TANZANIA ni nchi iliyojaliwa ardhi ambayo si mbaya kwa kilimo; ina madini tele yanayouzwa kwa bei sawa na bure kwa wageni; kuna mali asili tele; ina fukwe za bahari, maziwa na mito; ina milima kama Kilimanjaro na Meru; ina wanyama wasiopo kwingineko duniani; inaweza ikiwa kivutio kikubwa cha watalii miji, mitaa na mahoteli yakiwa na mandhari nzuri na usafi wa hali ya juu; inaweza ikawa na Dubai kadhaa za Afrika; inaweza ikawa na meli za kisasa za uvuvi; inaweza ikawa na mijidege ya kubeba mizigo toka China na Uarabuni kuja kuuzwa kwa Wakongomani, Burundi, Wazambia, Wazimbabwe, Wamalawi na Warundi na Wa nyaranda na kuwaondoa mamilioni ya Watanzania toka kwenye umasikini wa kutisha. Lakini umekwishajiuliza kwanini hakuna linaloendelea na badala yake wananchi wanaibiwa mchana kweupe na viongozi wao. Zipo sababu. Na baadhi yake ni hizi hapa:
i. Dhuluma serikali za awamu mbalimbali iilizowafanyia wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,
ii. Dhuluma waliyofanyiwa wajane wa maaskari waliokufa katika vita vya Kagera,
iii. Dhuluma wanayofanyiwa wapinzani na wale wasiokuwa wanachama wa chama tawala na viongozi na wanachama wa chama tawala,
iv. Dhuluma waliyofanyiwa na wanayoendelea kufanyiwa Waislamu ikiwemo kunyimwa Ofisi ya Kadhi, na upendeleo kwa wakiristo na hasa Wakatoliki,
v. Dhuluma ya ubia kati ya viongozi wa seirikali na wachimba madini kama vile almasi, dhahabu, tanzanite, vito na sasa uranium na platinum na mafuta ya peteroli wanayowafanyia Watanzania,
vi. Dhuluma inayofanywa na NSSF, PPF, LAPF na mifuko mbalimbali ikiwemo ile ya afya kwa Watanzania wafanyakazi,
vii. Dhuluma waliyofanyiwa na inayoendelea kufanyiwa wakulima na bodi au mamlaka za hiki au kile,
viii. Dhuluma wanayofanyiwa Watanzania na viongozi wao kutokana na mishahara na masurufu ya kufuru ikiwemo yale ya safari ambazo tayari zimekwishalipiwa na wahisani au nchi za nje,
ix. Dhuluma waliyofanyiwa Watanzania kwa kuuzwa mashirika ya umma na hata mmoja wao asillipwe hata senti tano,
x. Dhuluma inayofanywa na viongozi wa serikali kutumia matrilioni kwa magari, mafuta na meintenansi ya magari ya kifahari,
xi. Dhuluma wanayofanyiwa watoto kwa fedha yao inayotolewa na nchi za nje na Umoja wa Mataifa na hususan UNESCO kuliwa na wake na watoto wa wakubwa,
xii. Dhuluma wanayofanyiwa Watanzania na viongozi wao kwa kuuza miti na mali asili nyingine nje kwa bei sawa na bure,
xiiii. Dhuluma inayofanywa na benki na vyombo vingine vya fedha dhidi ya wanyonge na wajasiriamali wa Tanzania,
xiv. Dhuluma inayofanywa na Mamlaka za kodi dhidi ya watu wanaohangaika usiku na mchana kukidhi mahitaji yao ya msingi,
xv. Dhuluma inayofanywa na jumuiya au vyama vya hiki au kile dhidi ya wanachama wao ikiwemo wazee, wanawake, walimu, vijana na kadhalika,
xvi. Dhuluma wanayofanyiwa madaktari, manesi, walimu na wafanyakazi wengine,
xvii. Dhuluma wanayofanyiwa wanafunzi, machinga na vijana kwa ujumla,
xviii. Dhuluma wanayofanyiwa wapigania demokrasia na haki za binadamu,
xix. Dhuluma wanazofanyiwa wazee, walemavu, maalbino, masikini na wagonjwa,
xx. Dhuluma wanayofanyiwa wapiga kura wa nchi hii na chama tawala na mawakala wake,
xx. Dhuluma wanayofanyiwa Watanzania na baadhi ya mawaziri na wabunge ambao wanalipwa unono lakini wanachokifanya hakionekani,
xxi. Dhuluma, uonevu na unyanyaswaji wanayofanyiwa watembea kwa miguu na wale wenye magari wakiwemo wanasiasa na watumishi wa umma,
xxii. Dhuluma wanyofanyiwa baadhi ya watu na askari polisi vituoni na mabarabarani,
xxiii. Dhuluma wanayofanyiwa wananchi na wageni wanaowekeza au kuishi hapa nchini,
xiv. Dhuluma wanayofanyiwa wananchi na mahakama, bunge na vyombo vingine vinavyotegemewa kutetea haki zao,
xxv. Dhuluma inayofanyiwa vizazi vijavyo na chama tawala na viongozi walioko madarakani.
KWA MTAJI huu itakuwa ni vigumu sana kwa Watanzania kupata cha kutegemea achilia mbali neema au baraka inayoonekana na kuhesabika.
Na Watanzania wasimtegemee Muumba kuwa ndiye atakayebadili hali zao. Maana Muumba keshasema 'hatowasaidia watu hali zao kubadilika, hadi pale watakapomtambua na kujitambua wenyewe na kisha kuanza harakati za kubadilika wao wenyewe. '
TANZANIA KWA DHULUMA NDIYO YENYWE, NA MWENYEZI MUNGU KATU HAWAPENDI MADHALIMU. NI MSIBA MKUBWA ULIYOJE MAFISADI NA MADHALIMU KUIFANYA NCHI YETU ICHUKIWE NA MUUMBA NA MALAIKA WAKE!
huduma,
zanzibar
i. Dhuluma serikali za awamu mbalimbali iilizowafanyia wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,
ii. Dhuluma waliyofanyiwa wajane wa maaskari waliokufa katika vita vya Kagera,
iii. Dhuluma wanayofanyiwa wapinzani na wale wasiokuwa wanachama wa chama tawala na viongozi na wanachama wa chama tawala,
iv. Dhuluma waliyofanyiwa na wanayoendelea kufanyiwa Waislamu ikiwemo kunyimwa Ofisi ya Kadhi, na upendeleo kwa wakiristo na hasa Wakatoliki,
v. Dhuluma ya ubia kati ya viongozi wa seirikali na wachimba madini kama vile almasi, dhahabu, tanzanite, vito na sasa uranium na platinum na mafuta ya peteroli wanayowafanyia Watanzania,
vi. Dhuluma inayofanywa na NSSF, PPF, LAPF na mifuko mbalimbali ikiwemo ile ya afya kwa Watanzania wafanyakazi,
vii. Dhuluma waliyofanyiwa na inayoendelea kufanyiwa wakulima na bodi au mamlaka za hiki au kile,
viii. Dhuluma wanayofanyiwa Watanzania na viongozi wao kutokana na mishahara na masurufu ya kufuru ikiwemo yale ya safari ambazo tayari zimekwishalipiwa na wahisani au nchi za nje,
ix. Dhuluma waliyofanyiwa Watanzania kwa kuuzwa mashirika ya umma na hata mmoja wao asillipwe hata senti tano,
x. Dhuluma inayofanywa na viongozi wa serikali kutumia matrilioni kwa magari, mafuta na meintenansi ya magari ya kifahari,
xi. Dhuluma wanayofanyiwa watoto kwa fedha yao inayotolewa na nchi za nje na Umoja wa Mataifa na hususan UNESCO kuliwa na wake na watoto wa wakubwa,
xii. Dhuluma wanayofanyiwa Watanzania na viongozi wao kwa kuuza miti na mali asili nyingine nje kwa bei sawa na bure,
xiiii. Dhuluma inayofanywa na benki na vyombo vingine vya fedha dhidi ya wanyonge na wajasiriamali wa Tanzania,
xiv. Dhuluma inayofanywa na Mamlaka za kodi dhidi ya watu wanaohangaika usiku na mchana kukidhi mahitaji yao ya msingi,
xv. Dhuluma inayofanywa na jumuiya au vyama vya hiki au kile dhidi ya wanachama wao ikiwemo wazee, wanawake, walimu, vijana na kadhalika,
xvi. Dhuluma wanayofanyiwa madaktari, manesi, walimu na wafanyakazi wengine,
xvii. Dhuluma wanayofanyiwa wanafunzi, machinga na vijana kwa ujumla,
xviii. Dhuluma wanayofanyiwa wapigania demokrasia na haki za binadamu,
xix. Dhuluma wanazofanyiwa wazee, walemavu, maalbino, masikini na wagonjwa,
xx. Dhuluma wanayofanyiwa wapiga kura wa nchi hii na chama tawala na mawakala wake,
xx. Dhuluma wanayofanyiwa Watanzania na baadhi ya mawaziri na wabunge ambao wanalipwa unono lakini wanachokifanya hakionekani,
xxi. Dhuluma, uonevu na unyanyaswaji wanayofanyiwa watembea kwa miguu na wale wenye magari wakiwemo wanasiasa na watumishi wa umma,
xxii. Dhuluma wanyofanyiwa baadhi ya watu na askari polisi vituoni na mabarabarani,
xxiii. Dhuluma wanayofanyiwa wananchi na wageni wanaowekeza au kuishi hapa nchini,
xiv. Dhuluma wanayofanyiwa wananchi na mahakama, bunge na vyombo vingine vinavyotegemewa kutetea haki zao,
xxv. Dhuluma inayofanyiwa vizazi vijavyo na chama tawala na viongozi walioko madarakani.
KWA MTAJI huu itakuwa ni vigumu sana kwa Watanzania kupata cha kutegemea achilia mbali neema au baraka inayoonekana na kuhesabika.
Na Watanzania wasimtegemee Muumba kuwa ndiye atakayebadili hali zao. Maana Muumba keshasema 'hatowasaidia watu hali zao kubadilika, hadi pale watakapomtambua na kujitambua wenyewe na kisha kuanza harakati za kubadilika wao wenyewe. '
TANZANIA KWA DHULUMA NDIYO YENYWE, NA MWENYEZI MUNGU KATU HAWAPENDI MADHALIMU. NI MSIBA MKUBWA ULIYOJE MAFISADI NA MADHALIMU KUIFANYA NCHI YETU ICHUKIWE NA MUUMBA NA MALAIKA WAKE!
huduma,
zanzibar