Maajabu ya tumbuzi ya Arusha ya meneja TARURA kuwa hajaleta wananchi kushuhudia vishindo vya awamu ya tano tumeyaona.
Kuwa TANROADS au TARURA Biharamulo na Ngara wangali wanadunda maofisini hata katika ubovu huu wa barabara uliopo usio mfano? Ama kweli kama hii si moja ya maajabu ya Mussa basi maajabu hayo yatakuwa hayapo tena.
Mambo yamekuwa siasa siasa tu hadi ina kera kwa kweli. Kwamba ni tija katika utendaji? Basi Meneja TARURA yule asingetumbuliwa ila kwa sababu hakujaza watu kushuhudia vile vishindo vyetu vya awamu hii, basi jambo limezua jambo.
Hali Biharamulo, Ngara iko kama ilivyo pichani.
Mbaya zaidi kwa ubovu uhusiano na barabara ya Rusahunga Ngara na Rusumo, jana katika eneo la nyabugombe, moja ya maeneo yanayopigiwa kelele kila leo, pana mtu kafa pale kwa ajali ya gari.
Kwa hakika maisha yale hayakuwa na sababu yoyote ile ya kupotea kwani hizi ni zile ajali za wazi zinazosababishwa na mamlaka na ambazo zingeweza kuepukika.
Hadi wafe wangapi ndipo busara kuweza kutumika japo kufanya marekebisho kidogo tu?
Hata kama mameneja nyie mnahamasisha mno kisiasa na hivyo kuendelea kudunda, si muyazibe basi japo haya mashimo au kurekebisha hizi sehemu zilizo mbaya zaidi zenye kuhatarisha zaidi maisha ya watu? Hii ni hata kama mmeamua wenye magari yao wale hasara vilivyo?
Jafo fika barabara hii kumsaidia Eng. Kamwelwe kusafisha uozo huu.
Kuwa TANROADS au TARURA Biharamulo na Ngara wangali wanadunda maofisini hata katika ubovu huu wa barabara uliopo usio mfano? Ama kweli kama hii si moja ya maajabu ya Mussa basi maajabu hayo yatakuwa hayapo tena.
Mambo yamekuwa siasa siasa tu hadi ina kera kwa kweli. Kwamba ni tija katika utendaji? Basi Meneja TARURA yule asingetumbuliwa ila kwa sababu hakujaza watu kushuhudia vile vishindo vyetu vya awamu hii, basi jambo limezua jambo.
Hali Biharamulo, Ngara iko kama ilivyo pichani.
Mbaya zaidi kwa ubovu uhusiano na barabara ya Rusahunga Ngara na Rusumo, jana katika eneo la nyabugombe, moja ya maeneo yanayopigiwa kelele kila leo, pana mtu kafa pale kwa ajali ya gari.
Kwa hakika maisha yale hayakuwa na sababu yoyote ile ya kupotea kwani hizi ni zile ajali za wazi zinazosababishwa na mamlaka na ambazo zingeweza kuepukika.
Hadi wafe wangapi ndipo busara kuweza kutumika japo kufanya marekebisho kidogo tu?
Hata kama mameneja nyie mnahamasisha mno kisiasa na hivyo kuendelea kudunda, si muyazibe basi japo haya mashimo au kurekebisha hizi sehemu zilizo mbaya zaidi zenye kuhatarisha zaidi maisha ya watu? Hii ni hata kama mmeamua wenye magari yao wale hasara vilivyo?
Jafo fika barabara hii kumsaidia Eng. Kamwelwe kusafisha uozo huu.