Tanzania Ina Nini cha Kujivunia?

Dalali444

Member
Feb 7, 2010
7
0
Wana JF,

Wiki iliyopita nilipata mtihani mgumu baada ya mgeni wangu ambaye namuheshimu sana alipoamua kunitupia suala ambalo sikulitarajia.Sijui yalimjia mawazo gani lakini wakati tunakaribia kuagana ghafla aliniuliza kwa kizungu "Are you proud of your country?"

Nilishusha pumzi na kupepesapepesa macho nikijaribu kutafuta jibu la haraka nikashindwa. Kwa vile ni mtu ninayemuhesimu sana, sikuweza kumtoa njiani au kumdanganya. Nilijaribu kuwaza mambo ambayo naweza kuyaita yakujivunia nikashindwa.Kila kilichokuwa kikija mawazoni mwangu kilikuwa si cha kujivunia bali cha kutia uchungu. Mambo yaliyonijia haraka yalikuwa kama:

- rushwa iliyopindukia mipaka,
- viongozi mafisadi, wezi waliojaa kila sekta na taasisi za serikali ambao hujitajirisha kwa kila nafasi anayoipata mtu,
- miaka karibu 50 ya uhuru hatuna hata umeme wa uhakika,
- watoto wanakaa chini mashuleni na hakuna kinachosomeshwa,
- mahospitali hayana madawa,
- barabara yo yote inayojengwa au kufanyiwa ukarabati basi ni kwa pesa ya msaada,
- tumeshindwa hata kujilisha licha ya kuwa na ardhi ya kutosha ambayo kama ikitumiwa kitaalamu tunaweza kulisha eneo kubwa la Afrika
- hata kuvua samaki tukala sisi wenyewe na kusafirisha tumeshindwa licha ya kua na eneo kubwa la bahari
- hao tunaoambiwa ni wataalamu wetu hawana hata kitu kimoja walichovumbua,
- tumefanya mageuzi ya kutokana na udikteta wa chama kimoja tumeshidwa.Demokrasia imeshindwa kupiga hatua.Vyombo vyote vya dola vinafanya kazi na kutumikia chama tawala na hata uchaguzi ukifanyika ni mizengwe mitupu,
- hata kwenye mambo ya michezo ni aibu tupu. Tunashindwa hata kuingia kwenye mashindano ya kombe la Afrika.

Mwisho ilibidi nimeze mate machungu nimjibu "NO, I'm ashamed".

Dalali
 
Dalali ungemwambia tunamafisadi wa kufa mtu...
-Kiongozi akijiuzuru kwa kashfa akirudi kwao anapokelewa kwa mashangwe ya kufa mutu
-Rais wetu mpenda masifa
-ni nchi ya wasiopenda makuu na wasiojua rights zao
-hata wewe ukiwa kiongozi unaiba tuuu...
-ni nchi ukianzia na mtaji wa dola 100 utakuwa tajiri
-watoto wa vigogo ndo huandaliwa kuwa vigogo...
 
Yap.,pamoja na mabaya yetu hayo lakini tunajivunia kuwa Watanzania na Nyerere kuzaliwa kwetu.,hakika kuna watu wengi wanatamani mzee yule angezaliwa kwao ili awe sehemu ya historia ya nchi zao.
 
Yap.,pamoja na mabaya yetu hayo lakini tunajivunia kuwa Watanzania na Nyerere kuzaliwa kwetu.,hakika kuna watu wengi wanatamani mzee yule angezaliwa kwao ili awe sehemu ya historia ya nchi zao.
huyo Nyerere huko alipo sijui anasema nini, maana kazi aliyofanya hakuna kinachoendelea....
 
Yap.,pamoja na mabaya yetu hayo lakini tunajivunia kuwa Watanzania na Nyerere kuzaliwa kwetu.,hakika kuna watu wengi wanatamani mzee yule angezaliwa kwao ili awe sehemu ya historia ya nchi zao.
Acha hizo wewe hata kama kazaliwa kwetu viongozi wetu wamefanya nini ili kudumisha his heritage zaidi ya ufisadi?
 
tuna wababaishaji nchi nzima, na mafisadi wa kimataifa bila kusahau chama cha kihuni kuliko vyote africa, CCM
 
"Tanzania Ina Nini cha Kujivunia? "

Wananchi watulivu - shida ya maji, umeme, kazi na mengineyo mengi lakini wananchi siku zote wako shwari wanaendeleza maisha yao.
¬K
 
tunajivunia kasi yetu ya kutaka utajiri, kila mtu kuanzia huko juuuuuu mpaka kwa mwenyekiti wa mtaa tunataka kuwa mabilionea kama R al azzz, lowasa, kingunge, mramba, Mkapa nk
 
mount kilimanjaro,serengeti,ngorongoro crater,lake tanganyika(deepest in the world??),very long coast line with natural sandy beaches bila kusahau ukarimu wa watanzania.
hata kimoja hapo juu si cha kujivunia???
 
Acha hizo wewe hata kama kazaliwa kwetu viongozi wetu wamefanya nini ili kudumisha his heritage zaidi ya ufisadi?

Ndio maana nikasema cha kujivunia ni yeye tu kuzaliwa Tanzania otherwise hatuna cha kujivunia
 
tunajivunia uwanja wa kisasa wa mpira.......................................
 
Tunajivunia mashujaa wetu akina Mkwawa, Kinjekitile Ngwale, Mtemi Munyigumba, Mtemi Milambo.

Tunajivunia kuwa na lugha moja ya kiswahili inayotuunganisha

Tunajivunia rangi yetu (usiniulize kwanini)

Tunajivunia nchi yetu (Kila wakati ninapokuwa nje ya Tanzania, nakumbuka na kutamani kurudi Tz mapema)

Tunajivunia maliasili zetu (ingawa zinatumika kifisadi)

Tunajivunia nguvu ya jeshi letu (Vita vya kagera, na operation Ngadzija)

Tunajivunia jinsi tulivyosaidia ukombozi wa Afrika

Jamani, chako ni chako, usikionee haya!!!
 
Dalali444

Nashangaa ulishindwa kumjibu swali rahisi kama hili, kwa nini hukumwambia sisi tunajisifia kuwa ni taifa pekee South of Sahara in Afrika ambalo tunatumia lugha moja. Hali ya hewa nzuri all season, tupo just below equator etc. Next time mwambie jibu linakuja kwenye e-mail just email me.

Then mualike aje na familia yake Serengeti the seventh wonder of the world hasa mwezi wa Sept-October wakati wa migration ya wanyama pale, halafu aone the tallest free standing mountain etc. Aaaakhg mkuu umetuangusha lakini. Next time ukienda bongo mletee majani ya chai na kahawa aonje.
 
Wana JF,

Wiki iliyopita nilipata mtihani mgumu baada ya mgeni wangu ambaye namuheshimu sana alipoamua kunitupia suala ambalo sikulitarajia.Sijui yalimjia mawazo gani lakini wakati tunakaribia kuagana ghafla aliniuliza kwa kizungu "Are you proud of your country?"

Nilishusha pumzi na kupepesapepesa macho nikijaribu kutafuta jibu la haraka nikashindwa. Kwa vile ni mtu ninayemuhesimu sana, sikuweza kumtoa njiani au kumdanganya. Nilijaribu kuwaza mambo ambayo naweza kuyaita yakujivunia nikashindwa.Kila kilichokuwa kikija mawazoni mwangu kilikuwa si cha kujivunia bali cha kutia uchungu. Mambo yaliyonijia haraka yalikuwa kama:

- rushwa iliyopindukia mipaka,
- viongozi mafisadi, wezi waliojaa kila sekta na taasisi za serikali ambao hujitajirisha kwa kila nafasi anayoipata mtu,
- miaka karibu 50 ya uhuru hatuna hata umeme wa uhakika,
- watoto wanakaa chini mashuleni na hakuna kinachosomeshwa,
- mahospitali hayana madawa,
- barabara yo yote inayojengwa au kufanyiwa ukarabati basi ni kwa pesa ya msaada,
- tumeshindwa hata kujilisha licha ya kuwa na ardhi ya kutosha ambayo kama ikitumiwa kitaalamu tunaweza kulisha eneo kubwa la Afrika
- hata kuvua samaki tukala sisi wenyewe na kusafirisha tumeshindwa licha ya kua na eneo kubwa la bahari
- hao tunaoambiwa ni wataalamu wetu hawana hata kitu kimoja walichovumbua,
- tumefanya mageuzi ya kutokana na udikteta wa chama kimoja tumeshidwa.Demokrasia imeshindwa kupiga hatua.Vyombo vyote vya dola vinafanya kazi na kutumikia chama tawala na hata uchaguzi ukifanyika ni mizengwe mitupu,
- hata kwenye mambo ya michezo ni aibu tupu. Tunashindwa hata kuingia kwenye mashindano ya kombe la Afrika.

Mwisho ilibidi nimeze mate machungu nimjibu "NO, I'm ashamed".

Dalali

Sijui nini zaidi cha kujivunia zaidi ya uhuru wa bendera kama nao ni wa kujivunia,unless ujaribu kuwa narrow zaidi,kwa mfano ukawa more specific na uje na listi ili tufanye cross cheking.

Pia ukumbuke kuwa historia ya nchi yetu nayo bado changa sana,na kwahivyo as a Nation,toka tupate uhuru kuna wenye kuweza kujivunia uzalendo?Amani nayo pia haimaanishi maendeleo,lakini je si quality ambayo tunaweza kujivunia kwa upande mwingine?

Hivyo natoa changamoto utafakari tena kama kuna cha kujivunia ama la.....Ni kweli mawazo yako yalijikita mara moja kwenye mambo ambayo yamekuwa ni ya kukatisha tamaa hususan kasfha kama Richmond,EPA,Buzwagi,Rada,BOT Towers etc.

Umasikini unaoongezeka na mambo mengine ya kukatisha tamaa na huku viongozi wakionekana kutokujali...Na kwahivyo ni kweli jibu la papo kwa hapo linaweza kuwa either or depending on you priorities and your memories,na pia in what aspect are you looking at the issue,je unazungumzia kuwa ni nini cha kujivunia on what aspect in relation to the Nation as a whole?

Kama nilivyokupa mfano hapo awali,tunaweza kujivunia pia uhuru kama tutaweza kuupreserve in all its aspects....Kuweza kuutumia kwa kujiamulia mambo yetu kwa manufaa yetu wenyewe kama Taifa.....Kuweza kuondoa mfumo na tabaka la kinyonyaji lenye kuhujumu uchumi na rasilimali za Taifa letu....

Ni kweli kadri muda unavyozidi kwenda begining from the time we aquired our independence,mambo ya kujivunia yamekuwa yaki dimish in ana alarming rate,hivyo ni wazi kabisa kuwa direction tuliyoko as a nation ni wrong....Rate ya kuongezeka kwa umasikini ni kubwa kuliko the other way round.
 
Nimekumbuka, tuna rais anayecheka muda mwing na pengine muda wote na anawalinda mafisadi!
 
Back
Top Bottom