Tanzania Bara vs Kenya - Live

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
Dakika kumi zijazo mechi hiyo ya CECAFA (kati ya Tanzania na Kenya) itaanza kuchezwa uwanja wa Taifa wa zamani. Tutawaletea live show (via texts) hapa hapa.

Ahsante
 
Sasa hivi amemaliza kuhojiwa Mziray (huku akiwa amevaa t-shirt yake ya njano ya Kajumulo World Soka)
 
Kwa maelezo ya vipima joto; joto jijini Dar es Salaam limefikia sentigredi 34.
 
Timu zote sasa ziko kwenye uwanja tayari kukaguliwa. Kenya wakiwa na jezi zao nyeupe ambazo kwa namna moja ama nyingine naweza kuzifananisha na zile za Senegal. Uzi wa Stars ni ule ule tuliouzoea
 
Umemalizwa kupigwa wimbo wa taifa wa Kenya na sasa unaanza kupigwa wa Tanzania. Wachezaji wa Kenya wanaonekana kuwa na mori wa mchezo. Inashanghaza wa kwetu wamenuna; yawezekana ndiko kuikamia mechi yenyewe
 
Naam,

Wachezaji wamemaliza kusalimiana na sasa mambo ndiyo yanakaribia kuanza. Pitch ni nzuri sana (lakini ya uwanja wa zamani wa Taifa).

Hali ya hewa ni nzuri
 
Naam,

Kapteni wa Tanzania Henry Joseph anaonana na Mwamuzi. Na anaondoka na kuungana na wachezaji wenzake.
 
Dakika ya kwanza tu,

Tanzania wanakosa goli la wazi kwa 'pasi mbuzi' na huenda wakaikumbuka nafasi hii
 
Dak ya 6,

Nizar Khalfan anapiga nduki moja matata na anakosa shabaha. Mita chache juu ya mtambaa panya
 
Dakika ya 7, Kenya wanafanya shambulizi la kwanza lakini walikuwa offside.
 
Dakika ya 8

Tanzania inapata faulo kuelekeza katika kwenye lango la Kenya lakini kick imezuiwa na umekuwa mpira wa kurushwa
 
Erasto Nyoni anapiga tick tack kwenye lango la Kenya na kukosa.

Ochieng kwenye dakika ya 11 anaikosakosa Tanzania. Defense ya Tanzania inacheza kizembe bado
 
Wakenya wanaonekana kucheza mchezo mzuri na kuonana vema. Wanaonekana wameenda mbele kwa kiwango cha soka
 
Dakika ya 14

Tanzania inakosa tena goli la wazi kabisa. Maximo hata haamini kama mchezaji wake kashindwa kulenga golini. Danny Mrwanda huyo
 
Kenya wanaendelea kuonesha 'move' nzuri. Dakika ya 17 inakwenda.

Stars wanaonekana wazuri kwa mashambulizi
 
Vilabu vya Tanzania kwa kiwango cha soka kwenye ranks za Afrika Mashariki vinaonekana kuwa juu. Ajabu ni kuwa Taifa Stars ndiyo inalega lega kwenye ranks za Afrika Mashariki.

PENALTI!

Tanzania inapata Penalti!
 
GOOOOAAAAAAAL!

Nizar Khalfan anaipatia Tanzania bao la kwanza dakika ya 18 baada ya wachezaji wa Kenya kuunawa mkono.
 
Dakika ya 20 Kenya wanapata corner, inaondoshwa na defense ya Tanzania.
 
Kama nilivyosema Tanzania ni wazuri kwa ushambuliaji. Wasiwasi wangu ni defense yetu!
 
Back
Top Bottom