Dr Hassy Kitine msomi na mkurugenzi mstaafu wa usalama wa taifa UWT/TISS akizungumzia ushirikiano wa kikanda katika kipindi cha majadiliano TBC aliwahi kusema kuna nchi tatu tu katika afrika kusini mwa Equator ambazo zinalingana kwa utajiri wa rasilimali nazo ni DRC CONGO ANGOLA NA TANZANIA. Nchi hizi zina kila aina ya utajiri wa rasilimali( (natural resources) iwe ardhi madini maji misitu mafuta gesi asilia samaki etc etc. Akaendelea kusema ushirikiano kati ya nchi hizi tatu utakuwa wa usawa (equal patnership) hakuna atakayekuwa anachungulia kufaidi kwa mwenzake. Tunaoshirikiana nao kwa sasa hivi (EAC) hawana utajiri huo na wamekaa mkao wa fisi anayesuburi mkono(wa mtanzania)udondoke auokote. Haya si maneno yangu ni ya Dr Hassy Kitine. Kwenu waTanzania mlio humu jamvini.