Tanzania bara ndo nchi gani?

Kilalo

Member
Apr 29, 2013
65
12
Nimeuliza hivyo kwakuwa nakumbuka nilipokuwa nasoma na hata katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inatamka nchi iitwayo Tanganyika ndiyo iliyoungana na Zanzibar kuwa Tanzania.
Sasa hii Tanzania bara tunaitoa wapi? Nauliza hivi kwakuwa hata wasomi wetu nao utawasikia wakisema Tanzania bara na hata rais wetu Kikwete leo kwenye maadhimisho katamka hivyohivyo. Sasa hamuoni historia na uhalisia tu kuwa mnaviharibu?

Baraza la mitihani (NECTA) mfano likatunga swali lisemalo; Jaza sehemu iliyoachwa wazi kwenye sentensi hii- 9/12/1961 ni siku ya uhuru wa nchi ya_________( Akajaza Tanzania Bara) atakuwa kapata ama kakosea? Vinginevyo mnatuchanganya na kuchanganya watoto wetu.
Mnamdanganya na kumfariji nani kwa kutaja Tanzania bara badala ya Tanganyika?
 
swali gumu. subiri majibu rahisi. hata vyombo vya habari vinataja jina hilohilo utadhani wamiliki wamepewa vimemo na magamba.
 
Linchi kwa maigizo hili sijapata kuona! Labda wanataka kuanzisha nchi mpya kumpiku South Sudan.
 
Unadhani kwa nini bongo wanafeli?
Maswali yao yana utata sana, Hapo mtu akijibu Tanzania bara mpe tu
Nakumbuka lilikuja swali mock miaka hiyo
"Describe the problems associated with road accidents in Tz"
asilimia zaidi ya 80 wakajibu -poor road outlook, - carelessness of drivers ... etc
asilimia kama iliyobaki wakajibu - death - destruction to infrastructure etc...
Hapa hata mwenye marking scheme alikua kachemka... bongo bongo
 
Nimeuliza hivyo kwakuwa nakumbuka nilipokuwa nasoma na hata katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inatamka nchi iitwayo Tanganyika ndiyo iliyoungana na Zanzibar kuwa Tanzania.
Sasa hii Tanzania bara tunaitoa wapi? Nauliza hivi kwakuwa hata wasomi wetu nao utawasikia wakisema Tanzania bara na hata rais wetu Kikwete leo kwenye maadhimisho katamka hivyohivyo. Sasa hamuoni historia na uhalisia tu kuwa mnaviharibu?

Baraza la mitihani (NECTA) mfano likatunga swali lisemalo; Jaza sehemu iliyoachwa wazi kwenye sentensi hii- 9/12/1961 ni siku ya uhuru wa nchi ya_________( Akajaza Tanzania Bara) atakuwa kapata ama kakosea? Vinginevyo mnatuchanganya na kuchanganya watoto wetu.
Mnamdanganya na kumfariji nani kwa kutaja Tanzania bara badala ya Tanganyika?
Utakuwa bado una matongotongo usoni. Kanawe kwanza ndipo utajua maana ya Tanzania Bara
 
Madhali nimesikia matamshi mengi ya kimakosa,mfano Mkoa wa Bukoba badala ya Kagera,ama dhana kwamba Moshi ina jina kubwa kuliko mkoa wa Kilimanjaro sishangai hili...Matejoo wa Ngarenaro nao wanakwambia Ngarenaro ni kubwa kuliko Arusha!
 
hata me nashangaa kwakuwa hakuna nchi yoyote duniani iliyowahi kupata uhuru 9 december 1961 na ikaitwa Tanzania bara
 
Nimeuliza hivyo kwakuwa nakumbuka nilipokuwa nasoma na hata katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inatamka nchi iitwayo Tanganyika ndiyo iliyoungana na Zanzibar kuwa Tanzania.
Sasa hii Tanzania bara tunaitoa wapi? Nauliza hivi kwakuwa hata wasomi wetu nao utawasikia wakisema Tanzania bara na hata rais wetu Kikwete leo kwenye maadhimisho katamka hivyohivyo. Sasa hamuoni historia na uhalisia tu kuwa mnaviharibu?

Baraza la mitihani (NECTA) mfano likatunga swali lisemalo; Jaza sehemu iliyoachwa wazi kwenye sentensi hii- 9/12/1961 ni siku ya uhuru wa nchi ya_________( Akajaza Tanzania Bara) atakuwa kapata ama kakosea? Vinginevyo mnatuchanganya na kuchanganya watoto wetu.
Mnamdanganya na kumfariji nani kwa kutaja Tanzania bara badala ya Tanganyika?
kinachowafanya washindwe kutamka Tanganyika ni kule kuona kwamba Watanganyika halisi ni watu wa kigoma lililoko ziwa Tanganyika
 
Mkuu, hivi Zanzibar ni kitu gani? Maana mie najua kuna Unguja na Pemba. Hili la Zenji limetoka wapi?


Kwani COMORO imetokea wapi wakati ni kuna visiwa tu vy a Ngazija,Anjuan na mayote? Kama unafuatilia nchi nyingi duniani ambazo ni visiwa hautashangaa hili la zanzibar.Ni hivyo hivyo kwa visiwa vya Cape verde and many other Archipelagos all over the world.
 
Hakuna nchi katika historia ya dunia iliyopata uhuru inayoitwa Tanzania bara. Kwanza wanaposema bara wana maana gani? Mafia na ukerewe zitakuwa Tanzania bara au visiwani?
 
Unadhani kwa nini bongo wanafeli?
Maswali yao yana utata sana, Hapo mtu akijibu Tanzania bara mpe tu
Nakumbuka lilikuja swali mock miaka hiyo
"Describe the problems associated with road accidents in Tz"
asilimia zaidi ya 80 wakajibu -poor road outlook, - carelessness of drivers ... etc
asilimia kama iliyobaki wakajibu - death - destruction to infrastructure etc...
Hapa hata mwenye marking scheme alikua kachemka... bongo bongo

Hapo ni sawa tu kumpa marks km ni Mwl mwenye uerevu kwani kiakili huyo Mwanafunzi yupo sahihi

Ni sawa na kujibu Issa na Yesu ndio sawa na Tanganyika na Tanzania bara
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom