.k..
Kwa mfano,kunapotokea matatizo wapinzani hutoa ushauri wa nini kifanyike lakini hawa wenzetu kazi yao ya kwanza huwa ni moja tu nayo ni kukejeli na kubeza mawazo ya wapinzani.
Hata hivyo,mambo yanapoharibika, hawa jamaa wana tabia ya kujirudi na kuchukukua ushauri wa upinzani kimya kimya na kuufanyia kazi tena bila hata shukrani.
Cha ajabu na kushangaza,mambo yakikaa sawa hawa jamaa wanaanza tena kukodolea macho na kisha wanharibu kwa kugawana kilicho cha wote utazani ni chao peke yao.
Wakishaharibu wanabaki kukodoleana macho na kulindana huku hawajui wafanyaje.Hapo tena wapinzani kwa uzalendo wao wanajitosa na kuingilia kati na kutoa mawazo mbadala ya namna ya kurekebisha hali hiyo.Kama kawaida yao, watawakejeli na kuwabeza wapinzani alafu kimya kimya tena wanachukua ushauri wao na wao kuongeza mawazo yao kidogo then wanarekebisha hali ya mambo inakaa sawa.
Mambo yakitengemea wanaanza tena kuvuna na kujigawia(si huwa mnamsikia mh. analalamika kila mahali ni dili tu,ukigeuka ni dili tu?) na mchezo unakuwa ni ule ule as a result katika maeneo mengi kama Taifa tunajikuta tunapiga "mark time" tu huku miaka inaenda.
Angalieni hata wanavyoiba sera za upinzani ingawa wanashindwa kuzitekeleza vizuri mpaka tuwasaidie mawazo.
Fanya utafiti kidogo utakubaliana na mimi na kwa kuanza fuatilia hili sakata la mdororo wa uchumi hapa nchini uone mawazo /solution zinatolewa na watu gani na hali ikitengemaa ni kina nani watakuwa wa kwanza kuharibu.