Tanzania inahitaji mawaziri na manaibu wote hawa?

niweze

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
1,008
116
Wananchi Tunaoangalia na Kusoma Utaratibu wa Uongozi Inchi Zingine Tunaona Inchi Kama ya Tanzania Kuwa na Idadi Kubwa ya Baraza la Mawaziri na Manaibu ni Moja ya Uongozi Mbaya Tanzania. Hii Pia Inaonyesha Kweli CCM Hawajui Kusoma Matokeo ya Uchaguzi 2010. Wananchi Wamepiga Kura kwa Wingi Kutaka Inchi Ibadilike na Mwenendo Wake na Wengi Tunajua JK Kupitia Makame Wameona Matokeo ya Kweli. Inchi Haina Fedha na Tunategemea Wafadhiri, IMF na World Bank Kwanini Unakuwa na Wasimamizi Wengi Hivi? Wananchi Wengi Tunaofualia Maswala ya Global Recession, Tunaona Kila Inchi Kutoka EU, Asia na America Wanakata Government Spending in a Very Big Way. Inchi Kama Tanzania Yenyewe Inazidi Kugrow Everyday. Kwanini Waziri Mmoja Hawezi Kusimamia Departments Zaidi ya Tatu? Inamaasha They can't be Multi Tasks? Hizi Wizara Zilizotangazwa Tunaona Kuna Manaibu Wake, Wakufanya Kazi Gani? Hii ni Aibu kwa Inchi JK na CCM Wanatumia Hizi Posts za Kuteua Mawaziri na Manaibu ili Kuwaweka Wafanya Deals na Kulinda Wizi wa Pesa. Mimi Binafsi Nachangia Haya Sio Kwa Sababu CCM Ipo Madarakani kwa Nguvu Ila Hata Chadema Ikijafanyia Wananchi Namna Hii, Sitakaa Kimya Kamwe.

"Solution ya Hizi Issue za JK na Uraisi ni Katiba Mpya Ambayo Itaondoa na Kupunguza Madaraka kwa Raisi na Kuipa Bunge Nafasi ya Kupitisha Majina na Kuteua Viongozi Wasio Wakisiasa Kusimamia Serikali Yetu"
 
Hii nchi kuendelea kuwa chini ya CCM ni LAANA. Majitu ya CCM hayashauriki.
Namshangaa JK hakufuata hata ushauri ulio mzuri toka kwa Wapinzani wakti Lipumba alimkabidhi ILANI ya CUF na akasema atachukua yaliyo mazuri toka upinzani lakini hakuna hata moja alilochukua.

Mawaziri 50 NI MZIGO KWA WALIPA KODI WATANZANIA NA WAHISANI PIA.
Haingii akilini Tanzania iwe na Mawaziri 50 wakti nchi kama Marekani ina Wizara 16 tu kwa maana ya Mawaziri 32 ukijumlisha na Manaibu wao. Naamini kabisa hata nchi wahisani Wanamshangaa JK na huu utitiri wa Mawaziri. Hakika ni upuuzi mtupu.

Botswana ina Wizara 18 kwa maana ya Mawaziri 18x2 =36. Kumbuka Botswana ni nchi ya TATU kiuchumi barani Afrika.
Tanzania Wizara 29 kwa maana ya Mawaziri 29 ukijumlisha na Manaibu 21 kufanya idadi ya Mawaziri 50!
Kuna Wizara ya Fedha ina Manaibu 2 sijui wanafanya kazi gani hapo Wizara ya Fedha!

Hakika CCM wamelaamiwa!
 
mimi bado sielewi kazi ya waziri. Utata unakuwa mkubwa pale waziri anapewa wizara ambayo hana utaalamu wa mambo yanayohusika na wizara hio.
 
Kwangu namba si tatizo ila hela wanazokula, na kazi wanayofanya. napata homa sana maana hakuna wanachofanya ila kutuongezea gharama tu- kodi kibao
 
Pia Zaidi cha Kuongezea ni Kwamba Mishahara ya Kila Waziri na Naibu Wake ni Karibu Mamilioni kwa Kila Mmoja. Hapo Hatujazungumzia Yafuatayo:
  1. Marupurupu ya Waziri na Naibu Wake
  2. Mishahara kwa Masekretari wa Waziri na Naibu
  3. Mishahara kwa Wafanyakazi Wasaidizi wa Waziri na Naibu
  4. Mishahara kwa Wafanyakazi wa Nyumbani kwa Waziri na Naibu Waziri
  5. Mishahara kwa Madereva wa Waziri na Naibu - Wengine Wanapewa Dereva wa Waziri na Mkewe na Watoto
  6. Gharama za Umeme na Maintenances za Nyumba za Waziri na Naibu
  7. Gharama za Kusafiri Mikoani - Mahotelini (posho za safarini - dereva na walinzi)
  8. Mishahara ya Walinzi wa Waziri na Naibu Nyumbani na Safarini
  9. Gharama za Huduma Mahospitalini kwa Familia ya Waziri na Naibu na Wafanyakazi Wao (Walinzi na Wapishi)
  10. Gharama za Waziri au Naibu Akisafiri Nje ya Inchi - Mahotelini na Mikutanoni
  11. Gharama za Mikopo ya Magari na Nyumba na Incetives Zote za Kikubwa Tanzania
Vitu ni Vingi Vya Kuzungumzia Kuhusu Makosa ya Raisi Kuteua Mawaziri na Manaibu Wengi Hivi. Anaelipia Hizi Gharama si Chama cha CCM ni Kodi za Wananchi na Mikopo IMF na World Bank Ambayo Wananchi Tutalipa Viongozi wa CCM Wakiwa Hawapo Tena Katika Picha. Hii Ndio Sababu "Katiba Mpya ni Muhimu Sana Inchini" JK Kasoma Uchumi na Kuna Wananchi Wengi Wamesoma Uchumi Wanafanya Kazi Chini ya JK, Hivi Hawaoni Haya Makosa? Ila Wapinzani na Wananchi Wakizungumza Haya Usalama wa Taifa Unaanza Kuwafuata Kila Angle. Wananchi Tuendelee Kupigania Mabadiliko Kwa Ajili Hatuna Choice Nyingine.
 
inauma sana jinsi gani tunaliwa yani marekani ina wananchi mil 300 mawazili 32 tz wananchi mil 4o mawaziri 50. hivi nani ambaye anakubali kuliwa kiasi hiki. after all yani hao manaibu kazi kujibu maswali bungeni wakula
pesa za bwerere. hivi tutaliwa mpaka lini
 
Back
Top Bottom