nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
*
WAKATI hali ya mambo ndani ya Wizara ya Ujenzi ikiendelea kuwa tete, waziri wa wizara hiyo, Dkt. John Magufuli amerushiwa
lawama kwa kile kilichoelezwa kuwa kutotilia maanani matatizo ya ndani, badala yake kuweka kipaumbele kwa majukumu ya kisiasa yanayompa sifa binafsi.
Chanzo cha kuaminika ndani ya wizara hiyo kimeliambia gazeti hili kuwa imani waliyokuwa nayo wafanyakazi hao inazidi kushuka siku hadi siku kutokana na Dkt. Magufuli kushindwa kupatia ufumbuzi wa haraka kero zilizodumu kwa muda mrefu ndani ya wizara hiyo ikiwemo uteuzi wa wakala mbalimbali ikimewemo TANROADS.
"Wizara ya Ujenzi chini ya mheshimiwa Magufuli imepoteza mwelekeo kwa kile tunachoona, ameweka kipaumbele zaidi kwa shughuli zinazompa sifa binafsi, anatafuta 'cheap popularity' kwa wananchi na kujisahau kutekeleza vipaumbele vya majukumu muhimu ya Wizara yake," kilisema chanzo hicho na kuongeza;
"Inashangaza waziri kutembelea mikoani na kuwaamrisha wakuu wa mikoa na wilaya kuwaweka ndani makandarasi bila kufuata taratibu. Jambo hili analifanya kienyeji sana 'unprofessional.' Kuna utaratibu wa mambo yote kwenye mikataba na hatua za kuchukua kama mkandarasi anashindwa kufanya vizuri.
"Tatizo ni kwamba waziri hajui na hataki kujua labda kuponzwa na sifa anazomwagiwa na wananchi, ndio maana anaacha huku wizarani mambo yamelala wala haoni umuhimu wa kuwateua watendaji wakuu mapema."
Majira lilidokezwa kwamba tangu Dkt. Magufuli arudishwe wizarani hapo, kurugenzi na wakala zote za wizara zimeendelea kuwa na watendaji wakuu waliokaimishwa kwa muda usiojulikana.
"Hii imetuchanganya kwani tuliamini Mheshimiwa Rais Kikwete ametuletea Magufuli akiamini kwamba ana uwezo wa kudhibiti hali mbaya ya wizara na wakala zake. Badala yake Mheshimiwa Waziri yuko moto kutoa amri nzito zinazompa sifa binafsi, hata wakati mwingine kuvuka mipaka bila kushirikisha wakuu wake wa kazi."
"Kwa mfano amri za bomoabomoa nchi nzima na amri za kuwatisha makandarasi bila kufuata taratibu ni hatari katika kipindi hiki ambacho serikali inakabiliwa na changamoto nyingi juu ya kero za wananchi ambazo hazijazipatiwa ufumbuzi.
"Kwa ujumla wizara imepoteza mwelekeo, badala ya kuwa wizara ya kujenga, imekuwa ya bomoabomoa. Ikumbukwe kwamba hata hayo mabango yaliyowekwa barabarani yaliwekwa kwa ridhaa ya serikali hivyo kuyaondoa ni vyema utaratibu ukafuatwa kuepuka kuiingiza serikali katika kesi za fidia kama ilivyojitokeza katika uuzaji holela wa nyumba za serikali, Dowans nk. Hivi sasa wizarani hakuna anayejua afanye nini zaidi ya kusubiri utekelezaji wa Waziri Magufuli."
Chanzo kingine ndani ya Wizara hiyo kilisema hatua ya Dkt. magufuli kuchelewa kupanga miundo na watendaji wakuu wizarani na kwenye wakala imechangia kupunguza kasi ya utendaji wizarani hapo.
"Nashindwa kuelewa kwanini anachelewesha jambo hili au hajapata anaowataka yeye? Waziri Magufuli anasifiwa sana na wananchi wa kawaida ambao wao hawaoni kasoro hizi. Huenda amejisahau kwa sifa hizo na kusahau majukumu yake mengine ya ndani ya wizara. Aangalie matatizo yaliyo ndani ya wizara na kuyashughulikia haraka."
Vyanzo hivyo vilimshauri Dkt. Magufuli kutumia muda mwingi zaidi kupanga safu za wizara yake bila upendeleo ili kukabiliana na majukumu mazito yanayoikabili wizara na kuleta mafanikio kwa serikali na taifa kwa ujumla.
Majira lilipomtafuta Dkt. Magufuli simu yake iliita bila kupokelewa. Lilipotuma ujumbe wa maneno kuomba apokee simu, lilijibiwa kuwa "Unayemtafua yuko Kagera."
Lilipompigia simu msaidizi wake aliyefahamika kwa jina moja la Samike, alisema katibu mkuu ndiye mwenye jukumu la kutoa ufafanuzi wa masuala yote yanayohusu wizara hiyo kwa kuwa ndiye mtendaji mkuu.
WAKATI hali ya mambo ndani ya Wizara ya Ujenzi ikiendelea kuwa tete, waziri wa wizara hiyo, Dkt. John Magufuli amerushiwa
lawama kwa kile kilichoelezwa kuwa kutotilia maanani matatizo ya ndani, badala yake kuweka kipaumbele kwa majukumu ya kisiasa yanayompa sifa binafsi.
Chanzo cha kuaminika ndani ya wizara hiyo kimeliambia gazeti hili kuwa imani waliyokuwa nayo wafanyakazi hao inazidi kushuka siku hadi siku kutokana na Dkt. Magufuli kushindwa kupatia ufumbuzi wa haraka kero zilizodumu kwa muda mrefu ndani ya wizara hiyo ikiwemo uteuzi wa wakala mbalimbali ikimewemo TANROADS.
"Wizara ya Ujenzi chini ya mheshimiwa Magufuli imepoteza mwelekeo kwa kile tunachoona, ameweka kipaumbele zaidi kwa shughuli zinazompa sifa binafsi, anatafuta 'cheap popularity' kwa wananchi na kujisahau kutekeleza vipaumbele vya majukumu muhimu ya Wizara yake," kilisema chanzo hicho na kuongeza;
"Inashangaza waziri kutembelea mikoani na kuwaamrisha wakuu wa mikoa na wilaya kuwaweka ndani makandarasi bila kufuata taratibu. Jambo hili analifanya kienyeji sana 'unprofessional.' Kuna utaratibu wa mambo yote kwenye mikataba na hatua za kuchukua kama mkandarasi anashindwa kufanya vizuri.
"Tatizo ni kwamba waziri hajui na hataki kujua labda kuponzwa na sifa anazomwagiwa na wananchi, ndio maana anaacha huku wizarani mambo yamelala wala haoni umuhimu wa kuwateua watendaji wakuu mapema."
Majira lilidokezwa kwamba tangu Dkt. Magufuli arudishwe wizarani hapo, kurugenzi na wakala zote za wizara zimeendelea kuwa na watendaji wakuu waliokaimishwa kwa muda usiojulikana.
"Hii imetuchanganya kwani tuliamini Mheshimiwa Rais Kikwete ametuletea Magufuli akiamini kwamba ana uwezo wa kudhibiti hali mbaya ya wizara na wakala zake. Badala yake Mheshimiwa Waziri yuko moto kutoa amri nzito zinazompa sifa binafsi, hata wakati mwingine kuvuka mipaka bila kushirikisha wakuu wake wa kazi."
"Kwa mfano amri za bomoabomoa nchi nzima na amri za kuwatisha makandarasi bila kufuata taratibu ni hatari katika kipindi hiki ambacho serikali inakabiliwa na changamoto nyingi juu ya kero za wananchi ambazo hazijazipatiwa ufumbuzi.
"Kwa ujumla wizara imepoteza mwelekeo, badala ya kuwa wizara ya kujenga, imekuwa ya bomoabomoa. Ikumbukwe kwamba hata hayo mabango yaliyowekwa barabarani yaliwekwa kwa ridhaa ya serikali hivyo kuyaondoa ni vyema utaratibu ukafuatwa kuepuka kuiingiza serikali katika kesi za fidia kama ilivyojitokeza katika uuzaji holela wa nyumba za serikali, Dowans nk. Hivi sasa wizarani hakuna anayejua afanye nini zaidi ya kusubiri utekelezaji wa Waziri Magufuli."
Chanzo kingine ndani ya Wizara hiyo kilisema hatua ya Dkt. magufuli kuchelewa kupanga miundo na watendaji wakuu wizarani na kwenye wakala imechangia kupunguza kasi ya utendaji wizarani hapo.
"Nashindwa kuelewa kwanini anachelewesha jambo hili au hajapata anaowataka yeye? Waziri Magufuli anasifiwa sana na wananchi wa kawaida ambao wao hawaoni kasoro hizi. Huenda amejisahau kwa sifa hizo na kusahau majukumu yake mengine ya ndani ya wizara. Aangalie matatizo yaliyo ndani ya wizara na kuyashughulikia haraka."
Vyanzo hivyo vilimshauri Dkt. Magufuli kutumia muda mwingi zaidi kupanga safu za wizara yake bila upendeleo ili kukabiliana na majukumu mazito yanayoikabili wizara na kuleta mafanikio kwa serikali na taifa kwa ujumla.
Majira lilipomtafuta Dkt. Magufuli simu yake iliita bila kupokelewa. Lilipotuma ujumbe wa maneno kuomba apokee simu, lilijibiwa kuwa "Unayemtafua yuko Kagera."
Lilipompigia simu msaidizi wake aliyefahamika kwa jina moja la Samike, alisema katibu mkuu ndiye mwenye jukumu la kutoa ufafanuzi wa masuala yote yanayohusu wizara hiyo kwa kuwa ndiye mtendaji mkuu.