Tangu ulipoondoka mambo yamebadirika, miluzi imeongezeka

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,293
8,204
Tangu ulipoondoka mambo yamebadirika miluzi imeongezeka

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Watu waliookoka, wote wameshapotoka,
Twarudi tulikotoka, taifa linaanguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mafisadi wanacheka,
Uchumi umeanguka, keki inapukutika,
Rangi zinabadilika, vinyonga waongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mbwa wengi wanabweka,
Simba wameshatoweka, fisi wanaongezeka,
Uoto umetoweka, kijani kinafutika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, chama kinawatalaka,
Upendo umetoweka, taifa linachepuka,
Wazalendo tumechoka, wezi wameongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, rushwa imeongezeka,
Haki iyanizidi rika, utu unarukaruka,
Furaha meimarika, unyonge unaondoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, nia tumeshaizika,
Dira imetuponyoka, ghala limeshatoboka,
Bendera inachanika, tunu yetu menyofoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hasara zinasomeka,
Vifungo vinatoweka, habari zinasikika,
Na sauti zinatoka, na pingu zinakatika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wachache twanung'unika,
Wengi wanaburudika, hawanuni wanacheka,
Endapo ukifufuka, utalia hutocheka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, akili zimeondoka,
Imla uliyoandika, haiwezi kusomeka,
Kweli paka kiondoka, panya wanarukaruka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hatuna mchakamchaka,
Semi zimebadilika, hapa kazi kadhalika,
Wachache waheshimika, wengi wadharaulika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wameibuka vibaka,
Hazina wanaibaka, fafuyo inabomoka,,
Na keki uliyooka, bure inagawanyika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, bado tunakukumbuka,
Sijachoka kuandika, mema uliyoyaweka,
Hayawezi kuondoka, kichwani nitayaweka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, Bunge limebadilika,
Bunge linasikika, rangiye imechujuka,
Milango imedondoka, vitasa vimefunguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Najua umeshafika, kwa Mungu na Malaika,
Neno lako nakumbuka, lile "tutakukumbuka"
Kweli tushakukumbuka, kwetu umeadimika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Mwisho jipu laumuka, haliwezi kutumbuka,
Dakitari katoweka, sijui tutatibika?
Huduma imeondoka, hujuma twaialika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.
 
Tangu ulipoondoka mambo yamebadirika miluzi imeongezeka

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Watu waliookoka, wote wameshapotoka,
Twarudi tulikotoka, taifa linaanguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mafisadi wanacheka,
Uchumi umeanguka, keki inapukutika,
Rangi zinabadilika, vinyonga waongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mbwa wengi wanabweka,
Simba wameshatoweka, fisi wanaongezeka,
Uoto umetoweka, kijani kinafutika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, chama kinawatalaka,
Upendo umetoweka, taifa linachepuka,
Wazalendo tumechoka, wezi wameongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, rushwa imeongezeka,
Haki iyanizidi rika, utu unarukaruka,
Furaha meimarika, unyonge unaondoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, nia tumeshaizika,
Dira imetuponyoka, ghala limeshatoboka,
Bendera inachanika, tunu yetu menyofoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hasara zinasomeka,
Vifungo vinatoweka, habari zinasikika,
Na sauti zinatoka, na pingu zinakatika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wachache twanung'unika,
Wengi wanaburudika, hawanuni wanacheka,
Endapo ukifufuka, utalia hutocheka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, akili zimeondoka,
Imla uliyoandika, haiwezi kusomeka,
Kweli paka kiondoka, panya wanarukaruka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hatuna mchakamchaka,
Semi zimebadilika, hapa kazi kadhalika,
Wachache waheshimika, wengi wadharaulika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wameibuka vibaka,
Hazina wanaibaka, fafuyo inabomoka,,
Na keki uliyooka, bure inagawanyika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, bado tunakukumbuka,
Sijachoka kuandika, mema uliyoyaweka,
Hayawezi kuondoka, kichwani nitayaweka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, Bunge limebadilika,
Bunge linasikika, rangiye imechujuka,
Milango imedondoka, vitasa vimefunguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Najua umeshafika, kwa Mungu na Malaika,
Neno lako nakumbuka, lile "tutakukumbuka"
Kweli tushakukumbuka, kwetu umeadimika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Mwisho jipu laumuka, haliwezi kutumbuka,
Dakitari katoweka, sijui tutatibika?
Huduma imeondoka, hujuma twaialika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.
Shida za milele umuongezee eeh bwana na Giza la milele umzidishie.

Asipumzike kwa amani, Amen.
 
Tangu ulipoondoka mambo yamebadirika miluzi imeongezeka

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Watu waliookoka, wote wameshapotoka,
Twarudi tulikotoka, taifa linaanguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mafisadi wanacheka,
Uchumi umeanguka, keki inapukutika,
Rangi zinabadilika, vinyonga waongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mbwa wengi wanabweka,
Simba wameshatoweka, fisi wanaongezeka,
Uoto umetoweka, kijani kinafutika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, chama kinawatalaka,
Upendo umetoweka, taifa linachepuka,
Wazalendo tumechoka, wezi wameongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, rushwa imeongezeka,
Haki iyanizidi rika, utu unarukaruka,
Furaha meimarika, unyonge unaondoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, nia tumeshaizika,
Dira imetuponyoka, ghala limeshatoboka,
Bendera inachanika, tunu yetu menyofoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hasara zinasomeka,
Vifungo vinatoweka, habari zinasikika,
Na sauti zinatoka, na pingu zinakatika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wachache twanung'unika,
Wengi wanaburudika, hawanuni wanacheka,
Endapo ukifufuka, utalia hutocheka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, akili zimeondoka,
Imla uliyoandika, haiwezi kusomeka,
Kweli paka kiondoka, panya wanarukaruka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hatuna mchakamchaka,
Semi zimebadilika, hapa kazi kadhalika,
Wachache waheshimika, wengi wadharaulika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wameibuka vibaka,
Hazina wanaibaka, fafuyo inabomoka,,
Na keki uliyooka, bure inagawanyika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, bado tunakukumbuka,
Sijachoka kuandika, mema uliyoyaweka,
Hayawezi kuondoka, kichwani nitayaweka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, Bunge limebadilika,
Bunge linasikika, rangiye imechujuka,
Milango imedondoka, vitasa vimefunguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Najua umeshafika, kwa Mungu na Malaika,
Neno lako nakumbuka, lile "tutakukumbuka"
Kweli tushakukumbuka, kwetu umeadimika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Mwisho jipu laumuka, haliwezi kutumbuka,
Dakitari katoweka, sijui tutatibika?
Huduma imeondoka, hujuma twaialika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.
Sema wewe ndo umepotoka. Acha kumtegemea yule jizi kwani katuibia sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya Meko kuvuliwa nguo zote na watu wale wale aliowahi kuwateua, naona wapiga debe wake mmeamua kutunga mashairi ya kujifariji maana zile ngonjera zenu za kumpamba zimeyeyuka.

Na bado, hapa ni mwanzo tu, lile kaburi lake wapo watu watakwenda kulifunga pingu na kulichalaza fimbo. Watu wake wale wa karibu watasema marehemu alikuwa fisadi na muuaji mkubwa.
 
Tangu ulipoondoka mambo yamebadirika miluzi imeongezeka

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Watu waliookoka, wote wameshapotoka,
Twarudi tulikotoka, taifa linaanguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mafisadi wanacheka,
Uchumi umeanguka, keki inapukutika,
Rangi zinabadilika, vinyonga waongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, mbwa wengi wanabweka,
Simba wameshatoweka, fisi wanaongezeka,
Uoto umetoweka, kijani kinafutika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, chama kinawatalaka,
Upendo umetoweka, taifa linachepuka,
Wazalendo tumechoka, wezi wameongezeka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, rushwa imeongezeka,
Haki iyanizidi rika, utu unarukaruka,
Furaha meimarika, unyonge unaondoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, nia tumeshaizika,
Dira imetuponyoka, ghala limeshatoboka,
Bendera inachanika, tunu yetu menyofoka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hasara zinasomeka,
Vifungo vinatoweka, habari zinasikika,
Na sauti zinatoka, na pingu zinakatika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wachache twanung'unika,
Wengi wanaburudika, hawanuni wanacheka,
Endapo ukifufuka, utalia hutocheka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, akili zimeondoka,
Imla uliyoandika, haiwezi kusomeka,
Kweli paka kiondoka, panya wanarukaruka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, hatuna mchakamchaka,
Semi zimebadilika, hapa kazi kadhalika,
Wachache waheshimika, wengi wadharaulika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, wameibuka vibaka,
Hazina wanaibaka, fafuyo inabomoka,,
Na keki uliyooka, bure inagawanyika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, bado tunakukumbuka,
Sijachoka kuandika, mema uliyoyaweka,
Hayawezi kuondoka, kichwani nitayaweka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Tangu ulipoondoka, Bunge limebadilika,
Bunge linasikika, rangiye imechujuka,
Milango imedondoka, vitasa vimefunguka,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Najua umeshafika, kwa Mungu na Malaika,
Neno lako nakumbuka, lile "tutakukumbuka"
Kweli tushakukumbuka, kwetu umeadimika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.

Mwisho jipu laumuka, haliwezi kutumbuka,
Dakitari katoweka, sijui tutatibika?
Huduma imeondoka, hujuma twaialika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.
Tangu umeondoka wizi wako umejulikana,
Tangu umeondoka madudu yako yameanikwa,
Tangu umeondoka tumejua hila zako,
Tangu umeondoka nchi ina raha.
 
Tangu ulipoondoka, mbwa wengi wanabweka,
Simba wameshatoweka, fisi wanaongezeka,
Uoto umetoweka, kijani kinafutika,
Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika.
 
MAGUFULISM

Hii ni aina mpya ya Falsafa iliyoanzishwa katika Karne ya 21 haswa mwaka 2021 kutokana na falsafa za aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa Tanzania Dr. John Pombe Joseph Magufuli aliyeishi kati ya 1959-2021. Katika Falsafa ya Magufulism tutaangazia mitizamo ya mwanafalsafa huyu katika nyanja za Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii, Kidini, Kiutamaduni, Kielimu na Kisayansi. Falsafa hii imeandikwa na kubuniwa na mwanazuoni katika Elimu ya Saikolojia ya Watoto na mbobezi katika Historia kwa Ujumla.

MAGUFULIST

Hawa ni watu wote wanaoamini , wanaoishi na kuenenda katika falsafa ya Magufulism. Magufulist siku zote wanaamini kuwa maendeleo ya Taifa ama mtu binafsi yanatokana na kulinda raslimali tulizo nazo kwa nguvu zote na Kufanya kazi kwa uadilifu bila kutegemea misaada kutoka nje.

Hapa chini tutaichanganua falsafa ya MAGUFULISM katika nyanja mbalimbali ambapo tutaangalia Dr. John Pombe Magufuli alikuwa na mitizamo na falsafa gani kuhusu mambo mbalimbali:

MAGUFULI NA UCHUMI:

Dr. John Pombe Joseph Magufuli aliamini uchumi imara hutengenezwa kwa kutumia raslimali zilizotuzunguka kwa uaminfu na uadilifu. Dr, Magufuli aliamini pia kuwa endapo kila mmoja akitimiza wajibu wake wa kufanya kazi kwa bidii na kulipa Kodi kwa uaminifu basi uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla ungeimalika sana. Dr. Magufuli alipinga uwekezaji wenye masharti ya Unyonyaji kutoka kwa mataifa ya Nje hususani katika Sekta ya Madini, Bandari nk.

MAGUFULI NA SIASA:

Katika upande wa Siasa Dr. Magufuli aliamini katika uwepo wa Vyama vya siasa vyenye mlengo wa kuleta ushindani wa hoja na sio vyama vinavyotumiwa na mataifa ya Kigeni kutaka kuvuruga amani na mshikamano wa Taifa. Dr Magufuli alividhibiti kwa nguvu kubwa vyama vilivyokuwa vikitumiwa na mataifa ya Kigeni kupenyeza agenda za mataifa ya kigeni. Katika Upande mwingine Dr. Magufuli aliamini kuwa Maendeleo hayana chama. Katika kuonyesha kuwa maendeleo hayana chama , Dr. Magufuli aliwateua viongozi wengi wa Vyama vya Upinzani katika nyadhifa tofauti tofauti katika Serikali yake.

MAGUFULI NA JAMII

Dr. John Pombe Magufuli aliamini katika ustawi wa jamii na kupinga aina zote za unyanyasaji toka kwa watu wenye madaraka na matajiri. Katika kipindi chake cha uongozi ndipo jina "WANYONGE" lilipata umaarufu. Wananchi walipoona Msafara wa Dr. Magufuli waliukimbilia na kuona mtetezi wao amefika, naye Dr. Magufuli aliwapa nafasi ya Kuwasikiliza.

*MAGUFULI NA DINI"

Dr. Magufuli aliamini kuwa tunamuamini Mungu mmoja hivyo alihimiza usawa, upendo na mshikamano kati ya watu wa madhehebu yote. Alichangisha fedha za Kujenga Misikiti katika makanisa mbalimbali, na pia pesa za kujenga Makanisa kutoka misikiti mbalimbali. Dr. John Pombe Magufuli aliamini kuwa hakuna jambo linaloshindikana mbele za Mungu. Hata katika kipindi ambacho Dunia ilikuwa ikihangaika na janga la Corona Dr Magufuli alichukua msimamo tofauti na mataifa mengine, aliwahimiza watanzania kumuomba Mungu maana yeye hashindwi na jambo lolote lile.

MAGUFULI NA MAHUSIANO YA KIMATAIFA

Dr John Pombe Magufuli aliamini katika ushirikiano usio na chembe za unyonyaji kati ya Taifa lake na mataifa ya Kigeni. Dr Magufuli allikuwa tayari kusitisha uhusiano na Taifa lolote ama taasisi yoyote yenye lengo la kufanya unyonyaji kwa Taifa lake. Kwa Lugha rahisi Dr Magufuli hakuwa muumini wa Kujipendekeza kwa Taifa tajiri ama Taasisi za Kimataifa kwani aliona kuwa watu wote ni sawa hivyo hakuna sababu ya kuwanyenyekea wanyonyaji kutoka katika mataifa ya Kigeni.

MAGUFULI NA RUSHWA/UFISADI

Dr. Magufuli alichukia Rushwa na Ufisadi kwa dhati ya moyo wake. Alikuwa tayari kuvunja urafiki na mtu yeyote aliyetetea ama kufanya vitendo vya rushwa. Katika Kipindi chake cha Uongozi neno "KUTUMBUA MAJIPU" lilimaanisha kuondoa viongozi wote wasio waadilifu na kuwachukulia hatua.

Hii ni sehemu ndogo kati ya Historia ndefu na ya kusisimua kuhusu Kiongozi na mwana falsafa huyu aliyeishi katika Karne ya 21.
 
Back
Top Bottom