Tangazo la Nafasi ya Kazi ya Ikulu: Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2020-2025

Mama Amon tayari umenasa vichwa vingapi?

kwamba tuma maombi through ...gmail.com!

kwamba attach cv yako "ututumie"!

siku hizi ikulu mnatumia gmail! aisee!!
 
@Mama Amon tayari umenasa vichwa vingapi?

kwamba tuma maombi through ...gmail.com!

kwamba attach cv yako "ututumie"!

siku hizi ikulu mnatumia gmail! aisee!!
.
Kuna shida gani kutumia gmail?

Kwani hujui kwamba naweza kuingia gmail.com na kusajili email ya ikulu ikasomeke xyz@ikulu.co.tz wakati ni gmail.com hiyo hiyo?

Nitajibu zaidi, ngoja kwa sasa nimalizie usingizi......
 
Tangazo la Nafasi ya Kazi ya Ikulu: Urais wa JMT 2020-2025 (Updated: 11 May 2019 at 11.00 PM)


View attachment 1089251

I. UTANGULIZI

Unafahamu kwamba 2020 kutakuwa na Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani nchini Tanzania?

Unajua kuwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani nchini Tanzania hupitia hatua kuu mbili, yaani, kura za maoni ndani ya vyama na baadaye mchuano wa jukwaani kwa njia ya kampeni zinazofanyika kwa siku sabini?

Unakumbuka kuwa, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi (1977) hata CCM wanapaswa kuachana na mapokeo yasiyo na tija kwa Taifa, na badala yake, wakajielekeze katika kuendesha mchuano wa kura za maoni ndani ya chama kwa ajili ya kumtafuta mgombea Urais aliye na sifa za kutosha kila baada ya miaka mitano?

Umewahi kuwa na ndoto ya kuwa Mkuu wa Nchi, Amiri Jeshi Mkuu na Kiongozi wa Serikali ya Nchi huru, na ukawa na uhakika kwamna unajua na una uwezo wa kuheshimu mipaka ya majukumu yaliyopo kati ya Jeshi la Wanananchi (JWTZ), Jeshi la Polisi na Jeshi la Ukachero kwa Ajili ya Usalama wa Taifa (TISS)?

Basi, Kama umejibu "ndiyo" kwa maswali haya yote, basi kuna yamkini kwamba, wewe unaweza kuwa Rais wa Tanzania kuanzia Novemba 2020.


Sifa za mwombaji, masharti, majukumu husika na utaratibu wa kuomba nafasi hiyo vinatajwa hapa chini.

Watanzania wote wenye nia hiyo wanakaribishwa kutuma maombi kulingana na maelekezo yanayofuata hapa chini.

II. JUKWAA LA UWAJIBIKAJI (ACCOUNTING FORUM) WA RAIS WA JMT

1. Katika kutekeleza majukumu yake, Rais wa JMT atwajibika kutoa taarifa za utendaji kazi zake mara kwa mara kwa bosi na mwajiri wake mkuu ambaye ni mpiga kura, ambapo atalazimika kutoa taarifa husika angalau mara moja kila mwaka kwa kutumia njia mojawapo kati ya njia zifuatazo:

1. Kulihutubia Taifa kupitia Bungeni;

2. Kulihutubia Taifa Moja kwa moja kupitia mkutano wa vyombo vya upashanaji habari ulioandaliwa maalum kwa ajili hiyo ;

3. Kulihutubia Taifa kupitia vyombo vya upashanaji habari atakapokuwa katika matukio maalum ya kitaifa.

III. MAENEO MAKUU YA UWAJBIKAJI (KEY ACCOUNTABILITY AREAS) WA RAIS WA JMT

1. Rais wa JMT atakuwa na maeneo makuu matatu ya uwajibikaji (Key Resualt Areas) kwa mujibu wa Katika ya Nchi ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake mpaka sasa, ambayo ni:

(a) Kutekeleza majukumu ya Mkuu wa Nchi ya JMT,

(b) Kutekeleza majukumu ya Kiongozi wa Serikali ya JMT, na

(c) Kutekeleza majukumu ya Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya JMT.

2. Katika kutekeleza majukumu yake kama Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali, na Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa JMT atakuwa na mamlaka ya kuanzisha na kufuta nafasi za madaraka ya namna mbalimbali katika utumishi wa Serikali ya JMT kwa ajili ya kuhakikisha kwamba vipaumbele vya kitaifa vinakabidhiwa mikononi mwa watumishi wa umma wenye weledi, uzoefu na umakini wa kutosheleza mahitaji ya utendaji wenye tija.


