Tanzania customs na upotevu wa Makontena

Kweli

JF-Expert Member
Jul 14, 2007
1,152
302
Miaka nenda,miaka rudi tumekuwa tukisoma KERO zinazoiandama Bandari ya DAR kuhusiana na upotevu, uharibifu na ucheleweshaji wa huduma za makontena yanayoingia ama kupitia bandari hii ya DAR, wengi tunajua kuna ufisadi wa Hali ya juu huko TRA na Mamlaka ya Bandari na Serikali inapoteza mamillioni ya mapato kutokana na ufisadi na uzembe uliokithiri katika Idara hizi. Watanzania wengi wanaosafirisha vitu vyao nyumbani toka Ulaya na sehemu nyengine kwa huduma hii ya Kontena wanapata hasara kubwa, mimi binafsi nilipakia vitu vya nyumbani pamoja na gari mwezi wa December mwaka jana na kampuni ya Maersk na waliniahidi itafika baada ya mwezi,nilichukua likizo na kwenda nyumbani kufuatana na schedule ya meli ya Maersk lakini matokeo yake mpaka naondoka nikiwa nimechelewa kazini, nimeshapoteza nauli na hasara nyengine hakuna hio kontena??? lilipatikana baada ya miezi 5 baada ya kufuatilia sana.
Pengine Serikali ikianza kupata hasara kwa kila mteja kudai fidia kama huyu Mnaijeria Jude O Nwiza ndipo itawawajibisha watendaji wakuu wa THA na TRA.
Link ya habari hii hapa chini:
http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=6637
 
Clearing companies huwa wanatakiwa kulipa bond incase mizigo ikipotea wanatumia kufidia. Ila DSM Port hapafai, Bora kutumia bandari ya Mombasa. Dar usanii mwingi, jamaa wanachelewesha mizigo makusudi ili wapate hela za storage. Hii inafanyika makusudi kabisa na Viongozi wa nchi wanalifagilia
 
Ukweli ni kuwa hizo authorities zimekaa kama mitego kwa watanzania ambao hujaribu kuingiza mzigo ikiwa ni baada ya kujituma na kumwaga jasho kwa wingi na hao jamaa kuweka vikwazo alimradi uwape pesa za rushwa bila vigezo VYOVYOTE VYA MSINGI!
Wanafanya hivyo kwa kutumia mamlaka na majukumu waliyopewa kama waajiriwa na huku seriakli kwa ujumla, wizara na dept husika vikijua vilivyo nini kinaendelea!
Namna hii tutafika??????????
 
Back
Top Bottom