Tanzania: Chanzo cha kuporomoka kwa Maadili katika Jamii na Hatma ya Taifa!

Nyambala

JF-Expert Member
Oct 10, 2007
4,465
1,170
Nimekaa chini na kujaribu kukumbuka ni wapi watanzania tulianza kupotea kimaadili in gross terms na nimejikuta nikigota kipindi cha awamu ya pili. Pamoja na some good changes zilizofanyika kipindi hicho mfano re-introduction ya vyama vingi, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kushiriki/kushirikishwa, uhuru wa kuheshimu mawazo tofauti, kuondoa siasa mashuleni etc.

Lakini ni kipindi hiki hiki maneno kama "Dili" ikimaanisha biashara au shughuli ya kuingiza pesa chap chap (Whether legal or illegal) yalianza. Mengine pia kama Watu kutoheshimu amri za serikali, Misheni town, Uvamizi wa maeneo ya wazi, Waajiriwa hewa serikalini, Wizi mkubwa mkubwa wa mali ya umma, Kutoheshimu shule na proffesions, Kutoheshimu sheria, Uingizaji na uuzwaji Counterfeits bila woga, Kuporomoka kwa elimu, kutokulipa kodi, Kuongezeka kwa ujasiri wa kutenda uhalifu, Kuongezeka kwa uongo uongo etc. yalikuwa kwa kasi katika kipindi hiki.

Well najua kuna wengi watakuwa na maoni tofauti nadhani ni vema tujadili. Pia naomba nisieleweke kwamba hayo niliyoyataja hayakuwepo kabisa katika awamu ya kwanza. But it is the degree that do think should matter!


==========
SOMA ZAIDI:
==========

=> Mbowe alia na kuporomoka kwa Maadili! Soma - Kuyumba maadili chanzo cha gulio la kura - Mbowe

=> Maoni ya Mhe. Kigwangalla => Kuanguka kwa Nidhamu na Maadili Kutasababisha Kuanguka kwa Taifa!

ATHARI ZA KUPOROMOKA KWA MAADILI:
Maadili yatikisika ofisi nyeti nchini!

Raia Mwema - Mei 20, 2009

- Kuanzia Ikulu, Polisi hadi Magereza
- Vigogo wabweteka, sheria zavunjwa


HALI ya uadilifu miongoni mwa watendaji katika ofisi kubwa na nyeti za serikali kuanzia Ikulu, Ofisi ya Makamu wa Rais na hata katika vyombo vya ulinzi imetetereka, na hasa katika uzingatiaji wa matakwa ya kanuni na sheria za matumizi ya fedha.


Kuyumba kwa uadilifu katika ofisi hizo nyeti za serikali kumethibitishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, katika ripoti yake ya ukaguzi wa hesabu wa hadi Juni 30, mwaka jana.

Ikulu, ofisi ambayo ilipaswa kung'ara zaidi kimaadili mambo si swari ikibainika kuwa imekuwa ikifanya baadhi ya mambo shaghala baghala katika mipango yake ya ununuzi.

Doa hilo katika Ikulu linatajwa na CAG kuwa limetokana na ofisi hiyo nyeti kukiuka kifungu cha 45 kipengele &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];a' hadi &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];e' cha Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004.

Sheria hiyo iliyowahi kuwa gumzo katika mjadala wa kununua au kutonunua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans, inataka ununuzi ufanywe katika mpango mahsusi, unaokidhi mahitaji ya mwaka husika.

"Ofisi ya Rais &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; Ikulu haikuandaa mpango wa manunuzi na kufuata kama sheria inavyoelekeza," anaeleza CAG katika ripoti yake hiyo, ambayo pia iliwasilishwa katika Mkutano wa 15 wa Bunge, uliomalizika Aprili 30, mwaka huu.

Lakini si Ikulu pekee iliyobainika kukiuka sheria halali za nchi ambazo ofisi hiyo ilipaswa kuwa mfano katika kuziheshimu, bali hata Ofisi ya Makamu wa Rais.

Katika ofisi hiyo nyeti pia imebainika kuwa kulifanyika ununuzi wa samani kinyume cha matakwa ya sheria ya manunuzi.

"Manunuzi ya samani nje ya mpango wa manunuzi wa mwaka ya Sh 78,148,000 yalifanyika kwa kutumia njia ya moja kwa moja inayofaa kwa manunuzi madogo madogo, kinyume cha maelekezo ya kifungu namba 45 kipengele &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];a' na &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];d' cha Sheria ya Manunuzi ya Umma namba 21 ya mwaka 2004," anasema CAG.

Kuporomoka kwa maadili na kudharauliwa kwa sheria katika ofisi hiyo ya Makamu wa Rais pia kumebainishwa na CAG katika matumizi sahihi ya bajeti iliyotengwa.

Katika hilo, CAG anasema; "Malipo ya madeni ya Sh 89,244,290 yalifanyika kwenye bajeti ya mwaka huu ulioishia Juni 30, 2008, bila idhini. Risiti za kukiri malipo ya Sh. 8,920,000 hazikuwasilishwa kwa ukaguzi."

Mbali na hayo, CAG anasema kulikuwa na mali zenye thamani ya Sh. 191,124,623 ambazo hazikuingizwa kwenye rejesta ya mali za kudumu, hapa sababu za hali hiyo zikiwa hazijabainishwa japokuwa ni dhahiri kuwa kuna uzembe na utovu wa maadili.

Katika hatua nyingine, kwa mujibu wa ukaguzi wa hesabu na katika hali ya kuzua maswali mengi, imeelezwa kuwa madeni ya Sh 208,058,691 hayakukaguliwa kutokana na kukosekana nyaraka ambatanifu.

Hali hiyo inayotia shaka mustakabali wa Taifa kama itaachwa iendelee pia imeikumba Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali. Katika ofisi hii, inaelezwa kuwa mishahara ya jumla ya Sh 8,553,453.39 ililipwa kwa watu waliokwishaondoka katika utumishi wa umma.

Utata wa kimaadili katika ofisi nyeti za umma pia imevikumba vyombo vya dola ikiwa ni pamoja na Jeshi la Polisi na Magereza.

Katika idara ya polisi malipo ya Sh. 74,110,000 yalifanywa bila kuwapo nyaraka sahihi.

"Kufikia mwisho wa mwaka, Juni 30, 2008 kulikuwa na masurufu yasiyorejeshwa yanayofikia Sh 131,000,000. Huu ni ukiukaji wa kanuni namba 103 kifungu 1 ya kanuni za fedha za umma za mwaka 2001 (kama zilivyorekebishwa 2004)," anasema CAG na kufafanua kuwa;

"Kanuni hizo zinataka marejesho yafanyike mara baada ya mambo yaliyosababisha masurufu hayo kulipwa kukamilika au ifikapo siku ya mwisho ya mwaka ambao masurufu yalitolewa.

Jambo jingine la kutilia shaka ni kwamba taarifa za utendaji zinazoonyesha malengo mkakati, mafanikio yaliyotarajiwa na mafanikio halisi haikuwasilishwa kwa CAG pamoja na taarifa za fedha kinyume cha matakwa ya kifungu namba 8 kipengele cha 5 cha sheria ya fedha za umma namba 6 ya mwaka 2001.

Katika Idara hii ya Polisi kashfa kubwa zaidi iliyoibuka wakati wa ukaguzi wa CAG ni kufanya matumizi zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Taarifa ya fedha ilionyesha huduma ambazo hazijalipwa za jumla ya Sh. 2,024,920,000. Hii ina maana ofisa masuuli alitumia kiasi hicho, zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge. Kama kiasi hiki kingelipwa na kuingizwa kwenye taarifa ya matumizi fungu hili lingekuwa na malipo ya ziada ya kiasi hicho hicho.

"Taarifa ya fedha inaonyesha kiasi cha madeni ya Sh. 23,354,120,000 na hali hii ni uthibitisho kuwapo matumizi zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa" anasema CAG.

Kwa upande wa Idara ya Huduma za Magereza, uongozi uliidhinisha matengenezo ya magari ya Sh. 205,404,964 bila kupitia kwa Wakala wa Ufundi na Umeme kinyume cha matakwa ya kanuni namba 59 (1) &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; (2) ya kanuni za umma za manunuzi za mwaka 2005.

Kwa sababu hiyo, ubora wa matengenezo yaliyofanyika na thamani iliyopatikana kutokana na matumizi hayo haikuweza kuthibitishwa kwa vile magari husika hayahakikiwa na ofisa au fundi aliyeidhinishwa.

"Malipo ya Sh 824,563,334 yalifanywa bila kuwapo nyaraka sahihi. Kiasi cha Sh 16,536,960 kililipwa kwa ofisa aliyeenda India kwa matibabu bila kuwapo rufaa iliyoidhinishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

"Manunuzi ya Sh. 119,875,376 yalifanywa kwa kutumia kinukua bei na bila ya kupitisha kwenye Bodi ya Manunuzi kinyume na kifungu namba 30 cha sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004," anaeleza CAG katika taarifa yake kuhusu ukaguzi wa hesabu za serikali kuu.
 
  • Maendeleo ni hatua ya kuhama kutoka ngazi moja kuelekea ngazi nyingine iliyo bora zaidi kuliko ya awali. Kwa mfano, mawasiliano yamekuwapo toka zamani, lakini leo yameboreshwa zaidi. Chukulia mfano huu, zamani kukitokea msiba, alikuwa anatumwa mtu apelike taarifa kwa walio mbali, lakini leo ni ndani ya muda mfupi tu kupitia simu, taarifa zinamuwasilia mlengwa.
  • Lakini si kila maendeleo ni kwa ajili ya kusaidia watu, bali ni ili kuvuruga maadili bora. Na ndio maana leo simu zinauzwa bei nafuu, umeme unapaswa usambazwe hadi vijijini ili kile kinachotokea Marekani, kifanywe pia nchi za mbali na Marekani. Kwa mfano kama mwanamziki anaimba akiwa uchi na vitu vingine, vifanywe pia na watu walio katika mataifa ya mbali.
  • Mfano wa maendeleo yaliyosababisha mmomonyoko wa maadili ni huu ufuatao.
  • Zamani kulikuwa na watu ambao walikuwa wanachungulia watu wanaofanya mapenzi(wapiga chabo), na nyumba nyingi za wageni zilikuwa na madirisha ambayo nyavu zake zilikuwa zimetobolewa ili kurahisisha zoezi la kupiga chabo. Ili kurahisisha zaidi, leo hii iwe ni katika simu, kompyuta na tablet, mwanadamu amerahisishiwa kupiga chabo kwa kutosimama tena madirishani, bali leo ni kupitia kuangalia picha za ngono. Wapiga chabo wengi walikuwa wakikumbana na adha za kupigwa, kumwagiwa maji ya moto n.k, lakini wapiga chabo kwa njia ya kuangalia picha za ngono hawapati adha kama hizo(maendeleo).
  • Licha ya kutopambana na adha nyingi kama zamani(kuumwa na mbu, vipigo n.k), lakini bado kuna athari kubwa kwa wapiga chabo wa kisasa(waangalia picha za ngono), baadhi ni hizi zifuatazo.
    1. Kuongezeka kwa tama za mapenzi(waweza rejea kilichompata Daudi baada ya kumtazama mwanamke aliyekuwa anaoga). Na tama hizi zimepelekea wanadamu kutotofautiana na wanyama katika suala la mapenzi. Maana leo hii kutokana na picha za ngono, kumepatikana wazazi wanaofanya mapenzi na watoto wao, yaani unakuta baba anafanya mapenzi na binti yake, mama anafanya mapenzi na kijana wake pia dada na kaka yake katika familia.
    2. Mashoga na wasagaji wengi kuzalishwa kila siku kutokana na kutazama picha hizo.
    3. Nyingine ongezea mwenyewe.
Lakini maendeleo haya hayaletwi kwa ajili ya urafiki, bali lengo lake kuu ni kukupoteza, kukufanya uwe kipofu japo una macho. Tafakari na chukua hatua za kuondokana na huu upigaji chabo wa kisasa.

