Tanzania imebaki na vyama viwili - CCM na Chadema!

Magobe T

JF-Expert Member
Mar 19, 2008
4,619
2,567
Ndugu wana JF, kwa maoni yangu na kwa kuangalia upepo wa kisiasa unavyoenda hapa tanzania, ni kama chama shindani dhidi ya chama kinachoongoza serikali (CCM) kimebaki kimoja tu, yaani, Chadema.
1. CUF waliamua kujiunga na ccm kuanzia zanzibar na kuelekea tanzania bara.

2. Baadhi ya vyama shindani vlivyoamua kujitoa kwenye mchakato wa uchaguzi viliwahamasisha wanachama kukiunga mkono chama tawala kwenye mchakato wa kampeni mwaka jana. Hivi vyama vilipoteza sifa ya kuwa vyama shindani.
3. Baadhi ya vyama (wabunge wa vyama hivyo) walishirikiana na wabunge wa CCM kubadilisha vifungu vya kanuni za kudumu za bunge ili wakidhibiti chadema. Chama shindani kinaposhirikiana na chama kinachoongoza serikali kwa sababu ya kukidhoofisha chama shindani kingine, chama hicho pia kinakuwa kimepoteza sifa muhimu ya kuwa chama shindani.
4. Katika yale, ambayo chadema wanaona ni maslahi ya wananchi na wana wajibu wa kuikosoa serikali kwa kutumia haki yao ya kikatiba ya kufanya mikutano na maandamano, vyama kadhaa vimeungana na serikali kukikosoa chadema hata kuomba kifutwe. Vyama hivi navyo vimepoteza sifa ya kuwa vyama shindani.
5. Vyama shindani ni vile vinavyotoa changamoto kwa serikali ili iweze kuwajibika zaidi na kuleta maendeleo ya watu na vitu na siyo vile vinavyoi'fan' serikali ili izidi kulala usingizi.

kuna msemo unaosema kwamba utawala uliogawanyika hauwezi kuwa na nguvu - kwa maana kwamba kama vile ilivyo 'military strategy' kukabliana na 'common enemy', ndivyo pia ilivyo kwa siasa. Kama vyama shindani vinaungana na chama tawala haviwi tena na mlengwa mmoja (CCM) bali pia Chadema au zaidi sana mlengwa wao amekuwa Chadema. kwa namna nyingine (kwa kufanya hivi) CCM na vyama vingine vinakilenga chadema na kwa jinsi hiyo kukipa chadema nafasi kubwa ya kuwa na sifa ya chama (potential) kuongoza serikali.

q: Mna maoni gani?
 
Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ndio watakaokupa jibu sahihi la vyama vingapi vipo TZ.
Fanya haraka kuwasiliana nao. Kama unataka kujua idadi ya vyama ,kama unataka malumbano ya ushabiki usubiri hao wa vyama ulivyovitaja hapa na utafurahi watakapoanza kurushiana mamkombora. Sinema kamili. Filamu ya burudani..tafuta pop korn kaa tayari na coke yako.
 
ndugu wana jf, kwa kuangalia upepo wa kisiasa unavyoenda hapa tanzania, ninaona kuwa chama shindani dhidi ya chama kinachoongoza serikali (ccm) kimebaki kimoja tu, yaani, chadema.
1. Cuf waliamua kujiunga na ccm kuanzia zanzibar na kuelekea tanzania bara.
2. Baadhi ya vyama shindani vlivyoamua kujitoa kwenye mchakato wa uchaguzi viliwahamasisha wanachama kukiunga mkono chama tawala kwenye mchakato wa kampeni mwaka jana. Hivi vyama vilipoteza sifa ya kuwa vyama shindani.
3. Baadhi ya vyama (wabunge wa vyama hivyo) walishirikiana na wabunge wa ccm kubadilisha vifungu vya kanuni za kudumu za bunge ili wakidhibiti chadema. Chama shindani kinaposhirikiana na chama kinachoongoza serikali kwa sababu ya kukidhoofisha chama shindani kingine, chama hicho pia kinakuwa kimepoteza sifa muhimu ya kuwa chama shindani.
4. Katika yale, ambayo chadema wanaona ni maslahi ya wananchi na wana wajibu wa kuikosoa serikali kwa kutumia haki yao ya kikatiba ya kufanya mikutano na maandamano, vyama kadhaa vimeungana na serikali kukikosoa chadema hata kuomba kifutwe. Vyama hivi navyo vimepoteza sifa ya kuwa vyama shindani.
5. Vyama shindani ni vile vinavyotoa changamoto kwa serikali ili iweze kuwajibika zaidi na kuleta maendeleo ya watu na vitu na siyo vile vinavyoi'fan' serikali ili izidi kulala usingizi.

kuna msemo unaosema kwamba utawala uliogawanyika hauwezi kuwa na nguvu - kwa maana kwamba kama vile ilivyo 'military strategy' kukabliana na 'common enemy', ndivyo pia ilivyo kwa siasa. Kama vyama shindani vinaungana na chama tawala haviwi tena na mlengwa mmoja (ccm) bali pia chadema au zaidi sana mlengwa wao amekuwa chadema. kwa namna nyingine (kwa kufanya hivi) ccm na vyama vingine vinakilenga chadema na kwa jinsi hiyo kukipa chadema nafasi kubwa ya kuwa na sifa ya chama (potential) kuongoza serikali.

q: Mna maoni gani?

hiyo itategemea na jinsi sisi wanancham na wapenzi wa chadema tutakavyoweza kuuandaa umaa wa watanzania watuamiani zaidi. Moja ya njia hizo ni katika yale majimbo na kata tulizoshinda tujitoe na tushirikiane kuchapa kazi ili wakati wa uchaguzi wasiwe na cha kusema. Lakini tukirithi utaratibu wa kiccm wa kushindwa kujitoa tutashindwa kuwashawishi wananchi kuwa chadema ni chama mbadala.
 
Na ccm is in the final stages of declining. Itabaki chadema tu. CDM is growing very very very....very fast at, a supersonic speed. Go chadema go.
 
Vingine vimekufa natural death na kwa kadri siku zinakwenda vitazidi kufa zaidi na kuona kuwa kama kweli kuwa wanatka demokrasia basi wafanye vile wengi na demands za watu zinasema nini ila ni CHADEMA pekee ndio yenye nguvu sana na hata kimkakati na kwa hali zote sisi kama Watanzania tupo na CHADEMA
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom