Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
CHAMA Cha Wananchi (CUF) kimeanza harakati za kuzishawishi nchi za Jumuiya za Ulaya kuweka vikwazo kwa Tanzania kutokana na matatizo yanayojitokeza katika uandikishaji wa daftari la kudumu la wapigakura linaloendelea visiwani Zanzibar.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho, Mhene Said Rashid ambaye yupo mji wa Stockholm nchini Sweden akijaribu kuzishawishi nchi za ulaya ya kaskazini kuweka mbinyo kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya zanzibar kwa kutoheshimu demokrasia.
Mjumbe huyo ambaye anatarajiwa kutembelea katika nchi za Finland, Sweden na Denmark na kuonana na wajumbe mbali mbali kwa lengo la kuzishawishi nchi hizo ambazo zinaifadhili tanznaia katika suala zima la kusimamia demokrasia nchini.
Akizungumza katika Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani (DW) jana asubuhi Rashid alisema lengo la safari hiyo ni kuzishawishi nchi zinazoifadhili Tanzania ziwache kuisaidia kutokana na kutoheshimu misingi ya demokrasia kutokana na wananchi wa zanzibar kunyimwa haki yao ya kuandikishwa katika daftari la kudumu la wapigakura linaloendelea hivi sasa ambapo kikwazo kikubwa na kukosekana kwa vitambulisho vya mzanzibari mkaazi.
"Hakuna suala la kuingilia mambo ya ndani jambo la msingi ni kuwa unposema unasaidia fedha kwa kusaidia aktika shughuli za uchaguzi ni pamoja na demokrasia na misingi yake, halafu ushindwe kusimamia demokrasia yenyewe hilo ni tatizo kubwa" alisema Rashid alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa Dw.
Nchi ya Sweden hivi sasa ni raia wa jumuiya za ulaya na ina nafasi kubwa katika kuzishawishi nchi nyengine za jumuiya hiyo katika kufuatilia suala la demokrasia ambapo nchi hizo zinatoa fedha nyingi kuisiadia tanzania katika uchaguzi mkuu ujao wa 2010.
"Tuna matatizo ya uandikishaji na hivi sasa umeanza kw avurugu na watu wnegi hwana vitambulisho na daftari hili ndilo litakalotumika katika upigaji kura tunajua nchi nyingi zinatumia vutambulisho lakini kwa misingi ya haki sisi kwetu hakuna haki inayotendeka" alisema Mkurugenzi huyo.
Alisema lengo kuu ni kuzielewesha nchi za ulaya zifahamu kwamba Tanzania na hasa Zanzibar hakuna demokrasia ya kweli katika chaguzi zinazofanyika hivyo kama nchi hizo zina uwezo wa kusaidia ziweze kuisaidia Zanzibar iweze kufuata misingi ya sheria na haki.....
SOURCE:ZANZIBAR YETU WEB BLOG.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho, Mhene Said Rashid ambaye yupo mji wa Stockholm nchini Sweden akijaribu kuzishawishi nchi za ulaya ya kaskazini kuweka mbinyo kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya zanzibar kwa kutoheshimu demokrasia.
Mjumbe huyo ambaye anatarajiwa kutembelea katika nchi za Finland, Sweden na Denmark na kuonana na wajumbe mbali mbali kwa lengo la kuzishawishi nchi hizo ambazo zinaifadhili tanznaia katika suala zima la kusimamia demokrasia nchini.
Akizungumza katika Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani (DW) jana asubuhi Rashid alisema lengo la safari hiyo ni kuzishawishi nchi zinazoifadhili Tanzania ziwache kuisaidia kutokana na kutoheshimu misingi ya demokrasia kutokana na wananchi wa zanzibar kunyimwa haki yao ya kuandikishwa katika daftari la kudumu la wapigakura linaloendelea hivi sasa ambapo kikwazo kikubwa na kukosekana kwa vitambulisho vya mzanzibari mkaazi.
"Hakuna suala la kuingilia mambo ya ndani jambo la msingi ni kuwa unposema unasaidia fedha kwa kusaidia aktika shughuli za uchaguzi ni pamoja na demokrasia na misingi yake, halafu ushindwe kusimamia demokrasia yenyewe hilo ni tatizo kubwa" alisema Rashid alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa Dw.
Nchi ya Sweden hivi sasa ni raia wa jumuiya za ulaya na ina nafasi kubwa katika kuzishawishi nchi nyengine za jumuiya hiyo katika kufuatilia suala la demokrasia ambapo nchi hizo zinatoa fedha nyingi kuisiadia tanzania katika uchaguzi mkuu ujao wa 2010.
"Tuna matatizo ya uandikishaji na hivi sasa umeanza kw avurugu na watu wnegi hwana vitambulisho na daftari hili ndilo litakalotumika katika upigaji kura tunajua nchi nyingi zinatumia vutambulisho lakini kwa misingi ya haki sisi kwetu hakuna haki inayotendeka" alisema Mkurugenzi huyo.
Alisema lengo kuu ni kuzielewesha nchi za ulaya zifahamu kwamba Tanzania na hasa Zanzibar hakuna demokrasia ya kweli katika chaguzi zinazofanyika hivyo kama nchi hizo zina uwezo wa kusaidia ziweze kuisaidia Zanzibar iweze kufuata misingi ya sheria na haki.....
SOURCE:ZANZIBAR YETU WEB BLOG.