Tanzania govt on Homosexuality: We can do without UK aid

mnachekesha sana, je ingewafurahisha kama angeunga mkono kauli ya Cameroon? Kapinga, nongwa, angeunga mkono ndo kabisaaaa!! ngozi nyeusi kazi kwelikweli
 
Tunashangaa nini wana jopo? Tumesahau kwamba anayemlipa mpiga zumari ndiye anayechagua wimbo.Wenzetu Ghana Rais wao prof Atta Mills na Yule waziri wa kigeni Uganda wameshapinga kauli ya kushinikiza ushoga ya Cameron kitambo mbembe anaushawishi kikauli tu but sio utendaji........Kazi ni kwetu nchi watumai cha ndugu(WAKOLONI) like TZ.......
 
Haya angeyasema kule kule australia alipokuwa nao hao watoa hoja.....kuja kutueleza sisi huku haisaidii hata kidogo , alitakiwa asimame hadharani kupinga hoja hii lakini kule kule, ukute kule alikuwa mdogoo kama piritoni ametua hapa anajitutumua!

mix with yours

Watu wengine bana kwa hiyo wewe ujapenda Membe alivyosema?
 
110% naungana na serikali yangu kupinga ushoga ndani ya Tanzania. Na kama Uingereza wanataka kutumia mapesa yao kueneza ushoga ni kheri kufa masikini kuliko kufanywa mashoga.
 
Inaonekana Mr Cameron kuna jamaa kaishamtamani ndio maana anatumia cheo chake kushinikiza kuhalalisha hilo. kuna mtu anataka kum Cameron!!
 
Sina imani na hawa watawala wetu watatuzunguka tuu hawa
Na jinsi serikali ilivyo na ukata wa hela
 
Nimesoma kwa mshtuko sana kauli za waziri mkuu wa Uingereza kulchanganya basic needs za maskini na kykubali mashoga

nina maswali mawili tu
1. Kwanini ushoga ahead of ufisadi?
2. Vipi wasianze wao na prince Harry aoe dume?
 
Mh Membe leo amekutana na waandishi wa habari kutujulisha yaliyojiri kwenye mkutano wa Jumuiya ya Madola uliofanyika huko Australia hivi karibuni. Mh Membe ametoa tamko dhidi ya kauli iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Uingereza ya kutishia kusitisha misaada ya kiuchumi kwa nchi za Jumuiya ya Madola zinazopinga suala la mahusiano ya watu wa jinsia moja.

Mh Membe amesema Katiba ya nchi inatambua familia kwa maana ya mahusiano ya kijinsia kati ya mume na mke na si vinginevyo. Amesema pia jadi na utamaduni wa Watanzania unaruhusu uhusiano wa mwanaume na mwanamke tuu na si vinginevyo. Mh Membe amesema Tanzania haikubaliani kwa namna yoyote ile na kauli ya Cameron na kwamba tutakuwa tayari hata kujitoa kwenye Jumuiya ya Madola kama Uingereza itashinikiza Tanzania itambue mahusiano ya watu wa jinsia moja.

Kwanza nimpongeze Mh. Waziri kama ameyatamka hayo kwa kumaanisha na siyo jokes za kisiasa tulizozizoea. Ila hapo kwenye red kuna mambo kama matatu hivi:-

(i) "... familia kwa maana ya mahusiano ya kijinsia kati ya mume na mke" ingekuwa vizuri kama angesema "... mahusiano ya kijinsia kati ya mume na mke au wake ..." kwani Katiba yetu inatambua ndoa za wake wengi; mfano za kimila. Vinginevyo zitaanza kupigwa kelele hapa.

(ii) Huwa najiuliza; hivi jadi na utamaduni wa mtanzania ni upi? Hivi UFISADI, UBADHIRIFU, UFUJAJI MALI ZA UMMA, DHULUMA, UPENDELEO, KUTOJALI WANYONGE, KUTOWAJIBIKA, n.k. ni utamaduni au jadi ya mtanzania? Kama sivyo, mbona hatusikii viongozi wetu akiwepo Membe wakikemea kwa nguvu zote? Hofu yangu ni kwamba akina Membe wasidandie hoja ya ushoga kwa malengo ya kisiasa ili pengine kuwasahaulisha watanzania shida kibao walizo nazo. Ushoga ni mbaya na hakuna mtanzania asiyejua hilo hata kama Membe asingetamka hayo aliyoyasema. Mbona mwatema mmbu na kumeza ngamia enyi wanafiki?