3. Katika kutekeleza majukumu yake kama Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali ya JMT, na Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa JMT atahakikisha kwamba, anatumia nguvu kubwa kukuza na kuhami haki ya kila raia kuwa huru dhidi ya kifo cha holela na haki ya kila raia kuishi katika mazingira yenye amani ya moyo. Haki hizi mbili --uhai na amani--zitapaswa kuchukuliwa kuwa kikonyo cha haki nyingine zote kwa sababu marehemu hana haki hata moja, isipokuwa haki ya kuzikwa na ndugu zake au serikali.

4. Taarifa ya Rais wa JMT ya kila mwaka, au vinginevyo, itapaswa kuwa na maudhui yanayoonyesha kazi zilizofanywa na Rais wa JMT katika Maeneo yote ya Uwajibikaji yaliyotajwa hapo juu katika fungu cha pili (2).

IV. MADARAKA NA MAJUKUMU YA URAIS WA JMT

1. Katika kutekeleza majukumu yake kama KIONGOZI WA SERIKALI ya JMT, Rais wa JMT atakuwa na mamlaka juu ya mambo yote ya Muungano katika Jamhuri ya Muungano, na pia juu ya mambo mengine yote yahusuyo Tanzania Bara. Katika kutekeleza majukumu haya, Rais wa JMT atakuwa na mamlaka ya:

(a) kusimamia utekelezaji wa sheria zote halali zilizotungwa na Bunge;

(b) kusaini mikataba ya kimataifa;

(c) kusimamia utekelezaji wa maamuzi yaliyomo katika hukumu za kimahakama;

(d) kusababisha utengenezwaji na uboreshwaji na sera za JMT;

(e) kusimamia utekelezwaji wa sera za JMT;

(f) kusababisha kutengenezwa kwa bajeti ya nchi, kuhakikisha inawasilishwa Bungeni, kujadiliwa na kupitishwa;

(g) kusimamia utekelezwaji wa kwa bajeti ya nchi kwa mujibu wa maamuzi ya Bunge;

(h) kuteua watumishi wa umma wote;

(i) kuthibitisha miswada ya sheria iliyopitishwa na Bunge kwa kuisani ili igeuke kuwa sheria halali za JMT;

(j) kusimamia nidhamu ya watumishi wa umma wote;

(k) kuigawanya JMT katika mikoa na wilaya kulingana na mahitaji wa nyakati husika;

2. Katika kutekeleza majukumu yake kama KIONGOZI WA SERIKALI ya JMT, Rais wa JMT atahakikisha kwamba Shughuli zote za utendaji za Serikali ya JMT zinatatekelezwa nay eye mwenyewe moja kwa moja au kwa kukasimu madaraka hayo kwa watu wengine wenye madaraka katika utumishi wa Serikali ya JMT, ambao watatekeleza shughuli zote za utendaji za Serikali ya JMT kwa niaba ya Rais wa JMT.

3. Katika kutekeleza majukumu yake kama KIONGOZI WA SERIKALI ya JMT, Rais wa JMT atakuwa na madaraka ya kuteua watu wa kushika nafasi za viongozi wanaowajibika kuweka sera za idara na taasisi za Serikali katika utumishi wa Serikali ya JMT, kwa maana ya nafasi ambazo zimetajwa katika Katiba ya nchi au katika sheria mbalimbali zilizotungwa na Bunge kwamba zitajazwa kwa uteuzi unaofanywa na Rais wa JMT.

4. Katika kutekeleza majukumu yake kama KIONGOZI WA SERIKALI ya JMT, Rais wa JMT atakuwa na madaraka ya kuteua watu wa kushika nafasi za watendaji wakuu wanaowajibika kusimamia utekelezaji wa sera za idara na taasisi za Serikali katika utumishi wa Serikali ya JMT, kwa maana ya nafasi ambazo zimetajwa katika Katiba ya nchi au katika sheria mbalimbali zilizotungwa na Bunge kwamba zitajazwa kwa uteuzi unaofanywa na Rais wa JMT.

5. Katika kutekeleza majukumu yake kama KIONGOZI WA SERIKALI ya JMT, Rais wa JMT atakuwa na madaraka ya kuchukua hatua za kudhibiti nidhamu ya watumishi na utumishi katika Serikali ya JMT.

