Tangazo la Tanzania Tourist Board Linalorushwa CNN

Well done Geeque & Co.

naona kama ulivyoahidi ya kwamba utatumia eastafricantube kuitangaza Tanzania......kwa kweli kazi yako ni nzuri........keep it up na Hongera sana
 
Ahsanteni sana Ogah na mTz si unajua tena inabidi sisi wenyewe ndio tushike hatamu katika kujitahidi kuitangaza nchi yetu hasa unapokuwa na nyenzo nzuri kama tovuti.
 
Limetulia sana tangazo hilo. Inatakiwa watangaze na katika Tv nyingine.
 
GQ,
Heeeeeeeeeee,mzee mambo kwa upole zaidi,keep it up.leo wachanipate midundo ya nguvu mpata night kali kwa kujinafasi.
 
Mazee Qeeque,

Heshima mbele lovely, vitu vikali siku zote ninazimia na watu kama wewe, maana ndio future ya bongo,

Always Respect Mkuu!
 
Tangazo hilo ni zuri...limeanza na the famous known to address the little known Tanzania. I like it that way.
 
Hii link aliyoweka Geeque.............ni nzuri sasa watu tuifanyie kazi kwa kuwapa watu wengine popote pale tulipo ili tuitangaze Tanzania.........wale walio maofisini na vyuoni KAMA MWAWEZA tumeni hiyo link kwenye intramail zenu, na wale wenye marafiki mbali mbali watumieni hao marafiki ili tijitangaze.............................lakini kinachoniuma nipale pesa inapopatikana MAFISADI wanazichangamkia....................anyway iko siku tu
 
mbona iko fupi kidogo, na imegharimu kiasi gani. Nasikia kampuni iliyotengeneza hiyo ni ya Mtanzania na kuna mtu alikatiwa kitu kidogo kupeleka tenda hiyo? Ila ni advertisement nzuri.
 
I must be the only one that thinks its crap and they could have done a much better job. It looks very amatuerish, like something done by a high school student for his video editing class.

but thats just my opinion i guess
 
Samahani Geeque,
Mimi nafuatilia sana CNN na mtazamaji mzuri lakini mbona sijawahi kuona tangazo hilo hata siku moja?
Je, isijekuwa ndio kama nilivyosema toka mwanzo kuwa matangazo yote ktk CNN hutegemea na nchi kwani kila nchi hununua habari za CNN sio matangazo yake. Mathlan hapa nilipo matangazo mengi kama sio yote yanahusu mashirika yanayofanya biashara hapa. Matangazo ya kuzitangaza nchi za nje ambayo nimewahi kuyaona ni South Korea na Jamaica tu.
Nitarudia kusema navyofahamu mimi kila shirika la urushaji vipindi vya TV hununua rights za vipindi vyake pekee lakini sio pamoja na matangazo kwani haya hufanyika locally nikiwa na maana CNN kwa wakazi wa NY na CNN Toronto zina vipindi sawasawa kwa wakati mmoja lakini matangazo yake hutofautina.
Hata michezo ya Football ama Basket ball, huwa tunatofautiana matangazo hata kama sote tunatazama mechi moja toka ESPN.
Naomba maelekezo zaidi kuhusu hili yawezekana bado zijapata ufafanuzi mzuri.
 
Samahani Geeque,
Mimi nafuatilia sana CNN na mtazamaji mzuri lakini mbona sijawahi kuona tangazo hilo hata siku moja?
Je, isijekuwa ndio kama nilivyosema toka mwanzo kuwa matangazo yote ktk CNN hutegemea na nchi kwani kila nchi hununua habari za CNN sio matangazo yake. Mathlan hapa nilipo matangazo mengi kama sio yote yanahusu mashirika yanayofanya biashara hapa. Matangazo ya kuzitangaza nchi za nje ambayo nimewahi kuyaona ni South Korea na Jamaica tu.
Nitarudia kusema navyofahamu mimi kila shirika la urushaji vipindi vya TV hununua rights za vipindi vyake pekee lakini sio pamoja na matangazo kwani haya hufanyika locally nikiwa na maana CNN kwa wakazi wa NY na CNN Toronto zina vipindi sawasawa kwa wakati mmoja lakini matangazo yake hutofautina.Hata michezo ya Football ama Basket ball, huwa tunatofautiana matangazo hata kama sote tunatazama mechi moja ktk ESPN.
Naomba maelekezo zaidi kuhusu hili yawezekana bado zijapata ufafanuzi mzuri.

Nadhani jibu unalo ktk post yako...
 
Nyani Ngabu,
nimekusikia mkuu kwa hiyo haya matangazo wame target nchi zipi hasa na yanaonekana nchi ama miji ipi hadi sasa.
 
Binafsi nimeliona mara mbili mwezi huu October ktk local CNN mnamo mida ya saa 12 (Central US time) jioni na jingine likawa siku nyingine nalo niliona kama saa mbili unusu au tatu hivi usiku.

nafikiri hili tangazo lilikuwa na target ya ku-attract watalii toka US
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom