GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,466
- 108,621
R.I.P sana Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine uliyefia Morogoro njiani, R.I.P mno Marehemu Mjomba wangu Kipenzi Ian uliyefia njiani ukiwa unakuja kunipitia twende Kuiangalia Simba SC yetu, R.I.P wale Makomandoo Wawili mliofia njiani Morogoro, R.I.P Madereva wote wa Gari ndogo mnaokufa kila Uchao njiani Morogoro, R.I.P wale Marehemu wa Basi maarufu la Dar - Moro ambao huwa mkipata Ajali za Kikafara huko njiani Tajiri huwahi Kuwahonga Wanahabari wasitangaze, R.I.P Marehemu wa Ajali mbaya ya Lori la Mafuta Msamvu Morogoro na R.I.P mno Marehemu wote wa Ajali za Mabasi na Malori kama Tatu hivi zilizotokea njiani Mkoani Morogoro ndani ya Wiki Mbili na nyingine Mbichi kabisa ya leo.
Huenda neno Morogoro lina tatizo au labda mwenye nalo hakupenda litumike au hakumaliziwa chake au Tambiko halikuenda vyema hivyo nae sasa anaamua Kulipiza Kisasi kwa 'Kutuchukulia' tu Wapendwa Wetu kila mara.
Tafadhali Mamlaka husika hebu umulikeni vyema na kwa Jicho la Umakini kabisa huu Mkoa wa Morogoro ( alias ) Accident City kwani haiwezekani katika 100% ya Ajali zinazotokea Tanzania basi 75% ni kutoka Mkoani Morogoro tu hapo ( pale ) ambako hata Mimi GENTAMYCINE pia nina DNA napo Kihistoria kwa Marehemu Babu yangu Mpendwa upande wa Mama.
Sitaki kuamini ( ila taratibu ) naanza Kuamini Kauli niliyowahi kuambiwa huko miaka ya nyuma kuwa Tanzania nzima hakuna Mkoa wenye Waganga wazuri, hatari na wa Kweli 'Kiuchawi' kama wa kutoka Mkoani Morogoro, hivyo huenda hata hizi Ajali ni sehemu za 'Makafara' yao kwa Wateja wao mbalimbali ( japo inasemekana ) Wateja wao Wakubwa ni Wanasiasa, Viongozi ( Watawala ), Watendaji Serikalini, Mabosi katika NGO's, Wasanii wa Muziki, Wachezaji wa Mpira ( hasa wa Simba na Yanga ) na Watangazaji wa Television.
Na nimedokezwa kuwa kuna Mtanzania Mwenzetu Mmoja ( sasa Kalala mazima ) pembezoni mwa Ziwa Vicky ( Jirani na Kwetu GENTAMYCINE Mkoani Mara ) kumbe hata Yeye Safari yake ya Kuondoka 'Kimkakati' ilianzia Mkoani Morogoro hasa alipoanza 'Kumchana' Tajiri wa Mabasi Maarufu huku akimpongeza na Kumsifu Fisadi na Tajiri wa Gesi Taifani Kwetu kwani tokea pale Israeli alikuwa ameshaanza kuwa nae Ng'adu kwa Ng'adu ( kama Beki Mwamnyeto na Mshambuliaji Kagere ) mpaka ikatokea kweli na sasa kawa ni Historia.
Huenda neno Morogoro lina tatizo au labda mwenye nalo hakupenda litumike au hakumaliziwa chake au Tambiko halikuenda vyema hivyo nae sasa anaamua Kulipiza Kisasi kwa 'Kutuchukulia' tu Wapendwa Wetu kila mara.
Tafadhali Mamlaka husika hebu umulikeni vyema na kwa Jicho la Umakini kabisa huu Mkoa wa Morogoro ( alias ) Accident City kwani haiwezekani katika 100% ya Ajali zinazotokea Tanzania basi 75% ni kutoka Mkoani Morogoro tu hapo ( pale ) ambako hata Mimi GENTAMYCINE pia nina DNA napo Kihistoria kwa Marehemu Babu yangu Mpendwa upande wa Mama.
Sitaki kuamini ( ila taratibu ) naanza Kuamini Kauli niliyowahi kuambiwa huko miaka ya nyuma kuwa Tanzania nzima hakuna Mkoa wenye Waganga wazuri, hatari na wa Kweli 'Kiuchawi' kama wa kutoka Mkoani Morogoro, hivyo huenda hata hizi Ajali ni sehemu za 'Makafara' yao kwa Wateja wao mbalimbali ( japo inasemekana ) Wateja wao Wakubwa ni Wanasiasa, Viongozi ( Watawala ), Watendaji Serikalini, Mabosi katika NGO's, Wasanii wa Muziki, Wachezaji wa Mpira ( hasa wa Simba na Yanga ) na Watangazaji wa Television.
Na nimedokezwa kuwa kuna Mtanzania Mwenzetu Mmoja ( sasa Kalala mazima ) pembezoni mwa Ziwa Vicky ( Jirani na Kwetu GENTAMYCINE Mkoani Mara ) kumbe hata Yeye Safari yake ya Kuondoka 'Kimkakati' ilianzia Mkoani Morogoro hasa alipoanza 'Kumchana' Tajiri wa Mabasi Maarufu huku akimpongeza na Kumsifu Fisadi na Tajiri wa Gesi Taifani Kwetu kwani tokea pale Israeli alikuwa ameshaanza kuwa nae Ng'adu kwa Ng'adu ( kama Beki Mwamnyeto na Mshambuliaji Kagere ) mpaka ikatokea kweli na sasa kawa ni Historia.