Tanzania huru inakuja

Johnsecond

JF-Expert Member
May 4, 2010
1,076
211
Ukombozi wa wamarekani weusi ulionekana ni ndoto pale alipopigwa risasi Martin Luther King Jr, rais Keneddy na Malcom X. Lakini kwa kuwa mabadiriko hayakuwa kwa hao watatu pamoja na kufa kwao ukombozi ulipatikana na sasa tunashudia Nigro anaongoza Marekani. Zitto utakaa sawa sawa kwenye vitabu vya kumbukumbu kama CCM watakavyo kaa na kama chama kitakachokuja kutukomboa kitakavyokaa kwa sasa CHADEMA. Hivyo mkimuua Dr. Slaa sio suluhisho la ukombozi wetu bali Zitto utachukua vihela au mshahara wako kwa muda tu bado mabadiriko yatatokea. Inaniuma sana kuona kijana mdogo kama wewe umehongeka kirahishi kuharibu maisha ya ndugu zako wengi sana. Hata ungepewa pesa kiasi gani ndugu zako wengi watakuwa maskini tu huwezi saidia wote, hukupima thamani ya kile ulichouza kuwa umeuza cheni ya dhahabu kwa hela bandia.

Huko uliko kugeukwa ni rahisi sana mwanangu tumeona wengi, hao sio wenzio kila unachofanya ni huduma waliyoinunua. Kioindi cha majuto kipo hapa hapa utasifiwa na kuongea nao meza moja lakini yote hayo yana mwisho, kwanza kuna wengine mnakaa nao meza moja hawapendi kile unachokinya na kukuona msaliti, watakuja kutuambia wakistaafu.
 
Back
Top Bottom