Tanzania awards $500 mln oil supply deal to Swiss firm Augusta; GVT hope will lower prices...

Nipe muda ntakupa actual prices...mid of next week. Ila, Kwani Augusta alinunua wapi mafuta yale ya January? Halafu si kweli kwamba Addax ilununua magazeti. Kwani nani asiyejua jinsi tunavyoyapeleka mambo TZ. Anayesema ukweli ndo anaambiwa mzushi na muongo ili mradi watu walinde maslahi yao!
Na kaka naamini sote tuna nia njema na Tanzania. Augusta kwani ni ya nani? Sio yule muitaliano aliyekuwa AGIP au Tiper hapa hapa Tanzania anayewakilishwa na ex Addax(Mgoa)?
Halafu standard zetu za kukataa tender ni namna ya kufunga tender document kwenye bahasha???? Well, time will prove us right or wrong. What I suspect ni kuwa hatujui tunachofanya. Tuendelee kushupaa na kujenga haya makampuni makubwa ya nje. Tutakaojililia ni sisi maana hela za kwetu na uwezo wa kujenga kampuni zikawa kubwa pia tunao.Tunaposhindwa ni tamaa zetu na njaa ndogo ndogo tu, however clean we try to convince people that we are.

Mkuu duh, umejuaje kama mimi ni kaka?

Sijui hasa Augusta inamilikiwa na nani. Ila ukiangalia ina anuani ya Swiss, japo unayemtaja anaweza kuwa mwakilishi au shareholder. Sijui alinunua wapi mkuu yale mafuta. Ila ni kweli kuna malalamiko yanachunguzwa, dizaini jamaa kama wanachakachua na ethanol. Next week labda watatoa matokeo ya sampuli zinazopimwa. Ila iliendeshwa kampeni kubwa sana na magazeti mkuu, najua unaifahamu.

Kuonyesha kuwa walikuwa wanafitini, sources za malalamiko zilikuwa zinajificha...na magazeti zaidi ya sita yaliandika stori inayofanana kila kitu. najua uliziona zile mkuu. Unajua ile ni business worth over $100 million a month wakati walipokuwa wanajiagizia wenyewe, sishangai wanatoana macho.

Kuhusu criteria, hayo ni masharti ya tender nyingi tu, na unaweza kuangalia hata kwenye other sources. Ubaya wa tender mkuu, ni kuwa ukikosea masharti hata kiduchu halafu ukapewa tu, upo uwezekano wa wenzako kwenda kublock ushindi mahakamani, na process nzima ikasimamishwa. lazima tukumbuke hilo pia.

La mwisho, cha maana makampuni yalichoomba ni kufungua second window ya prequalification criteria, ambayo itawawezesha hata wenye mitaji midogo hasa wa ndani kushiriki. Kwa sasa requirement ya kuingiza mzigo wa kutosha miezi miwili inawatoa jasho kwa kuwa ni pesa nyingi. Serikali imeanza process ya kulifanya hilo liwezekane soon. Hii ina maana washiriki wa zabuni watakuwa wengi zaidi na premiums zitazidi kushuka na hata pengine kuifikia za Mozambique ($25).
 
All in all, tulichotegemea ni mafuta kushuka. Ila toka haya mambo ya bulk procurement yameanza, bei ya mafuta inapaa! Kuna faida gani? Ni afadhali kila kampuni ya mafuta iagize inavyoona inafaa. Kazi ya serikali iwe kudhibiti ubora.



Ndugu Njaare,

pendekezo langu ni kuomba tuupe utaratibu huu mpya muda fulani tuone wakati utatufundisha nini. Hali iliyokuwapo kabla ya utaratibu huu kuanza ilitufundisha kuwa wauza mafuta walikuwa wanakula njama kudai mafuta hakuna, wakati mwingine wakitaja bei za manunuzi kubwa kuliko matazamio. Na ilikuwa vigumu kuwabishia kwa kuwa kila mtu alichagua ananunua lini na kwa bei ipi. Kwa hiyo ilikwa vigumu sana kupata ushike wapi katika kulalamikia bei zao na upatikanaji wa mafuta. Hebu tuwape muda--tutazamie tuone litazuka lipi.
 
Ndahani, lakini kwani mfumo huu wa tenda unakuwaje hasa na nini mapungufu yake? Maana wengi hawaongelei hili, wanakimbilia tu kusema kuna rushwa, unahisi hivyo wewe pia? Mbona unasema Augusta inawakilishwa na Mgoa wa Addax wakati yule ni mzungu pure na alijitetea mbele ya kamati ya makamba kwamba yeye hakufitini kwenye magazeti, na akaapa kwamba hana kinyongo na ushindi wa Augusta, na kwamba atashiriki hata zabuni ya tatu?
 
