Tanzania iliyokomaa kisiasa.

Maendeleo101

Member
Nov 5, 2010
5
0
Midaharo yote iliyoendeshwa karibia kipindi chote cha kampeni imeleta changamoto kubwa sana.Hata hivyo mdahalo kuhusu kambi ya upinzani ndani ya bunge umekuwa wa aina yake hasa katika kuonyesha ni jinsi gani wanasiasa walio wengi bado hawajakomaa au basi hawajui kanuni na taratibu za midahalo kama hiyo.

Nimesikitishwa sana kuona watu walivyo na jaziba katika mambo madogo sana ya kutofautiana kwa hoja.Wale wenye uchanga wa namna hii wa kuhamaki kwa hoja aliyotoa mtu bila kugusa nafsi ya mtu fulani wachukue muda wao wajifunze kutoka wa midahalo ya wenzetu,hasa Wamarekani na Waingereza.
Tunapokuwa kwenye midahalo kama hiyo nguvu ya hoja ndo inayotawala sio kutoa mafumbo ya matusi ambayo watu walio makini watayatasri.Toa hoja nzito utasikilizwa.

Wale wanaojiita wanaharakati nao,hawana budi kujifunza kuongea bila ya kuwa na jaziba.Ni vizuri sana kupunguza hisia (emotions) katika midahalo kama hii na hasa itikadi iliyokidhiri(extremism) inayoweza pengine kusababisha kelele na mabishana na hatimaye kuzua ugomvi. Nenda youtube tafuta midahalo kati ya Obama na Hilary au Obama na McCain au Camerun and Goldon Brown,kama una nia ya kujifunza utapata mengi ya kujifunza kwenye midahalo kama hiyo.
 
Mbona hauko wazi ndugu?!
Watu wana jazba, akina nani? Wataje kama ulivyowataja Obama, McCain.
Usiogope! ni jambo jema unalotaka kutueleza.
 
Mbona hauko wazi ndugu?!
Watu wana jazba, akina nani? Wataje kama ulivyowataja Obama, McCain.
Usiogope! ni jambo jema unalotaka kutueleza
.

Wakati wa mdahalo kuhusu kambi ya upinzani,nilikuwa naangalia kupitia luninga yangu,mpaka kamera ziliondolewa kwa muda.Sikunoti nani alianzisha ila niliona mpaka watu walinyanyuka,na hii inaaashiria kupandwa na jaziba.

Nimefuatilia pia hoja za Mbowe na Hamadi.Nimeona Hamadi akigusa nafsi jambo ambalo si zuri mf pale aliposema Dk Slaa alimwambia ndoa ya pamoja imekwisha na wakati mwingine alipozungumzia udini alisema mtu fln alisema "kafu inawekuwa na uislamu slamu na yeye akijibu chadema ukatoliki ukatoliki"hakumtaja aliyesema.Alijitamba wakati fulani kuhusu ukongwe wake katika siasa,jambo ambalo halikuwa la msingi.Wakati anahitimisha kuna statement moja ya fumbo alisema "... waliokuwa kwenye kanisani na mashirikani warudi na waliokuwa wanafanya siasa waendelee kufanya siasa" Hili ni fumbo ila anayejua kufumbua fumbo ataelewa.

Dini zinaamsha sana hisia za watu,na inawezekana kabisa watu kuacha kuzungumzia hoja iliyo mezani pale hisia zao zinapoamshwa.Kwa hiyo watu wawe makini sana na hoja zao.Ukomavu wa kisiasa ni kuacha tofauti za udini na ukabila pembeni na kutumia nguvu ya hoja.

Hiyo ndo mifano ndugu.
 
Back
Top Bottom