Tangazo La Dharura: Hali Mbaya Ya Mgonjwa, Mtanzania Mwenzetu.

Status
Not open for further replies.
Apr 27, 2006
26,588
10,364
- Wakuu wote hapa na ndugu zangu, kwa masikitiko makubwa sana ninaomba kuwafahamisha up-todates, za mgonjwa ndugu yetu Sister Pendo Magaluda ambaye amekuwa akisumbuliwa sana na ugonjwa wa Breast Cancer, habari ambazo ziliwahi kutolewa huko nyuma kwenye chombo cha habari cha Brother Michuzi.

- Since then, ndugu yetu mpendwa Sister Pendo, amekuwa akipata nafuu na kuzidiwa pia, lakini recently hali yake imekua sio nzuri sana kwa wale mnaofahamu vizuri madhara ya ugonjwa huu hatari ninaamini kuwa mnaelewa ninachokisema. Baada ya kutibiwa sana between USA, Tanzania, South Africa, na back tena to New York City, USA, Pendo alihamishiwa katika Hospitali ya kitongoji cha Rochester, yaani Up-Sate New York umbali wa maili 350 kutoka NYC.

- Ninamfahamu Sister Pendo, na mumewe Abel na watoto wao wadogo watatu wa kiume, mkubwa mwenye umri wa miaka 11, anayemfuatia miaka 9 na mdogo mwenye miaka 4 na wote wa kiume, na hii familia nzima wako pamoja huko Hospitali Rochester. Betweeen kumhudumia mkewe na watoto katika hiki kipindi kigumu sana kifamilia, ndugu yangu Abel ilibidi aache kazi na ku-dedicate muda wake wote kumuuguza mkewe, ninamuombea nguvu zaidi na busara za Mwenyezi Mungu zimtangulie mbele ili asikate tamaa.

- Sasa ndugu zangu kama kawaida yetu bina-adam, kusaidiana kwa hali na mali na hasa katika kipindi cha matatizo kama hiki kwa hawa ndugu zetu, ambao kwa kweli bado ni vijana sana in their 30s, ambao walikuwa huko US kwa ajili ya masomo na matibabu pia. Hivi ninapoandika nipo njiani nikielekea huko Rochester kwenda kuwaona na kutathmini kwa karibu hali halisi, ninawaomba tena ndugu zangu kwamba kwa yoyote mwenye kujaaliwa na Mwenyezi Mungu kuwa na uwezo wa msaada wa aina yoyote ile, kuwasaidia hawa ndugu zetu, unaweza kutuma kwenye:-

-Checking Account # 526-410-230, benki ya HSBC, kwa kutumia majina ya Pendo au Abel Magaluda

- Kwa yoyote mwenye maswali zaidi, tafadhali tuwasiliane kwenye PM, na pia kwa wale walioko karibu na huo mji wa Rochester, ndugu zetu wako kwenye Hospital ya Rochester University unaweza kuwapata kwenye namba ya simu 1-585-414-1481, kutokana na pilika pilika walizonazo, sio rahisi kuwapata kwa mara moja kwa hiyo tafadhali jaribu kuacha ujumbe ikibidi na watakujibu baadaye.

Ninaomba kuchukua fursa hii kuwashukuru wale wote ambao wamekua wakiwasaidia ndugu zetu kwa muda sasa, na pia kwa wale wote walionipatia misaada mbali mbali mzito ya kuwafikishia huko ninakokwenda kuwaona, na ninategemea kuwepo nao huko kwa siku mbili zijazo, Mungu awabariki na awazidishie zaidi.

Samahani sana wana-JF, na hasa Mods kwa kuiweka hapa hii ni kwa sababu tu ya udharura wa hali halisi, lakini mnaweza kuipeleka inapotakiwa ikibidi.

FMES.
 
- Wakuu wote hapa na ndugu zangu, kwa masikitiko makubwa sana ninaomba kuwafahamisha up-todates, za mgonjwa ndugu yetu Sister Pendo Magaluda ambaye amekuwa akisumbuliwa sana na ugonjwa wa Breast Cancer, habari ambazo ziliwahi kutolewa huko nyuma kwenye chombo cha habari cha Brother Michuzi.