Mimi nawaaga kwenye hili! Nice topic lakini nasikitika kuona kila siku Tanzania kuna watu wanafikiria watajifaidisha vipi kibinafsi badala ya kujali maisha ya watu wote. Kitu kimoja ambacho Watanzania wengi hawajui ni kwamba nchi ikiendelea na ikawa na uwazi kila mtu anafaidika tena sana hatuna sababu ya msingi ya watu kula pesa ya wananchi maskini kwa tender za kijinga kijinga tu na ku take advantage ya Watanzania masikini. Mfano mzuri wa mafanikio ni Brazil walikuja kuelewa kila mtu ana loose hata wachache wala rushwa walikuwa wana loose maana hawana hospitali za maana, barabara n.k lakini sasa Brazil kila mtu ana win. Kama biashara za mafuta na umeme zinafanywa na serikali badala ya kampuni binafsi sithani kama tutaendelea kwani serikali watu wanakuja na kuondoka hivyo hawaoni sababu ya kutokuiba au ku sign mikataba mibovu. Mungu katusaidia wengine hapa hatujawahi kuchukua rushwa hata siku moja toka tuzaliwe na tunafanikiwa kwenye nchi za ugenini wakati tuna kila kitu Tanzania lakini viongozi wacheche ndiyo wanataka kuwa wafanyabishara na kutuma wapambe kudanganya watu kuhusu manufaa ya vitu wanavyofanya ili tu waweze kula zaidi. Nasikika sana kwa nchi yangu Tanzania.
Najua kunawanaosema sisomi wala sielewi lakini nasoma na naelewa nia za watu hapa vizuri sana maana sina cha kufaidia kwenye deal yeyote.
 
Kamundu, at least sasa naanza kukuelewa. Una majibu ya jumla kwenye specific problem. Lawama zako basi ni kwenye mfumo ambao nchi ilichukua kujiondoa kwenye biashara karibu 20 years ago. Remedy yake siyo kulalamika sasa kwa nini hakiwi vile au hivi. Tulikosea wakati ule. Ni kweli hatukupaswa kuiachia private sector kila kitu...we did wrong.

Lakini suala la wewe kutotoa rushwa huko ugenini, hili ni thread nyingine kabisa inayotakiwa kujadiliwa kwa mapana, kwa sababu ni la kimfumo zaidi. Huhitaji kutoa rushwa kwa askari Japan ili akuachie ume overspeed kwa sababu mfumo ndiyo utakao deal na wewe wala si individuals. Na wala hutakuwa na muda wa kumpigia simu IGP kumweleza "vijana wako wananikamata bwana inakuwaje?"

Lakini mfumo wetu ni mbaya na unakulazimisha u compromise baadhi ya mambo wakati fulani, upende usipende. Matatizo mengi ya nchi zetu hizi ni ya msingi mbaya, ambapo kurekebisha inahitahi kuweka misingi mipya na wala si juu juu tu. Viongozi wetu hawataki kusikia haya kwa sababu wanaona ni kazi ngumu na wao wanapenda nyepesi.

Ni vema kuelezea nia yako "njema" kwenye nchi hii, lakini si vema hata kidogo kupoint eti wengine "wana nia mbaya" na nchi hii. Conclusion za namna hii ni dalili za kukosa uvumilivu wa kusikilizana...dialogues kwenye social media kama hii ni kusikilizana kwa tuo.
 
Nakubaliana na mawazo haya ndugu Mbalamwezi. Mimi ni Mtanzania ninayeyafahamau na kuyapigania mema ya soko huria, lakini soko huria si jibu la kila tatizo la kiuchumi.

Wamarekani ambao ndio wengi huwatumia kama mfano wa uchumi uliofanikiwa kwa kutumia mfumo wa soko huria, bado walifika mahali wakakubali kosa la kufungua milango nchi ikawa shamba la bibi. Zikatungwa anti-trust laws kubana mapungufu mengi ya soko huria kwa sababu mwanadamu ukimwachia huru sana hulka ya unyama itajitokeza tu. Kuna biashara bado zinashikiliwa na serikali kule marekani. Labda hapa niitaje biashara ya kusafirisha vifurushi kwa shirika la US Postage. Watu binafsi wanafanya biashara hii. lakini kwa kushindana na serikali. Uingereza kuna biasahara bado zinaendeshwa na serikali.

Pamoja na damu yangu ya kupenda ubepari, bado naona mkono wa serikali uwepo katika biashara mbalimbali nyeti nchini, sema tu pafanyike jitihada kubwa sana ya kufumua kabisa mfumo wa utawala ili kuweka watu wenye mawazo yanayovuka mipaka ya matumbo yao, ili biashara zinazobakia katika mikono ya serikali ziwe efficient--na hapa sijui kiswahili cha efficient ni nini. Nadhani ndo mnaita tija!


