BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,994
Watanzania wakataa shirikisho Afrika Mashariki
*Asilimia 76 hawataki liwepo kabisa
*Kikwete asema maoni hayo yataheshimiwa
Na Ramadhan Semtawa
KAMATI ya kukusanya maoni kuhusu uharakishwaji (fast tracking) wa uanzishwaji wa Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki, imewasilisha ripoti yake kwa Rais Jakaya Kikwete, huku asilimia 75.9 ya Watanzania, wakipinga mpango huo.
Ripoti hiyo inaonyesha jinamizi la kero za muungano bado linaitafuna Tanzania, kwani idadi hiyo iliyopinga, imetaka kwanza kero hizo zitatuliwe kabla ya kukimbilia kwenye shirikisho.
Wakati hao wakipinga baada ya kuulizwa, wengine asilimia 3.3, bila ya kuulizwa, walituma maoni yao kukataa kabisa kuwepo kwa shirikisho hilo.
Akiwasilisha ripoti hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa kamati ya kukusanya maoni kuhusu mpango huo, Profesa Samwel Wangwe, alisema asilimia 20.8, waliunga mkono mpango huo kasi.
Katika ripoti hiyo, inaelezwa kuwa jumla ya Watanzania 65,000 walipata fursa ya kutoa maoni yao katika mikoa na wilaya zote, ambazo kamati ilifika.
Ripoti hiyo ambayo imegawanyika katika vitabu viwili pamoja na mkanda wa video, imegawanwa katika makundi mawili ambayo ni kisiasa na jamii.
Inaeleza kwamba Watanzania waliopinga shirikisho wamekuwa na sababu mbalimbali, ambazo moja ni ya kisiasa, kwamba hawalifahamu shirikisho hilo.
Sababu nyingine ni pamoja na demokrasi na utawala bora, ambapo Watanzania wana shaka kama vitu hivyo viwili vipo katika nchi nyingine.
Watanzania hao pia wameangalia suala la ulinzi, usalama na amani na tofauti za kiitikadi na pia walipinga kutokana na tofauti ya maendeleo ya kiuchumi kati ya nchi hizo na Tanzania hasa kulinganisha na Kenya.
Sababu nyingine ni kutaka kwanza, Tanzania itatue kero zake za muungano na Zanzibar kwani hadi sasa hazijamalizwa.
Akizungumza sababu za kuchelewa kuwasilisha ripoti hiyo, Profesa Wangwe, alisema kamati ilichukua maoni kwa njia mbalimbali ambazo ni pamoja na vyombo vya habari, kujaza dodoso na mtandao wa kompyuta kwa ajili ya kuwezesha hata Watanzania walio nje kupiga kura.
Rais Kikwete akizungumzia suala hilo, alisema maoni hayo ya Watanzania yataheshimiwa.
Alisema ingekuwa ni tatizo kama Watanzania hao wangesema hawataki shirikisho, lakini kwa kuwa hawataki liharakishwe, yeye haoni kama ni tatizo.
Rais Kikwete alisema ripoti hiyo itapelekwa katika ngazi ya Baraza la Mawaziri, ili ifanyiwe kazi na kisha kupelekwa katika wizara husika ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kuendelea na mchakato.
Kama maoni hayo yatazingatiwa, mchakato wa kuundwa kwa shirikisho utakwenda kama ilivyoelezwa katika mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Tayari hadi sasa nchi za EAC, zimeanza kutumia mfumo mmoja wa forodha (Customs Union), huku makubaliano mengine kama soko la pamoja (Common Market), sarafu ya pamoja (Monetary Union) na shirikisho la kisiasa (Political Federation) yakiwa bado hayajakamilika.
Tume hiyo ilianza kazi yake Oktoba 13 mwaka jana na imekabidhi ripoti yake Julai 13, ikiwa ni zaidi ya miezi sita imepita tangu ripoti hiyo ilipotakiwa kuwasilishwa.
*Asilimia 76 hawataki liwepo kabisa
*Kikwete asema maoni hayo yataheshimiwa
Na Ramadhan Semtawa
KAMATI ya kukusanya maoni kuhusu uharakishwaji (fast tracking) wa uanzishwaji wa Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki, imewasilisha ripoti yake kwa Rais Jakaya Kikwete, huku asilimia 75.9 ya Watanzania, wakipinga mpango huo.
Ripoti hiyo inaonyesha jinamizi la kero za muungano bado linaitafuna Tanzania, kwani idadi hiyo iliyopinga, imetaka kwanza kero hizo zitatuliwe kabla ya kukimbilia kwenye shirikisho.
Wakati hao wakipinga baada ya kuulizwa, wengine asilimia 3.3, bila ya kuulizwa, walituma maoni yao kukataa kabisa kuwepo kwa shirikisho hilo.
Akiwasilisha ripoti hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa kamati ya kukusanya maoni kuhusu mpango huo, Profesa Samwel Wangwe, alisema asilimia 20.8, waliunga mkono mpango huo kasi.
Katika ripoti hiyo, inaelezwa kuwa jumla ya Watanzania 65,000 walipata fursa ya kutoa maoni yao katika mikoa na wilaya zote, ambazo kamati ilifika.
Ripoti hiyo ambayo imegawanyika katika vitabu viwili pamoja na mkanda wa video, imegawanwa katika makundi mawili ambayo ni kisiasa na jamii.
Inaeleza kwamba Watanzania waliopinga shirikisho wamekuwa na sababu mbalimbali, ambazo moja ni ya kisiasa, kwamba hawalifahamu shirikisho hilo.
Sababu nyingine ni pamoja na demokrasi na utawala bora, ambapo Watanzania wana shaka kama vitu hivyo viwili vipo katika nchi nyingine.
Watanzania hao pia wameangalia suala la ulinzi, usalama na amani na tofauti za kiitikadi na pia walipinga kutokana na tofauti ya maendeleo ya kiuchumi kati ya nchi hizo na Tanzania hasa kulinganisha na Kenya.
Sababu nyingine ni kutaka kwanza, Tanzania itatue kero zake za muungano na Zanzibar kwani hadi sasa hazijamalizwa.
Akizungumza sababu za kuchelewa kuwasilisha ripoti hiyo, Profesa Wangwe, alisema kamati ilichukua maoni kwa njia mbalimbali ambazo ni pamoja na vyombo vya habari, kujaza dodoso na mtandao wa kompyuta kwa ajili ya kuwezesha hata Watanzania walio nje kupiga kura.
Rais Kikwete akizungumzia suala hilo, alisema maoni hayo ya Watanzania yataheshimiwa.
Alisema ingekuwa ni tatizo kama Watanzania hao wangesema hawataki shirikisho, lakini kwa kuwa hawataki liharakishwe, yeye haoni kama ni tatizo.
Rais Kikwete alisema ripoti hiyo itapelekwa katika ngazi ya Baraza la Mawaziri, ili ifanyiwe kazi na kisha kupelekwa katika wizara husika ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kuendelea na mchakato.
Kama maoni hayo yatazingatiwa, mchakato wa kuundwa kwa shirikisho utakwenda kama ilivyoelezwa katika mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Tayari hadi sasa nchi za EAC, zimeanza kutumia mfumo mmoja wa forodha (Customs Union), huku makubaliano mengine kama soko la pamoja (Common Market), sarafu ya pamoja (Monetary Union) na shirikisho la kisiasa (Political Federation) yakiwa bado hayajakamilika.
Tume hiyo ilianza kazi yake Oktoba 13 mwaka jana na imekabidhi ripoti yake Julai 13, ikiwa ni zaidi ya miezi sita imepita tangu ripoti hiyo ilipotakiwa kuwasilishwa.