Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,913
- 30,254
TBC imekuwa ikirusha kipindi, ''Kutoka Maktaba,'' kipindi hicho kikionyesha
mahojiano aliyofanya Ally Sykes na TBC 1 wakati wa uhai wake kuhusu
maisha yake akiwa Burma wakati wa WWII hadi kwisha kwa vita na kuanza
harakati za kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika:
''Wakiwa pale Kurnegala, askari Waafrika walipata mafunzo ya kupigana msituni kwa miezi minne na kisha wakaondoka kwenda Burma kupitia Trincomalee.
Kutoka hapo wakaelekea Chittagong.
Wakati wote huo wakiwa katika msafara walisindikizwa na British Royal Navy, meli zao zikienda polepole kwa tahadhari, zikipita njia ambayo walihisi ni shwari kutokana na mashambulizi ya Wajapani.
Ilikuwa hapo Chitagong ambapo askari walipata kwa mara ya kwanza kuonja kile kilichokuwa kikiwangoja.
Kulikuwa na kitambo cha takribani kilometa kumi baina ya bandari na kambi.
Barabara ilikuwa mbaya na ilikuwa imejaa matope ambayo yalifika kina cha kifundo cha miguu kutokana na mvua kubwa za monsoon.
Kambi ilikuwa chafu kwa matope yaliyotapakaa kila mahali. Askari ilibidi abebe mzigo wake mzito wa vifaa na zana, bunduki na risasi.
Vilevile ilibidi wachimbe mahandaki siku hiyo hiyo kwa ajili yao wenyewe na kwa maafisa wao Wazungu.
Kambi iiliwapa picha kamili ya kilichokuwa kikiwasubiri hata kabla hawajasikia milio ya bunduki za Wajapani."
''Ilikuwa ni pale Anfal ambapo, huku vita vinafikia ukingoni, Abdulwahid na askari wenzake wa Burma walikaa kitako kutafakari mambo yaliyowasibu katika vita na kuufikiria mustakbal wa Tanganyika.
Iliamuliwa kuwa askari wa Burma kutoka Tanganyika waliokuwa 6th Battalion (Batalioni ya Sita) wawe ndio chanzo cha chama cha siasa kupigania uhuru wa Tanganyika kwa kuuhamasisha umma.
Wote waliafiki wazo hilo.
Jina lililochaguliwa kukitambulisha chama hicho lilikuwa Tanganyika African National Union (TANU).
Ally Sykes anamkumbuka Abdulwahid kuliandika jina la chama hicho kilichokusudiwa ndani ya shajara yake.
Hawa askari wa Burma walikuwa wakifahamu vyema kuwa tayari huko nyumbani kulikuwapo na African Association, chama ambacho kilikuwa kikipigania haki za Waafrika.
Abdulwahid alitarajiwa afahamu hili zaidi ya wenzake kwa sababu baba yake ndiye aliyekianzisha chama hicho akiwa katibu wake wa kwanza.
Lakini suala la jinsi wangekiunganisha chama hicho kipya cha TANU na kile cha African Association halikujadiliwa.''
Kulia Abdulwahid Sykes na mdogo wake Ally katika uniform ya King's African Rifles (KAR)
Burma Infantry. Picha hii ilipigwa Burma mwaka wa 1942.
Kutoka: ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)...''
mahojiano aliyofanya Ally Sykes na TBC 1 wakati wa uhai wake kuhusu
maisha yake akiwa Burma wakati wa WWII hadi kwisha kwa vita na kuanza
harakati za kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika:
''Wakiwa pale Kurnegala, askari Waafrika walipata mafunzo ya kupigana msituni kwa miezi minne na kisha wakaondoka kwenda Burma kupitia Trincomalee.
Kutoka hapo wakaelekea Chittagong.
Wakati wote huo wakiwa katika msafara walisindikizwa na British Royal Navy, meli zao zikienda polepole kwa tahadhari, zikipita njia ambayo walihisi ni shwari kutokana na mashambulizi ya Wajapani.
Ilikuwa hapo Chitagong ambapo askari walipata kwa mara ya kwanza kuonja kile kilichokuwa kikiwangoja.
Kulikuwa na kitambo cha takribani kilometa kumi baina ya bandari na kambi.
Barabara ilikuwa mbaya na ilikuwa imejaa matope ambayo yalifika kina cha kifundo cha miguu kutokana na mvua kubwa za monsoon.
Kambi ilikuwa chafu kwa matope yaliyotapakaa kila mahali. Askari ilibidi abebe mzigo wake mzito wa vifaa na zana, bunduki na risasi.
Vilevile ilibidi wachimbe mahandaki siku hiyo hiyo kwa ajili yao wenyewe na kwa maafisa wao Wazungu.
Kambi iiliwapa picha kamili ya kilichokuwa kikiwasubiri hata kabla hawajasikia milio ya bunduki za Wajapani."
''Ilikuwa ni pale Anfal ambapo, huku vita vinafikia ukingoni, Abdulwahid na askari wenzake wa Burma walikaa kitako kutafakari mambo yaliyowasibu katika vita na kuufikiria mustakbal wa Tanganyika.
Iliamuliwa kuwa askari wa Burma kutoka Tanganyika waliokuwa 6th Battalion (Batalioni ya Sita) wawe ndio chanzo cha chama cha siasa kupigania uhuru wa Tanganyika kwa kuuhamasisha umma.
Wote waliafiki wazo hilo.
Jina lililochaguliwa kukitambulisha chama hicho lilikuwa Tanganyika African National Union (TANU).
Ally Sykes anamkumbuka Abdulwahid kuliandika jina la chama hicho kilichokusudiwa ndani ya shajara yake.
Hawa askari wa Burma walikuwa wakifahamu vyema kuwa tayari huko nyumbani kulikuwapo na African Association, chama ambacho kilikuwa kikipigania haki za Waafrika.
Abdulwahid alitarajiwa afahamu hili zaidi ya wenzake kwa sababu baba yake ndiye aliyekianzisha chama hicho akiwa katibu wake wa kwanza.
Lakini suala la jinsi wangekiunganisha chama hicho kipya cha TANU na kile cha African Association halikujadiliwa.''
Kulia Abdulwahid Sykes na mdogo wake Ally katika uniform ya King's African Rifles (KAR)
Burma Infantry. Picha hii ilipigwa Burma mwaka wa 1942.
Kutoka: ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)...''