Kamundu, at least sasa naanza kukuelewa. Una majibu ya jumla kwenye specific problem. Lawama zako basi ni kwenye mfumo ambao nchi ilichukua kujiondoa kwenye biashara karibu 20 years ago. Remedy yake siyo kulalamika sasa kwa nini hakiwi vile au hivi. Tulikosea wakati ule. Ni kweli hatukupaswa kuiachia private sector kila kitu...we did wrong.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Ni kweli AK 48, lakini nini kiwe kiini cha mabadiliko haya ya kimfumo tunayohitaji? Ni kwa kila mtu kujituma kutimiza wajibu wake. watu wetu wengi huwa hawapendi kushiriki kwenye michakato mbali mbali yenye mustakabali wa taifa hili. Mathalan, achilia mbali chaguzi, lakini hata tunapotakiwa kutoa maoni juu ya mambo nyeti, wengi wetu huona huo ni wajibu wa wengine...wengine akina nani? Tatizo letu pia limekuwa kuacha kujifunza mambo ya msingi ili kupata uzoefu wa kutatua matatizo yetu wenyewe. Hata thread nyingi humu jamvini zinazohitaji kufikiria sana au ku reasearch, huoni kama zina wachangiaji wengi...wengi wetu tunachangia kwenye mambo rahisi rahisi, ya kuropoka ropoka. Aina hii ya society haiwezi kuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo yake yenyewe, kwa hiyo wachache wanaweza kuamua kwa niaba ya wengi lakini kwa maslahi yao wachache...then, baada ya madhara kuanza kujitokeza kwa wengi, sasa ndo utasikia malalamiko kila kona...nina imani sijamuudhi yoyote kwa maoni yangu haya, Ndugu AK48.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
DSN, tuwe fair. mfumo unaouongelea ulianza kubuniwa 2008. Kwa hiyo, utakuwa husemi ukweli kuuhusisha na mgomo wa juzi. Research kwanza before you speak.
Inaonekana ni Insider wa EWURA how dare unakataa kuwa hii style ya ununuaji wa BULK haikuanza baada ya shaortage,wakati Masebu kajijitetea sana live ITV na TBC mpaka vijana wake wameenda kwenye Pima joto.Ebu acha utetezi usio na mashiko mkuu wala haikuitaji m Reserch tumewasikia sana wakisisitiza mpaka jinsi upakuaji wa meli moja moja unavyoleta matatizo kwenye dock yetu,nawasikia kwa maelezo yao tena jana mmoja mwakilishi wa waagizaji anaelezea wanavyopta shida kwenye upakuzi kwamba kuna msululu wa meli kusubilia upakuaji kwenye dock.Mkuu unaonekana umebezi kwenye research za makalatasi na sio reality ya maisha tuunayoishi amabayo mimi nategemea mafuta sana katika almost ninachofanya kila siku.

Kubuni ni jambo jingine utekelezaji ni jambo jingine,uoni hata aibu mkuu kusema imebuniwa mwaka 2008 utekelezaji 2012 four years doing nothing mpaka inatokea crisis inayumbisha uchumi wa Nchi na ustawi wa maisha ya mtanzania, nawe unaibuka utetezi usio na tone la aibu eti tufanye Research,tufanye hivi kuna Reseach zaidi ya reality ya watu waliopigika na maisha nchi nzima kwa ukosefu wa mafuta kulikopelekea gharama za maisha kupanda na mpaka leo hazijashuka sehemu yoyote.Huo ubunifu umeleta nafuu gani,hakika ningekuwa kikwete nikikupa UMD wa taasisis nikasikia crisis upande wako nakupa ultimatum uje na jibu positive ndani ya miezi sita nje ya hapo una kazi.

Ebu mkuu fanya utetezi usio na ujima,manake wewe kuilewa sekta ya mafuta basi hata sie watanzania wa kawaida hatuna ufahamu japo kidogo wa kuona hii ni reality.Ama kweli umewaibisha Masebu na Team zake za EWURA,na wasomi wwote wa Gas and Fuel Economic Management EWURA,inawachukua miaka minne kubuni kitu ambacho kinaweza kuchukua miezi sita na utekelezaji ukaanza ndani ya miezi hiyo sita...........shame!!!!Tena gradute kabisa ahhhhhhhhh!!!

Mkuu Mkandara,

naona unachanganya vitu vingi sana kwenye hii topic.

1. Tunajadili ufanisi wa Bulk Procurement.
2. Unalaumu serikali kununua mafuta nje ya nchi.
3. Unalaumu kwa nini serikali inanunua mafuta kwa kisai chote hicho cha fedha huku ikiwa haiuzi kitu nje.
4. Umependekeza Rais angeingia mkataba na nchi zenye mafuta.
5. Unaongelea Hisa...
Mwingine anaongelea madini

Nadhani tungerejea kwenye point kwamba, uendeshaji wa uchumi hutegemea mafuta. Kwa muda mrefu sana, (toka 1999 soko huria la mafuta lilipoanza rasmi) wauza mafuta wamekuwa wakinunua kwa mfumo ambao baadaye wachumi wameona ni inefficient.

Ninakubaliana nawe kuwa we import too much. Toka ndege hadi toothpick. lakini je, wewe unashtuka ku import mafuta leo? tumekuwa tunaagiza mafuta toka nchi hii ipate uhuru. So, kwa kuanzia, kuagiza mafuta ni jambo ambalo kwa sasa hatuwezi kulibishania, maana inabidi iwe hivyo hadi tutakapothibitisha yapo ardhini na tunaweza kuyachimba.

la muhimu, ni kuongeza export kwa, pamoja na mambo mengine, kuprocess mazao ya biashara yatukomboe, hasa kwa kuwa watu wengi wanategemea kilimo na hii inaweza kusaidia kuupunguza umasikini. Mikataba mizuri ya madini ni lazima ili tunufaike pakubwa.

Lingine, ni kuongeza uzalishaji wa gesi asilia tufulie umeme ili tuweze ku export kujaribu kupunguza trade deficit.

Kuuliza kwa nini tunaendelea kununua mafuta (eti kwa kuwa tu Marekani kapiga marufuku kununua mafuta ya Iran) ni nje ya topic na pia ni utumwa wa kifikra.
Anajalibu kuona tumefikaje hapo ndio maana akaona tumekaa kama wachuuzi je,kwa style uchumi wetu kimapato na manunuzi yetu tunaposhirikiana na mataifa mengine.Kwa picha yke hiyo hata nami nikasupport hivi kuna faida gani ya kuwa na soko huria wakati kila siku linakupa headache na kuzidisha umasikini wa watu wako kuendesha nchi yako why all that?
 
DSN, mkuu unatumia nguvu nyingi sana kunidhibiti nisikueleze ukweli. Wewe unaongelea hisia, ndo maana nimekwambia fanya hata simple research. Hupendi kuambiwa ufanye research? Mimi siyo mwanasiasa bwana, na huchangia kile tu ninachokifahamu kwa lengo la kuelimishana. Soma mtandao ukuze ufahamu wako. Hii kelele ya Bulk procurement nimeisikia miaka hiyo, na kwa sababu mimi pia shughuli zangu zinategemea mafuta, nimejenga interest...si wewe tu unayetegemea mafuta mkuu.

1. It was very clear kwamba nimehint tu kwamba unasema bulk procurement imeanza juzi wakati wa mgomo wa wauza mafuta. Nimekuelimisha/kukukumbusha kwamba nimeanza kuisikia toka 2008. Hata hivyo, ukweli niliouona mtandaoni ni kuwa umebuniwa 2007. Sasa kwa nini umechelewa ni jambo lingine.

Uongo wangu uko wapi? hebu soma hii link:

http://www.ewura.com/pdf/keynotespeech/DG's SPEECH ON BULK PROCUREMENT REPORT Report.pdf
 
DSN, tuwe fair. mfumo unaouongelea ulianza kubuniwa 2008. Kwa hiyo, utakuwa husemi ukweli kuuhusisha na mgomo wa juzi. Research kwanza before you speak.

Mkuu Mkandara,

naona unachanganya vitu vingi sana kwenye hii topic.

1. Tunajadili ufanisi wa Bulk Procurement.
2. Unalaumu serikali kununua mafuta nje ya nchi.
3. Unalaumu kwa nini serikali inanunua mafuta kwa kisai chote hicho cha fedha huku ikiwa haiuzi kitu nje.
4. Umependekeza Rais angeingia mkataba na nchi zenye mafuta.
5. Unaongelea Hisa...
Mwingine anaongelea madini

Nadhani tungerejea kwenye point kwamba, uendeshaji wa uchumi hutegemea mafuta. Kwa muda mrefu sana, (toka 1999 soko huria la mafuta lilipoanza rasmi) wauza mafuta wamekuwa wakinunua kwa mfumo ambao baadaye wachumi wameona ni inefficient.

Ninakubaliana nawe kuwa we import too much. Toka ndege hadi toothpick. lakini je, wewe unashtuka ku import mafuta leo? tumekuwa tunaagiza mafuta toka nchi hii ipate uhuru. So, kwa kuanzia, kuagiza mafuta ni jambo ambalo kwa sasa hatuwezi kulibishania, maana inabidi iwe hivyo hadi tutakapothibitisha yapo ardhini na tunaweza kuyachimba.

la muhimu, ni kuongeza export kwa, pamoja na mambo mengine, kuprocess mazao ya biashara yatukomboe, hasa kwa kuwa watu wengi wanategemea kilimo na hii inaweza kusaidia kuupunguza umasikini. Mikataba mizuri ya madini ni lazima ili tunufaike pakubwa.

Lingine, ni kuongeza uzalishaji wa gesi asilia tufulie umeme ili tuweze ku export kujaribu kupunguza trade deficit.

Kuuliza kwa nini tunaendelea kununua mafuta (eti kwa kuwa tu Marekani kapiga marufuku kununua mafuta ya Iran) ni nje ya topic na pia ni utumwa wa kifikra.
Mkuu wangu uanchagnaya vitu sana tu.. Sijazungumzia swala la kuagiza mafuta kwa jinsi ulivyolizungumzia. Kwanza kabisa trade deficit haihusiani na sisi kuzalisha toothpick au lini tumeanza kuagiza mafuta au sijui mikataba ya madini hivi na vile..Vyote havihusiani na kile nachokizungumzia hapa kuhusu hizi Tender..Uwezo wetu kuzalisha toothpick au dawa ya mswaki kulingana na mahitajoi yetu ni kitu tofauti kabisa maana mafuta hatuwezi kuzalisha ila nachosema tunatakiwa kufanya mabadilishano na nchi tunayotaka kununua mafuta hayo sio kutoa Tender kwa wafanyabiashara ati ndio Ubepari..

Unazunguka sana mkuu wangu ktk vitu ambavyo havihusiani na nachokisema mimi. Binafsi yangu nimekuja ktk mada hii na kupinga mfumo unaotumika iwe toka mwaka 2008 au jana haufai kiuchumi kutoa tender kwa shirika bnafsi ambalo hatuna mabadilishano ya kibiashara isipokuwa kwa hardcash hii tunawajenga wao na kuelekea ktk deficit.. na wewe ukajibu kwa kunipinga kwamba ndivyo inatakiwa kutolewa tender ni mashirika binafsi yaliyoamua sio swala la serikali..Nikajieleza zaidi na zaidi lakini bado hujanielewa..

Nachozungumzia ni mtindo wa kutoa Tender ktk biashara inayogusa uchumi wetu mahala ambapo nchi nyingine hutazama mabadilishano kwanza tupate kuuza pia mali zetu nje na sio kwenda gengeni..Utandawazi unahusu nchi kutrade rasilimali zake na sio Cash money. Wewe unachokisema ni ni njia gani bora zitumike kukidhi mahitaji ya ndani kama mafuta (supply and distribution). Hivyo hata kama tungeingia Mkataba na Saudia au UAE kutuuzia mafuta in bulk through EWURA, nasi tukawauzia spicies, nyama na Korosho bado haitapoteza maana yako ila itatupa wananchi nasi soko la moja kwa moja kwa mali zetu hivyo kusukuma nguvu ya uzalishaji wa vitu hivyo. Hii ndio kazi ya Ikulu, wanaposisitiza wananchi what we can do for the country ni kwa sababu serikali imeandaa mazingira ambayo wananchi wake wanaweza kuzalisha na sio serikali ina andaa jinsi ya kuwa feed wananchi wake.

Kifupi unachokitazama wewe ni sawa na mama wa Kiafrika (serikali) ambaye ndiye anatazama malezi na makuzi ya watoto - watakula nini, watavaa nini na watalala wapi hivyo tunatafuta msheta kwa tender, nchi za magharibi mchati wa leo ndio watuletee fedha za matumizi au watupe grocery coupons za kufanyia shopping magunia la mchele, mafuta na kadhalika. Sivyo, mkuu wangu uchumi hauendeshwi hivyo.. Serikali ni mzazi na kazi yake kubwa ni kuandaa mazingira ambayo sisi rasilimali watu tuna andiliwa kwa maisha ya kesho, maisha ya ushindani na kuzalisha maana ubora wa maisha unatokana na kile unachoweza kuuza wewe sio uwezo wa kununua kwanza. Serikali sio tu inatuandaa bali pia inatuandalia masoko ya kuuza mali zetu ndivyo nguvu yetu ya kuzalisha inavyokuwa motivated maana soko lipo. Hivi unaposikia Marekani inadaiwa na China Trilioni 3 unafikiri deni hilo limetokanaje?...Yaani hata sijui nikwambie vipi upate kunielewa..
 
Tunachozungumzia ni mtindo wa kutoa Tender ktk biashara inayogusa uchumi wetu mahala ambapo nchi nyingine hutazama mabadilishano upate kuuza pia mali zetu nje..Wewe unachokisema ni ni njia gani bora zitumike kukidhi mahitaji ya ndani..Hivyo hata kama tungeingia Mkataba na Saudia au UAE kutuuzia mafuta in bulk nasi tukawauzia spicies, nyama na Korosho inatupa soko la mojakwa moja kwa mali zetu hivyo kusukuma nguvu ya uzalishaji wa vitu hivyo...[/QUOTE]

Mkandara, ninakuelewa sana. Tatizo ni:

Hatuna exports za maana kama unavyorecommend hapo juu. Vyote hivi tumebinafisha. Sasa hivi JK anagombana na wanunuzi wa Korosho kusini huko....Nyama tunashindwa kuuza nje hata ikiwa ni kweli kuwa Tz ni ya 3 kwa kuwa na mifugo mingi Afrika, tunashindwa hata na Botswana yenye mifugo michache mno. Hivyo wazo la kuingia mikataba na wauza mafuta kama Saudis, sisi tungewapa nini wakati kila kitu kiko in shambles...mfano kahawa, chai, pamba (wanapewa mbegu feki), nyama (Tanganyika Packers iko wapi?) exports zetu kwa sasa zinaporomoka kila siku, na demand for import iko juu kila siku. Hii ina maana tulikosea miaka mingi tuliporekebisha uchumi kwa kuruhusu private sector bila uangalifu.

Ninapotoa mfano wa exports versus imports (hata toothpick) lazima ikustue akilini kwamba tuna import too much na kutumia dola za ngama tulizonazo kwa mambo ya kipuuzi, na hivyo kuidhoofisha zaidi shilingi, elewa hivyo.
.
Ninajua sana umuhimu wa kuwa na balanced trade na ndiyo maana hata majadiliano ya Economic Partnership Agreement (EPA) baina ya EU na nchi za ACP tunaona utakuwa mzigo mwingine na tunaionya sana serikali isikubali kwa sababu tutashindwa kulitumia vema soko ilhali wao watakuja
 
Mkandara, ninakuelewa sana. Tatizo ni:

Hatuna exports za maana kama unavyorecommend hapo juu. Vyote hivi tumebinafisha. Sasa hivi JK anagombana na wanunuzi wa Korosho kusini huko....Nyama tunashindwa kuuza nje hata ikiwa ni kweli kuwa Tz ni ya 3 kwa kuwa na mifugo mingi Afrika, tunashindwa hata na Botswana yenye mifugo michache mno. Hivyo wazo la kuingia mikataba na wauza mafuta kama Saudis, sisi tungewapa nini wakati kila kitu kiko in shambles...mfano kahawa, chai, pamba (wanapewa mbegu feki), nyama (Tanganyika Packers iko wapi?) exports zetu kwa sasa zinaporomoka kila siku, na demand for import iko juu kila siku. Hii ina maana tulikosea miaka mingi tuliporekebisha uchumi kwa kuruhusu private sector bila uangalifu.

Ninapotoa mfano wa exports versus imports (hata toothpick) lazima ikustue akilini kwamba tuna import too much na kutumia dola za ngama tulizonazo kwa mambo ya kipuuzi, na hivyo kuidhoofisha zaidi shilingi, elewa hivyo.
.
Ninajua sana umuhimu wa kuwa na balanced trade na ndiyo maana hata majadiliano ya Economic Partnership Agreement (EPA) baina ya EU na nchi za ACP tunaona utakuwa mzigo mwingine na tunaionya sana serikali isikubali kwa sababu tutashindwa kulitumia vema soko ilhali wao watakuja
Tunashidwa au viwanda viko taabani kwa sababu ya mifumo kama hii mkuu wangu!. Hatuwezi kusafirisha nyama ikiwa serikali yetu haiwezi kusisitiza nchi tunazobalishana kununua mali zetu, sisi tunatazama kununua tu na kutoa tender za share ya 10% wa kiongozi au mwanaye akasome nje. JK anapokwenda nje anatakiwa kuonyesha tuna rasilimali zipi tunauza nasi tunahitaji vitu kadhaa wa kadha kutoka kwenu...kwani Malaysia, Singapore na sasa Vietnam wameweza vipi?

Swala sio kubinafsishwa hata kidogo bali hivyo viwanda vimekosa masoko ya kuuza mali zao, tazama korosho viwanda vimekufa kumbe serikali iliondoa liseni za kuuza nje sasa mwenye kiwanda azalishe Korosho ili auze wapi?. Kilichotakiwa ni serikali kuhakikisha tunapata soko la Korosho kama walivyofanya kwa Sangara, na mfanyabiashara (binafsi) atazalisha kutokana na masoko yetu ni haya na haya. Tutaweza vipi kulipa madeni yetu ikiwa nchi haizalishi, unataka kunambia tunalipa cash money?..

Kufa kwa viwanda vyetu kumetokana na mfumo mbaya wa kiuchumi ambao sisi tuliuza viwanda na mashirika kama Liquidation yaani mashirika hayo yameingia Bankruptcy badala ya kufikiria kwamba tunaingia Ubepari ni nani atakayeweza kuyaendeleza na soko ni hili..

Tanganyika Packers na mashirika yote tumeyaua wenyewe na nakuhakikishia hakuna shirika hata moja lilonunuliwa mnunuzi alipewa source na soko ama taarifa ya biashara hiyo ilipokuwa ikishikwa na serikali yaani sisi tulinunua malighafi hapa na pale na tuliwauzia hawa na hawa sasa wewe endeleza uzalishaji. Ubinafsishaji nchini haukufanyika bali kilichofanyika ni Liquidation!..
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Mkandara,

uko sahihi, lakini unadhani JK akienda nje kutengeneza masoko, kwa bidhaa zipi? kwa ubora gani? kwa mazingira gani ya production ilhali umeme hakuna? Je, si bora tunge concentrate kuinua viwanda vyetu kwanza, kwa kuhimiza uzalishaji competitive ili bidhaa hizi ziweze kushindana na masoko ya nje?

Chukulia mfano cement tu hapa...production yake inaathiriwa sana na suala la umeme, udhaifu wa shilingi na transport system, kiasi kwamba ikipambana na cement toka nchi za COMESA (hata itoke Egypt) hii yetu inapoteza soko kwa kuwa production costs ni juu.