6. Katika kutekeleza majukumu yake kama KIONGOZI WA SERIKALI ya JMT, Rais wa JMT Rais atakuwa na hiari ya kufuata au kupuuzia ushauri wowote atakaopewa na mtu yeyote, isipokuwa tu pale anapotakiwa na Katiba ya nchi au na sheria nyingine yoyote kufanya jambo lolote kulingana na ushauri anaopewa na mtu au mamlaka yoyote.


7. Katika kutekeleza majukumu yake kama MKUU WA NCHI, Rais wa JMT atakuwa na mamlaka na majukumu yafuatayo.

(a) kuenenda kama alama na taswira ya Jamhuri ya Muungano na watu wake;

(b) kusimama kama alama ya umoja na uhuru wa nchi pamoja na mamlaka yake.

(c) kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mbele ya mahakama kwa kosa lolote, na aweza kutoa msamaha huo ama bila ya masharti au kwa masharti, kwa mujibu wa sheria;

(d) kumwachilia kabisa au kwa muda maalum mtu yeyote aliyehukumuwa kuadhibiwa kwa ajili ya kosa lolote ili mtu huyo asitimize kabisa adhabu hiyo au asitimize adhabu hiyo wakati wa muda huo maalum;

(e) kuibadilisha adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa kosa lolote iwe adhabu tahafifu;

(f) kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa ajili ya kosa lolote; na

(g) kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu ya kutoza, au kuchukua kitu cha mtu mwenye hatia ambacho vinginevyo kingechukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

9. Katika kutekeleza majukumu yake kama AMIRI JESHI MKUU, Rais wa JMT atakuwa na mamlaka yafuatayo:

(a) kutangaza kuwapo kwa vita kati ya JMT na nchi nyingine yoyote;

(b) kuyaamuru majeshi ya nchi yatende mambo yanayohusika na vita vya ulinzi wa JMT,

(c) kuyaamuru majeshi ya nchi yatende mambo ya kuokoa maisha na mali ya watu katika hali ya hatari;

(d) kuyaamuru majeshi ya nchi yatende mambo mengineyo ambayo Amiri Jeshi Mkuu ataona yahitajika, ama ndani au nje ya Tanzania;

(e) kuwateua viongozi katika majeshi ya ulinzi ya JMT;

(f) kuwateua watu watakaojiunga na majeshi ya ulinzi na madaraka ya kuwaondoa jeshini wanajeshi;

(f) kuwateua wanajeshi watakaoongoza vikosi mbali mbali vya majeshi ya ulinzi;

(g) kumwamuru mwanajeshi yeyote asitumie madaraka yoyote aliyokabidhiwa na ambayo yanaambatana na kuwa kwake mwanajeshi; na

(h) kuamrisha kazi yoyote itakayotekelezwa na mwanajeshi yoyote baada ya kujiridhisha kwamba ni kazi halali kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya nchi.

V. SIFA ZA KIKATIBA ZA MWOMBAJI WA NAFASI YA URAIS WA JMT

Mtu yeyote anayetaka kuomba kugombea nafasi ya Urais wa JMT atapaswa kuthibitisha, kwa kuambatanisha ushahidi, kwamba anazo sifa zifuatazo:

1. ni raia wa kuzaliwa wa JMT kwa mujibu wa Sheria ya Uraia;

2. ametimiza umri wa miaka arobaini;

3. ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;

4. anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge;

5. katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu awe hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

VI. UKOMO WA MUDA WA URAIS WA JMT

Ukomo wa muda wa Urais wa JMT utazingatia miongozo ifuatayo:

1. Kipindi kimoja cha Urais wa JMT ni miaka mitano tu;

2. Hakuna Rais atakayetumikia mihula zaidi ya miwili hata kama ni kiongozi bora mithili ya malaika.

3. Rais aliyetumikia muhula wa kwanza wa Urais wa JMT atakuwa na sifa ya kugombea katika muhula wa pili endapo katika muhula wa kwanza amefanikiwa kutekeleza majukumu yaliyotajwa katika Hati ya Majukumu ya Urais wa JMT hapo juu kwa wastani wa 51% au zaidi, ambapo “skimu ya uhakiki (marking scheme)” itakayotumika kupima kiwango cha ufanisi wake ni Hati ya Majukumu ya Urais wa JMT kama ilivyotajwa hapo awali katika uzi huu.

VII. MSHAHARA WA RAIS WA JMT

1. Rais wa JMT atalipwa mshahara na malipo mengineyo, na atakapostaafu atapokea malipo ya uzeeni, na kiinua mgongo, kadri itakavyoamuliwa na Bunge.

