Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,898
Tunajua kuwa VODACOM ni kampuni ya kibiashara na haifungamani na upande wowote ule katika masuala ya kisiasa hata kama baadhi ya wamiliki/wenye hisa wake ni wafuasi wa vyama vya siasa.
Siku za hivi karibuni kampuni hiyo imezindua TANGAZO la kuhamasisha matumizi ya intaneti ya 4G iliyozinduliwa miezi michache iliyopita.
Maudhui ya TANGAZO yanachanganya maana hayaoneshi dhima iliyo nyooka. MPOKI ambaye ametumika kufikisha ujumbe wa 4G amefanya madoido yanayo ashiria mamlaka ya kisiasa na siyo mamlaka ya kampuni.
Kwanza ameongea kwa kumuiga Mh. Magufuli (Raisi wa Tanzania kupitia CCM ), anaonekana akijibu swali la mwandishi wa habari aliye muuliza kwa niaba ya WANANCHI na siyo WATEJE WA VODACOM, Anatoa ahadi kama mwanasiasa na siyo muhusika mkuu wa kampuni ya VODACOM, Mwishoni Mwandishi anamalizia kwa kutumia slogani ya HAPA KASI TU ikinasibu ile ya Mh. Magufuli ya HAPA KAZI TU.
Kwa kuwa sehemu kubwa ya Tangazo imeonekana kukopi falisafa ya Mh.Magufuli(ambaye ni mwenyekiti mtarajiwa wa CCM)sitokuwa nimekosea kama nikisema yafuatayo juu ya Vodacom.
1. Kwamba Vodacom wanamkubali sana Mh. na falisafa zake.
2. Kwamba kwa kuwa Mh.ni mwenyekiti mtarajiwa wa CCM na wao wanamkubali sana na wanamuunga mkono basi Vodacom wako tayari kukiunga mkono pia chama atakacho kiongoza muda mfupi ujao.
3. Kwamba kwa misingi hiyo ya upendo wao kwa Mh.na chama chake ndo maana wakajikuta wanaongea kisiasa kana kwamba wanaongea na wanachama badala ya wateja wasio na chama.
4. Kwamba Vodacom wako tayari kutengana na watu/wateja ambao hawafuati fikra/falsafa za Mh.
Yapo mengi sana ila itoshe kuwambia Vodacom kwamba wametukwaza sana sisi tusiozikubali falisafa za huyu wanaye muonesha akiongea na wananchi badala ya wateja.
Sisi wateja wa Vodacom tusio penda matangazo ya biashara yenye chembe chembe za kisiasa tunatoa siku mbili tusilione hilo tangazo tena mpaka hapo watakapo libadilisha vinginevyo kama wakikaidi tutasusia kutumia mtandao wao milele. Tutawahamasisha na Wengine ili waone namna siasa inavyojipenyeza kila kona na mwisho wake ni hatari kwa mustakabali wetu kama Taifa.
Siku za hivi karibuni kampuni hiyo imezindua TANGAZO la kuhamasisha matumizi ya intaneti ya 4G iliyozinduliwa miezi michache iliyopita.
Maudhui ya TANGAZO yanachanganya maana hayaoneshi dhima iliyo nyooka. MPOKI ambaye ametumika kufikisha ujumbe wa 4G amefanya madoido yanayo ashiria mamlaka ya kisiasa na siyo mamlaka ya kampuni.
Kwanza ameongea kwa kumuiga Mh. Magufuli (Raisi wa Tanzania kupitia CCM ), anaonekana akijibu swali la mwandishi wa habari aliye muuliza kwa niaba ya WANANCHI na siyo WATEJE WA VODACOM, Anatoa ahadi kama mwanasiasa na siyo muhusika mkuu wa kampuni ya VODACOM, Mwishoni Mwandishi anamalizia kwa kutumia slogani ya HAPA KASI TU ikinasibu ile ya Mh. Magufuli ya HAPA KAZI TU.
Kwa kuwa sehemu kubwa ya Tangazo imeonekana kukopi falisafa ya Mh.Magufuli(ambaye ni mwenyekiti mtarajiwa wa CCM)sitokuwa nimekosea kama nikisema yafuatayo juu ya Vodacom.
1. Kwamba Vodacom wanamkubali sana Mh. na falisafa zake.
2. Kwamba kwa kuwa Mh.ni mwenyekiti mtarajiwa wa CCM na wao wanamkubali sana na wanamuunga mkono basi Vodacom wako tayari kukiunga mkono pia chama atakacho kiongoza muda mfupi ujao.
3. Kwamba kwa misingi hiyo ya upendo wao kwa Mh.na chama chake ndo maana wakajikuta wanaongea kisiasa kana kwamba wanaongea na wanachama badala ya wateja wasio na chama.
4. Kwamba Vodacom wako tayari kutengana na watu/wateja ambao hawafuati fikra/falsafa za Mh.
Yapo mengi sana ila itoshe kuwambia Vodacom kwamba wametukwaza sana sisi tusiozikubali falisafa za huyu wanaye muonesha akiongea na wananchi badala ya wateja.
Sisi wateja wa Vodacom tusio penda matangazo ya biashara yenye chembe chembe za kisiasa tunatoa siku mbili tusilione hilo tangazo tena mpaka hapo watakapo libadilisha vinginevyo kama wakikaidi tutasusia kutumia mtandao wao milele. Tutawahamasisha na Wengine ili waone namna siasa inavyojipenyeza kila kona na mwisho wake ni hatari kwa mustakabali wetu kama Taifa.