- Since then, ndugu yetu mpendwa Sister Pendo, amekuwa akipata nafuu na kuzidiwa pia, lakini recently hali yake imekua sio nzuri sana kwa wale mnaofahamu vizuri madhara ya ugonjwa huu hatari ninaamini kuwa mnaelewa ninachokisema. Baada ya kutibiwa sana between USA, Tanzania, South Africa, na back tena to New York City, USA, Pendo alihamishiwa katika Hospitali ya kitongoji cha Rochester, yaani Up-Sate New York umbali wa maili 350 kutoka NYC.

- Ninamfahamu Sister Pendo, na mumewe Abel na watoto wao wadogo watatu wa kiume, mkubwa mwenye umri wa miaka 11, anayemfuatia miaka 9 na mdogo mwenye miaka 4 na wote wa kiume, na hii familia nzima wako pamoja huko Hospitali Rochester. Betweeen kumhudumia mkewe na watoto katika hiki kipindi kigumu sana kifamilia, ndugu yangu Abel ilibidi aache kazi na ku-dedicate muda wake wote kumuuguza mkewe, ninamuombea nguvu zaidi na busara za Mwenyezi Mungu zimtangulie mbele ili asikate tamaa.

- Sasa ndugu zangu kama kawaida yetu bina-adam, kusaidiana kwa hali na mali na hasa katika kipindi cha matatizo kama hiki kwa hawa ndugu zetu, ambao kwa kweli bado ni vijana sana in their 30s, ambao walikuwa huko US kwa ajili ya masomo na matibabu pia. Hivi ninapoandika nipo njiani nikielekea huko Rochester kwenda kuwaona na kutathmini kwa karibu hali halisi, ninawaomba tena ndugu zangu kwamba kwa yoyote mwenye kujaaliwa na Mwenyezi Mungu kuwa na uwezo wa msaada wa aina yoyote ile, kuwasaidia hawa ndugu zetu, unaweza kutuma kwenye:-

-Checking Account # 526-410-230, benki ya HSBC, kwa kutumia majina ya Pendo au Abel Magaluda

- Kwa yoyote mwenye maswali zaidi, tafadhali tuwasiliane kwenye PM, na pia kwa wale walioko karibu na huo mji wa Rochester, ndugu zetu wako kwenye Hospital ya Rochester University unaweza kuwapata kwenye namba ya simu 1-585-414-1481, kutokana na pilika pilika walizonazo, sio rahisi kuwapata kwa mara moja kwa hiyo tafadhali jaribu kuacha ujumbe ikibidi na watakujibu baadaye.

Ninaomba kuchukua fursa hii kuwashukuru wale wote ambao wamekua wakiwasaidia ndugu zetu kwa muda sasa, na pia kwa wale wote walionipatia misaada mbali mbali mzito ya kuwafikishia huko ninakokwenda kuwaona, na ninategemea kuwepo nao huko kwa siku mbili zijazo, Mungu awabariki na awazidishie zaidi.

Samahani sana wana-JF, na hasa Mods kwa kuiweka hapa hii ni kwa sababu tu ya udharura wa hali halisi, lakini mnaweza kuipeleka inapotakiwa ikibidi.

FMES.

Pole sana mkuu kwa kuuguliwa na hao wapendwa wetu. Mwenyezi Mungu awajaze nguvu na neema zake mgonjwa apone haraka.

Tuko pamoja katika sara zetu.

Wengine tuko huku mbali mikoani lakini I hope wenye uwezo ambao wako karibu wanaweza kusaidia chochote.

Once again poleni sana na Mungu mwenye rehema awape nguvu za kumuuguza dada yetu na amponye na huo ugonjwa.

Masanja,
 
Friends in need is a friend indeed. Hapa ndipo haswa ninapoipa heshima ya pekee JF. Member wa JF tunaungana na kuunganisha nguvu na sala zetu pamoja to wish Pendo a speedy recovery.

