Kitu kimoja ambacho watu wengi hawafahamu ni kwamba Watanzania wengi waliopo nje walienda kwasababu ya kazi na elimu. Diaspora wa Botswana na Namibia walienda kuanzia wakati wa Nyerere na walikuwa wanatuma pesa zao nyumbani. Fundisho kwa vijana ambao walikuwa wanapiga madongo diaspora watajifunza ni bora kupata kazi sehemu yeyote Duniani na kusaidia familia yako kuliko kushinda siku hadi siku kuomba kazi serikalini na kusubiri kupandishiwa mishahara ambayo ni midogo. Kule kuiba iba serikalini vilevile kunapungua na serikali inataka kupunguza matumizi. Hivyo nashauri vijana msiogope kutafuta kazi nje au hata kama upo hapo jiendeleze na tafuta kazi ambazo unaweza kufanyia bongo lakini kampuni za nje. Mahitaji ya kazi ni makubwa kuliko kasi ya serikali. Vilevile miradi kama ya kilimo cha kisasa na uvuvi wa kisasa sio vya kupuuza. Msije kupoteza muda mkawa wabangaizaji tu na degree zenu mjini jitumeni. Sisi miaka ya 1990’s tuliondoka kutafuta maisha baada ya kukataa kuwa mission town kila siku mnatakiwa kuangaika na kujipanga vizuri. Sasa mtakuja kugundua diaspora sio hao ambao mnawasema vibaya ni vijana wengi waliondoka kutafuta maisha kwasababu nchi haikuwa tayari kwa mahitaji na mategemeo ya wakati huo. Acheni kulalamikia serikali kazi wakati bado nchi iko chini sana na vijana chini ya miaka 25 ni asilimia 67