Askari Mnoko
Senior Member
- Oct 5, 2019
- 149
- 101
TANROAD mkoa wa Pwani, kwa kushirikiana na mwenyekiti wa Serikari ya Mtaa wa Bamba uliopo Kongowe, katika wilaya ya Kibaha. Wanaendekeza dhuluma dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo, wanaofanya shughuli zao katika eneo la hifadhi ya barabara, kwa kuwatoza Kodi Kila mwezi, kiasi Cha tsh 30,000/ na tsh 15,000/.
Kiasi hicho cha Kodi ukusanywa na mama Mmacha, ambaye anadai amemilikishwa eneo Hilo la hifadhi ya barabara na TANROAD mkoa wa Pwani, wakati Kuna alama kubwa ya mawe ya TANROAD. Baada ya kukusanya Kodi ndiyo mgao wa makusanyo hufanyika.
Wafanyabiashara wadogowadogo walijaribu kufuatilia uhalali wa mama Mmacha wa kukusanya Kodi, lakini waliambulia vitisho kutoka kwa uongozi wa Serikari ya Mtaa wa Bamba,"Kama mnataka kufanyabiashara lipeni Kodi na kama hamtaki kumlipa Kodi mama Mmacha acheni kufanya biashara".
Wanajamvi ninawaomba mtupe ushauri, hatua gani tuchukue kukomesha dhulma hii dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo.
Kiasi hicho cha Kodi ukusanywa na mama Mmacha, ambaye anadai amemilikishwa eneo Hilo la hifadhi ya barabara na TANROAD mkoa wa Pwani, wakati Kuna alama kubwa ya mawe ya TANROAD. Baada ya kukusanya Kodi ndiyo mgao wa makusanyo hufanyika.
Wafanyabiashara wadogowadogo walijaribu kufuatilia uhalali wa mama Mmacha wa kukusanya Kodi, lakini waliambulia vitisho kutoka kwa uongozi wa Serikari ya Mtaa wa Bamba,"Kama mnataka kufanyabiashara lipeni Kodi na kama hamtaki kumlipa Kodi mama Mmacha acheni kufanya biashara".
Wanajamvi ninawaomba mtupe ushauri, hatua gani tuchukue kukomesha dhulma hii dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo.