Tanzania Automotive Technology (Nyumbu): Si Kama Unavyoifikiria

Yutong kule China kilikuwa ni kiwanda kikubwa kilichokuwa kikitengeneza zana za kivita, kiwanda kimebadilishwa sasa kinatengeneza mabasi na mitambo mingine ya kiraia, mabasi ya Yotong yamefika hata hapa kwetu TZ. Ni muda muafaka kwa Serikali kuiwezesha Nyumbu pamoja na zana za kivita, kiwanda kitengeneze magari kwa ajili ya matumizi ya kiraia, tutaokoa mamilioni ya dola tunazopeleka Japan kununua magari tena mitumba. Kiwanda hiki kinaweza kutoa mchango mkubwa sana katika pato la Taifa na hivyo kupunguza umaskini tulio nao leo. Kutakuwa na haja gani ya kuagiza magari mitumba toka Japan na kwingineko wakati yapo magari mapya hapa nchini ambayp bila shaka bei itakuwa nzuri tu.

Nyerere alikuwa na dira akaona haja ya kuwa na kiwanda hicho, Warithi ni kama vile wamekitelekeza sana, wakumbuke kuwa hakuna maendeleo popote duniani bila ya kuwa na mageuzi ya Sayansi na Tekinolojia.

Bila wauzaji kujua watanufaikaje na mauzo, hakuna kitakachouzwa.....lakini kama kweli tunataka kufika tunakokwenda, manufacturing lazima tuifufue upya, hakuna jinsi
 
hello,
Ndugu zangu hivi mnafahamu kuwa sisi watanzania tunalo gari letu wenyewe linatengenezwa ama linaundwa kuanzia kila kitu toka malighafi hadi kuwa gari kamili? tena kwa kutumia watalamu wetu wazalendo wa humuhumu nchini? kama ilivyo wajerumani wana mercedes benz,bmw,opel, bugati nk. waingereza wana rover, land rover, jaguar, layland nk wajapan wa toyota,nissan,mitsubish ink, wahindi wana tata na nchi kadhaa ulimwengu zilizoendelea kiuchumi wanayo magari yao kadhalika nasi tunalo gari linaitwa NYUMBU tena linatengenezwa Kibaha ktk kambi ya jeshi.
swali linakuja; kwanini sisi kuanzia serikali, wanaharakati wa maendeleo hadi wanajeshi wenyewe hatulithamini gari letu ama kwanini hatuliendelezi likawa miongoni mwa magari ya kutumainiwa duniani? je kuna tatizo gani? ukiangalia Nyumbu iliyotengenezwa mwaka 1995 haipishani kabisa na nyumbu ya mwaka 2012 yaani kilakitu ni kilekile, yyani gari iko vile vile miaka nenda rudi huwezi kuona tofauti, jambo ambalo ni tofauti na magari mengine toyota ya mwaka 1995 huwezikuilinganisha na toyota ya mwaka 2012 kuna vikorombwezo vingi vimeongezwa. lkn sisi tupo vile vile je hakuna innovetors au madesignors.
mwaka 2005 ktk maonesho ya sabasaba niliwahi kumuuliza afisa wa jeshi aliyekuwa ktk maonesho ya sabsaba kwamba 'je mnao mkakati gani wa kulifanya gari likawa la kisasa zaidi na mkawauzia wananchi magari ya humuhumu ndani pengine gari letu likawa bora kuliko faw ya mchina' jibu lilikuwa ni rahisi sana 'hakuna mpango wa kutengenega kisha kuwauzia gari wananchi' fullstop
sasa mi' nafikiri ni jambo la kizamani sana......! kwamba teknolojia ile ya kutengeneza gari ni jambo la siri kubwa za jeshi kiasi kwamba huwezi na ni hatari kwa usalama wa taifa kuuza....! mi' nafikiri ni jambo la upumbavu yaani ni kupumbaa kwa akili, tusinge nunua sisi yaho mascania yangebaki hukohuko wanapoweza kutunza siri kubwa.
hoja kwa nini na sisi tusiwe na hata salon zetu "nyumbu" badala ya kung'ng'ania mark11, au chaser, gx110 za kijapan? tena kwa kuwa kuna uhaba wa ajira serikali ingeamua ika install likiwanda pale mwendapole, tungepunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ajira na hata hela zetu zisingeenda kwenye mashangingi. ni kiasi gani cha pesa tungeokoa, peleka nyumbu kwenye ofisi zote za serikali waziri nyumbu, katibu mkuu nyumbu hapana kununua mashangingi tena; likiharibika spea zinatoka japan tunalipa kwa pesa za kigeni. nyumbu yetu spea zitatoka mwendapole nauli yake shilingi 1,100/=
mimi ningekuwa mkuu wa nchi ningewaita wale wataalam wote wa pale nyumbu kisha ningewauliza 'ninyi vijana mnalo tatizo gani? afu ningewapa gari moja luxury sema benz jipya kabisa nikawaambia nataka nyumbu ile luxury zaidi ya hii benzi, sawa? wale maafande wangeitika tuu SAWA AFANDE.........! biashara imekwisha.
lkn hili jambo linataka utashi wa kimapinduzi ya kifikra kwani tunao watu wengi ambao ni wataalam wa kutegemewa na wanafanya mabo makubwa katika tasnia ya sayansi na ufundi;lkn tunafanya nini? mwaka juzi km nipo sahihi niliwahi kusikia wanajeshi wa kitanzania walifanya vizuri ktk kudesign na kutengeneza engine za speed boat uarabuni. wako wapi wale vijana, zikozwapi hizo engine au ndio mali ya jeshi na siri za jeshi? hv hatujui kuwa kuna makampuni yanatengeneza engine tuu ama mitambo na kuingiza pesa za kigeni na kutoa ajira kwa vijana wetu? au lengo ni kuwafundisha mpaka wakajua kuunda engine na kuunda magari kwaajili ya kuua watu (vita)? hii ni suala mtambuka tena la kimapinduzi kiviwanda kwa nchi kama Tanzania. tuache zile porojo za kisiasa tuchape kazi. India sasa wanatengeneza tata luxury na zimeanza ku compite na gari za ulaya, na wao walianza kwa kuangalizia benz truck kwa mikataba na kampuni ya benz. tubadilike tuache zile fikra za mafundi vibatari, hebu angalia kibatari alichotumia babu wakati akiwa kijana, hakina tofauti na kibatari utakachonunua leo ukiwa mzee. ni kilekile hakina improvement yeyote toka design mpaka ufanyaji kazi. na hakuna anayeshtuka. sasa huu ufundi gani? huna mabadiliko "creativity" lkn kibatari hichohicho km angekuwa amekiunda mjerumani.......! pengine sasa hv kingekuwa kinatumia nishati ya jua
 
nyumbu-truck.jpg

Hivi Tanzania tuna kiwanda cha Matairi??.....tusende kwenye vingine........
 
General tyre Njiro kinaanza mwakani

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
hizo nyumbu
  • zimetegezwa/ zimekuwa assembled ngapi toka zianze
  • zinatumia engine gani tata, landlrover MAN
  • kama zikizalishwa for lkuuza ztagharimu shiligi ngapi

Mbona hatuzioni barabarani au spesho kwa vita?

Ni spesho kwa maonyesho
 
Ninajua hakifanyi kazi majengo na mitambo inaliwa tu na kutu huku tukiagiza matairi nje.Hili Linawezekana Tanzaniatu.
 
Jamani inasikitisha sana na hiki kiwanda cha nyumbu kama angekuwa mtoto angekuwa amedumaa vibaya, tatizo ni hii serikali ya magamba yaani hata vitu vidogo tu wanashindwa kuiga ambavyo vingetusaidia sana, mimi nipo hapa South Korea ni nadra sana kuona gari kutoka nje ya korea may be kila magari 100 utakayoyaona magari matatu3 ndo ya kigeni japo wao wapo karibu sana na Japan hawa import magari wao wana imitate technology ya wajapan tu wanapeleka watu wao kwenye viwanda vya japan wanarudi na technology wanazaidi ya makampuni matano ya magari KIA, HYUNDAI, SUMSUNG, Daewoo na mengine ikumbukwe tu mwaka 1960 South korea ilikuwa maskini kama tanzania na pengine ilikuwa maskini zaidi yetu, Japan na nchi zingine wakitoa brand mpya ya Magari wao wanaiga wanatoa the same na gari zinauzwa bei rahisi sana so wananchi hawaoni haja ya kuagiza magari nje, Ethiopia majirani zetu hapo Jeshi lao mwaka jana wametoa mabasi ya abiria kama hayo yanayozunguka hapo dar na wametoa brand nyingine mwaka huu. huwa najiuliza sana hivi hawaviongozi wetu wanatembelea sana nchi hizi hawana wivu na kutamani wenzao wanavyofanyaa?:A S embarassed:
 
Jamani inasikitisha sana na hiki kiwanda cha nyumbu kama angekuwa mtoto angekuwa amedumaa vibaya, tatizo ni hii serikali ya magamba yaani hata vitu vidogo tu wanashindwa kuiga ambavyo vingetusaidia sana, mimi nipo hapa South Korea ni nadra sana kuona gari kutoka nje ya korea may be kila magari 100 utakayoyaona magari matatu3 ndo ya kigeni japo wao wapo karibu sana na Japan hawa import magari wao wana imitate technology ya wajapan tu wanapeleka watu wao kwenye viwanda vya japan wanarudi na technology wanazaidi ya makampuni matano ya magari KIA, HYUNDAI, SUMSUNG, Daewoo na mengine ikumbukwe tu mwaka 1960 South korea ilikuwa maskini kama tanzania na pengine ilikuwa maskini zaidi yetu, Japan na nchi zingine wakitoa brand mpya ya Magari wao wanaiga wanatoa the same na gari zinauzwa bei rahisi sana so wananchi hawaoni haja ya kuagiza magari nje, Ethiopia majirani zetu hapo Jeshi lao mwaka jana wametoa mabasi ya abiria kama hayo yanayozunguka hapo dar na wametoa brand nyingine mwaka huu. huwa najiuliza sana hivi hawaviongozi wetu wanatembelea sana nchi hizi hawana wivu na kutamani wenzao wanavyofanyaa?:A S embarassed:
TUmeshindwa kutunza kiwanda cha matairi kilichokuwa kinahit mbaya! tuweze kufanya mambo makubwa? Angalia sherehe za kenya wanasherehekea miaka 50 ya uhuru na maonyesho ya magari ya kutumia umeme, jua nk!! Sisi tunafanya utani ambao unatakiwa uwepo kila siku. Wazee wetu aka viongozi wetu wamechoka kufikiria, they can't take risks for the future of our country. Cha msingi ni kukataa viongozi wachumia tumbo, viongozi vibaraka wa nchi za kigeni, kukataa viongozi wasiokuwa na vision!! mimi nawewe tunaweza kama tutaamua.
 
Huwezi kufanya mambo kama hayo kama mtu hukuzoea kutake risks toka utotoni, huwezi kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya nchi au ya watu wengine kama hukuwahi kufanya hivyo kabla au kama kundi ulilonalo hakuna hata mmoja aliyewahi kufanya hivyo. Ujanja, wizi wizi na magumashi gumashi ndo sifa za viongozi wetu wengi.
 
Mkuu hivyo vitu matata sana, mimi nina imani tutafika tuu, sio lazima tutengeneze kila kitu, tunaweza kushirikiana na mataifa mengine tukapata vifaa bora tukaassemble hapa hapa kwetu, nilikua naangalia documentary ya bmw z4, mkuu kila kitu kimotoka eneo mbalimbali na vimekua assembled eneo lingine kabisa, mfano mjerumani katengeneza engine, ikatumwa us, seat kuna kampuni nyingine imetengeneza, yaani ni ushirikiano matata na mwisho kinatoka kitu matata pia, pia angalia ndege ya airbus karibia mataifa matano kila moja limetengeza kifaa mojawapo, kuanzia engine, mabawa nakadhalika kisha wakaassemble . Nimecheck website ya nyumba wanaushirikiano na mataifa mengi tuu ila lbda bado hawajafikia hatua muhimu za kufanya kazi wote, kudos nyumbu, at least we have something

Mkuu umenena wewe jee viongozi wetu wa sasa wana maono gani? Picha zote zilizo hapo juu ni wakati wa Nyerere na Mwinyi. Mkapa hakuwahi kukanyaga nyumbu, na huyu wa sasa bado, unatarajia tutafika kama wengine? Tatizo let ni kuwa viongozi wetu wa sasa hawana vision. Wakifika ulaya na kuchekelewa na viongozi wa huko wanadhani maendeleo
 
MKUU HIKI KITU CHA VETA KIPO SABASABA, NADHANI HAKITUMII WESE
MAMA_AKIANGALIA_GARI_LINALOTUMIA_SOLA.jpg

Huyu mwenye nguo nyekundu ni Waziri wa nini? Mbona ana kihelehele sana huyu, hilo gari lina mhusu nini? Arudi jikoni akampikie muzee!
 
Huyu mwenye nguo nyekundu ni Waziri wa nini? Mbona ana kihelehele sana huyu, hilo gari lina mhusu nini? Arudi jikoni akampikie muzee!

Mmmh haya makubwa tena. By the way wapo wapi watu wa nyumbu watueleze mkakati wao kuhusu shirika hili!
 
Back
Top Bottom