Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,227
- 113,583
Nimeanza kuona na kusikia vijimaneno maneno hususan humu kwenye mitandao kwamba sasa Tanzania siyo nchi ya amani.
Mimi sikubaliani kabisa na hiyo dhana. Nakataa kabisa. Tanzania bado ni nchi ya amani.
Matokeo machache ya watu kupoteza maisha yao au kushambuliwa kwa risasi hakuifanyi nchi kwa ujumla wake isiwe na amani.
Wote wanaodai kuwa Tanzania siyo nchi ya amani sijui wao wanaishi dunia gani maana nchi zisizo na amani zipo tele tu.
Huko kwenye hizo nchi watu hufa kwa mafungu mafungu. Unakuta watu 200 wanauliwa kwa kulipuliwa na mabomu kanisani au msikitini, mara usikie watoto 100 wa shule za chekechea wameuliwa kwa mpigo, mara sijui bomu limelipuka katikati ya mji wa Baghdad na kuua watu 90 papo hapo, na kadhalika, na kadhalika.
Sasa ni lini hapa kwetu mmewahi kusikia mambo kama hayo?
Nani kati yenu ana wasiwasi na usalama wa mwanae kesho hapo shuleni kwao?
Nani kati yenu ana hofu ya kwenda msikitini Ijumaa akiogopa usalama wake? Nani hatokwenda kanisani ifikapo Jumapili kisa tu anahofu na hali ya usalama?
Nani hatoenda sokoni kwa kuhofia huenda akauliwa akiwapo huko?
Nani kaahirisha mipango yake ya kwenda baa au sehemu zingine za starehe kisa amani hakuna?
Hata kwenye nchi zenye amani watu hufa. Na hufa kwa sababu mbalimbali.
Hata kwenye nchi zenye amani matendo maovu huwepo. Na ndo maana kunakuwepo na vyombo vya ulinzi na usalama.
Popote pale penye binadamu uovu nao huwepo.
Lakini yote hayo hayaifanyi nchi kwa ujumla wake isiwe nchi yenye amani.
Kama mnadhani Tanzania sasa amani hakuna basi hamieni Damascus huko. Au nendeni Kabul au Kandahar huko. Nendeni Lahore huko. Kama vipi mnaweza hata kwenda Somalia tu hapo kama huko kwingine mtapaona ni mbali.
Nendeni huko mkaishi kwa amani. Naamini mtakuwa salama zaidi huko kwani Tanzania sasa haina amani tena!
Mimi sikubaliani kabisa na hiyo dhana. Nakataa kabisa. Tanzania bado ni nchi ya amani.
Matokeo machache ya watu kupoteza maisha yao au kushambuliwa kwa risasi hakuifanyi nchi kwa ujumla wake isiwe na amani.
Wote wanaodai kuwa Tanzania siyo nchi ya amani sijui wao wanaishi dunia gani maana nchi zisizo na amani zipo tele tu.
Huko kwenye hizo nchi watu hufa kwa mafungu mafungu. Unakuta watu 200 wanauliwa kwa kulipuliwa na mabomu kanisani au msikitini, mara usikie watoto 100 wa shule za chekechea wameuliwa kwa mpigo, mara sijui bomu limelipuka katikati ya mji wa Baghdad na kuua watu 90 papo hapo, na kadhalika, na kadhalika.
Sasa ni lini hapa kwetu mmewahi kusikia mambo kama hayo?
Nani kati yenu ana wasiwasi na usalama wa mwanae kesho hapo shuleni kwao?
Nani kati yenu ana hofu ya kwenda msikitini Ijumaa akiogopa usalama wake? Nani hatokwenda kanisani ifikapo Jumapili kisa tu anahofu na hali ya usalama?
Nani hatoenda sokoni kwa kuhofia huenda akauliwa akiwapo huko?
Nani kaahirisha mipango yake ya kwenda baa au sehemu zingine za starehe kisa amani hakuna?
Hata kwenye nchi zenye amani watu hufa. Na hufa kwa sababu mbalimbali.
Hata kwenye nchi zenye amani matendo maovu huwepo. Na ndo maana kunakuwepo na vyombo vya ulinzi na usalama.
Popote pale penye binadamu uovu nao huwepo.
Lakini yote hayo hayaifanyi nchi kwa ujumla wake isiwe nchi yenye amani.
Kama mnadhani Tanzania sasa amani hakuna basi hamieni Damascus huko. Au nendeni Kabul au Kandahar huko. Nendeni Lahore huko. Kama vipi mnaweza hata kwenda Somalia tu hapo kama huko kwingine mtapaona ni mbali.
Nendeni huko mkaishi kwa amani. Naamini mtakuwa salama zaidi huko kwani Tanzania sasa haina amani tena!