Tanzania imepokea bilioni 67.82 kutoka Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo ya KfW

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,969
Tanzania imepokea msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82 kutoka Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo ya KfW, kwa ajili ya mradi wa Uhifadhi endelevu wa Maliasili na Mifumo ya Ikolojia nchini.

Mkataba wa msaada huo umesainiwa jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, kwa niaba ya Serikali ya Ujerumani.

Bw. Tutuba alisema kuwa fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuendeleza na kuhifadhi maliasili katika hifadhi ya Serengeti pamoja na kugharamia mradi wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia katika maeneo ya ushoroba wa Katavi – Mahale.

“Lengo la mradi wa Serengeti ni kuchangia katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na usimamizi endelevu wa maliasili katika Wilaya ya Bariadi, Bunda, Serengeti na Ngorongoro wakati mradi wa Ushoroba wa Katavi- Mahale unalenga usimamizi wa maliasili sambamba na kuboresha maisha ya wananchi kwa kuhusisha matumizi bora ya ardhi na utoaji wa Hati miliki za kimila”, alieleza Bw. Tutuba.

Alisema kuwa kiasi cha shilingi bilioni 21.7 zitatumika katika mradi wa kuendeleza na kuhifadhi maliasili katika hifadhi ya Serengeti na shilingi bilioni 46.12, zitatumika katika mradi wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya Ikolojia ushoroba wa Katavi – Mahale.

Kwa upande wake Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess, aliahidi kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi ambayo hayaiathiri Tanzania pekee bali Dunia kwa ujumla.

Naye Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, alisema kuwa Benki hiyo itaendelea kuisaidia Tanzania katika Sekta ya Utalii kwa kuboresha maeneo ya hifadhi pamoja na kuziwezesha jamii zinazozunguka maeneo hayo ili waweze kutunza hifadhi hizo.

Tanzania imekuwa ikinufaika na ufadhili wa Serikali ya Ujerumani katika sekta ya afya, maji, nishati, matumizi endelevu ya maliasili na usimamizi bora wa fedha za umma ambapo kiasi cha shilingi bilioni 678.54 zilitolewa kwa ajili ya miradi inayoendelea kutekelezwa na shilingi bilioni 599.23 kwa miradi iliyokamilika.
3.jpg

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakionesha Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, baada ya kusainiwa, jijini Dar es Salaam.
1.jpg

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakisaini Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
6.jpg

Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, akieleza nia ya nchi yake kuongeza msaada wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika hafla ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, jijini Dar es Salaam
5.jpg

Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess, akieleza umuhimu wa utunzaji wa mazingira, wakati wa hafla ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
1631102522475_2.jpg

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakipongezana baada ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
4.jpg

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, akielezea malengo ya Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, zilizotolewa na Serikali ya Ujerumani kuwa ni uhifadhi madhubuti na endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 
Hawa wadau wetu wa maendeleo tuwe nao makini sana maana mikopo kama hii inawafanya wawe mabeberu wakati mwingine.
 
Tuwaite wajerumani wachukue mali zao walizoficha nchini tugawane asilimia kuna jumla ya site 3300 zimefichwa mali password na codes wanazo wao
 
Tanzania imepokea msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82 kutoka Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo ya KfW, kwa ajili ya mradi wa Uhifadhi endelevu wa Maliasili na Mifumo ya Ikolojia nchini.

Mkataba wa msaada huo umesainiwa jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, kwa niaba ya Serikali ya Ujerumani.

Bw. Tutuba alisema kuwa fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuendeleza na kuhifadhi maliasili katika hifadhi ya Serengeti pamoja na kugharamia mradi wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia katika maeneo ya ushoroba wa Katavi – Mahale.

“Lengo la mradi wa Serengeti ni kuchangia katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na usimamizi endelevu wa maliasili katika Wilaya ya Bariadi, Bunda, Serengeti na Ngorongoro wakati mradi wa Ushoroba wa Katavi- Mahale unalenga usimamizi wa maliasili sambamba na kuboresha maisha ya wananchi kwa kuhusisha matumizi bora ya ardhi na utoaji wa Hati miliki za kimila”, alieleza Bw. Tutuba.

Alisema kuwa kiasi cha shilingi bilioni 21.7 zitatumika katika mradi wa kuendeleza na kuhifadhi maliasili katika hifadhi ya Serengeti na shilingi bilioni 46.12, zitatumika katika mradi wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya Ikolojia ushoroba wa Katavi – Mahale.

Kwa upande wake Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess, aliahidi kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi ambayo hayaiathiri Tanzania pekee bali Dunia kwa ujumla.

Naye Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, alisema kuwa Benki hiyo itaendelea kuisaidia Tanzania katika Sekta ya Utalii kwa kuboresha maeneo ya hifadhi pamoja na kuziwezesha jamii zinazozunguka maeneo hayo ili waweze kutunza hifadhi hizo.

Tanzania imekuwa ikinufaika na ufadhili wa Serikali ya Ujerumani katika sekta ya afya, maji, nishati, matumizi endelevu ya maliasili na usimamizi bora wa fedha za umma ambapo kiasi cha shilingi bilioni 678.54 zilitolewa kwa ajili ya miradi inayoendelea kutekelezwa na shilingi bilioni 599.23 kwa miradi iliyokamilika.
View attachment 1929268
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakionesha Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, baada ya kusainiwa, jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929269
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakisaini Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929270
Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, akieleza nia ya nchi yake kuongeza msaada wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika hafla ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, jijini Dar es Salaam
View attachment 1929271
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess, akieleza umuhimu wa utunzaji wa mazingira, wakati wa hafla ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929272
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakipongezana baada ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929284
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, akielezea malengo ya Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, zilizotolewa na Serikali ya Ujerumani kuwa ni uhifadhi madhubuti na endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Ifike na wakati tuwe na aibu.

Ni lini serikali ya Tanzania itaanza kutoa misaada ya hali na mali kwa mataifa mengine nje ya Afrika ?
 
Hivi hiyo bln 67.82 ikigawanywa kwa watu mln 50,kila mtu atapata bei gani?
Mi naona mara moja moja serikali infetufanyia suprise igawie kila mtanzania,chake aitumie ajuavyo..kama mm nkipata ntaipigia mtungi
Poa tu ni mimi
Mshana Jr

Ova
 
da hapa lazima waje wapinga maendeleo kina lissu wanaotaka tusipewe misaada mama samia piga kazi utalii ujulikane duniani
Enzi ya mwendazake mlikuwa mnawaita hao wanaotoa misaada kuwa ni mabeberu na wanataka kuendeleza ushoga. Vipi siku hizi mbona mnawashangilia au hawataki tena kuendeleza ushoga?
 
Enzi ya mwendazake mlikuwa mnawaita hao wanaotoa misaada kuwa ni mabeberu na wanataka kuendeleza ushoga. Vipi siku hizi mbona mnawashangilia au hawataki tena kuendeleza ushoga?
kama ulikuwaga unasikiliza hotuba za JPM kwa makini hakuna sehemu alishasema hivyo ila kama ulikuwa unazisikiliza kwa ushabiki ule wa kebehi ni kweli alisema hivyo
 
kama ulikuwaga unasikiliza hotuba za JPM kwa makini hakuna sehemu alishasema hivyo ila kama ulikuwa unazisikiliza kwa ushabiki ule wa kebehi ni kweli alisema hivyo
hujajibu swali, je siku hizi mabeberu hawasupport tena ushoga hadi mnakubali pesa zao? Umesahau kuwa magufuli alisema sisi ni dona kantre?
 
Ni lini hawa watu watatupa msaada wa mbegu bora ili wakulima wetu waweze kupata mazao mengikwenye kilimo chao?

Hawa watu mara nyingi wanatudharau kama sisi ni watu tusiokuwa na akili vichwani.
 
Tanzania imepokea msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82 kutoka Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo ya KfW, kwa ajili ya mradi wa Uhifadhi endelevu wa Maliasili na Mifumo ya Ikolojia nchini.

Mkataba wa msaada huo umesainiwa jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, kwa niaba ya Serikali ya Ujerumani.

Bw. Tutuba alisema kuwa fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuendeleza na kuhifadhi maliasili katika hifadhi ya Serengeti pamoja na kugharamia mradi wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia katika maeneo ya ushoroba wa Katavi – Mahale.

“Lengo la mradi wa Serengeti ni kuchangia katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na usimamizi endelevu wa maliasili katika Wilaya ya Bariadi, Bunda, Serengeti na Ngorongoro wakati mradi wa Ushoroba wa Katavi- Mahale unalenga usimamizi wa maliasili sambamba na kuboresha maisha ya wananchi kwa kuhusisha matumizi bora ya ardhi na utoaji wa Hati miliki za kimila”, alieleza Bw. Tutuba.

Alisema kuwa kiasi cha shilingi bilioni 21.7 zitatumika katika mradi wa kuendeleza na kuhifadhi maliasili katika hifadhi ya Serengeti na shilingi bilioni 46.12, zitatumika katika mradi wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya Ikolojia ushoroba wa Katavi – Mahale.

Kwa upande wake Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess, aliahidi kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi ambayo hayaiathiri Tanzania pekee bali Dunia kwa ujumla.

Naye Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, alisema kuwa Benki hiyo itaendelea kuisaidia Tanzania katika Sekta ya Utalii kwa kuboresha maeneo ya hifadhi pamoja na kuziwezesha jamii zinazozunguka maeneo hayo ili waweze kutunza hifadhi hizo.

Tanzania imekuwa ikinufaika na ufadhili wa Serikali ya Ujerumani katika sekta ya afya, maji, nishati, matumizi endelevu ya maliasili na usimamizi bora wa fedha za umma ambapo kiasi cha shilingi bilioni 678.54 zilitolewa kwa ajili ya miradi inayoendelea kutekelezwa na shilingi bilioni 599.23 kwa miradi iliyokamilika.
View attachment 1929268
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakionesha Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, baada ya kusainiwa, jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929269
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakisaini Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929270
Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, akieleza nia ya nchi yake kuongeza msaada wa uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika hafla ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, jijini Dar es Salaam
View attachment 1929271
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess, akieleza umuhimu wa utunzaji wa mazingira, wakati wa hafla ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929272
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) wa Umoja wa Afrika, Bw. Christoph Tiskens, wakipongezana baada ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, kwa ajili ya miradi ya uhifadhi endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.
View attachment 1929284
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, akielezea malengo ya Msaada wa Euro milioni 25 sawa na shilingi bilioni 67.82, zilizotolewa na Serikali ya Ujerumani kuwa ni uhifadhi madhubuti na endelevu wa maliasili na mifumo ya ikolojia, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Beberu anazidi kuwaaibisha Chadomo.

Sio tuu Ujerumani hata Italy imetoa pesa pia👇

Screenshot_20210908-145827.png
 
Ni lini hawa watu watatupa msaada wa mbegu bora ili wakulima wetu waweze kupata mazao mengikwenye kilimo chao?

Hawa watu mara nyingi wanatudharau kama sisi ni watu tusiokuwa na akili vichwani.
Umeona tatizo ni mazao hayazalishwi au soko?
 
Back
Top Bottom