Tanzania inahitaji Rais anayejiamini na mwenye uhakika wa Jambo lake na Maamuzi yake

Mleta mada nikuulize yule Mkuu wa wilaya aliyeteuliwa enzi za mwandazake akafika hadi ukumbini kwa ajili ya kula kiapo na muda mfupi akatolewa kwamba sio yeye je ulimwanzishia uzi? Au umeona kuwa sasa uko huru hata kutaja majina ya watu humu jukwaani tena kwa kijinasibu kuwa unajiamini? Leta hiyo thread humu nijue una msimamao tangu mwanzo.
 
Mtaanza sasa Kutulazimisha kuamini kuwa Watu wa Jinsia fulani si ' Competent ' kwa nafasi ya ' Head of State ' na akina GENTAMYCINE tukiamini hivyo msituchukie au msianze ' Kutubatiza ' Jina lenu la SUKUMA GANG mkimaanisha ni Wapinzani ' Tukuka ' wa Utawala huu wa Rais ( Mama ) Samia Suluhu Hassan.

Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.

Kibinadamu Tukio moja linasameheka kwani hata Mimi GENTAMYCINE na hata Wewe ' Member ' pia huwa tunakosea ila Mtu huyo huyo akilirudia tena Tukio ( Kosa ) hilo hilo anaanza kututia Mashaka na kuanza kutupa Mtihani mzito wa Kumjibia kutoka kwa wale wasiomkubali.

Nina mengi Moyoni na Rohoni ila kabla tu Hasira zangu hazijanipanda zaidi kwa Upuuzi unaoanza Kuzoeleka natoa Ushauri wa bure kwa wale Watanzania ambao watagombea Urais miaka ijayo GENTAMYCINE nawaombeni teueni Makamu wa Rais Vijana ( Damu Changa ) na pia wawe ' very intelligent ' ili hata ikitokea Mmekufa ( Mmefariki ) watakaotwaa Madaraka ' Kikatiba ' wawe ni Watu ambao hawatotupa Mashaka Mashaka katika Kuwaamini kama ninavyoanza kupata Mashaka hayo sasa.

Najua kwa Uzi huu leo nami nitabatizwa kuwa natokea SUKUMA GANG hivyo nikiitwa hivyo kwa kusema huu Ukweli wangu nitalipokea hilo Jina ila pamoja na kwamba Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi.

Mlio karibu na Mheshimiwa Rais nanyi pia ni sehemu ya tatizo kwani hamumsaidii hadi Mama kila mara anatoa ' Maboko ' yake tu ya ' Kuteua Kutengua ' au yawezekana pia mkawa katika Mpango ' Maalum ' wa Kumpigisha Shoti ( Kumuhujumu Mama ) ili aharibikiwe na achekwe Yeye na tuchekwe pia Sisi wana CCM wote.

Mwisho namalizia kwa Mama ( Mheshimiwa Rais ) hebu punguza sana kuwa karibu kwa 99% na Rais Mstaafu Kikwete ( hasa Kiushauri ) kwani Kitendo hiki ' Kinawakera ' baadhi ya Watendaji wako ( tena Waandamizi kabisa ) na usipokuwa nacho makini kitakuja Kukugharimu na utakuja Kunikumbuka GENTAMYCINE niliyenyimwa Utajiri na Nguvu ila niliyepewa Fikra na Maono na Mwenyezi Mungu.

Sisemi usimsikilize Mzee Kikwete bali acha Kumfanya ndiyo kila Kitu Kwako Kiushauri bali Shirikisho pia na Watu ( Wastaafu ) wengine lakini pia Waamini na hao Watendaji wako ulionao sasa Serikalini kwani huenda na Wao wakawa na Mawazo Cbanya Kwako Kimaendeleo na Kiuongozi hata kuliko hayo unayoyapata kwa Mzee Kikwete.

Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
Hapo kwenye umri umechemka, rais wa sasa wa US ana miaka mingapi?
Mwache Mama achape kazi, hayo ni mambo madogo yatarekebika with time.
 
Wabongo mna vipaji vya kulalamika , kulaum na unafiki.

Mama wewe chapa kazi ukiona Shida mahali itatue papo hapo.

Ulidhani mama anashindwa kuwaacha hao walioteuliwa bahati mbaya waendelee kuchapa kazi mpaka baadae kabisa Kama wakina Kitwangwa?

Anachokifanya Rai's anakifanya Kwa nia njema kabisa.
 
Siku zote marais wastaafu wanakuwa ni sehemu ya washauri wa marais waliopo madarakani. Hii ipo dunia nzima. Mzee Biden pamoja na kuwa anamzidi Obama miaka 19 lakini kwa Obama kumtangulia kuwa rais tayari ni sehemu ya washauri wake muhimu na wa karibu.

Urais ni cheo kikubwa sana, na Mzee Kikwete ni mwanadiplomasia mzoefu, hivyo kwa Rais Samia kumkwepa ni suala lisilowezekana. Kikwete ni muhimu kwa Samia kwa sasa kuliko wakati wowote ule.

Rais wa sasa ni mwanamke wa kwanza kuongoza Tanzania, hawezi kufanya baadhi ya maamuzi kama ambayo yangefanywa na rais mwanaume. Ni kumvumilia na kumtia moyo.
 
Kuwa na kiongozi ambaye anafanya teuzi halafu ndani ya muda mfupi anafanya utenguzi kabla ya wateuliwa aliowapitisha kuapishwa kuna shida mahali, hii inaonesha ni kwa jinsi gani mama si msomaji ama mfuatiliaji mzuri wa mambo.

Kuna shida mahali kwa washauri wa mama, pia namshauri aongeze umakini sana kama anaanguka mapema kwenye masuala ya uteuzi, je ataweza kuongoza taifa kweli?

Kuna kitu hakiko sawa kwa huyu kiongozi wetu

Tukisema akina warumi, tunaonekana sukuma Gang... raisi hatuna hapa kwa kweli
 
"Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi."

Hayo maneno yako ndio Usukuma Gang wenyewe. JPM huyu huyu aliyemini Kabudi Nguli wa sheria anafaa Mambo ya nje na Mahiga Nguli wa diplomasia anafaa sheria?

Pia tambua kwamba hakuna haja ya kutoa mfananisho wa Samia mtoto Pwani , mtoto wa mjini na JPM aliyekulia porini akichunga ng'ombe akaishia kuwa mshamba wa madaraka.

Umakini wa Kiongozi ni kuchukua hatua papo hapo ili mradi anafanya hivyo Kwa nia njema.
 
Ukiona mpaka kigwangala anaanza kujipendekeza kwa kikwete, unapata picha kuwa watu sio wapumbavu, wanajua wanachokifanya
Hahaha mambo ya CCM nawaachia CCM wenyewe, tangu watuidanganye kuhusu ile 50m kwa kila kijiji na Laptop kila mwalimu nimeamini kuwa mkweli ni Pombe tu, wengine wote waongo tu
 
Rais ana majukumu mengi hivyo kutimiza yote bila kuwa na wasaidizi wenye weredi kutakuwa hakuna tija ndio maana teuzi zipo na zinazingatia sheria zote

Kitendo cha kumsema mzee JK kuwa ndo anashika kalamu bila ushaidi huu ni uzandiki mkuu mbona kipindi Mzee JPM alipokuwa karibu sana na hayati BWM hukuja na uzi wa kumshauri? Leo Mama pia kafanya lile lile kama la JPM kuwa karibu na BWM yeye kawa karibu na Jk sasa ndo imekuwa udwazi?
 
Back
Top Bottom