Asante FMES, Tuko pamoja waiting for more update.
BWANA akutangulie, na kusimamia uponyaji.
Kwa YEYE, yote yanawezekana.
 
Ni maombi yangu kwa Molla mgonjwa apate ahueni na kurejea afya njema. Amina.

SteveD.
 
Ni maombi yangu kwa Molla mgonjwa apate ahueni na kurejea afya njema. Amina.

SteveD.

Mkuu mbona siku hizi unapotea sana? zamani nilijua ni kwa sababu umeme unaleta shida huko Malampaka kama kwetu Kwimba..sasa mwenzangu naona siku hizi uko Mysore India..na huko kuna shida ya umeme? au ilikuwa ni pilika pilika za kuhama ;-)

Anyway...Its good to see you once again....

Weekend njema,

Masanja
 
namuombea mgonwja apate nafuu na kupona haraka. familia ipate nguvu ya kuyashinda majaribu wanayokabiliana nayo kwa sasa-amen
 
- Shukrani wakuu kwa sala na salam, sasa hivi nipo Hospitali na mgonjwa tayari nimemuona baada ya ku-pick up gari NYC na kuendesha usiku kucha kuweza kufika hapa, kwa kweli hali kama nilkivyosema huko nyuma sio njema kabisa, again ninasema shukrani kwa sister kutoka Adis Ethiopia kwa msaada wako mzito wa dola $ 500 za US,

- Pia natoa shukrani nzito kwa Mama Migiro, kwa msaada wako na ushirikiano mkubwa on this situation na ofisi yetu ya ubalozi wa New York, na hasa Sister Rose Mkapa, na wengine wote maofisa wa ubalozi wetu huu kwa misaada yenu mbali mbali, Mungu awabariki wote,

NDUGU ZANGU KABLA HATUJAFA HATUJAUMBWA, JUST THINK ABOUT IT.
 
Mwenyezi Mungu awasaidie katika kipindi hiki kigumu kwa familia hiyo na pia ampe nafuu mgonjwa dhidi ya ugonjwa unaomkabili.
 

-Checking Account # 526-410-230, benki ya HSBC, kwa kutumia majina ya Pendo au Abel Magaluda
FMES.

Ndugu zangu acheni kuyeyusha, mshapewa account namba hapo juu lakini mmeng'ang'ana na kumuombea kwa Mungu amsaidie! kinachotakiwa hapa ni hela, maombi yenu mnaweza kuyafanya kivyenuvyenu kimyakimya bila hata kuyaleta hapa.
 
Ndugu zangu acheni kuyeyusha, mshapewa account namba hapo juu lakini mmeng'ang'ana na kumuombea kwa Mungu amsaidie! kinachotakiwa hapa ni hela, maombi yenu mnaweza kuyafanya kivyenuvyenu kimyakimya bila hata kuyaleta hapa.

Mtu akituma fedha au msaada wowote kwa mlengwa si lazima atangaze hapa. Nakushangaa Mkuu K-K-N kuweka ujumbe kama huu hapa. watu wanaweza toa pole na salamu hapa na si lazima waeleze wanafanya nini Behind The Scene.
 
Sijasema kuwa mtu akitoa mchango atangaze hapa, nilitegemea kuona kauli nyingi za "ntarekebisha kesho mkuu" au "angalio salio mkuu" na sio "Mungu amsaidie" kwa sana. FEMEs ametoa account namba hapa na ni wazi nini kinahitajika, wanaotaka kumtumia mgonjwa salamu watafute address ya hospitali wamtumie kadi, tuache longolongo jamani.
 
- Ndugu zangu Wa-Tanzania wenzangu wote kwa hapa sasa ni saa za jioni ni baridi isiyokua mfano, nipo nyumbani kwa familia ya mgonjwa sister wetu Pendo, after a very long day ndio kwanza tumemaliza kufanya shughuli za shopping kwa ajili ya familia hii kujitayarisha kurudi nyumbani next week kama itawezekana kutokana na kibali cha madakitari kwa ajili ya kuweza ku-board kwenye ndege, ninasema iwapo itawezekana maana inategemea majaliwa na Mungu.