  • Maendeleo ni hatua ya kuhama kutoka ngazi moja kuelekea ngazi nyingine iliyo bora zaidi kuliko ya awali. Kwa mfano, mawasiliano yamekuwapo toka zamani, lakini leo yameboreshwa zaidi. Chukulia mfano huu, zamani kukitokea msiba, alikuwa anatumwa mtu apelike taarifa kwa walio mbali, lakini leo ni ndani ya muda mfupi tu kupitia simu, taarifa zinamuwasilia mlengwa.
  • Lakini si kila maendeleo ni kwa ajili ya kusaidia watu, bali ni ili kuvuruga maadili bora. Na ndio maana leo simu zinauzwa bei nafuu, umeme unapaswa usambazwe hadi vijijini ili kile kinachotokea Marekani, kifanywe pia nchi za mbali na Marekani. Kwa mfano kama mwanamziki anaimba akiwa uchi na vitu vingine, vifanywe pia na watu walio katika mataifa ya mbali.
  • Mfano wa maendeleo yaliyosababisha mmomonyoko wa maadili ni huu ufuatao.
  • Zamani kulikuwa na watu ambao walikuwa wanachungulia watu wanaofanya mapenzi(wapiga chabo), na nyumba nyingi za wageni zilikuwa na madirisha ambayo nyavu zake zilikuwa zimetobolewa ili kurahisisha zoezi la kupiga chabo. Ili kurahisisha zaidi, leo hii iwe ni katika simu, kompyuta na tablet, mwanadamu amerahisishiwa kupiga chabo kwa kutosimama tena madirishani, bali leo ni kupitia kuangalia picha za ngono. Wapiga chabo wengi walikuwa wakikumbana na adha za kupigwa, kumwagiwa maji ya moto n.k, lakini wapiga chabo kwa njia ya kuangalia picha za ngono hawapati adha kama hizo(maendeleo).
  • Licha ya kutopambana na adha nyingi kama zamani(kuumwa na mbu, vipigo n.k), lakini bado kuna athari kubwa kwa wapiga chabo wa kisasa(waangalia picha za ngono), baadhi ni hizi zifuatazo.
    1. Kuongezeka kwa tama za mapenzi(waweza rejea kilichompata Daudi baada ya kumtazama mwanamke aliyekuwa anaoga). Na tama hizi zimepelekea wanadamu kutotofautiana na wanyama katika suala la mapenzi. Maana leo hii kutokana na picha za ngono, kumepatikana wazazi wanaofanya mapenzi na watoto wao, yaani unakuta baba anafanya mapenzi na binti yake, mama anafanya mapenzi na kijana wake pia dada na kaka yake katika familia.
    2. Mashoga na wasagaji wengi kuzalishwa kila siku kutokana na kutazama picha hizo.
    3. Nyingine ongezea mwenyewe.
Lakini maendeleo haya hayaletwi kwa ajili ya urafiki, bali lengo lake kuu ni kukupoteza, kukufanya uwe kipofu japo una macho. Tafakari na chukua hatua za kuondokana na huu upigaji chabo wa kisasa.
 
Nadhani kwa mawazo yangu, kujadili lini maadili yalianza kuporomoka si jambo la msingi sana.

Wote tunakubaliana kwamba maadili yameporomoka. Kama kuna wasio kubali, basi hao wana ajenda zao za siri.

Nadhani la msingi kujadiliwa ni jinsi ya kurekebisha hali hiyo, ili Tanzania isizidi kuelekea "to the abyss."
 
Nyambala,

Kichwa cha hoja yako kinasema "Maadili Tanzania yalianza kuporomoka". wakati huo huo kwenye ufafanuzi wako unasema "yalikuwa kwa kasi katika kipindi hiki".

Ni dhahiri hujui, sijui na hakuna ajuaye maadili yalianza kuporomoka wapi na lini.

Kama alivyosema Tikerra muda sio hoja, muhimu ni kuwa kutoka hapa tulipo tuende wapi kwa kutumia njia gani?
 
Kichwa cha hoja yako kinasema "Maadili Tanzania yalianza kuporomoka". wakati huo huo kwenye ufafanuzi wako unasema "yalikuwa kwa kasi katika kipindi hiki". Ni dhahiri hujui, sijui na hakuna ajuaye maadili yalianza kuporomoka wapi na lini. Kama alivyosema Tikerra muda sio hoja, muhimu ni kuwa kutoka hapa tulipo tuende wapi kwa kutumia njia gani?
Nyambala kasema,maadili yalianza kuporomoka awamu ya pili ya uongozi wa Taifa letu.
Hivyo,awamu ya kwanza ili kwanza ilikuwa shwari;kwa hiyo utamaduni wa awamu ya kwanza urudishe katika matumizi ya maisha yetu ya kila siku.
 
Nyambala kasema,maadili yalianza kuporomoka awamu ya pili ya uongozi wa Taifa letu.
Hivyo,awamu ya kwanza ili kwanza ilikuwa shwari;kwa hiyo utamaduni wa awamu ya kwanza urudishe katika matumizi ya maisha yetu ya kila siku.