(iii) Mahusiano ya mume na mke/wake: Na tulipaswa kwenda mbali zaidi Cameroon na wenzake waambiwe hata hayo mahusiano ya mume na mke sharti yawe katika maumbile na njia ile inayofaa kama alivyoumba Mwenyezi Mungu. Kufanya kinyume (mfano kinyume na maumbile au kunyonyana sehemu nyeti) hata kama ni mume na mke halali kwa mujibu wa sheria na dini hakuna tofauti na ushoga tunaopigia kelele hapa!

Nasikia kuna jamaa fulani kwao mahusiano ya kinyume mradi ni mume na mke inaruhusiwa! Ole ni siku ile ya mwisho.
 
Haya angeyasema kule kule australia alipokuwa nao hao watoa hoja.....kuja kutueleza sisi huku haisaidii hata kidogo , alitakiwa asimame hadharani kupinga hoja hii lakini kule kule, ukute kule alikuwa mdogoo kama piritoni ametua hapa anajitutumua!

mix with yours

waziri mkuu wa UK hakutoa tamko katika kikao hicho cha jumuia ila alitoa nje ya kikao alipozungumza na wandishi wa habari hata Waziri wa mambo ya nje wa Kenya jana alisema kama angetoa tamko hilo katika kikao basi wangempinga vibaya sana
 
Hivi huyu Cameroun alidhamiria au anafanya utani! Yaani kututaka sisi kua mashoga ili watupe misaada!!? Duh! mbona yeye hajaolewa au kuoa mwanaume mwenzie? Aonyeshe mfano kwa vitendo,na hata kama jamani hatulikubali hili na Viongozi wetu lisimamieni kwa vitendo.Lets say NO!
 
Nimesoma kwa mshtuko sana kauli za waziri mkuu wa Uingereza kulchanganya basic needs za maskini na kykubali mashoga

nina maswali mawili tu
1. Kwanini ushoga ahead of ufisadi?
2. Vipi wasianze wao na prince Harry aoe dume?

Ushoga Uingereza unaruhusiwa -na kisheria watu wa jinsia moja wanaruhusiwa kuoana. Mfano ni Sir Elton John.

Lakini bado mimi sijaelewa haya makelele yanatoka wapi? David Cameron katoa masharti kwa Matonya kwamba ukipeleka kibakuli basi sharti ukubali 'kuhalalisha' ushoga. Hutaki peleka bakuli lako kwingine. Very simple. After all hela anayowapa inatokana na kodi za watu wa huko wengine wakiwa mashoga.

Mnaacha wajanja wanawaibia madini, voda wanakwepa kodi lakini mnamsumbuwa Cameron kila siku mnaomba chakula. Sasa kawapa masharti- no such thing as free lunch!
 
ndo mkome kuomba omba, tena mwambieni mkweree wenu kama vipi aanze yeye kuuza ule mtandao wa "O" kule uingereza
 
Kwani mtu anapopenda na kuamua kuwa shoga kunatatizo gani?Je kama mnasema Mungu amekataza kitu hicho nadhani mnatumia vitabu kama Quran na Biblia ambavyo ni mwongozo wa dini. Je Tanzania ni taifa la dini au vipi?Kama ni mambo yamakatazo ya dini yasiingilie privacy na haki ya mtu.
USHOGA SIO DHAMBI.

Bwana bshweko, kuna mambo mengine kwa kutumia akili ya kawaida tu bila kutumia bible ama quran unaweza kugundua kuwa kuna tatizo. Ukiangalia tu hata maumbile yenyewe hayaruhusu! Kila kiungo ktk mwili wa binadamu kinakazi maarumu, na kinaweza kuperform kazi yake kutokana na mechanism pamoja na virutubisho vilivyopo ktk hicho.., naturally! Sasa ktk hili wewe huoni kama kuna tatizo, tena ni tatizo la kiakili? Kuna vitu vya kuhalarisha, lakini si kila kitu chafaa!
 
Ushoga Uingereza unaruhusiwa -na kisheria watu wa jinsia moja wanaruhusiwa kuoana. Mfano ni Sir Elton John.

Lakini bado mimi sijaelewa haya makelele yanatoka wapi? David Cameron katoa masharti kwa Matonya kwamba ukipeleka kibakuli basi sharti ukubali 'kuhalalisha' ushoga. Hutaki peleka bakuli lako kwingine. Very simple. After all hela anayowapa inatokana na kodi za watu wa huko wengine wakiwa mashoga.

Mnaacha wajanja wanawaibia madini, voda wanakwepa kodi lakini mnamsumbuwa Cameron kila siku mnaomba chakula. Sasa kawapa masharti- no such thing as free lunch!

Asante Mkuu! Tumesahau hata ile methali ya wahenga kwamba; "Cha mwenzio Mavi kiteme mate" Leo tunalalamika! malalamiko yetu ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.
 
Back
Top Bottom