Ninakubaliana na wewe kila kitu hapo, lakini kuna basic things ilikuwa tuanze navyo then tuvutie wawekezaji au hata kutafuta masoko ya nje. Mimi ninafuatilia sana foreign reserves, ambazo kwa kiwango kikubwa inakuwa boosted na what we export. Mathalan, wakati Mkapa anaondoka 2005, FR ilifikia ya kutosha imports za miezi 8.5, lakini kuna wakati ilishuka hadi miezi 3, why?
 
Ni kweli AK 48, lakini nini kiwe kiini cha mabadiliko haya ya kimfumo tunayohitaji? Ni kwa kila mtu kujituma kutimiza wajibu wake. watu wetu wengi huwa hawapendi kushiriki kwenye michakato mbali mbali yenye mustakabali wa taifa hili. Mathalan, achilia mbali chaguzi, lakini hata tunapotakiwa kutoa maoni juu ya mambo nyeti, wengi wetu huona huo ni wajibu wa wengine...wengine akina nani? Tatizo letu pia limekuwa kuacha kujifunza mambo ya msingi ili kupata uzoefu wa kutatua matatizo yetu wenyewe. Hata thread nyingi humu jamvini zinazohitaji kufikiria sana au ku reasearch, huoni kama zina wachangiaji wengi...wengi wetu tunachangia kwenye mambo rahisi rahisi, ya kuropoka ropoka. Aina hii ya society haiwezi kuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo yake yenyewe, kwa hiyo wachache wanaweza kuamua kwa niaba ya wengi lakini kwa maslahi yao wachache...then, baada ya madhara kuanza kujitokeza kwa wengi, sasa ndo utasikia malalamiko kila kona...nina imani sijamuudhi yoyote kwa maoni yangu haya, Ndugu AK48.



Maelezo yako ni mema na sidhani atajitokeza mtu kuyapinga. Ila katika kukuunga mkono, naomba niseme ni kweli watanzania tuna tatizo la kukwepa mambo ambayo yanahitaji kufikiri sana, na yale ambayo yanahitaji pro-active approaches. tunapenda zaidi kuletewa jibu au solution, hasa kwa sisi wenye umri mkubwa kidogo. Na si kitu kizuri.

Jambo hili ni tatizo la kimila, na halitaweza kuisha haraka haraka kama ambavyo tungependa. matatizo cultural huwaga yanachukua muda sana kuisha, japo watoto wetu wameanza kuonesha kutofautiana na sisi kwa kiasi fulani, which is a a good sign change is on its way. lakini kumbuka lazima tutakuwa tumewaambukizapo hivi vijitabia vyetu.

Ukiangalia magazeti yanayouzika kwa wingi sana utakuta ni yale yanayoweka mambo ya ngono, starehe, na vitu vingine ambayo havihitaji kufikiri sana. Ukishaanza kuzungumzia econometrics kwenye gazeti, au habari za kina Plato na Socratise, au time dialation za kina Einstein, ujue gazeti hilo linafungwa kesho. Ila mdororo uliopo katika siasa za nchi yetu umekuwa mkubwa mno kiasi kwamba kwa kweli wakati wa kujihusisha moja kwa moja umefika. Hili la kuwaachia watu wengine kufanya maamuzi kwa ajili yetu halitusaidii sana.

So I think its time to get going....actively, pro-actively, kila mmoja wetu kadri ya kipawa chake.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
AK 48,

Kuna mtu humu Avatar yake ili sum up ulicoelezea. Kwamba wenye makosa ni wale wanaokaa kimya wakati makosa yanatendeka. Kwa hili, sisi tumo sana, ndo maana hasa tumekuwa taifa la walalamikaji. Tunakuwa wavivu sana kujihushisha na mambo yanayotuzunguka na kuathiri maisha yetu. Hata wengine wanapojaribu kujadili mambo ya maana, wengine waliospecialize kutibua basi huingiza pumba. Wakati JF ilipokuwa mbichi, miaka ya 2006, ilikuwa hujadili jambo bila kuwa na credible source au ufahamu wa kutosha, unless unauliza ufahamishwe.

Lakini nadhani time is everything...siwasomi tena akina Icadon, Malaria Sugu, Mgonjwa wa Ukimwi, Field Marshal, Philemon, na wengine weengi...
 
DSN, mkuu unatumia nguvu nyingi sana kunidhibiti nisikueleze ukweli. Wewe unaongelea hisia, ndo maana nimekwambia fanya hata simple research. Hupendi kuambiwa ufanye research? Mimi siyo mwanasiasa bwana, na huchangia kile tu ninachokifahamu kwa lengo la kuelimishana. Soma mtandao ukuze ufahamu wako. Hii kelele ya Bulk procurement nimeisikia miaka hiyo, na kwa sababu mimi pia shughuli zangu zinategemea mafuta, nimejenga interest...si wewe tu unayetegemea mafuta mkuu.

1. It was very clear kwamba nimehint tu kwamba unasema bulk procurement imeanza juzi wakati wa mgomo wa wauza mafuta. Nimekuelimisha/kukukumbusha kwamba nimeanza kuisikia toka 2008. Hata hivyo, ukweli niliouona mtandaoni ni kuwa umebuniwa 2007. Sasa kwa nini umechelewa ni jambo lingine.

Uongo wangu uko wapi? hebu soma hii link:

http://www.ewura.com/pdf/keynotespeech/DG%27s%20SPEECH%20ON%20BULK%20PROCUREMENT%20REPORT%20%20Report.pdf

It is from this background that, in accordance with Section 9(2) (b) of the

EWURA Act, Cap 414, EWURA conducted an Inquiry to seek stakeholders'
comments before making a decision on the matter. The Inquiry process was
initiated on 6th November 2011 by publishing a Notice in the Government
and
by posting public notices in newspapers and on the EWURA website. A
stakeholders' meeting was held on 22nd November 2011 where f
urther
comments on the pricing formula were received. The consultation process was
concluded by an exit meeting 10th December 2011
that was attended by
representatives of key stakeholders, after which the Board of Directors of
EWURA, in its 55th Ordinary Meeting that was held on the 15th December 2011,
deliberated and approved a revised pricing formula.

Cha msingi sioni lolote naona ni Politic as usual kipya nini hapa kama sio mchakato umeaanza mwaka jana wakati wa crisis.Kusema na kuweka kwenye makarabrasha ndio mambo tusiyo yataka vijana kitu kinazungumzwa mwaka 19 kweusi eti mchakato almost 4 f-years, wakati wote huo wanafanya nini?Tena kama sio crisis walishaamua kunyuti,kuna watu wanasema Tanzania its rhe best country in creating Policy,but when it comes to implementation Kenya,Uganda, Rwand and the lest of Africa they just came and pick to use for their benefit of the Country.Huku tukikwama wanakuwa wa kwanza kutufunilia makarabrasha tizama tulikuwa kwenye mchakato,mchanganuo,na mengineyo yote yenye dalili ya watu walio bweteka doing nothing.

Na wewe Mzee wetu Mbalamwezi unakumbatia kukubali kuwa iko sawa ebu tizama hivi hapa kitu rasmi ni hiyo mwaka 2008 ujayongangania Mzee au ni hayo maelezo yenye nyekundu.Hii ni dalili ya politics kwenye maswla nyeti ya Uchumi.!We new generation uwa atupendi sound is umeongea na mzee mwenzio kuwa kuna wale waliojengwa kutibua ndio wenye kutumika kuludisha nyuma maendeleo ebu pata picha wazo mwaka 2008 utekelezaji ni baada ya Crisis ya Mafuta mwaka jana,ebu pata picha hapa katikati miaka minne nini kilizuia zoezi lilochukua only mwezi mmoja.Nisichopenda kwako its the waya you support as nothing wrong with these EWURA people ndio kusema walikuwa ok its just the process.Ahhhhh acha mzee hatutafika na ndio maana tumestack na mwenendo huu wa aian ya watu.
 
DSN umeiliza swali zuri muda wote huo walikuwa wapi...kama unakumbuka vema, baada ya sheria kupitishwa na bunge, waziri mwenye dhamana ilimchukua miaka kadhaa kutunga kanuni zinazotumika sasa! Na wengine wanasema kulikuwa na upinzani mkali wa mfumo huu hasa baadhi ya wabunge ambao poa ni wenye biashara ya mafuta kwa sababu walijua mwisho wa ujanja wao ulifika. Hivyo baada ya waziri kutunga kanuni kayikayi ya mwaka jana, wadau wa mafuta wakaunda kampini hii inayosimamia uagizaji mafuta kwa pamoja. Ni kweli tabia yetu waswahili ya kuchelewa inakera nakubali. Mimi si kwamba natetea mfumo, ila najaribu kukueleza namna unavyifanya kazi na uukosoe ukiwa na full knowledge. Nimekuwa nikiufutilia kwa sababu ya interest ya kujua mambo ya nyumbani yanayogusa mageuzi ya uchumi.
 
Mkuu DSN, hii taarifa ina background nzuri ya unachokipigia kelele hadi mapovu yanakutoka, sidhani kama mtumiaji wa mafuta umewahi kuiona japo ikuwa ni public information.

Sasa baada ya hapo, lete hoja za msingi, bila kashfa kwa sababu sote tu watu wazima.

http://www.ewura.com/pdf/pressreleases/NEW FORMULAR FOR BULK PROCUREMENT.pdf


Haya Mzew wangu na JF nisaidieni kujua hoja hii Mzee wangu Mbalamwezi nasema taaarifa hii ni toka mwaka 2008 ,lakini utekelezaji mwaka 2012.Haya wadau naomba mnisaidie vingeleee hivi vya taarifa hizi za EWURA
1: Moja ni Speech ya Mkurugenzi wa EWURA bwana Masebu
2: Moja ni Taarifa ya EWURA kwa vyombo vya habari Nchini


 
Back
Top Bottom