Agreed!!
 
Juzi nimemsikia Mzee Mwinyi akisema alileta sera za "ruksa" kuliua azimo la Arusha.
Lakini alichokifanya ni kama mzazi kumwaga chini maji ya beseni huku mtoto akiwa ndani ya beseni. Arusha lilikuwa na maadili ya uongozi. Zanzibar likayafuta. Matokeo yake ni huu ufisadi uliokithiri hadi Ikulu
 
Last edited:
Nyambala anasema alijaribu kukumbuku ni lini maadili yalianza kuoromoka, nadhani akaishia nusu ya ufunuo na akanza kuandika je anakumbuka majina na maneno haya yalikuwepo wakati gani? RTC BOT NBC GAPEX UGAWAJI MADUKA YA USHIRIKA ULANGUZI MIKINGAMO nk na JOKERI la la kumalizia mchezo ilikua OPERESHENI ya marehemu SOKOINE??????

Nyambala,

Kichwa cha hoja yako kinasema "Maadili Tanzania yalianza kuporomoka". wakati huo huo kwenye ufafanuzi wako unasema "yalikuwa kwa kasi katika kipindi hiki".

Ni dhahiri hujui, sijui na hakuna ajuaye maadili yalianza kuporomoka wapi na lini.

Kama alivyosema Tikerra muda sio hoja, muhimu ni kuwa kutoka hapa tulipo tuende wapi kwa kutumia njia gani?
 
Maadili yalianza kuporomoka pale walipo-dhulumiwa watu mali zao na kufanywa mali za umma.

Nani ataewajibika ikiwa ni mali ya umma?
 
Nyambala,

Inawezekana awamu ya pili ilikuwa ni mwanzo wa mambo mengi lakini hili la kuporomoka maadili nahisi halikuanzia hapa. Sioni haja ya kuzunguka sana kujaribu kutetea hoja yangu isipokuwa kama tutajuuliza awamu hiyo ilipochukuwa hatamu mashirika ya umma mangapi yalikuwa yakifanya kazi au kulikuwa hakuna waliokuwa na maisha mazuri kwa kutumia nyenzo za umma na kuwaacha wengine wakiwa na maisha duni.

Aidha juu ya utajiri na nguvu za wananchi kuwepo mbona tulifikia hatuwa ya kula dona la Yanga? Pengine katika historia ya Tanzania hatujawahi kuwa na maisha magumu kama tuliyoyapat mwisho wa awamu ya Kwanza.

Suala la kujiuliza hapa kuwa kuanzia 1961 hadi 1985 karibu miaka 25 chini ya utawala wa maadili ni nini kilitusibu hadi tukawa fukara mbali ya umasikini?

Hata hivyo ushahidi ulikuwapo kuwa bado viongozi hawakuwa na matatizo ya maisha kama wananchi walivyokuwa na tabu za maisha, sasa uadilifu ulikuwepo wapi?
 
Juzi nimemsikia Mzee Mwinyi akisema alileta sera za "ruksa" kuliua azimo la Arusha.
Lakini alichokifanya ni kama mzazi kumwaga chini ya maji ya beseni huku mtoto akiwa ndani ya beseni. Arusha lilikuwa na maadili ya uongozi. Zanzibar likayafuta. Matokeo yake ni huu ufisadi uliokithiri hadi Ikulu

Kuna ushahidi wowote nkuwa hilo Azimio likifuatwa?
 
Ngekewa,

Ili kupata ufumbuzi mwema na bora ni lazima tuanzie mwanzo: kwani miaka 25 ni muda mrefu kwa hali yeyote na katika fani yeyote.

Kwa hiyo swala la umaskini na ufukara tumetoka navyo awamu ya kwanza (Pamoja na SIFA NJEMA kwa Mwalimu za kutuachia zaidi ya 3/4 ya MALI ASILI ikiwa haijaguswa)
 
Kuna sababu nyingi za chanzo cha kuporomoka maadili zinazotajwa na wataalamu wa masuala ya elimu jamii wewe binafsi unadhani mambo gani yamechangia maadili ya jamii hasa Tanzania kuporomoka kiasi hiki, hasa umalaya, kuvaa uchi, ulevi, utovu wa adabu, wizi, lugha chafu na mengineyo?
 
Rejea maandiko matakatifu. MATH24:3- Kaka huo bado ni mwanzo tu. Kama wadada wa university wanavaa masalawili na vipedo, unatarajia nani wa kurekebisha jamii.

Nina imani hata humu JF wamo wa dada wanavaa vibaya au kina kaka wanayapenda mavazi mabovu. Ingawa maadaili si mavazi tu, hata lugha. Wasomi nao wanachangia.
 
Watu wameachana na mafunzo yote ya mila zao achilia mbali dini zao ndo Tv, internet, simu zimekuwa walimu siku hz na huu ni mwisho wa dunia unaaproach kabisa.

Masharobaro na masista du ndo ful kuiga akina justin biebier, Kim kardashian, Lil Wayne na wamarekani weusi wakidhani ni UJANJA au ndo kwenda na wakati mi nawaonea huruma sana watu kama hawa hasa akina dada imagine mtu kavaa skin tight jua kali ama night dress kariakoo sa saba mchana?

Wanapiga jeki manyonyo na kuyaacha wazi mi sipendi uhalo huu jamani..we acha tu hata humu Jf wamo lets wait for ther comments
 
Nashindwa kupata jibu hapa nani wakumlaumu kwa matukio yote machafu yanayofanywa na jeshi la police.

je ni viongozi wa ngazi zajuu katika jeshi la police,raisi wetu kwauteuzi mbovu wa viongozi wa jeshi la police,katiba yetu iliyompa madaraka makubwa raisi au mmomonyoko wa maadili katika jeshi letu la police unaosababishwa na ajira za kindugu zilizopelekea jeshi la police kuwa jalala la wahuni.

Nasema jalala sababu jeshi la police limejaa vilaza,wavuta bangi na waliofake vyeti.

Kwa maoni yangu mimi nailaumu katiba tuliyonayo sasa &[HASHTAG]#305[/HASHTAG];mempa raisi madaraka makubwa sana ya uteuzi, waliyotunga katiba hawakukumbuka kuwa akili za wanadamu hazifanani matatizo yamekuja pale nchi ilipokabidhiwa kilaza namajuku yote muh&[HASHTAG]#305[/HASHTAG];mu ya nchi hususani uteuz&[HASHTAG]#305[/HASHTAG]; wa v&[HASHTAG]#305[/HASHTAG];ongoz&[HASHTAG]#305[/HASHTAG]; yako ch&[HASHTAG]#305[/HASHTAG];n&[HASHTAG]#305[/HASHTAG]; yake wewe unategemea n&[HASHTAG]#305[/HASHTAG];n&[HASHTAG]#305[/HASHTAG]; k&[HASHTAG]#305[/HASHTAG];tafany&[HASHTAG]#305[/HASHTAG];ka.

WATANZAN&[HASHTAG]#304[/HASHTAG];A TUSIFANYIE MZAA KATIKA HAYA TUNAYOYAONA SASA HUN&[HASHTAG]#304[/HASHTAG];MWANZO TU KTAKUJA KILAZA KINGINE KIFANYE MADUDU ZAIDI YA KILAZA ALIYETOKA. TUSIKUBALI KUBURUZWA KATIKA MCHAKATO WAKUPATA KATIKA MPYA.ASANTEN&[HASHTAG]#304[/HASHTAG]; ...... AMAN&[HASHTAG]#304[/HASHTAG]; NA UPENDO DAIMA.
 
Polisi ni jamii part ya jamii yetu ila siku hizi hampendwi kila kona,Wakuu wa idara hii inabidi mchukue hatua vijana wenu wanawawakilisha vibaya huku mitaani.
 
serikali ndio yakulaumiwa sababu mishahara inayowalipa askari wa jeshi la polisi haikizi mahitaji yao ndomana wanatafuta njia nyingine za kuongeza kipato chao.Wanachojua viongozi wetu ni kujilimbikizia mali ya uma na si kuboresha maisha ya watumishi wao ndomana haya yote yanatokea.
 
ilaumiwe ccm. Kwa swali la pili nini kifanyike ccm iondolewe madarakani... Over!!!
 
Swali hilo ukimuuliza Juma Nkamia, Mbunge wa Kondoa atakujibu Jamii Forums ndio walaumiwe!
 
Back
Top Bottom