Tangu nilivyoanza kupendwa na wanawake wengi, pesa haikai kabisa

Tangu nilivyoanza kupendwa na wanawake wengi, pesa haikai kabisa

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
38,861
Reaction score
59,468
Kila ninachokipata kinapotea kwenye mazingira yasiyoeleweka, kichwa kikuu kimeshindwa kabisa kufanya maamuzi magumu ya kuzuia pesa isipotee.

Maendeleo yangu yamekuwa ni yakusua sua, wakati mwingine naonekana kama vile nimechanganikiwa, wazee wenzangu hawanipi heshima tena kama mwanzo.

Sasa wakuu, nitumie njia gani kurejesha uchumi, heshima, utulivu wa akili n.k nilivyokuwa navyo kabla ya kupendwa na wanawake?

Kwa sasa nataka nitulie na mmoja tu, wengine sitaki wanipende tena.​
 
Kila ninachokipata kinapotea kwenye mazingira yasiyoeleweka, kichwa kikuu kimeshindwa kabisa kufanya maamuzi magumu ya kuzuia pesa isipotee.

Maendeleo yangu yamekuwa ni yakusua sua, wakati mwingine naonekana kama vile nimechanganikiwa, wazee wenzangu hawanipi heshima tena kama mwanzo.

Sasa wakuu, nitumie njia gani kurejesha uchumi, heshima, utulivu wa akili n.k nilivyokuwa navyo kabla ya kupendwa na wanawake?

Kwa sasa nataka nitulie na mmoja tu, wengine sitaki wanipende tena.​
Kujua tatizo ni nusu ya kutatua tatizo. Maadam umejua shida, mwombe Mwenyezi Mungu akusaidie kushinda jaribu lako
 
Fanya kazi za umachinga yani utembee umbali mrefu kwa siku ukirudi umechokaa hutawaza wala kutamani papuchi ya mja na pesa itakaa
 
Unaweza kumshauri huyu jamaa halafu kesho akaja na Uzi Unaosema “NINA KILO MIA ZA MAHARAGE NATAFUTA MDADA WA KULA NAE “
JF VAR CHECK
 
Back
Top Bottom