Msambichaka Mkinga
JF-Expert Member
- Oct 22, 2015
- 1,649
- 2,911
Maendeleo ya nchi yoyote na hata mtu binafsi ni mabadiliko chanya ya wakati husika, ukilinganisha na ilivyokuwa kabla ya kipindi kinachofanyiwa tathmini. Maendeleo kwa Taifa, huangalia uchumi (wa nchi na wananchi wake), demokrasia, haki na uhuru (huangaliwa sheria, mifumo na utekelezaji wake).
Tanganyika ilifanya uchaguzi wake wa kwanza kuwapata wajumbe wa Legislative council (sawa na Bunge la leo) mwaka 1958 kule Tabora. Uchaguzi ule, kwa jina maarufu, uliitwa uchaguzi wa Kura Tatu. Uliitwa uchaguzi wa Kura Tatu, kwa sababu kila mjumbe alitakiwa kupiga kura 3. Alitakiwa kumpigia kura mgombea mzungu, mhindi na mwafrika.
Ili kuhakikisha, wanapatikana wajumbe wanaofaa kuingia kwenye hilo Bunge la mwanzo, kwanza kuliwekwa sifa za mtu anayeruhusiwa kupiga kura:
1) Asiwe anayeweza kuhongwa au kuhongeka kiurahisi (maana yake asiuze kura). Hivyo ni lazima awe na kipato kisichopungua pauni 400 kwa mwaka.
2) Awe ni mtu mwenye uelewa wa kumtambua mgombea mwenye uwezo, anayeweza kuwakilisha vizuri. Hivyo mjumbe wa kupiga kura alitakiwa kuwa na elimu siyo chini ya darasa la 12.
3) Awe ni mtu ambaye hawezi kuhongwa kwa ahadi ya kutafutiwa kazi kama mgombea atakayempigia kura akachaguliwa. Hivyo mjumbe wa kupiga kura lazima awe na ajira rasmi. Maana yake asiwe mbangaizaji.
Kwa kutazama sifa za wajumbe wa kupiga kura, unaweza kuona kukikwa na ubaguzi wa aina fulani. Lakini kwa upande mwingine ni kwamba ulikuwa ni ubaguzi wenye dhamira njema. Ni ubaguzi uliolenga kuwapata wawakilishi wanaofaa kwa sababu anayewachagua ana uelewa wa kutosha. Leo tuna wapiga kura wanaohongwa mpaka kilo ya sukari, ubwabwa, sh 5,000, na wengine kudanganywa kuwa mgombea akichaguliwa atamtafutia kazi. Leo tuna wapiga kura ambao hawajui hata kusoma na kuandika lakini tunaamini wana uwezo wa kutambua kuwa mgombea fulani anafaa kuwa Rais au hafai!
Jambo la pili ni kwamba uchaguzi uliangalia uwakilishi wa makundi ya kijamii, kuhakikisha hakuna jamii inayoachwa kwenye uongozi. Unaweza kusema uchaguzi ulipalilia kuimarika kwa makundi ya kijamii na pengine kujenga fikra za ubaguzi wa rangi. Lakini leo, tuna ubaguzi ulio mbaya zaidi kuliko huu uchaguzi ulioendeshwa na mkoloni. Leo, kiuhalisia, ili ushiriki uongozi, ni lazima uwe mwanaCCM. Ukiwa wa chama kingine, halafu unataka kuwa kiongozi, utatengenezwa kila aina ya mizengwe na tuhuma mbaya za ajabu. Utabambikiwa kesi za uchochezi (Sugu, Lisu, Mdee, Mbowe, Zito, n.k.), wote wamewahi kubambikiwa kesi na baadaye mahakama kuthibitisha kuwa ni uwongo, na walionewa. Utabambikiwa kesi za madawa ya kulevya (Mbowe na Lisu ni mfano mzuri), kesi za ugaidi (sote tunajua). Wapo wagombea wa vyama vya uoinzani waliowahi kushambuliwa na kujeruhiwa wakati wa vipindi vya uchaguzi. Yote hiyo, indirectly ni kuambiwa hawatakiwi kushiriki kwenye uongozi. Kwa taswira hii, na kwa vigezo vya ushahidi uliopo, ina maana mkoloni mwingereza alikuwa na unafuu katika kuheshimu misingi ya demokrasia kuliko watawala wa leo ambao ni waafrika wenzetu na waafrika wenzetu.
Kwa kumbukumbu zilizopo, hakuna mgombea aliyeenguliwa na Tume ya uchaguzi mwaka 1958. Hakuna aliyepita bila kupingwa. Chaguzi za Tanzania ya leo, ni vituko, ni uchafu, ni vurumai, ni matukio ya aibu na yanayotia kinyaa kwa watu wastaarabu, wenye akili na utashi wa kibinadamu. Tume ya Mahera ilichofanya mwaka 2020, ni maajabu ya Dunia. Hakuna nchi yoyote Duniani iliyowahi kufanya uchafu wa kiwango hicho kwenye uchaguzi. Tume ya uchaguzi ya Mahera iliengua zaidi ya 50% ya wagombea wote kutoka vyama vya upinzani. Tamisemi chini ya Jafo, iliengua zaidi ya 90% ya wagombea wote kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa na vijiji. Halafu mtu bila aibu wala kinyaa, anasimama na kusema chama tawala kimepata ushindi wa kishindo. Yaani mambo ya aibu ndiyo kwayo tunasimama kujivunia na kutamba.
Kufanya matukio yanayofanyika hapa Tanzania kwenye demokrasia na haki , kwa kuzingatia mifano michache niliyoitoa, ni lazima uwe ni mtu uliyekosa ustaarabu wa kibinadamu, lazima uwe na roho ya kiharamia, lazima uwe mbumbumbu usiyejua Dunia inaenda wapi, lazima uwe ni mtu ambaye huna uzalendo kwa Tanzania na Watanzania wenzako, lazima uwe na chuki kubwa dhidi ya Watanzania wenzako.
Kwa ujumla, Taifa letu, japo watu wanafikiri tunaenda mbele, kiuhalisia kwenye maeneo mengi tumerudi nyuma:
1) kwenye demokrasia tumeporomoka ajabu. Mifano imetolewa
2) kwenye viwanda tumeporomoka. Miaka ya nyuma tulikuwa tunaunganisha malori aina ya scania pale Kibaha, leo hatuunganishi gari lolote. Tulikuwa tunaunganisha matrekta imara na ya ubora wa hali ya juu, matrekta ya Valmet, hatuunganishi hata trekta moja. Wanunuzi wa magari, zamani, karibia wote walikuwa wanaagiza magari mapya, leo karibia wote wanaonunua magari used. Zamani kuvaa nguo ya mtumba (ilikuwa inaitwa kafaulaya) ilikuwa ni aibu, leo ni ufahari. Zamani ufahari ilikuwa ni kuvaa kitenge na kanga bora zilizotengenezwa Tanzania, ukiwa na hela pungufu unavaa kanga ya India au China (za ubora duni), leo kuna bidhaa ambazo kiubora unaweza kuita takataka, kutoka China zimezagaa kila mahali. Kulikuwa na kiatu 100% leather cha Bora Shoes, leo tuna plastic za China kila mahali, halafu tunaamini kuwa tumeendelea.
3) kwenye uongozi, ndiyo balaa kabisa. Zamani ukimsikia mtu ni kiongozi, kweli ni kiongozi hasa, kuanzia haiba yake, uelewa, akili na maadili. Ukisikia DC au RC, unajua ni mtu mweledi hasa, leo tuna mpaka majambazi ni maDC, na wala sina shaka mpaka maRC, maWaziri, watakuwepo. Leo tuna maDC, maRC, maWaziri, ambao kazi yao kubwa ni kumsifia Rais. Zamani, ukisikia kesi ipo kwa Jaji, basi unajua haki itatendeka. Nani leo wa kumlinganisha na Jaji Lugakingira, Nyalali, Samatta, Augustino Ramadhani, n.k. Hawa walikuwa ni wajuzi wa sheria, wenye maadili na weledi wa hali ya juu. Kila mtu alikuwa akisikia majina yao, anataka kusikia kitakachotoka vinywani mwao. Bungeni huko, ilikuwa ukisikia Spika leo ataongea, unarekebisha ratiba yako ili usikose kusikia Spika atasema nini. Leo, wapo watakaozima TV au tu hawana hata muda wa kusikiliza kwa maana wanajua kuwa Spika zaidi ataongelea kuwasuta watu badala ya kuelezea weledi wa taasisi yake. Jaji Mkuu, alikuwa Jaji mkuu hasa. Leo unasikia Jaji mkuu akiwaagiza majaji eti wahukumu kwa kuangalia mihimili mingine inataka nini!aana yake nini? Yaani wasiangalie sheria wala misingi ya haki, bali waangalie mihimili mingine inataka nini? Maajabu makubwa!
Leo hata ile miiko ya kimaadili haipo. Majaji wanapandishwa vyeo katikati ya kesi, kesi ambayo serikali ndiyo mlalamikaji. Mlalamikaji anampandisha cheo jaji anayesikiliza kesi yake. Siyo ajabu, siku hizi mtu akiwa na kesi, haijalishi ana haki au hana, unasikia ndugu wanasema, wachangishane ili wakamwone hakimu. Na inaonekana ni jambo la kawaida.
Kama Taifa, tunapoelekea kwenye kumbukumbu ya Uhuru wa Tanganyika, tunastahili kujitafakari tunakoenda. Mungu alitupendelea, akatupatia rasilimali nyingi, tulichokosa, kwa uhakika wa 100%, ni uongozi wenye maono, uongozi unatoa njia ili watu watembee kwenye njia zilulizo sahihi. Njia za ubunifu, njia za haki, njia za demokrasia sahihi na utawala/uongozi shirikishi.
Ukiwa kiongozi haina maana una akili kuliko watu wote, una uwezo kuliko watu wote, una maono kuliko watu wote. Utambue kuwa nje ya utawala na nje ya Serikali, kuna watu kila nyanja, wapo wanaokuzidi. Kazi yako kubwa ni kutengeneza uwanja wezeshi ili hawa watu wenye uwezo mbalimbali, fani mbalimbali, vipaji na karama mbalimbali, waweze kuutumia uwanja huo kuchangia maendeleo ya jamii na Taifa. Kama hili litaendelea kutofanyiwa kazi, Tanzania, kila wakati tutakuwa watu wa kuongelea namna mataifa mengine yalivyofanikiwa.
Tanganyika ilifanya uchaguzi wake wa kwanza kuwapata wajumbe wa Legislative council (sawa na Bunge la leo) mwaka 1958 kule Tabora. Uchaguzi ule, kwa jina maarufu, uliitwa uchaguzi wa Kura Tatu. Uliitwa uchaguzi wa Kura Tatu, kwa sababu kila mjumbe alitakiwa kupiga kura 3. Alitakiwa kumpigia kura mgombea mzungu, mhindi na mwafrika.
Ili kuhakikisha, wanapatikana wajumbe wanaofaa kuingia kwenye hilo Bunge la mwanzo, kwanza kuliwekwa sifa za mtu anayeruhusiwa kupiga kura:
1) Asiwe anayeweza kuhongwa au kuhongeka kiurahisi (maana yake asiuze kura). Hivyo ni lazima awe na kipato kisichopungua pauni 400 kwa mwaka.
2) Awe ni mtu mwenye uelewa wa kumtambua mgombea mwenye uwezo, anayeweza kuwakilisha vizuri. Hivyo mjumbe wa kupiga kura alitakiwa kuwa na elimu siyo chini ya darasa la 12.
3) Awe ni mtu ambaye hawezi kuhongwa kwa ahadi ya kutafutiwa kazi kama mgombea atakayempigia kura akachaguliwa. Hivyo mjumbe wa kupiga kura lazima awe na ajira rasmi. Maana yake asiwe mbangaizaji.
Kwa kutazama sifa za wajumbe wa kupiga kura, unaweza kuona kukikwa na ubaguzi wa aina fulani. Lakini kwa upande mwingine ni kwamba ulikuwa ni ubaguzi wenye dhamira njema. Ni ubaguzi uliolenga kuwapata wawakilishi wanaofaa kwa sababu anayewachagua ana uelewa wa kutosha. Leo tuna wapiga kura wanaohongwa mpaka kilo ya sukari, ubwabwa, sh 5,000, na wengine kudanganywa kuwa mgombea akichaguliwa atamtafutia kazi. Leo tuna wapiga kura ambao hawajui hata kusoma na kuandika lakini tunaamini wana uwezo wa kutambua kuwa mgombea fulani anafaa kuwa Rais au hafai!
Jambo la pili ni kwamba uchaguzi uliangalia uwakilishi wa makundi ya kijamii, kuhakikisha hakuna jamii inayoachwa kwenye uongozi. Unaweza kusema uchaguzi ulipalilia kuimarika kwa makundi ya kijamii na pengine kujenga fikra za ubaguzi wa rangi. Lakini leo, tuna ubaguzi ulio mbaya zaidi kuliko huu uchaguzi ulioendeshwa na mkoloni. Leo, kiuhalisia, ili ushiriki uongozi, ni lazima uwe mwanaCCM. Ukiwa wa chama kingine, halafu unataka kuwa kiongozi, utatengenezwa kila aina ya mizengwe na tuhuma mbaya za ajabu. Utabambikiwa kesi za uchochezi (Sugu, Lisu, Mdee, Mbowe, Zito, n.k.), wote wamewahi kubambikiwa kesi na baadaye mahakama kuthibitisha kuwa ni uwongo, na walionewa. Utabambikiwa kesi za madawa ya kulevya (Mbowe na Lisu ni mfano mzuri), kesi za ugaidi (sote tunajua). Wapo wagombea wa vyama vya uoinzani waliowahi kushambuliwa na kujeruhiwa wakati wa vipindi vya uchaguzi. Yote hiyo, indirectly ni kuambiwa hawatakiwi kushiriki kwenye uongozi. Kwa taswira hii, na kwa vigezo vya ushahidi uliopo, ina maana mkoloni mwingereza alikuwa na unafuu katika kuheshimu misingi ya demokrasia kuliko watawala wa leo ambao ni waafrika wenzetu na waafrika wenzetu.
Kwa kumbukumbu zilizopo, hakuna mgombea aliyeenguliwa na Tume ya uchaguzi mwaka 1958. Hakuna aliyepita bila kupingwa. Chaguzi za Tanzania ya leo, ni vituko, ni uchafu, ni vurumai, ni matukio ya aibu na yanayotia kinyaa kwa watu wastaarabu, wenye akili na utashi wa kibinadamu. Tume ya Mahera ilichofanya mwaka 2020, ni maajabu ya Dunia. Hakuna nchi yoyote Duniani iliyowahi kufanya uchafu wa kiwango hicho kwenye uchaguzi. Tume ya uchaguzi ya Mahera iliengua zaidi ya 50% ya wagombea wote kutoka vyama vya upinzani. Tamisemi chini ya Jafo, iliengua zaidi ya 90% ya wagombea wote kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa na vijiji. Halafu mtu bila aibu wala kinyaa, anasimama na kusema chama tawala kimepata ushindi wa kishindo. Yaani mambo ya aibu ndiyo kwayo tunasimama kujivunia na kutamba.
Kufanya matukio yanayofanyika hapa Tanzania kwenye demokrasia na haki , kwa kuzingatia mifano michache niliyoitoa, ni lazima uwe ni mtu uliyekosa ustaarabu wa kibinadamu, lazima uwe na roho ya kiharamia, lazima uwe mbumbumbu usiyejua Dunia inaenda wapi, lazima uwe ni mtu ambaye huna uzalendo kwa Tanzania na Watanzania wenzako, lazima uwe na chuki kubwa dhidi ya Watanzania wenzako.
Kwa ujumla, Taifa letu, japo watu wanafikiri tunaenda mbele, kiuhalisia kwenye maeneo mengi tumerudi nyuma:
1) kwenye demokrasia tumeporomoka ajabu. Mifano imetolewa
2) kwenye viwanda tumeporomoka. Miaka ya nyuma tulikuwa tunaunganisha malori aina ya scania pale Kibaha, leo hatuunganishi gari lolote. Tulikuwa tunaunganisha matrekta imara na ya ubora wa hali ya juu, matrekta ya Valmet, hatuunganishi hata trekta moja. Wanunuzi wa magari, zamani, karibia wote walikuwa wanaagiza magari mapya, leo karibia wote wanaonunua magari used. Zamani kuvaa nguo ya mtumba (ilikuwa inaitwa kafaulaya) ilikuwa ni aibu, leo ni ufahari. Zamani ufahari ilikuwa ni kuvaa kitenge na kanga bora zilizotengenezwa Tanzania, ukiwa na hela pungufu unavaa kanga ya India au China (za ubora duni), leo kuna bidhaa ambazo kiubora unaweza kuita takataka, kutoka China zimezagaa kila mahali. Kulikuwa na kiatu 100% leather cha Bora Shoes, leo tuna plastic za China kila mahali, halafu tunaamini kuwa tumeendelea.
3) kwenye uongozi, ndiyo balaa kabisa. Zamani ukimsikia mtu ni kiongozi, kweli ni kiongozi hasa, kuanzia haiba yake, uelewa, akili na maadili. Ukisikia DC au RC, unajua ni mtu mweledi hasa, leo tuna mpaka majambazi ni maDC, na wala sina shaka mpaka maRC, maWaziri, watakuwepo. Leo tuna maDC, maRC, maWaziri, ambao kazi yao kubwa ni kumsifia Rais. Zamani, ukisikia kesi ipo kwa Jaji, basi unajua haki itatendeka. Nani leo wa kumlinganisha na Jaji Lugakingira, Nyalali, Samatta, Augustino Ramadhani, n.k. Hawa walikuwa ni wajuzi wa sheria, wenye maadili na weledi wa hali ya juu. Kila mtu alikuwa akisikia majina yao, anataka kusikia kitakachotoka vinywani mwao. Bungeni huko, ilikuwa ukisikia Spika leo ataongea, unarekebisha ratiba yako ili usikose kusikia Spika atasema nini. Leo, wapo watakaozima TV au tu hawana hata muda wa kusikiliza kwa maana wanajua kuwa Spika zaidi ataongelea kuwasuta watu badala ya kuelezea weledi wa taasisi yake. Jaji Mkuu, alikuwa Jaji mkuu hasa. Leo unasikia Jaji mkuu akiwaagiza majaji eti wahukumu kwa kuangalia mihimili mingine inataka nini!aana yake nini? Yaani wasiangalie sheria wala misingi ya haki, bali waangalie mihimili mingine inataka nini? Maajabu makubwa!
Leo hata ile miiko ya kimaadili haipo. Majaji wanapandishwa vyeo katikati ya kesi, kesi ambayo serikali ndiyo mlalamikaji. Mlalamikaji anampandisha cheo jaji anayesikiliza kesi yake. Siyo ajabu, siku hizi mtu akiwa na kesi, haijalishi ana haki au hana, unasikia ndugu wanasema, wachangishane ili wakamwone hakimu. Na inaonekana ni jambo la kawaida.
Kama Taifa, tunapoelekea kwenye kumbukumbu ya Uhuru wa Tanganyika, tunastahili kujitafakari tunakoenda. Mungu alitupendelea, akatupatia rasilimali nyingi, tulichokosa, kwa uhakika wa 100%, ni uongozi wenye maono, uongozi unatoa njia ili watu watembee kwenye njia zilulizo sahihi. Njia za ubunifu, njia za haki, njia za demokrasia sahihi na utawala/uongozi shirikishi.
Ukiwa kiongozi haina maana una akili kuliko watu wote, una uwezo kuliko watu wote, una maono kuliko watu wote. Utambue kuwa nje ya utawala na nje ya Serikali, kuna watu kila nyanja, wapo wanaokuzidi. Kazi yako kubwa ni kutengeneza uwanja wezeshi ili hawa watu wenye uwezo mbalimbali, fani mbalimbali, vipaji na karama mbalimbali, waweze kuutumia uwanja huo kuchangia maendeleo ya jamii na Taifa. Kama hili litaendelea kutofanyiwa kazi, Tanzania, kila wakati tutakuwa watu wa kuongelea namna mataifa mengine yalivyofanikiwa.