Ningependa nipate mafunzoya URAIS yanatolewa wapiNafasi ya uraisi imemuangukia tu hakujiandaa kwa majukumu hayo mazito ya kazi ya lawama. sidhani kama ni sawa kuendelea kumjudge bado ana mengi ya kujifunza. Japokua binafsi naona still she is a weak president.
Hapo kwenye umri umechemka, rais wa sasa wa US ana miaka mingapi?Mtaanza sasa Kutulazimisha kuamini kuwa Watu wa Jinsia fulani si ' Competent ' kwa nafasi ya ' Head of State ' na akina GENTAMYCINE tukiamini hivyo msituchukie au msianze ' Kutubatiza ' Jina lenu la SUKUMA GANG mkimaanisha ni Wapinzani ' Tukuka ' wa Utawala huu wa Rais ( Mama ) Samia Suluhu Hassan.
Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.
Kibinadamu Tukio moja linasameheka kwani hata Mimi GENTAMYCINE na hata Wewe ' Member ' pia huwa tunakosea ila Mtu huyo huyo akilirudia tena Tukio ( Kosa ) hilo hilo anaanza kututia Mashaka na kuanza kutupa Mtihani mzito wa Kumjibia kutoka kwa wale wasiomkubali.
Nina mengi Moyoni na Rohoni ila kabla tu Hasira zangu hazijanipanda zaidi kwa Upuuzi unaoanza Kuzoeleka natoa Ushauri wa bure kwa wale Watanzania ambao watagombea Urais miaka ijayo GENTAMYCINE nawaombeni teueni Makamu wa Rais Vijana ( Damu Changa ) na pia wawe ' very intelligent ' ili hata ikitokea Mmekufa ( Mmefariki ) watakaotwaa Madaraka ' Kikatiba ' wawe ni Watu ambao hawatotupa Mashaka Mashaka katika Kuwaamini kama ninavyoanza kupata Mashaka hayo sasa.
Najua kwa Uzi huu leo nami nitabatizwa kuwa natokea SUKUMA GANG hivyo nikiitwa hivyo kwa kusema huu Ukweli wangu nitalipokea hilo Jina ila pamoja na kwamba Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi.
Mlio karibu na Mheshimiwa Rais nanyi pia ni sehemu ya tatizo kwani hamumsaidii hadi Mama kila mara anatoa ' Maboko ' yake tu ya ' Kuteua Kutengua ' au yawezekana pia mkawa katika Mpango ' Maalum ' wa Kumpigisha Shoti ( Kumuhujumu Mama ) ili aharibikiwe na achekwe Yeye na tuchekwe pia Sisi wana CCM wote.
Mwisho namalizia kwa Mama ( Mheshimiwa Rais ) hebu punguza sana kuwa karibu kwa 99% na Rais Mstaafu Kikwete ( hasa Kiushauri ) kwani Kitendo hiki ' Kinawakera ' baadhi ya Watendaji wako ( tena Waandamizi kabisa ) na usipokuwa nacho makini kitakuja Kukugharimu na utakuja Kunikumbuka GENTAMYCINE niliyenyimwa Utajiri na Nguvu ila niliyepewa Fikra na Maono na Mwenyezi Mungu.
Sisemi usimsikilize Mzee Kikwete bali acha Kumfanya ndiyo kila Kitu Kwako Kiushauri bali Shirikisho pia na Watu ( Wastaafu ) wengine lakini pia Waamini na hao Watendaji wako ulionao sasa Serikalini kwani huenda na Wao wakawa na Mawazo Cbanya Kwako Kimaendeleo na Kiuongozi hata kuliko hayo unayoyapata kwa Mzee Kikwete.
Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
Huenda tukawa na Raisi wa hovyo Zaid kuwahi kutokea baada ya mwendazake ngoja tuone
Kuwa na kiongozi ambaye anafanya teuzi halafu ndani ya muda mfupi anafanya utenguzi kabla ya wateuliwa aliowapitisha kuapishwa kuna shida mahali, hii inaonesha ni kwa jinsi gani mama si msomaji ama mfuatiliaji mzuri wa mambo.
Kuna shida mahali kwa washauri wa mama, pia namshauri aongeze umakini sana kama anaanguka mapema kwenye masuala ya uteuzi, je ataweza kuongoza taifa kweli?
Kuna kitu hakiko sawa kwa huyu kiongozi wetu
nadhani pale VETA wanatoaNingependa nipate mafunzoya URAIS yanatolewa wapi
We baki na mambo yako ya umbea achana na siasaSio huenda, that’s a reality , hatuna raisi hapa
Una ushahidi kuwa anamsikiliza Kikwete? Umenasa mawasiliano yao yoyote au unapiga ramli tu?
Huyu atamaliza miaka 4 anateua na kutengua hakuna jipya
Kama mwendazake ndiye alikuwa na sifa ambazo mama hana. Ni kheri mno mama azikose kabisa.
Mama akaze uzi hapo hapo tayari dawa inapenya.
Hahaha mambo ya CCM nawaachia CCM wenyewe, tangu watuidanganye kuhusu ile 50m kwa kila kijiji na Laptop kila mwalimu nimeamini kuwa mkweli ni Pombe tu, wengine wote waongo tuUkiona mpaka kigwangala anaanza kujipendekeza kwa kikwete, unapata picha kuwa watu sio wapumbavu, wanajua wanachokifanya
Tukisema akina warumi, tunaonekana sukuma Gang... raisi hatuna hapa kwa kweli