2. Malipo yote ya Rais wa JMT yatatokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya JMT.

3. Malipo yote ya Rais wa JMT hayatapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya nchi.

VIII. UTARATIBU WA KUPOKEZANA OFISI YA URAIS WA JMT

1. Endapo Rais atakuwa hayupo katika Jamhuri ya Muungano, shuhguli zake zitatekelezwa na mmoja wapo na wafuatao, kwa kufuata orodha kama ilivyopangwa, yaani: (a) Makamu wa Rais au, kama naye hayupo; basi (b) Spika wa Bunge au, kama naye hayupo; basi (c) Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufani ya JMT.

2. Endapo kiti cha Rais wa JMT kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka Rais atapendekeza jina la mtu atakae kuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua asilimia hamsini ya Wabunge wote.

IX. KINGA DHIDI YA MASHATAKA

1. Wakati wote Rais wa JMT atakapokuwa bado ameshika madaraka yake, itakuwa ni marufuku kumshitaki au kuendesha mashataka ya aina yoyote juu yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

2. Wakati wote Rais wa JMT atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye binafsi kama raia wa kawaida ama kabla au baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.

3. Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais wa JMT kutokana na kushitakiwa na kutiwa hatiani kupitia Bungeni, itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba.


X. UTARATIBU WA KUCHAGULIWA KATIKA NAFASI YA URAIS WA JMT

Mtu yeyote anayetaka kugombea nafasi ya Urais wa JMT atachaguliwa kwa kufuata utaratibu ufuatao:

1. Mtangaza nia kutuma maombi kwenye email tzpresidency@gmail.com baada ya kusoma na uelewa maelekezo yote katika uzi huu na kisha kuambatanisha nakala ya wasifu inayoonyesha taarifa zifuatazo: majina yake kamili; jina la chama cha siasa anachotaka kimdhamini; tathmini yake ya serikali ya sasa kwa kuzingatia vipaumbele vya kitaifa vilivyotajwa katika kipengele cha tano (5) kwenye Hati ya Majukumu ya Urais wa JMT hapa kwenye uzi huu; nakala ya cheti cha kuzaliwa; vyeti vya elimu rasmi aliyo nayo; na taarifa nyingine muhimu.

2. Taasisi ya Mama Amon Limited (MAL) kukusanya maombi yote, kuyafomati vizuri bila kuyahariri, kuyachapisha upya kwenye Jukwaa la JamiiForums, na hatimaye kuwaalika wananchi kutoa maoni yao juu ya sifa za waombaji wote kupitia kitufe cha “Reply” katika uzi husika.

3. Taasisi ya MAL kuyachuja mamobi yote, kulingana na maoni ya wananchi, na kubakiza waombaji kumi tu watakaokidhi vigezo vizuri zaidi kwa kila chama cha siasa kitakachokuwa kimetajwa na waombaji;

4. Taasisi ya MAL Kuwasilisha majina kumi bora kwa Makatibu Wakuu wa vyama vya siasa kwa ajili ya mchujo zaidi kwa mujibu wa vikao vya kikatiba ndani ya vyama vya siasa husika;

5. Kuvunjwa kwa Bunge la JMT kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu unaofuata.

6. Baada ya Bunge kuvunjwa, kila chama cha siasa kinachopenda kushiriki katika uchaguzi wa Rais kuwasilisha kwa Tume ya Uchaguzi, kwa mujibu wa sheria, jina la mwanachama wake mmoja kinayetaka asimame kama mgombea katika uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na jina la mwananchama wake mwingine kinayempendekeza kwa nafasi ya Makamu wa Rais.

7. Mapendekezo ya majina ya wagombea katika uchaguzi wa Rais yatawasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi katika siku na saa itakayotajwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na mtu hatakuwa amependekezwa kihalali isipokuwa tu kama kupendekezwa kwake kunaungwa mkono na wananchi wapiga kura kwa idadi na kwa namna itakayotajwa na sheria iliyotungwa na Bunge.

8. Endapo itafika saa na siku iliyotajwa kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya majina ya wagombea, ni mgombea mmoja tu ambaye anapendekezwa kihalali, Tume itawasilisha

jina lake kwa wananchi, nao watapiga kura ya kumkubali au kumkataa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii na ya sheria iliyotungwa na Bunge.

9. Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano utafanywa siku itakayoteuliwa na Tume ya Uchaguzi kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge.

10. Mambo mengine yote yahusuyo utaratibu wa uchaguzi wa Rais yatakuwa kama itakavyofafanuliwa katika sheria iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo.

11. Mgombea yeyote wa kiti cha Rais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa Rais iwapo tu amepata kura nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote.

12. Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.

13. Rais mteule wa JMT atashika madaraka ya Rais mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote itabidi ashike madaraka kabla ya kupita siku saba.

14. Mtu aliyechaguliwa kuwa Rais atashika kiti cha Rais hadi: (a) siku ambapo mtu atakayemfuatia katika kushika kiti hicho atakula kiapo cha Rais; au (b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka; au (c) siku atakapojiuzulu; au (d) siku atakapoacha kushika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti mengine ya Katiba ya katiba ya nchi.

XI. UTARATIBU WA KUTATHMINI UTENDAJI KAZI (PERFORMANCE APPRAISAL) WA RAIS WA JMT

1. Utekelezaji wa majukumu yake Rais wa JMT utaongozwa na vipaumbele vya kitaifa vifuatavyo, ambapo Rais wa JMT atapatiwa ama gredi ya "KUPASI" kama ufanisi ni angalau 50% au gredi ya "KUFELI" kama ufanisi ni chini ya 50% katika muhula husika wa uongozi.

2. Katika kutathmini utendaji wa Rais wa JMT, kila kipaumbele cha kitaifa kitabeba asilimia za juu zilizoonyeshwa kwenye mabano katika orodha hapa chini:

(a) Sekta ya Afya kipengele cha Mama na Mtoto (2%);

(b) Sekta ya Afya kipengele cha Wazee, Walemavu, Yatima na Wajane (2%);

(c) Sekta ya Elimu kipengele cha Elimu ya Msingi (2%);

(d) Sekta ya Elimu kipengele cha Elimu ya Sekondari (2%);

(e) Sekta ya Elimu kipengele cha Elimu ya Juu (2%);

(f) Sekta ya Elimu kipengele cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi (2%)

(g) Sekta ya Mazingira kipengele cha kipengele cha kukabiliana na Madhara ya Mabadiliko ya Tabianchi (2%);

(h) Sekta ya Mazingira kipengele cha kukabiliana na Chimbuko la Mabadiliko ya Tabianchi (2%);

(i) Sekta ya Mazingira kipengele cha ukusanyaji wa taka ngumu katika miji, majiji na manispaa (2%);

(j) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uhuru wa Habari na vyombo vya upashananji habari (2%);

(k) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uhuru wa Kukusanyika hadharani au ukumbini (2%);

(l) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uhuru dhidi ya utekwaji na uteswaji wa raia unaoweza kufanywa na vyombo vya dola dhidi ya raia kinyume cha utaratibu wa kisheria (10%);

(m) Sekta ya Usalama kipengele cha kulinda uhai wa watu dhidi ya vifo holela kinyume cha sheria za nchi (10%); na

(n) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uchaguzi ulio huru, wazi na unaofanyika kwa haki (2%);

(o) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Ujenzi wa Imani ya Jamii ya Kitaifa (National Social Doctrine) kupitia hotuba zinazotolewa na Rais wa JMt katika matukio muhimu ya kitaifa (2%);

(p) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Michezo, Sanaa na Burudani (2%);

(q) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uhuru wa kuabudu (2%);

(r) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uhuru wa Bunge (2%);

(s) Sekta ya Utawala Bora kipengele cha Uhuru wa Mahakama (2%);

(t) Sekta ya Uchumi kipengele cha Usafirishaji kwa njia ya Anga (2%);

(u) Sekta ya Uchumi kipengele cha Usafirishaji kwa njia ya Majini (2%);

(v) Sekta ya Uchumi kipengele cha Usafirishaji kwa njia ya Barabara (2%);

(w) Sekta ya Uchumi kipengele cha Usafirishaji kwa njia ya Reli na Bomba (2%);

(x) Sekta ya Uchumi kipengele cha Mawasiliano ya Simu, Intaneti na Mitandao ya Kijamii (2%);

(y) Sekta ya Uchumi kipengele cha Sayansi, Tekinolojia na Uvumbuzi (2%);

(z) Sekta ya Uchumi kipengele cha Kilimo (2%);

(aa) Sekta ya Uchumi kipengele cha Ufugaji (2%);

(ab) Sekta ya Uchumi kipengele cha Uvuvi (2%);

(ac) Sekta ya Uchumi kipengele cha Mazao ya Misitu (2%);

(ad) Sekta ya Uchumi kipengele cha viwanda (2%);

(ae) Sekta ya Uchumi kipengele cha biashara (2%);

(af) Sekta ya Uchumi kipengele cha utalii (2%);

