Tanzania inahitaji Rais anayejiamini na mwenye uhakika wa Jambo lake na Maamuzi yake

Msitake kumfananisha mama na mwenda zake,ni watu wawili tofauti,na Wana mitazamo tofauti,na hata kijinsia ni tofauti,mwenda zake aliishia kutumbua alio wachagua na mwisho akajitumbua mwenyewe kwa ukaidi wake,mama asisemwe anajua anacho kifanya,nampongeza mama kwa huu muda mfupi tu naona maisha yangu yameanza kubadilika na kuwa na furaha na amani moyoni iliyo kuwa imetoweka kwa miaka mitano ya mwenda zake
 
Mtaanza sasa Kutulazimisha kuamini kuwa Watu wa Jinsia fulani si ' Competent ' kwa nafasi ya ' Head of State ' na akina GENTAMYCINE tukiamini hivyo msituchukie au msianze ' Kutubatiza ' Jina lenu la SUKUMA GANG mkimaanisha ni Wapinzani ' Tukuka ' wa Utawala huu wa Rais ( Mama ) Samia Suluhu Hassan.

Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.

Kibinadamu Tukio moja linasameheka kwani hata Mimi GENTAMYCINE na hata Wewe ' Member ' pia huwa tunakosea ila Mtu huyo huyo akilirudia tena Tukio ( Kosa ) hilo hilo anaanza kututia Mashaka na kuanza kutupa Mtihani mzito wa Kumjibia kutoka kwa wale wasiomkubali.

Nina mengi Moyoni na Rohoni ila kabla tu Hasira zangu hazijanipanda zaidi kwa Upuuzi unaoanza Kuzoeleka natoa Ushauri wa bure kwa wale Watanzania ambao watagombea Urais miaka ijayo GENTAMYCINE nawaombeni teueni Makamu wa Rais Vijana ( Damu Changa ) na pia wawe ' very intelligent ' ili hata ikitokea Mmekufa ( Mmefariki ) watakaotwaa Madaraka ' Kikatiba ' wawe ni Watu ambao hawatotupa Mashaka Mashaka katika Kuwaamini kama ninavyoanza kupata Mashaka hayo sasa.

Najua kwa Uzi huu leo nami nitabatizwa kuwa natokea SUKUMA GANG hivyo nikiitwa hivyo kwa kusema huu Ukweli wangu nitalipokea hilo Jina ila pamoja na kwamba Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi.

Mlio karibu na Mheshimiwa Rais nanyi pia ni sehemu ya tatizo kwani hamumsaidii hadi Mama kila mara anatoa ' Maboko ' yake tu ya ' Kuteua Kutengua ' au yawezekana pia mkawa katika Mpango ' Maalum ' wa Kumpigisha Shoti ( Kumuhujumu Mama ) ili aharibikiwe na achekwe Yeye na tuchekwe pia Sisi wana CCM wote.

Mwisho namalizia kwa Mama ( Mheshimiwa Rais ) hebu punguza sana kuwa karibu kwa 99% na Rais Mstaafu Kikwete ( hasa Kiushauri ) kwani Kitendo hiki ' Kinawakera ' baadhi ya Watendaji wako ( tena Waandamizi kabisa ) na usipokuwa nacho makini kitakuja Kukugharimu na utakuja Kunikumbuka GENTAMYCINE niliyenyimwa Utajiri na Nguvu ila niliyepewa Fikra na Maono na Mwenyezi Mungu.

Sisemi usimsikilize Mzee Kikwete bali acha Kumfanya ndiyo kila Kitu Kwako Kiushauri bali Shirikisho pia na Watu ( Wastaafu ) wengine lakini pia Waamini na hao Watendaji wako ulionao sasa Serikalini kwani huenda na Wao wakawa na Mawazo Cbanya Kwako Kimaendeleo na Kiuongozi hata kuliko hayo unayoyapata kwa Mzee Kikwete.

Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
Wale wale the Gang. Let the President work, msimlazimishe cha kufanya, Mama yetu Rais Piga kazi. Era imepita tulieni dawa iingie.
 