- Again hali ya mgonjwa sio nzuri na haina unafuu kabisaa, toka asubuhi imekua in and out between nyumbani na Hospitali, na hapa nipo na watoto wadogo watatu wa mgonjwa ambao kwa kweli kama mnavyojua malaika wa Mungu, hawana habari kabisa na kinachoendelea, wao wanachojali ni kukutana na watoto wangu na mchezo mpaka lyamba, lakini nimefarijika na mume wa mgonjwa kutokana na moyo wa ujasiri alionao na kuweza kukubali reality as it is. Na pi animefarijika na wana-JF walioitika mwito, again proud to be Mwana-JF, maana tupo kila mahali.

- Again ahsante kwa kila kitu hasa misaada, ninaomba ndugu zangu tuzidishiwe na Mungu wetu wa maajabu ili tuweze kuwasaidia ndugu zetu hawa wapendwa, shukrani kwa wote popote mlipo, sasa hivi ninarudi tena Hospitali kabla ya kuanza kujitayarisha na safari tena. Shukrani kwa wote na tuzidi kuwa na moyo wa upendo wa kusaidiana.

Ahsanteni na Baadaye!
 
FMES,
Mkuu kwanza shukran kwa taarifa hii, nadhani tumewahi kuzungumza siku za nyuma..Itakuwa vizuri sana kama unaweza kufuatilia mawazo ya Zakumi...tupo pamoja katika kila la kheri..
 
Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita nimepoteza ndugu watatu kwa tatizo la namna hiyo; kweli inakatisha tamaa sana kwa ndugu wa karibu wa mgonjwa hasa kwa vile mgonjwa mwenyewe anakuwa anapata maumivu makali sana yanayomfanya kuwa analalama muda mwingi na hivyo kuwafanya ndugu nao waumie sana

Natoa pole sana kwa mgonjwa na wote waliokaribu naye kwa vile katika kipindi hiki wana wakati mgumu sana.

FMES,

Account ya Benki inasaidia tu kwa wale ammbao wanaweza kupata muda wa kukimbia kwenye benki zao na kutuma wire; siyo benki nyingi zinazoruhusu kutuma wire online. Hivyo, wengine ambao wanakuwa kibaruani muda mrefu wanaweza kuchelewa kutuma michango yao. Ningeshauri uweke taratibu mbadala za utumaji pesa kama vile Paypal, Westernunion, Moneygram na njia nyingezo zinazoweza kutumiwa baada ya saa za kazi.
 
Dada Pendo, Mungu akuzidishie nguvu na kwa wale tunaoamini katika miujiza yake Muumba kwa pamoja, Bwana aweze kutenda Muujiza katika afya yake Dada pendo. Nakukumbuka sana tulipokuna ukiwa na watoto wako watatu wadogo wakati tukishughulikia wote Viza, Nyumbani Tanzania.

Naomba Mungu atende Muujiza wake. Mungu amjalie Mumeo nguvu ya kusimama na kutokata tamaa.

Kwa jina la Bwana, naamini Bwana muumba wetu atatenda muujiza.

Amen
 
I am sorry labda nimeona vibaya au miwani yangu imeharibika. ACC OK. I did not see is the sort code. Ta
 
Mkuu Zakumi, Bob na Kichuguu,

- Nimewasikia kuhusu maoni yenu on paypal na moneygram, naomba mnipe muda kidogo on that, lakini kwa wengine wote mnaoweza tafadhali ni kutuma tukwenye hiyo account.

- Now naomba tena niikweke hii ishu inapotakiwa, ni kwamba hali ya mgonjwa imekua haina unafuu kabisa, kwa hiyo uamuzi umekua ni kujaribu kumfikisha nyumbani Tanzania na hasa kwao Mwanza. Mume na watoto wanazo return tickets za ndege kwa hiyo sio tatizo kwao nauli.

