Tanzania haiwezi kubadilika iwapo tutabaki kuwa kondoo

Singida ndio home

JF-Expert Member
Feb 23, 2012
3,192
3,351
Katika pita pita zangu mtandaoni nimeona jinsi nchi nyingi zilivyodai haki za kisiasa kwa kubishana na maamuzi ya kinyanyasaji yanayofanywa na serrikali zao kitu kinacholeta vurugu na umwagaji damu ndani ya nchi, ila mwishowe muungano wa wananchi katika kufanya sauti yao isikike huleta tunda katika taifa na huifanya nchi iwe imara maradufu.

Sasa nikija hapa kwetu Tanzania naona wazi kabisa jinsi wananchi wa hii nchi walivyo tofauti na nchi za wenzetu katika kudai haki, kila lifanywalo na serikali ndilo litakalokuwa, wananchi wanabaki kulalamika chini kwa chini kwa siku mbili tatu na ndio mwisho wa mjadala, Chukua mfano wa hili sakata la escrow kiukweli kila mwananchi mwenye uchungu wa maendeleo ya nchi hii aliumizwa, ishu ikawa juu kila kona ni escrow but the end result mawaziri wengi hawakujiuzulu, kiufupi hakuna uwajibikaji, ila wananchi wengi hawakufuraishwa na hiki kitendo kwani wananchi walitaka adhabu kali zitolewe kwa hawa watu, kiukweli niliona wananchi wengi walioumia lakini hakuna kitu kilichofanyika.

Wananchi wa hii serikali ni yetu, inatengenezwa na sisi na kwa manufaa ya kila mtanzania, Pale tunapoona serikali haiendi kunako stahili haina budi kuikalia serikali hadi kieleweke katika kutimiza wajibu wake, msione watu kwenye nchi nyingine wanagoma hadi kumwaga damu mkafikiri wanapenda, ni kwa ajili tu ya kuifanya serikali itanbue serikali haipo kwa manufaa ya wanasisa bali ni kwa ajili ya wananchi wote,
 
Wanasema ati, jeshi ni lao, polisi ni wao, wakidai haki wapigwe tu!!!! Hivi na sisi wananchi ni mali yenu...??? AMKA MTANZANIA HII NCHI NI YETU SOTE!!!
 
natumaini una mengi ya kujifunza kabla ya kujipa fikra mbovu kichwani kwako! tatzo lililopo litaisha mwakani, muhimu kuomba tumpate kiongozi bora na mwenye uchungu na nchi hii!!
Kumbuka kuombea amani!
 
natumaini una mengi ya kujifunza kabla ya kujipa fikra mbovu kichwani kwako! tatzo lililopo litaisha mwakani, muhimu kuomba tumpate kiongozi bora na mwenye uchungu na nchi hii!!
Kumbuka kuombea amani!

litaisha mwakani! naomba utupe mkakati uliokwishaandaliwa kusupport point yako, rais mwenye uchungu yuko wapi kama wanaogombea nafasi ya mwenyekiti pale c.c.--- kuna kina lowa---
 
Ni rahisi kunung'unika kuliko kudai haki.

Kila Mtanzania ana msubiri jamaa fulani ndani ya serikali shujaa kweli kweli aje apigane kufa kwa niaba yake.

Kila Mtanzania huyu yuko tayari kukaa mbele ya TV na kumsapoti shujaa huyushujaaa akirusha madongo na magongo hata ikibidi siku nzima.

Akisikia akina Dr Ulimboka wana andama anasahau kabisa ushujaa wake mbele ya TV na kuanza kuzoza.
Hawa madakitari hawana adabu kweli.

Tumewasomesha kwa hela zetu nyingi, mishahara wanalipwa mikubwa sana halafu wanajifanya kuandamana kweli si afadhari wapigwe tu hawa?

Huyo ni kilaMtanzania Typical na si ajabu ni wewe.
 
Hii pesa ya ESIKUROO kwa taarifa yako ni ya Kampeni za CCM mwakani.
Kwa hiyo usiwe na hofu watawagawia wananchi kwa uaminifu kadri wanavyoweza.
Sasa hivi hawa akina DR Tibaijuka ni makastodiani tu, wakati ukifika kila Mtanzania atapata sehemu ya maradi wa ESIKUROO na mambo yatakuwa safi.
Acheni kupiga kelele za kipuuzi. Hili dili la ESIKUROO ni kwa manufaa yenu wananchi.
MSiwasikilize akina Zitto wametumwa wale kuvuruga mipango kabambe ya maendeleo ya wananchi wa Tanzania.
KWanza Zitto ni Mtusi Banyamlenge yule raia wa Goma kama siyo Kongo.:becky:
 
Kuitoa ccm madarakani ni ndoto labda tusaidiwe na wazungu

CCM haitaondolewa na watu itaanguka yenyewe!!! Mugabe hataondolewa na wazimbabwe, ataondoka mwenyewe. Roman empire was not removed by Romans, it removed itself! Historia ni mwalimu mzuri sana. Yanayoendelea ndani ya CCM hayaashirii uhai wa milele, bali kuwa CCM imekaribia mwisho wake!
Chunguza historia utaona kuwa kila kilichoanzishwa na watu hufikia mwisho wake. Hata microsoft si wafalme tena wa software za computa; nani alijua kuwa NOKIA leo ingekuwa historia kwenye simu za mikononi. Ukitaka kuthibitisha kuwa kifo kipo, angalia makaburi!
 
Mkuu umeongea kweli tupu.Watanzania ni mabingwa wa kulalamika tu,linapokuja swala la utendaji,hapo ndipo utakapoona ushujaa wetu wa mdomoni unavyowekwa pembeni.
Hakuna kitu kibaya kama kuwa tegemezi. Utegemezi mbaya zaidi ni wa kifikra.Kwa nini unategemea mtu mwingine akuamulie mambo ya msingi badala ya wewe mwenyewe kujiamulia kwa kuufikirisha ubongo wako? Kwa nini uamini kuwa fulani ndiye anayeweza kuleta mabadiliko kwenye maisha yako na si wewe mwenyewe?Tuache kuweka matumaini yetu kwa mtu,tuweke matumaini yetu kwetu wenyewe kwa kufanya yale yanayotupasa kuyafanya huku tukimshirikisha Mungu.
Watanzania tuamke,tufanye maamuzi magumu kwa maslahi ya wananchi wote,na njia sahihi zaidi ni kwa kuanza na pale ulipo ama kwa kutoa elimu ya uraia na kujitambua,hasa ngazi ya kaya.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom