Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Nimekaa chini na kujaribu kukumbuka ni wapi watanzania tulianza kupotea kimaadili in gross terms na nimejikuta nikigota kipindi cha awamu ya pili. Pamoja na some good changes zilizofanyika kipindi hicho mfano re-introduction ya vyama vingi, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kushiriki/kushirikishwa, uhuru wa kuheshimu mawazo tofauti, kuondoa siasa mashuleni etc.
Lakini ni kipindi hiki hiki maneno kama "Dili" ikimaanisha biashara au shughuli ya kuingiza pesa chap chap (Whether legal or illegal) yalianza. Mengine pia kama Watu kutoheshimu amri za serikali, Misheni town, Uvamizi wa maeneo ya wazi, Waajiriwa hewa serikalini, Wizi mkubwa mkubwa wa mali ya umma, Kutoheshimu shule na proffesions, Kutoheshimu sheria, Uingizaji na uuzwaji Counterfeits bila woga, Kuporomoka kwa elimu, kutokulipa kodi, Kuongezeka kwa ujasiri wa kutenda uhalifu, Kuongezeka kwa uongo uongo etc. yalikuwa kwa kasi katika kipindi hiki.
Well najua kuna wengi watakuwa na maoni tofauti nadhani ni vema tujadili. Pia naomba nisieleweke kwamba hayo niliyoyataja hayakuwepo kabisa katika awamu ya kwanza. But it is the degree that do think should matter!
==========
SOMA ZAIDI:
==========
=> Mbowe alia na kuporomoka kwa Maadili! Soma - Kuyumba maadili chanzo cha gulio la kura - Mbowe
=> Maoni ya Mhe. Kigwangalla => Kuanguka kwa Nidhamu na Maadili Kutasababisha Kuanguka kwa Taifa!
ATHARI ZA KUPOROMOKA KWA MAADILI:
Lakini ni kipindi hiki hiki maneno kama "Dili" ikimaanisha biashara au shughuli ya kuingiza pesa chap chap (Whether legal or illegal) yalianza. Mengine pia kama Watu kutoheshimu amri za serikali, Misheni town, Uvamizi wa maeneo ya wazi, Waajiriwa hewa serikalini, Wizi mkubwa mkubwa wa mali ya umma, Kutoheshimu shule na proffesions, Kutoheshimu sheria, Uingizaji na uuzwaji Counterfeits bila woga, Kuporomoka kwa elimu, kutokulipa kodi, Kuongezeka kwa ujasiri wa kutenda uhalifu, Kuongezeka kwa uongo uongo etc. yalikuwa kwa kasi katika kipindi hiki.
Well najua kuna wengi watakuwa na maoni tofauti nadhani ni vema tujadili. Pia naomba nisieleweke kwamba hayo niliyoyataja hayakuwepo kabisa katika awamu ya kwanza. But it is the degree that do think should matter!
==========
SOMA ZAIDI:
==========
=> Mbowe alia na kuporomoka kwa Maadili! Soma - Kuyumba maadili chanzo cha gulio la kura - Mbowe
=> Maoni ya Mhe. Kigwangalla => Kuanguka kwa Nidhamu na Maadili Kutasababisha Kuanguka kwa Taifa!
ATHARI ZA KUPOROMOKA KWA MAADILI:
Maadili yatikisika ofisi nyeti nchini!
Raia Mwema - Mei 20, 2009
- Kuanzia Ikulu, Polisi hadi Magereza
- Vigogo wabweteka, sheria zavunjwa
HALI ya uadilifu miongoni mwa watendaji katika ofisi kubwa na nyeti za serikali kuanzia Ikulu, Ofisi ya Makamu wa Rais na hata katika vyombo vya ulinzi imetetereka, na hasa katika uzingatiaji wa matakwa ya kanuni na sheria za matumizi ya fedha.
Kuyumba kwa uadilifu katika ofisi hizo nyeti za serikali kumethibitishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, katika ripoti yake ya ukaguzi wa hesabu wa hadi Juni 30, mwaka jana.
Ikulu, ofisi ambayo ilipaswa kung'ara zaidi kimaadili mambo si swari ikibainika kuwa imekuwa ikifanya baadhi ya mambo shaghala baghala katika mipango yake ya ununuzi.
Doa hilo katika Ikulu linatajwa na CAG kuwa limetokana na ofisi hiyo nyeti kukiuka kifungu cha 45 kipengele &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];a' hadi &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];e' cha Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004.
Sheria hiyo iliyowahi kuwa gumzo katika mjadala wa kununua au kutonunua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans, inataka ununuzi ufanywe katika mpango mahsusi, unaokidhi mahitaji ya mwaka husika.
"Ofisi ya Rais &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; Ikulu haikuandaa mpango wa manunuzi na kufuata kama sheria inavyoelekeza," anaeleza CAG katika ripoti yake hiyo, ambayo pia iliwasilishwa katika Mkutano wa 15 wa Bunge, uliomalizika Aprili 30, mwaka huu.
Lakini si Ikulu pekee iliyobainika kukiuka sheria halali za nchi ambazo ofisi hiyo ilipaswa kuwa mfano katika kuziheshimu, bali hata Ofisi ya Makamu wa Rais.
Katika ofisi hiyo nyeti pia imebainika kuwa kulifanyika ununuzi wa samani kinyume cha matakwa ya sheria ya manunuzi.
"Manunuzi ya samani nje ya mpango wa manunuzi wa mwaka ya Sh 78,148,000 yalifanyika kwa kutumia njia ya moja kwa moja inayofaa kwa manunuzi madogo madogo, kinyume cha maelekezo ya kifungu namba 45 kipengele &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];a' na &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];d' cha Sheria ya Manunuzi ya Umma namba 21 ya mwaka 2004," anasema CAG.
Kuporomoka kwa maadili na kudharauliwa kwa sheria katika ofisi hiyo ya Makamu wa Rais pia kumebainishwa na CAG katika matumizi sahihi ya bajeti iliyotengwa.
Katika hilo, CAG anasema; "Malipo ya madeni ya Sh 89,244,290 yalifanyika kwenye bajeti ya mwaka huu ulioishia Juni 30, 2008, bila idhini. Risiti za kukiri malipo ya Sh. 8,920,000 hazikuwasilishwa kwa ukaguzi."
Mbali na hayo, CAG anasema kulikuwa na mali zenye thamani ya Sh. 191,124,623 ambazo hazikuingizwa kwenye rejesta ya mali za kudumu, hapa sababu za hali hiyo zikiwa hazijabainishwa japokuwa ni dhahiri kuwa kuna uzembe na utovu wa maadili.
Katika hatua nyingine, kwa mujibu wa ukaguzi wa hesabu na katika hali ya kuzua maswali mengi, imeelezwa kuwa madeni ya Sh 208,058,691 hayakukaguliwa kutokana na kukosekana nyaraka ambatanifu.
Hali hiyo inayotia shaka mustakabali wa Taifa kama itaachwa iendelee pia imeikumba Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali. Katika ofisi hii, inaelezwa kuwa mishahara ya jumla ya Sh 8,553,453.39 ililipwa kwa watu waliokwishaondoka katika utumishi wa umma.
Utata wa kimaadili katika ofisi nyeti za umma pia imevikumba vyombo vya dola ikiwa ni pamoja na Jeshi la Polisi na Magereza.
Katika idara ya polisi malipo ya Sh. 74,110,000 yalifanywa bila kuwapo nyaraka sahihi.
"Kufikia mwisho wa mwaka, Juni 30, 2008 kulikuwa na masurufu yasiyorejeshwa yanayofikia Sh 131,000,000. Huu ni ukiukaji wa kanuni namba 103 kifungu 1 ya kanuni za fedha za umma za mwaka 2001 (kama zilivyorekebishwa 2004)," anasema CAG na kufafanua kuwa;
"Kanuni hizo zinataka marejesho yafanyike mara baada ya mambo yaliyosababisha masurufu hayo kulipwa kukamilika au ifikapo siku ya mwisho ya mwaka ambao masurufu yalitolewa.
Jambo jingine la kutilia shaka ni kwamba taarifa za utendaji zinazoonyesha malengo mkakati, mafanikio yaliyotarajiwa na mafanikio halisi haikuwasilishwa kwa CAG pamoja na taarifa za fedha kinyume cha matakwa ya kifungu namba 8 kipengele cha 5 cha sheria ya fedha za umma namba 6 ya mwaka 2001.
Katika Idara hii ya Polisi kashfa kubwa zaidi iliyoibuka wakati wa ukaguzi wa CAG ni kufanya matumizi zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"Taarifa ya fedha ilionyesha huduma ambazo hazijalipwa za jumla ya Sh. 2,024,920,000. Hii ina maana ofisa masuuli alitumia kiasi hicho, zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge. Kama kiasi hiki kingelipwa na kuingizwa kwenye taarifa ya matumizi fungu hili lingekuwa na malipo ya ziada ya kiasi hicho hicho.
"Taarifa ya fedha inaonyesha kiasi cha madeni ya Sh. 23,354,120,000 na hali hii ni uthibitisho kuwapo matumizi zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa" anasema CAG.
Kwa upande wa Idara ya Huduma za Magereza, uongozi uliidhinisha matengenezo ya magari ya Sh. 205,404,964 bila kupitia kwa Wakala wa Ufundi na Umeme kinyume cha matakwa ya kanuni namba 59 (1) &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; (2) ya kanuni za umma za manunuzi za mwaka 2005.
Kwa sababu hiyo, ubora wa matengenezo yaliyofanyika na thamani iliyopatikana kutokana na matumizi hayo haikuweza kuthibitishwa kwa vile magari husika hayahakikiwa na ofisa au fundi aliyeidhinishwa.
"Malipo ya Sh 824,563,334 yalifanywa bila kuwapo nyaraka sahihi. Kiasi cha Sh 16,536,960 kililipwa kwa ofisa aliyeenda India kwa matibabu bila kuwapo rufaa iliyoidhinishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
"Manunuzi ya Sh. 119,875,376 yalifanywa kwa kutumia kinukua bei na bila ya kupitisha kwenye Bodi ya Manunuzi kinyume na kifungu namba 30 cha sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004," anaeleza CAG katika taarifa yake kuhusu ukaguzi wa hesabu za serikali kuu.