- Tatizo liko kwa tickets za mgonjwa, kwa sababu shirika la ndege lina utaratibu wake, kama litakubali kumchukua alivyo sasa, safari itakuwa anytime kuanzia Jumatatu kuna fomu moja inayotakiwa kukukubaliwa nao, baada ya kua approved na madakitari kwamba it si okay kumchukua na kumsafirisha. Hilo linaendelea kwa kasi kubwa sana likisukumwa na Sister Rose Mkapa wa ubalozi wetu NY Mungu ambariki sana.

- Shirika la ndege wameshafahamisha kwamba ili wamchukue na kumsafirisha, basi itabidi awe katika machela yake na hivyo kuwapeleka wao kuondoa viti sita vya abiria ili waweze ku-fit machela ya mgonjwa, sasa ni lazima hivi viti sita vilipiwe kama vilivyo, I mean kwa ajili ya abiria sita mgonjwa anayo return moja kwa hiyo kuna kulipia extra five seats. Hapa ndio penye a real ishu inayonifanya niwaombe ndugu zangu ku-chip in kwa chochote kile.

Again, familia inatoa shukrani kwa misaada na sala zetu, na pia binafsi bado ninaomba niwashukuru sana wote waliokwisha itikia wito kati ya juzi na jana, na leo pia, na wale wote walionikabidhi misaada, yote ilifika.

Otherwise, heshima zangu kwa wote na tutanguliwe na Mungu ili kuweza kuisaidia hii familia ya ndugu yetu Sister Pendo, ambaye ni hivi karibuni tu alimaliza Masters ya Accounts, huko Universty of Rochester.

Mungu Aibariki Tanzania.
 
Mkuu Zakumi, Bob na Kichuguu,

- Nimewasikia kuhusu maoni yenu on paypal na moneygram, naomba mnipe muda kidogo on that, lakini kwa wengine wote mnaoweza tafadhali ni kutuma tukwenye hiyo account.

- Now naomba tena niikweke hii ishu inapotakiwa, ni kwamba hali ya mgonjwa imekua haina unafuu kabisa, kwa hiyo uamuzi umekua ni kujaribu kumfikisha nyumbani Tanzania na hasa kwao Mwanza. Mume na watoto wanazo return tickets za ndege kwa hiyo sio tatizo kwao nauli.

- Tatizo liko kwa tickets za mgonjwa, kwa sababu shirika la ndege lina utaratibu wake, kama litakubali kumchukua alivyo sasa, safari itakuwa anytime kuanzia Jumatatu kuna fomu moja inayotakiwa kukukubaliwa nao, baada ya kua approved na madakitari kwamba it si okay kumchukua na kumsafirisha. Hilo linaendelea kwa kasi kubwa sana likisukumwa na Sister Rose Mkapa wa ubalozi wetu NY Mungu ambariki sana.

- Shirika la ndege wameshafahamisha kwamba ili wamchukue na kumsafirisha, basi itabidi awe katika machela yake na hivyo kuwapeleka wao kuondoa viti sita vya abiria ili waweze ku-fit machela ya mgonjwa, sasa ni lazima hivi viti sita vilipiwe kama vilivyo, I mean kwa ajili ya abiria sita mgonjwa anayo return moja kwa hiyo kuna kulipia extra five seats. Hapa ndio penye a real ishu inayonifanya niwaombe ndugu zangu ku-chip in kwa chochote kile.

Again, familia inatoa shukrani kwa misaada na sala zetu, na pia binafsi bado ninaomba niwashukuru sana wote waliokwisha itikia wito kati ya juzi na jana, na leo pia, na wale wote walionikabidhi misaada, yote ilifika.

Otherwise, heshima zangu kwa wote na tutanguliwe na Mungu ili kuweza kuisaidia hii familia ya ndugu yetu Sister Pendo, ambaye ni hivi karibuni tu alimaliza Masters ya Accounts, huko Universty of Rochester.

Mungu Aibariki Tanzania.
Poleni sanana Pole kwa familia.
FMES!
Tafadahali weka hata adress yao hapa ili iwe rahisikutuma kwa westunion,moneyorder na njia nyingine.Tukiwa na adress ni rahisi, weka adress yao tafadhali.
 
Status
Not open for further replies.
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom