Tanzania Automotive Technology (Nyumbu): Si Kama Unavyoifikiria

Hivi viwanda vilianzishwa na J.Nyerere ili kukabiliana na ajira sambamba na kuongezeka kwa watu enzi za TANU, miaka ya 60 na 70. Ilivokuja CCM mwaka 77 uroho ukaimaliza ndoto ya viwanda tz. Vilivyokuwa viwanda kuna mikono ya wahindi nyuma yake na kifo cha viwanda hivyo ndio utajiri maridhawa wa wahindi hao marafiki na wabia wa viongozi au waliokuwa viongozi. Aidha wanafadhili ccm au ni wabunge wa ccm. Viongozi wanapolewa utajiri huo wanaanza kuwazuga wtz. Eti ukosefu wa ajira ni bomu linalotaka kupasuka. Wanasahau kuwa wameliunda wao. Likipasuka wao wataponea wapi?
 
Sina sababu ya kubishana na wewe, lakini nakuhakikishia hata fundi wa VETA au kishoka mzowefu pale gerezani anaweza fanya welding nzuri kuliko hii, embu angalia wewe kweli unaweza kununua bidhaa kama hii?

attachment.php

tehe tehe haya bhana ila na mm nikuhusie tu ck moja jitahid ufikepo mwenyew yawezekana hiyo sample moja kati ya nyingi zingine ukazipenda na pale pia utabahatika kuona gar aina ya NYUMBU ambalo ni moja ya research zao sema kiukwel undelezaj in terms of production ndo serikali bado haijajipanga research nying zinaishia kweny maonyesho ya sabasaba tu basi
 
kaka kiukweli jambo usilolijua ni usiku wa giza amini usiamin ukwel ni kwamba tanzania technology ya kutengeneza gari tena kwa kutumia hawa hawa wazawa wa nyumbu inao fanya siku moja kama utapata kibali cha kufikapo maana pako chin ya JWTZ ufike pale utakuta wataalam nyanja mbalimbali wengi eg foundary machineshop maintainance design nk

Je wajua kuwa siku hizi bajeti wanayopewa NYUMBU kwa ajili ya research zao haitoshi hata kutengeneza tractor moja?
 
Kweli mkuu, nakkumbuka zamani tulikuwa na asembly za magari hapa hapa; SCANIA, NISSAN PATROL, right? Hivi baiskeli za Swala zilitengenezwa hapa ama? Leo kuna sababu gani ya kuhalalisha vifo vya Viwanda kama hivi ambavyo obviously bei za bidhaa zao zingekuwa cheap kuliko za kutoka China na Japan?..........SAD, SO SAAAAAD!

ccm = 0. No vision at all in ccm
 
Endeleeni kuiponda lakini NYUMBU wanatengeneza new team sasa hivi,wametangaza ajira mpya nyingi sana juzijuzi,wameongezewa budget na serikali. Sasa hivi mtasikia wanatengeneza drones!
 
Nyumbu wakiweza kutengeneza hata bajaji ya miguu mitatu yenye sura mbaya kama fissi kwa ajili ya matumizi ya raia, bei yake itakuwa kiama, italingana na bei ya Hammer mpya. Halafu serikali itaweka ushuru wa kufa mtu kwa magari toka nje ili kulonda soko la ndani! Shuhudia bidhaa toka nje kama cementi, sukari, viberiti, mafuta ya kula nk.
 
Endeleeni kuiponda lakini NYUMBU wanatengeneza new team sasa hivi,wametangaza ajira mpya nyingi sana juzijuzi,wameongezewa budget na serikali. Sasa hivi mtasikia wanatengeneza drones!

Drones zipi hizo mkuu, au camera inayopelekwa na helcopter?
 
Endeleeni kuiponda lakini NYUMBU wanatengeneza new team sasa hivi,wametangaza ajira mpya nyingi sana juzijuzi,wameongezewa budget na serikali. Sasa hivi mtasikia wanatengeneza drones!

Nyumbu wakiweza kutengeneza hata bajaji ya miguu mitatu yenye sura mbaya kama fissi kwa ajili ya matumizi ya raia, bei yake itakuwa kiama, italingana na bei ya Hammer mpya. Halafu serikali itaweka ushuru wa kufa mtu kwa magari toka nje ili kulonda soko la ndani! Shuhudia bidhaa toka nje kama cementi, sukari, viberiti, mafuta ya kula nk.


MKuu tungeanza na TRACTORS
 
Israel 2/3 la wanacheshi wake ni wataalamu wa IT na Technologia zote nchini humo makampuni yote ya technologia wamiliki wake ni wanajeshi na technology yote ni product ya Jeshini, sasa siis Jeshi letu asilimia kubwa utasikia ni Askari wa Miguu front.

Na wizi wa mabenki na kukwapua kwa risasi
 
Nyumbu kwenyewe miaka kumi wanatengeneza gari moja.

Nchi Hii hakuna aliyekuwa na dira ya viwanda ,Sayansi na technology Kama Mwalimu .

Alianzisha viwanda 400 Nchi nzima
Alianzisha Backbone Industry tena Za Aina yake kwa miaka Hiyo Afrika

1 Man'gula Complex ( morogoro ) ...Hiki kinaweza kuyeyusha chuma na kufytua copy yeyote mikubwa( mama Rwakatare KAPEWA na Kauza MITAMBO yote
2. Kilimanjaro Machine Tools ...chenye uwezo wa Kuchonga spare zote ndogo ..na Za Kati
3. Kiwanda cha Mzinga ...chenye kutoa risasi ,mizinga ya Masafa mafupi na Kati ,mabomu,na milipuko...
4.Mufindi Paper Complex ...Kiwanda kikubwa Afrika ukiondoa south upande wa Karatasi
5. Nyumba Project ...chenye jukumu la kutoa Magari ya usafrishaji ,Magari ya deraya,zimamoto ,vifaru ...etc ...na kilimudu kutafiti na KUZALISHA vitu vyote Hivyo ...kwa uchache..kwa kutumia vijana wa KITANZANIA ambao Sasa ni Wazee ...hawa Mwalimu aliwachukua mlimani waliofaulu Sana karibu 30 akawapeleka ulaya kusoma kwa miaka Mitano ...na Ndio walioanzisha Kiwanda

Tanzania ilikuwa na Kiwanda cha kila kitu kuanzia ..Vyakula Vya watoto,NGuo ,beef ( Tanganyika packers ...Ndio walikuwa wauzaji wakubwa wa beef kwenda uingereza kabla ya Botswana kuteka soko ) ..Tanganyika packers ilikuwa na eneo kuanzia Pugu station hadi kawe ya Leo ... Na Jina kawe linatokana na Njia ya Ngome ..( cow way ) ....ambako walikuwa wakishashushwa na treni wanaswagwa taratibu kupita maeneo ya kimara hadi wanafikia kiwandani ...Njia yote wanakula,..kutibiwa ..na kupumzika ili kupata nyama bora ...

Ni Mwalimu pekee ambaye alikuwa na Ndoto ya kujenga Science village akilenga kuchukua watoto wenye vipaji Afrika yote kuanzia primary hadi chuo kikuu ...na tayari alikuwa ametenga eneo Arusha ,..Ndio mradi wake wa mwisho kisayansi .......Tulivo wajinga time chukua replica ya mradi wa Mwalimu Mandela university ,Tengeru ....same idea sema mandela inalenga wanafunzi wa Uzamili Afrika na tumeijenga kwa pesa zetu ...
 
Misri almost uchumi na shuglu zotekubwa kubwa ni mali ya Jeshi. Jeshi lina hadi Bakery kubwa za Mikate kwa ajili ya Kulisha wamisri. Hili jeshi letu alijuhi kulima Hata Mchicha.

Viongozi wetu wanachojua ni kukaa kwenye ma-VX kukwepa foleni na kushinda bar kunenepeana. Kichwani kweupe sana.

Hakuna innovation.
 
Nchi Hii hakuna aliyekuwa na dira ya viwanda ,Sayansi na technology Kama Mwalimu .

Alianzisha viwanda 400 Nchi nzima
Alianzisha Backbone Industry tena Za Aina yake kwa miaka Hiyo Afrika

1 Man'gula Complex ( morogoro ) ...Hiki kinaweza kuyeyusha chuma na kufytua copy yeyote mikubwa( mama Rwakatare KAPEWA na Kauza MITAMBO yote
2. Kilimanjaro Machine Tools ...chenye uwezo wa Kuchonga spare zote ndogo ..na Za Kati
3. Kiwanda cha Mzinga ...chenye kutoa risasi ,mizinga ya Masafa mafupi na Kati ,mabomu,na milipuko...
4.Mufindi Paper Complex ...Kiwanda kikubwa Afrika ukiondoa south upande wa Karatasi
5. Nyumba Project ...chenye jukumu la kutoa Magari ya usafrishaji ,Magari ya deraya,zimamoto ,vifaru ...etc ...na kilimudu kutafiti na KUZALISHA vitu vyote Hivyo ...kwa uchache..kwa kutumia vijana wa KITANZANIA ambao Sasa ni Wazee ...hawa Mwalimu aliwachukua mlimani waliofaulu Sana karibu 30 akawapeleka ulaya kusoma kwa miaka Mitano ...na Ndio walioanzisha Kiwanda

Tanzania ilikuwa na Kiwanda cha kila kitu kuanzia ..Vyakula Vya watoto,NGuo ,beef ( Tanganyika packers ...Ndio walikuwa wauzaji wakubwa wa beef kwenda uingereza kabla ya Botswana kuteka soko ) ..Tanganyika packers ilikuwa na eneo kuanzia Pugu station hadi kawe ya Leo ... Na Jina kawe linatokana na Njia ya Ngome ..( cow way ) ....ambako walikuwa wakishashushwa na treni wanaswagwa taratibu kupita maeneo ya kimara hadi wanafikia kiwandani ...Njia yote wanakula,..kutibiwa ..na kupumzika ili kupata nyama bora ...

Ni Mwalimu pekee ambaye alikuwa na Ndoto ya kujenga Science village akilenga kuchukua watoto wenye vipaji Afrika yote kuanzia primary hadi chuo kikuu ...na tayari alikuwa ametenga eneo Arusha ,..Ndio mradi wake wa mwisho kisayansi .......Tulivo wajinga time chukua replica ya mradi wa Mwalimu Mandela university ,Tengeru ....same idea sema mandela inalenga wanafunzi wa Uzamili Afrika na tumeijenga kwa pesa zetu ...

Mkuu, wewe acha tu. Inauma sana
 
mkuu umenena, mbali na yutong hapa china, ukiwa mitaani utagundua kwamba magari yote maarufu duniani ni wameassemble hapa hapa kwao, mfano kila mji unakiwanda kinachoassemble magari brand flani utakuta beijing hyundai, beiijing jeep, beijing benz , huko guangzhou ambako ndio moyo wa china unadunda ndio usiseme, guangzhou toyota, guangzhou honda, nk, pia unakuta wanatumia kampuni zao hizi kununua kampuni kubwa kubwa, mfano geely ya china ishanunua volvo, sasa hivi wanazifyatua hpahapa kama matofali, sichuan waliikosa kosa hummer mwaka jana na ingeshanunuliwa, hapo shanghai ndio usiseme VW(shanghai volkswagen), kila kitu kinawezekana kma serikali inasupport, china makampuni yana support kubwa sana kutoka serikalini (chama ,teh teh)ingawa wengi hawakipendi kama sisi tusivyopenda ccm. lakini ccm huwezi kulinganisha na hiki cha china


Kwanza nadhani hatukustahili kabisa kusema jambo lolote zuri kuhusu nyumbu kwani walipaswa kuona JKT inaelekea wapi na inatoka wapi, pili muda waliokaa kwenye game ni kama technological revolution decade 3-4. so ktk mapinduzi haya walipaswa kujitathmini kama bado wanapaswa kuendelea kuwepo sokoni au lah.
Mimi nipo katika sector ya uzalishaji wa bidhaa za viwanda vidogo vidogo kama kutengeneza machine za kukamua alizeti, kuchana mbao, kufyatua matofali fenicha za vyuma na zingine ndogo ndogo,
Niseme tu kuwa hatuwezi kwenda popote mimi wala nyumbu, kwani machine ni lazima tuziuze bei ya juu kulingana na gharama za uzalishaji kuwa juu.
Mashine nikimaliza kutengeneza siwezi kushindana kisoko na bidhaa toka asia kwani bei yao ipo chini karibu kwa 40% ukilinganisha na bidhaa yangu.
Barani asia:- Korea, Malaysia, China, Singapore, India na Vietnam wana silaha kubwa sana katika sector hii, nayo ni Nishati ya bei rahisi na ya uhakika. Sisi hatuna kitu hiki hadi ifikapo mwaka wa 2100 Mungu akijaalia pale tutakapompata raisi toka mbinguni, mawaziri watakapokuwa malaika ,na katiba itakapokuwa Biblia/Msahafu na hakimu/jaji kuwa Mungu pekee.
Nishati ya makaa ya mawe, gesi na Nuklia zaweza kutukomboa kama jinsi walivyofanya wenzetu, hapa wao hawana muujiza bali nishati endelevu na bei rahisi, kwani katika kiwanda cha aina yeyote kuna material supplier ambao nao huzalisha material tegemezi kwa bei rahisi hivyo assembles na finished products ni lazima iwe bei chini kwa kuwa material ambatanishi zimepatikana kwa bei ya chini hiyo bidhaa inayozalishwa ni lazima itamudu ushindani na kupenya katika masoko husika. sisi bila nishati tutaimba nyimbo zote na kuchagua wabunge wa kila chama lkn abadan si suluhu.

mfano rahisi nyumbu ananunua rangi toka gold star, ananunua U chennel toka Sita Steel, ananua Kioo toka Kioo limited, matairi toka Yana, Mild Steel Plates to Simba, Lami toka Tipper, Oil toka Oryx/ GBP, Umeme toka Tanesco. Plastic toka Simba, Chuma toka Congo, Copper wire toka Zambia. hawa wote ni wadau baadhi tu ili gari liwe gari sasa jiulize wao je wanazalisha kwa nishati ipi? na je kama ni sector endelevu kiuchumi wanapata ruzuku, au wanapewa punguzo la umeme, hapo majibu yote ni hapana,

Hivyo tutegemee miujiza kulifanya taifa kuwa nchi ya viwanda.

Natamani siku moja niwe kama Tanga Cement nipate kuwa na uwezo kifedha wa kujizalishia nishati yangu peke yangu tena ya bei rahisi kabisa.

Note:---
hata naangalia website yao akina Nyumbu naona kama alodizaini ni mtu alokuwa akifanya majaribio ya web design. nimetembelea website yao (www.tatcnyumbu.org/) jinsi ilivyo mbaya ni taswira tosha kuwa si watu walio siriaz na biashara yao.
 
Nyumbu wakiweza kutengeneza hata bajaji ya miguu mitatu yenye sura mbaya kama fissi kwa ajili ya matumizi ya raia, bei yake itakuwa kiama, italingana na bei ya Hammer mpya. Halafu serikali itaweka ushuru wa kufa mtu kwa magari toka nje ili kulonda soko la ndani! Shuhudia bidhaa toka nje kama cementi, sukari, viberiti, mafuta ya kula nk.

!
!
tanzania we are good for nothing...hata hakuna cha research wala nini, hapo ni swala la kuungaunga hiki na kile na kuunga jodi gari inatembea. Kuanzia matairi engine zote ni kutoka nje.
 
Unanikumbusha sana Foxconn, huyu ndiyo bingwa wa dunia pale Uchina anaetengeneza vipuri vya electronic products, kama Apple, Samsung, Google, Dell, IBM and HP nk bidhaa zote hizi zinafanyiwa design california na canada, ila manufacturing na assembling ni Uchina kwa Foxconn, then zinachapwa Made in China, China wanapata ajira, wanapata export duty, wanapata payee toka kwa employee na foreign currency, sasa tujiulize kwaninihawa wanaenda kuzalishia uchina na je wachina wana akili sana kuliko american, au wachina wana kodi ndogo ya production na export/import au hawakusanyi kodi,
Jibu ni kuwa wana Umeme wa kueleweka na unaonunulika, soko imara la ndani, na ruzuku katika electronic products, pia uchina wao wana sera yao wanasema umeme ni basic needs kama chakula na malazi, hivyo wana needs 4 ambazo ni chakula , malazi, mavazi na umeme. tanzania bana hata sijui tuiseme vp. eti mimi naweza kujibu email za ofisini kwangu usiku maana mchana sina umeme na bahati mbaya nimejiajiri mwenyewe. haya bana
 
Endeleeni kuiponda lakini NYUMBU wanatengeneza new team sasa hivi,wametangaza ajira mpya nyingi sana juzijuzi,wameongezewa budget na serikali. Sasa hivi mtasikia wanatengeneza drones!

We unazijua drones au unasikia tu?
 
Back
Top Bottom