Tanzania haitambui ushindi wa Mugabe - Membe

Mafuchila

JF-Expert Member
Apr 29, 2006
751
65
Date::7/3/2008
Tanzania yatangaza kutotambua urais wa Robert Mugabe Zimbabwe
*Yasema uchaguzi ulikiuka vigezo vyote vya demokrasia

Na Muhibu Said


TANZANIA imesema haimtambui Robert Mugabe kama Rais halali wa Zimbabwe kwa kuwa amechaguliwa katika uchaguzi uliokiuka vigezo vyote vya demokrasia.


Msimamo huo wa Tanzania, ambao ni wa kwanza kutolewa tangu uchaguzi wa rais Zimbabwe urudiwe Juni 27, mwaka huu na kumrejesha Mugabe madarakani, ulitangazwa jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.


Waziri Membe aliwaambia waandishi wa habari katika makao makuu ya wizara hiyo, jijini Dar es Salaam kuwa msimamo huo umefikiwa kwa vile ushindi wa sasa wa Mugabe ni sawa na kufunga goli la kuotea katika mpira wa miguu.


''Uchaguzi wa Zimbabwe ni sawa na mchezo wa mpira. Goli la Mugabe limekuwa offside (la kuotea),'' alisema Membe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika (AU).

?Alisema ukiukwaji wa vigezo vya demokrasia katika uchaguzi wa rais wa Zimbabwe, ulibainishwa na ripoti ya waangalizi zaidi ya 413 walioshuhudia uchaguzi huo.


Membe alisema baadhi ya waangalizi, wanatoka Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Bunge la Afrika, wote waliridhika kuwa uchaguzi huo ulipoteza sifa ya kuwa huru na wa haki.


Alisema katika uchaguzi huo baadhi ya vyama (isipokuwa Zanu-PF cha Mugabe) havikuruhusiwa kufanya kampeni na baadhi ya wagombea walinyimwa fursa ya kutumia vyombo vya habari.


Alisema pia vitisho vilikithiri kwa wapiga kura na kwamba, hata vyombo vya habari vilivyojaribu kuwapa fursa baadhi ya wagombea vilifukuzwa Zimbabwe.


Kutokana na hali hiyo, alisema uchaguzi huo hautambuliki na hawaoni sababu ya kuwa na kigugumizi katika kulieleza jambo hilo.


''Hilo halitambuliki, sasa hapo kigugumizi kiko wapi? Kwa sababu ukikubali ripoti ya waangalizi, hutakuwa na haja ya kuuliza kama tunamtambua Mugabe kama Rais halali au la. Uchaguzi hautambuliki,'' alisema Membe alipokuwa akijibu swali la mwandishi mmoja wa habari jana.


Alisema msimamo wa kutotambua uchaguzi wa Zimbabwe, unaungwa mkono pia na AU na Sadc, baada ya kuridhika na ripoti ya waangalizi wa uchaguzi huo.


''Katika mkutano wa wakuu wa nchi za AU nchini Misri, hakuna kiongozi aliyeunga mkono wala kupongeza uchaguzi wa Zimbabwe,'' alisema Membe.


Alisema baada ya mkutano huo uliofanyika katika mji wa Sharm El-Sheikh wiki iliyopita, Mwenyekiti wa AU, Rais Jakaya Kikwete, aliteta na Mugabe na kumtaka ayazingatie yote yaliyozungumzwa katika mkutano huo juu ya hali tete iliyopo nchini mwake.


Hata hivyo, Waziri Membe alisema, AU imeiagiza Sadc ianze juhudi ya kuvikutanisha vyama vya MDC (cha Morgan Tsivangirai) na Zanu-PF, vikutane ili viunde serikali ya mpito, ikiwa ni njia pekee ya kuleta suluhu ya mgogoro wa kisiasa unaoikabili nchi hiyo hivi sasa.


''Hakuna chama kimoja kinachoweza kutawala peke yake kutokana na hali tete iliyopo Zimbabwe. Sasa hivi Zimbabwe haitawaliki. Zanu-PF haiwezi kutawala,'' alisema Membe na kuonya kuwa:


''Kama mazungumzo yakikwama, vikwazo ndio vitakavyokuwa silaha pekee Zimbabwe,''

alisema.

Source: Mwananchi 03/07/2008 in http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=6448
 
Last edited by a moderator:
Angalia makala yangu ya leo kwenye Tanzania Daima. Bernard Membe amesema kuwa Umoja wa Afrika hautambui Mugabe kama Rais wa Zimbabwe. Zaidi ya yote kwa niaba ya Mawaziri wa SADC amesema kuwa Au haiutambui uchaguzi uliofanyika huko Zimbabwe.
 
Ni Bora ila wasifanye kwa mashinikizo ya nje mbona walimkubali Kibaki?

This is double stadards, japo naunga mkono kutokumtambua Mugabe.
 
Kazi imeanza sasa, watafikia wapi kwenye hili?

Niliona PBS ya jumatatu kama sio jumanne wakiongelea hili ikabidi niunganishe ile interview ya Brokaw na Bill Gates ambapo Brokaw alimuuliza Bill Gates kama hajapata African fatigue (something like that) kwa kusaidia wasiosaidika?
 
ziunganisheni na hiyo nyingine.. naona mimi na Mafuchila tumegongana. Soma pia makala yangu ya Tanzania Daima leo. We dare to go where no one even think about...

Kwa hili serikali inahitaji pongezi.
 
Mbona wasimueleze hayo walipokuwa nae Egypt, wamekula na kunywa pamoja sasa hayuko machoni ndio wanatoa vistatement vyao, kule wnapongezana kisha huku wanalete story za ajabu ajabu. Wanaogopa joto ya jiwe!
 
Angalia makala yangu ya leo kwenye Tanzania Daima. Bernard Membe amesema kuwa Umoja wa Afrika hautambui Mugabe kama Rais wa Zimbabwe. Zaidi ya yote kwa niaba ya Mawaziri wa SADC amesema kuwa Au haiutambui uchaguzi uliofanyika huko Zimbabwe.

Bernard Membe toka lini anaiwakilisha AFRIKA?
Maslahi ya AFRIKA yalishamalizwa huko EGYPT...SASA MEMBE KAJIPA CHEO CHA UMAKAMU WA MWENYEKITI WA AU?
NB:NANI BADO ANAMSIKILIZA MEMBE?
 
Maslahi ya AFRIKA yalishamalizwa huko EGYPT...SASA MEMBE KAJIPA CHEO CHA UMAKAMU WA MWENYEKITI WA AU?

Membe anamuongelea mwenyekiti wa AU.

Lakini, hilo tamati African Union wamelifikia kwenye kikao gani? Mkutano wa Egypt si ulikwisha. Kwa nini hawakutangaza back then?

Na Mugabe alikubaliwa kuja Egypt kama nani, mwandishi wa habari?

Au ni Mwenyekiti wa AU kaamua akiwa Ikulu, akamtuma foreign minister wake aendee ukumbi wa Maelezo akatangaze.

Na kwanini waandishi wa media hawajasema ni kikao gani kimefikia hilo tamati?

Tanzania hakuna press.

Mushi bonge la pointi.
 
Hivi Tanzania inawezaje kuona umuhimu wa serikali ya mpito na umoja wa kitaifa kwa Zimbabwe, bila kwanza kupractise ushauri huo kwenye mgogoro wa CUF na CCM Zanzibar?
 
Membe ni mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa AU. labda hawakutaka kumuumbua Mugabe kule Egypt na kuwapa wazungu ujiko...
 
Mwanakijiji samahani, naona habari zetu zimegongana, lakini hata hivyo nilivyoelewa mimi Membe hakuzungumza kama mwenyekiti wa AU, ingawa kauli hiyo inaweza kugonga vichwa na kusaidia sana propaganda za vyombo vya magharibi, kwani Tanzania kama mwenyekiti wa AU tunapaswa kuwa makini sana na statement zetu kwani Wazungu wanachotafuta ni turufu tu, ikumbukwe kikao cha sekretarieti ya usalama Angola, Swaziland na Tanzania walivyokitengenezea mazingira ya kuwa ndio kauli ya Afrika.
 