Tukisema akina warumi, tunaonekana sukuma Gang... raisi hatuna hapa kwa kweli
Huyu mama msimchukilie poa sio kilaza yuko smart anajua mambo humdanganyi, sababu anasoma nakufuatilia mambo..ila nahisi hajiamini anawatu amewaestablish yeye km authority figures wake...kwahio wakimshauri otherwise anakwenda nalo...mimi naona tumuencourage asimame yeye km yeye aamue anachokiamini yeye moyoni mwake bila kushikiwa maamuzi...asifanye kwa kumfurahisha mtu ama taifa fulani akihisi kwamba ataonekana ni smart kuliko waliomtangulia, being sharp and smart ni relative, utakuwa smart kwa taifa hili sababu wanamaslahi na uamuzi wako, kwa taifa lingine wakakuona otherwise au hata hao hao behind the scene wakakuzomea...so asimame imara km simba... ushauri asikilize ila achanganye na hisia zake..maana kiapo alikiapa yeye...

Mimi kwangu nilihisi kazi yake itakuwa rahisi sababu ameshafunguliwa njia na JPM angepita humo humo sasa inamuwia vigumu sana sababu amekaribisha figures zingine zinazompeleka njia nyingine tofauti ambapo yeye ana muda mchache mpaka uchaguzi, njia ikibackfire imekula kwake na kwa CCM...sasa najiuliza either njia ya JPM ni ngumu sana haiwezi na hao anaowaamini hawawezi kumback up aipite au labda haikuwa na maslahi yao, au labda wanamset ama labda alikuwa haiamini yeye binafsi..time will tell...kazi iendelee
 
Msitake kumfananisha mama na mwenda zake,ni watu wawili tofauti,na Wana mitazamo tofauti,na hata kijinsia ni tofauti,mwenda zake aliishia kutumbua alio wachagua na mwisho akajitumbua mwenyewe kwa ukaidi wake,mama asisemwe anajua anacho kifanya,nampongeza mama kwa huu muda mfupi tu naona maisha yangu yameanza kubadilika na kuwa na furaha na amani moyoni iliyo kuwa imetoweka kwa miaka mitano ya mwenda zake
Na ndio maana tunawaambia Mama aachwe afanye kazi na neema zitapatikana kwa kila mmoja wetu
 
Huyu mama msimchukilie poa sio kilaza yuko smart anajua mambo humdanganyi, sababu anasoma nakufuatilia mambo..ila nahisi hajiamini anawatu amewaestablish yeye km authority figures wake...kwahio wakimshauri otherwise anakwenda nalo...mimi naona tumuencourage asimame yeye km yeye aamue anachokiamini yeye moyoni mwake bila kushikiwa maamuzi...asifanye kwa kumfurahisha mtu ama taifa fulani akihisi kwamba ataonekana ni smart kuliko waliomtangulia, being sharp and smart ni relative, utakuwa smart kwa taifa hili sababu wanamaslahi na uamuzi wako, kwa taifa lingine wakakuona otherwise au hata hao hao behind the scene wakakuzomea...so asimame imara km simba... ushauri asikilize ila achanganye na hisia zake..maana kiapo alikiapa yeye...

Mimi kwangu nilihisi kazi yake itakuwa rahisi sababu ameshafunguliwa njia na JPM angepita humo humo sasa inamuwia vigumu sana sababu amekaribisha figures zingine zinazompeleka njia nyingine tofauti ambapo yeye ana muda mchache mpaka uchaguzi, njia ikibackfire imekula kwake na kwa CCM...sasa najiuliza either njia ya JPM ni ngumu sana haiwezi na hao anaowaamini hawawezi kumback up aipite au labda haikuwa na maslahi yao, au labda wanamset ama labda alikuwa haiamini yeye binafsi..time will tell...kazi iendelee
Unamshauri Mama a-follow her instincts sio?? Basi anavyofanya ndivyo anavyotaka kufanya.

Tumuamini Mheshimiwa rais na tufuate miongozo yake. Ndio kiongozi wetu, ambae hataki basi akae chonjo atuache Sisi tujenge nchi.

Hivyo basi Mama aachwe afanye kazi na neema zitapatikana kwa kila mmoja wetu.
 
Sitaki kuchangia kuna mambo ya ajabu sana nayaona mpaka nashangaa, Nyumbu wengi hawajui wapige wapi hivyo siwaoni kusema kisa mwenyekiti wa maisha hajampiga mama. Jiaadhalini sana na hawa vijana wa Ufipa hawatumii akili zao.
Mleta mada leo mimi sichangii kwanza, naangalia trendi.
 
Back
Top Bottom