Tanzania Bara vs Kenya - Live

Hapo utapata kuangalia mechi mbalimbali duniani kama vile ligi za UK, Italy, Spain n.k.
 
Invisible,
tunashukuru kwa kukosha nyoyo kwa dakika hizi,kwani kama nilikuwa kwenye pitch vile,walau tumesahau machungu kwa muda.
 
duh safi sana,CCM CCM CMM CCM

CCM CCM Zilipendwa hizo au kaulimbiu hiyo imepitwa na Wakati. Sisiem ya Sasa ni ya Chukua chako mapema, chumba cha matajiri, chama cha maja...., chama cha Mafis... mengine watamalizia wengine.

Asante "Invisible" kwa kutuhabaribisha tulio mbali na Bongo, God Bless!!! I salute you
 
Nashaurii tuwe tunatoa draw na watani zetu, EAC isije ikafa hivi hivi bure!
 
tunawapongeza watanganyika kwa ushindi ila jina hili litaleta mgogoro jiiteni mount kilimanjaro kakakuona ila hili lenye herufi zetu tulitumie kwa taifa stars tu au hili pia mpaka tuliundie kamati?

hata hivyo tuiombee dua timu yetu ya zanzibar heroes au mapinduzi team ifanye vyema
 
Inshallah,

Tuombe uzima. Nitajitahidi kuileta mechi hiyo. Sintobagua wala kuchagua; ili mradi ni "watanzania" wanaocheza. Inafurahisha hii; timu ya taifa inaitwa Tanzania na ya Zanzibar inaitwa Zanzibar... Nadhani kuna makosa!

Ilibidi nyingine iitwe Tanganyika sio? LoL

Timu ya Tanzania Bara inaitwa Kilimanjaro Stars
 
Hivi ni kwa nini wachezaji wetu ni wafupi kuliko wa nchi zingine haswa W. Afrika? Na tufanyeje kurekejisha hali hii? Any suggestions?
 
Asante sana invisible kwa kutuletea habari

Mkuu usijali; labda kwa nyongeza tu...

DSC09935.JPG

Hawa ndio Harambee waliokuwepo leo na kukandamizwa kibara
 
DSC09933.JPG

Kikosi cha Stars kilichowabamiza Harambee Stars.

Nashukuru Dua kwa kunikumbusha kuwa hii ni Kilimanjaro Stars. Thanks mkuu
 
Ua.JPG

Utadhani ugomvi lakini hapa ni mwanzoni ambapo Danny Mrwanda aliumizwa. Huyu ndiye aliyewasumbua sana wakenya.

Shangilia.JPG

Hapa walikuwa wakishangilia bao nadhani lile la kwanza.

Mrwanda.JPG

Danny Mrwanda (Mkuki kwa wakenya) akiukokota mpira.

Maximo.JPG

Nili-ripoti kuwa Stars walikuwa wameonekana kuamsha mori nyakati za mwisho mwisho huku Maximo kiti kikiwa cha moto. Mambo yalikuwa hivi baada ya stars kupata bao la pili na la ushindi!

Danny.JPG

Danny Mrwanda akawa ametutoa kimasomaso
 
We kweli Robot. Natamani kukuona. Ntakuonaje? Njoo basi ofisini kwangu siku moja. Nawapongeza Kilimanjaro kwa kusimamisha Mwenge wa Uhuru.

Asha
 
Zawadi nzuri sana ya siku ya Uhuru...Pongezi kwa kikosi kizima....
 
Back
Top Bottom