(ag) Sekta ya Uchumi kipengele cha Nishati (2%);

(ah) Sekta ya Uchumi kipengele cha Madini (2%);

(ai) Sekta ya Jamii kipengele cha Maji (2%)

(aj) Sekta ya Jamii kipengele cha Ajira kwa Vijana (2%);

(ak) Sekta ya jamii kipengele cha ujinsia, ndoa, familia na haki za wanawake (2%);

(al) Sekta ya jamii kipengele cha Mipango miji (2%);

(am) Sekta ya jamii kipengele cha hifadhi ya jamii (2%);

(an) Sekta ya jamii kipengele cha kuhifadhi haki za watu wenye jinsia tata (2%);

(an) Sekta ya Usalama kipengele cha kulinda usalama wa mali za watu (2%);

(ao) Sekta ya Diplomasia kipengele cha Mahusiano ya Kimataifa (2%).

XII. UKOMO WA MUDA WA KUTUMA MAOMBI

Kuna njia mbili za kutuma maombi.

Njia ya kwanza ni kutuma maombi kupitia email ifuatayo: tzpresidency@gmail.com.

Na njia ya pili ni kutumia kitufe cha "Reply" na kisha ku-attach CV yake kupitia uzi huu.

Maombi yote yatumwe kabla ya sikuku ya Saba Saba 2019.

Maombi yote yatakayotumwa baada ya siku hiyo hayatapokelewa na MAL wala kufanyiwa kazi.

Karibuni Watangaza nia wote.
Hongera sana mtangaza nafasi ya kazi kwa ujasiri mkubwa huenda ukapata maombe mengi sana na kuwanyima baadhi ya Watanzania wasio na internet access ya kutuma CV zao.

Tatizo moja la watu wote wanaojidai kuonesha nia ni kukosa maono na wenye maono pia hawajui kuyaunganisha maono yao ni mahitaji wa Watanzania. Na kwa mkakati huo wanafeli mapema hata kabla hawajatoka nje kutangaza nia.
Kwa msingi huo JPM atashinda kiulaini sana 2020-25; na kama ikitokea ili movement ya iliyoanzia China kum-elevate Xi Jing Ping kwenye level ya Mao na kumpa nafasi ya kutawala mpaka achoke, ambayo pia Misri nao wameona bora Field Marshal Asis nae atawale mpaka achoke;

Ujerumani mwaka 2017 hawakuwa na mbadala wa Angela Markel ambae alikaa madarani toka 2005 wakati JK anaingia, mpaka leo yupo na anakidhi mahitaji wa Wajerumani ndiyo maana 2017 ushindi wake haukuwa na chembe ya mashaka.

Kwa msingi huo JPM atashinda maana hana mpinzani ndani ya CCM kwa mujibu wa katiba na tamaduni za CCM. Maana 2020 atakuwa anamaliza dakika ya 45 za first half na utamaduni wa CCM lazima apige 2nd half. Pengine jaribu kutafuta wagombea kwa ajili ya 2025 kabla pengine haijatokea nyongeza ya dakika 30 za ziada ili kujenga mazingira ya kupiga penalty. Waamuzi wa haya ni Watanzania. Tunafahamu kuwa kama msingi wa maendeleo ingekuwa demokrasi kama wanavyotudanganya mabeberu, basi Oman, Bahrain, Qatar, UAE, Saudia na Kuwait wangekuwa choka mbaya kiuchumi. Kule ni mfalme anatawala na maisha yanakwenda. Kwa cultural setting za nchi zetu hizi, masuala ya kuchagua kuna wakati mabeberu wanashiriki sana tu kututafutia vibaraka wao ili waendelee kukwapua rasilimali zetu kwa mikataba kama ya akina Mangungo. Wengi tunakumbuka msomi wa Havard hapahapa kwetu alihusika sana kwenye deals ambazo tumepigwa kwa miaka mingi sana. Yule mzee siju alikuwa recruited kama asset yao. Sijui. Ila matendo aliyoitenda nchi hii kwenye nafasi aliyoikalia kwa miaka zaidi ya 13; tulitendwa jambo baya sana na mali zetu kukwapuliwa huku tunaona mchana kweupe.

Na kwa move iliyopo sasa kuna watu sijui kama nawe uko miongoni mwao wako funded na mabeberu ili kutikisa kiberiti kwa jina la haki za binadamu, uhuru wa kujieleza, wakahamia kwenye bring back mdude, sasa hivi wameibuka na single ya kutoa picha za ma-DED ambao ni makada wa chama tawala.

Tanzania ilimhitaji mtu wa aina ya JPM kushika nchi mara baada ya mwl kung'atuka. Pengine baada ya Edward Moringe kuondoka katika mazingira kama ilivyokuwa imechukua muda kumpata mtu mwenye haiba ya uongozi thabiti wenye nia ya kulinda utu wa Mtanzania na sovereignty yetu sisi Watanzania. Kumpata JPM napo ilikuwa kama bahati, maana kama sio bifu la boyz II men, huenda safari hii hali ingekuwa mbaya baada ya mzawa wa msoga kuachia kijiti.

Suala la msingi ambalo vijana wa JPM wana wajibu wa kufanya kwa sasa ili mzee huyu apate kukaa madarakani kwenye hii transition ya economic war, ni kumsaidia apate watu wenye business IQ ili kusisimua ukuaji wa uchumi mdogomdogo (micro-economic development) ambayo itachangia ukuaji wa uchumi mkubwa.

Jana nimevunjia moyo kumsikia Waziri wa Viwanda kuwataka Watanzania wale korosho kama mbadala wa kuzifanya korosho zimalizike toka kwenye maghala. Hapana jamani. Mhe Rais, tafuta watu wenye kufikiri kimkakati kwa kutumia strategic economic intelligence tool ili korosho iwe moja ya zao linalouzwa ndani na nje ya Tanzania na kuingiza forex za kutosha. Wakati huo kazi endelevu zikiwa zimetengenezwa kwa vijana kuwa na hakika ya mishahara na ikiwezekana wakulima wa korosho kupitia mauzo ya korosho wawe beneficiaries wa bima ya afya. Hili linawezekana kama utakuwa open minded kutumia Watanzania nje ya circle yako. Huenda walikuzunguka either wanakuogopa, au kuna kusudi pia la Mungu ili hata hawa walio nje ya circle yako wapate fursa ya kukupa information mbadala on how to go about. Iliwahi kutokea kwa akina Farao kupata strategic economic intelligence tool ya kukusanya chakula na kuhifadhi miaka 7 ya chakula cha kutosha kwa ajili yao na mataifa ya jirani wakati wa msoto ukija.

Wasaidizi wa JPM, kuweni na ujasiri wa kumsaidia namba moja. Tukianzia kwenye ku-cut down imports in exchange of producing consumable hapa ndani, mbona uchumi utasisimka kwa haraka.

Ushauri wangu wa mwisho, msichukulie poa kuwasikiza layman.
1099926


1099927


Mkifanikiwa kusoma kitabu cha Start-up nation mtakuja kungundua kila mwanadamu ana-treasure ambayo ikiwa harnessed kila mmoja atafaidika. Let's play as a team. Our common enemies are the same and it is high time to get rid of them together.

Mabeberu wanawatumia hawa wenye njaa wachache kwa gharama ya wao waendelee kuvuna na kukwapua rasilimali zetu
 
Ngoja tuafuatilie mjadala. Nimejifunza bonge la elimu hapa kutoka kwa mama Amon. #Yes we Can
 
Hongera sana mtangaza nafasi ya kazi kwa ujasiri mkubwa huenda ukapata maombe mengi sana na kuwanyima baadhi ya Watanzania wasio na internet access ya kutuma CV zao.

Tatizo moja la watu wote wanaojidai kuonesha nia ni kukosa maono na wenye maono pia hawajui kuyaunganisha maono yao ni mahitaji wa Watanzania. Na kwa mkakati huo wanafeli mapema hata kabla hawajatoka nje kutangaza nia.
Kwa msingi huo JPM atashinda kiulaini sana 2020-25; na kama ikitokea ili movement ya iliyoanzia China kum-elevate Xi Jing Ping kwenye level ya Mao na kumpa nafasi ya kutawala mpaka achoke, ambayo pia Misri nao wameona bora Field Marshal Asis nae atawale mpaka achoke;
Ujerumani mwaka 2017 hawakuwa na mbadala wa Angela Markel ambae alikaa madarani toka 2005 wakati JK anaingia, mpaka leo yupo na anakidhi mahitaji wa Wajerumani ndiyo maana 2017 ushindi wake haukuwa na chembe ya mashaka.

Kwa msingi huo JPM atashinda maana hana mpinzani ndani ya CCM kwa mujibu wa katiba na tamaduni za CCM. Maana 2020 atakuwa anamaliza dakika ya 45 za first half na utamaduni wa CCM lazima apige 2nd half. Pengine jaribu kutafuta wagombea kwa ajili ya 2025 kabla pengine haijatokea nyongeza ya dakika 30 za ziada ili kujenga mazingira ya kupiga penalty. Waamuzi wa haya ni Watanzania. Tunafahamu kuwa kama msingi wa maendeleo ingekuwa demokrasi kama wanavyotudanganya mabeberu, basi Oman, Bahrain, Qatar, UAE, Saudia na Kuwait wangekuwa choka mbaya kiuchumi. Kule ni mfalme anatawala na maisha yanakwenda. Kwa cultual setting za nchi zetu hizi, masuala ya kuchagua kuna wakati mabeberu wanashiriki sana tu kututafutia vibaraka wao ili waendelee kukwapua rasilimali zetu kwa mikataba kama ya akina Mangungo. Wengi tunakumbuka msomi wa Havard hapahapa kwetu alihusika sana kwenye deals ambazo tumepigwa kwa miaka mingi sana. Yule mzee siju alikuwa recruited kama asset yao. Sijui. Ila matendo aliyoitenda nchi hii kwenye nafasi aliyoikalia kwa miaka zaidi ya 13; tulitendwa jambo baya sana na mali zetu kukwapuliwa huku tunaona mchana kweupe.

Na kwa move iliyopo sasa kuna watu sijui kama nawe uko miongoni mwao wako funded na mabeberu ili kutikisa kiberiti kwa jina la haki za binadamu, uhuru wa kujieleza, wakahamia kwenye bring back mdude, sasa hivi wameibuka na single ya kutoa picha za ma-DED ambao ni makada wa chama tawala.

Tanzania ilimhitaji mtu wa aina ya JPM kushika nchi mara baada ya mwl kung'atuka. Pengine baada ya Edward Moringe kuondoka katika mazingira kama ilivyokuwa imechukua muda kumpata mtu mwenye haiba ya uongozi thabiti wenye nia ya kulinda utu wa Mtanzania na sovereignty yetu sisi Watanzania. Kumpata JPM napo ilikuwa kama bahatu, maana kama sio bifu la boyz II men, huenda safari hii hali ingekuwa mbaya baada ya mzawa wa msoga kuachia kijiti.

Suala la msingi ambalo vijana wa JPM wana wajibu wa kufanya kwa sasa ili mzee huyu apate kukaa madarakani kwenye hii transition ya economic war, ni kumsaidia apate watu wenye business IQ ili kusisimua ukuaji wa uchumi mdogomdogo (micro-economic development) ambayo itachangia ukuaji wa uchumi mkubwa.

Jana nimevunjia moyo kumsikia Waziri wa Viwanda kuwataka Watanzania wale korosho kama mbadala wa kuzifanya korosho zimalizike toka kwenye maghala. Hapana jamani. Mhe Rais, tafuta watu wenye kufikiri kimkakati kwa kutumia strategic economic intelligence tool ili korosho iwe moja ya zao linalouzwa ndani na nje ya Tanzania na kuingiza forex za kutosha. Wakati huo kazi endelevu zikiwa zimetengenezwa kwa vijana kuwa na hakika ya mishahara na ikiwezekana wakulima wa korosho kupitia mauzo ya korosho wawe beneficiaries wa bima ya afya. Hili linawezekana kama utakuwa open minded kutumia Watanzania nje ya circle yako. Huenda walikuzunguka either wanakuogopa, au kuna kusudi pia la Mungu ili hata hawa walio nje ya circle yako wapate fursa ya kukupa information mbadala on how to go about. Iliwahi kutokea kwa akina Farao kupata strategic economic intelligence tool ya kukusanya chakula na kuhifadhi miaka 7 ya chakula cha kutosha kwa ajili yao na mataifa ya jirani wakati wa msoto ukija.

Wasaidizi wa JPM, kuweni na ujasiri wa kumsaidia namba moja. Tukianzia kwenye ku-cut down imports in exchange of producing consumable hapa ndani, mbona uchumi utasisimka kwa haraka.

Ushauri wangu wa mwisho, msichukulie poa kuwasikiza layman.
View attachment 1099926

View attachment 1099927

Mkifanikiwa kusoma kitabu cha Start-up nation mtakuja kungundua kila mwanadamu ana-treasure ambayo ikiwa harnessed kila mmoja atafaidika. Let's play as a team. Our common enemies are the same and it is high time to get rid of them together.

Mabeberu wanawatumia hawa wenye njaa wachache kwa gharama ya wao waendelee kuvuna na kukwapua rasilimali zetu
Atakae pinga hii mchawi
 
Back
Top Bottom