zenmoster
JF-Expert Member
- Oct 3, 2011
- 951
- 201
Tanzania ikipeleka jeshi Kongo bi Joyce Banda karibu Tanzania waislamu tutakupa msaada kuchukua ziwa lote la Nyasa na hata ukitaka kuchukua kipande cha nchi kavu mpaka Mtwara.
Hatuoni sababu ya kuunga mkono jeshi letu kwenda Kongo huku serikali hiyo hiyo imepuuza madai yetu yote na hata masheikh kadhaa bado wako ndani ambapo msingi wa tuhuma dhidi yao ni madai ya waislamu.
Kwa upande mwengine jeshi litakalokwenda huko tutamuomba Mungu awapatie kipigo baada ya kipigo ikiwa si kutoka M23 basi janga baada ya janga kama vile Ebola au kipindupindu.
Tunajua kuwa hii ni kazi ya kutumwa kama ilivyokuwa kwa Uganda,Burundi na Kenya huko Somalia.Nchi hizo pamoja na kufanya kazi zilizotumwa lakini zinaambulia matusi na kejeli tu.Kwa akili zetu za kiafarika bado ziko mbioni kuitikia utumwa mwengine.
Kufanikiwa kwa jeshi huko DR of Congo tunajua itakuwa ni madhila mengine makubwa kwetu waislamu baada ya makampuni ya kiyahudi kudhibiti uchumi wote wa Kongo kwa msaada wa Tanzania.
Faida za kiuchumi kama matumizi ya bandari kupeleka mizigo huko wala si faida kitu kulinganisha na utu na imani zetu.Tumepata uzoefu wa hasara ambazo wenzetu wa Pakistan wamezipata kwa kusaidia kupitisha mizigo kupeleka Afghanistan.
Akili yako ndo imefikiri mpka hapo tu...kuombea ubaya nchi yako ya tanzania? Ukisema madai hayasikilizwi, kwanini msimlaumu Jk ambae pia ni mwislamu mwenzenu aliebariki kutiwa ndani kwa masheik wenu? Hadi suleimani kova pia mwislamu, said mwema pia mwislamu hadi jaji mkuu nae...wote hawa waislamu ila wamebariki kutiwa ndani kwa ponda na wenzake maana ni janga kwa taifa na hawana msaada wowote...hivyo kama umekasirishwa sana anza na hao viongozi wako ambao wote ni waislamu