Nkundwanabhake
New Member
- Oct 22, 2012
- 2
- 2
Awali ya yote napenda kuwapongeza wana Jf kwa kuendeleza kile kinachoitwa "uhuru wa fikra",nimekuwa mfuatiliaji wa maoni katika jukwaa hili. Kwa mara ya kwanza najiunga na forum hii kama Mtanzania mwenye uchungu na nchi yangu na mada hiyo hapo juu baada ya kutafiti na kugundua kuwa nchi yetu inapungukiwa na uongozi bora na ndiyo maana hatuendelei kwa spidi inayotakiwa tangu tuwe huru kuanzia mwaka 1961.
Tuna Raslimali za kutosha kuijenga nchi hii iwe sawa na nchi nyingine zilizoendelea, Mungu ametupatia mali asili hizi ili nchi yetu iwe mahali bora pa kuishi, kwa sababu ya kuwa na viongozi Wabinafsi wengi, hawa wachache wasio wabinafsi wanapojaribu kusukuma ili mambo yafanyike wanashindwa kwa sababu ya mfumo ama "System".
Hapa kinachotakiwa kwa Watanzania Wazarendo, wanaoumia kwa madudu yanayoendelea katika nchi hii ni kubadili Mfumo uliopo ama utawala uliokwishakita mizizi kwa muda mrefu na kujisahau.Tuna Madini ya vito, tuna dhahabu, tuna almasi tuna mbuga za wanyama kibao na sasa mafuta ya Gesi, Mungu atupe nini zaidi?
Lazima Watanzania tufanye maamuzi magumu ya kuondoa mfumo uliozoeleka tangu uhuru, tuondoe hofu ya kuvunjika amani, hatuwezi kuendelea hivi ati kwa kuogopa kusababisha vita, nani atakayeleta vita?
Lengo langu hapa ni kwamba tuondoe Mafisadi kwenye mfumo wa utawala halafu bila kujali vyama tuweke watu waadilifu kwenye mfumo wa Utawala, utaona matokeo yake ndani ya miaka 20 ijayo, Tanzania itakuwa nchi bora ya kuishi.
Tuna Raslimali za kutosha kuijenga nchi hii iwe sawa na nchi nyingine zilizoendelea, Mungu ametupatia mali asili hizi ili nchi yetu iwe mahali bora pa kuishi, kwa sababu ya kuwa na viongozi Wabinafsi wengi, hawa wachache wasio wabinafsi wanapojaribu kusukuma ili mambo yafanyike wanashindwa kwa sababu ya mfumo ama "System".
Hapa kinachotakiwa kwa Watanzania Wazarendo, wanaoumia kwa madudu yanayoendelea katika nchi hii ni kubadili Mfumo uliopo ama utawala uliokwishakita mizizi kwa muda mrefu na kujisahau.Tuna Madini ya vito, tuna dhahabu, tuna almasi tuna mbuga za wanyama kibao na sasa mafuta ya Gesi, Mungu atupe nini zaidi?
Lazima Watanzania tufanye maamuzi magumu ya kuondoa mfumo uliozoeleka tangu uhuru, tuondoe hofu ya kuvunjika amani, hatuwezi kuendelea hivi ati kwa kuogopa kusababisha vita, nani atakayeleta vita?
Lengo langu hapa ni kwamba tuondoe Mafisadi kwenye mfumo wa utawala halafu bila kujali vyama tuweke watu waadilifu kwenye mfumo wa Utawala, utaona matokeo yake ndani ya miaka 20 ijayo, Tanzania itakuwa nchi bora ya kuishi.