Wanasubiri G8 summit huko JAPAN...Nyie mmesahau sisi ni kama wafungwa na viongozi wetu ni kama MANYAPARA?
WAMECHANGANYIKIWA!
HUKO IMF NI MCHINA NA MMAREKANI WANAPIGANA!
SASA HAWA KINA MEMBE NA MAFISADI WENGINE..BAADA YA KUONA MWANAWASA KAFARIKI...SASA WANAJISHIKA NA TSIVANGIRAI!
BUSH MWENYEWE HAPA KABLA YA KWENDA HUKO KWENYE G8 SUMMIT...AMEONDOA HATA ULE USEMI WAKE WA VIKWAZO VYA UCHUMI.
LAKINI SASA HUKO EUROPE MASLAHI NA ZIMBAWE NI MAKUBWA NA HAWATAKI DILI LOTE LIFE!
WAO KWA KUSHIRIKIANA NA MAFISADI WA NDANI...WAMETUPOTEZEA UHURU WETU!
 
Membe ni mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa AU. labda hawakutaka kumuumbua Mugabe kule Egypt na kuwapa wazungu ujiko...

Mkutano wa Waafrika unawahusu nini Wazungu? Wazungu na pilipili zao wanatuwashia nini wao wako shamba Downing street huko?

Na Mugabe kama sio Rais, aliingia kwenye kikao cha Viongozi wa Afrika kama nani, bodi gadi wa mtu?

Hicho kikao ambacho kina Membe wameamua kutokumtambua Mugabe kimefanyika lini na wapi? Kura zilikuwaje humo? Debate iliendaje? Transparency iko wapi?
 
Kwani wote walioingia Egypt walikuwa ni Marais..??

Yes!

Katiba ya AU inasema kikao cha Marais Mwanakijiji na Kuhani hawawezi kuingia. Unless ni wapiga picha au waleta chai au wabeba ma briefcase (ma foreign ministers wamo humu).

Mugabe aliingia kufanya nini, kumletea mtu chai?
 
ziunganisheni na hiyo nyingine.. naona mimi na Mafuchila tumegongana. Soma pia makala yangu ya Tanzania Daima leo. We dare to go where no one even think about...

Kwa hili serikali inahitaji pongezi.

Ile yako ni tofauti na hii!
Ile yako MEMBE AMEIWAKILISHA AFRIKA NA HII KAIWAKILISHA TANZANIA!
 
Hapa tupo pamoja bwana Membe. Ni mabadiliko makubwa sana kwenye sera yenu ya mambo ya nje na hasa kuhusu Zimbabwe, well, kama mnayo anyway!
 
membe Ni Mwenyekiti Wa Baraza La Mawaziri Wa Mambo Ya Nje Wa Au. Labda Hawakutaka Kumuumbua Mugabe Kule Egypt Na Kuwapa Wazungu Ujiko...

Hawakutaka Kumpa Mzungu Ujiko Egypt...na Hapa Tanzania Ndio Wampe Ujiko?
Ama Hiyo Mikataba Ya Kifisadi Si Ya Weupe?
Sinclair Ni Mwekundu,bluu,ama Mweusi?
 
Soma pia makala yangu ya Tanzania Daima leo. We dare to go where no one even think about...

Kwa hili serikali inahitaji pongezi.

Nakubali mkuu, kama vile mlikubaliana kabla hujaandika makala yako na Membe hajaitisha hiyo press conference.

Kwa hili hata mimi naipongeza sana serikali yetu kwa ujasiri. Maana hili ni jambo zito bwana, siku hizi ukimpinga Mugabe unaonekana umetumwa na wazungu. Eti sasa hivi u-panafricanism unapimwa kwa kumuunga mkono Mugabe, huu uhuni mimi nimeukataa, kama ni hivyo ndivyo kuwa pan africanist mimi nijitoe huko!
 
Back
Top Bottom