Tangu kifo cha Hayati Dkt. Magufuli, kumeonekana wazi CHADEMA wakiacha agenda zao na kuanza kumpigia makofi Rais Samia

USSR

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
9,883
22,593
Chadema wamekuwa kama fisi wanaonyemelea mtu akitembea na kutupatupa mikono wakingojea eti mikono itadondoka wake, mmekuwa kama fisi anadanganywq mkono wa binadamu unaweza kudondoka mle na nyie unatoa akili na kugonja.

Tangu kifo cha hayati magufuli kumeonekana wazi chadema wakiacha agenda zao na kuanza kumpigia makofi mama samia suluhu hasani aka SASHA as if ni kiongozi aliyetokana na chadema na kusahau kuwa huyu ni mwanaccm mkomavu na hapa analinda na kusimamia ilani ya CCM 2020-2025 na hana agenda za upinzani wala wanaharakati wa ufipa na wale wa ulaya

Nilistushwa kuona CHADEMA wameitisha mkutano kupitia BAVICHA kwa kutangulizwa na wakubwa wao kupeleka mguu kwenye ziwa lenye kina kirefu na wakakuta urefu ni uleule wakatulia, eti walidhani wataruhusiwa kuanza biashara ya kuuza skafu na T-shirts kwa watanzania kama kawaida yao huku wakipanga kutumia kamkutano hako kuombea msamaha watu wenye jinai Rais awasamehe .

SASHA kama mwanaccm na mwanadamu anajua mnavyomvuta kwa kamba za umoja wa kitaifa (who cares about your national unity agenda ) hii hoja huja na vioja ,wakati mnamshinikiza Kikwete awape katiba aka-buy agenda na baadaye mkamgeuka na kukimbia Bungeni kisha mkamtosa kwenye hotuba ya kuvunja Bunge akabaki anasema CHADEMA ni kiwanda cha uongo bado mpo kwenye kumbukumbu kuwa hamuaminiki na nyie ni vinyonga ,nani awaamini.

Samia ni mwanaccm kindakindaki na sasa kanunua ndege zote tatu, kaliacha baraza la Mawaziri kama lilivyo,kasaini mikataba kule Uganda na kukataa mambo za kelele za misiasa isiyoisha na mjue hata kubali wanaccm wenzake wamuone kawasaliti ,CCM ni imani na sio mtu na hunia mamoja. Alivyofanya Nyerere, Mwinyi, Kikwete, Magufuli na Samia hivyo hivyo .

Mama huyu aliwaambia wazi kuwa amaefundwa na JPM na anamuona kama role model wake so kaeni mkao wa kula nyie bado sana kwa CCM, mpaka leo wameshatumia mbinu 1 out of 100 so mbinu 99 zote zimebakia.

Kwa taarifa tu SASHA anaompango wa kuongoza hadi 2030 ndio atoke maana katiba na CCM vyote vinamruhusu, yupo kimkakati

USSR.Chato Geita
 
Hilo jina SASHA umelitoa wapi? Mbona mnapenda kukurupuka na kuanza kuita watu majina ya ajabu ajabu kama unalipenda sana si ukamwite mkeo au mtoto wako?
 
Sawa dada yetu Dkt. Gwajima tumekusikia.


IMG_20210413_095621.jpeg
 
Hilo jina SASHA umelitoa wapi? Mbona mnapenda kukurupuka na kuanza kuita watu majina ya ajabu ajabu kama unalipenda sana si ukamwite mkeo au mtoto wako?
Samia Suluhu Hassani aka SASHA kama mmeo amelipenda akuita japo upate kina zuri sio kuitwa mwajuma .pwagu wewe
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom