kelao
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 8,132
- 5,785
Wakuu poleni na majukumu ya kila siku.
Hivi majuzi kuna ajali ya Noah ilisombwa na maji huko Tanga, sasa nimempata habari kuwa waliokuwa kwenye gari ni mtu na familia yake, na waliangamia kwenye hiyo ajali.
Kuna taarifa kuwa ni watu wa nyumbani na wanazikwa huko Mbeya leo.
Naomba kama kuna anayefahamu lolote kuhusu msiba huu atusaidie taarifa zaidi kama vile majina ya waliofariki nk.
Shukrani.
----- UPDATE----
Watu hao 10 walipoteza maisha baada ya gari aina ya Toyota Noah yenye namba za usajili T890 CCX kutumbukia kwenye korongo lilosababishwa na kukatika daraja kipande cha barabara ya Handeni-Korogwe eneo la Sindeni kutokana na mafuriko ya maji yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe alithibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kubainisha kuwa kati ya watu hao 10, watu wazima ni nane na watoto wawili.
----
Picha: Majeneza yaliyobeba miili ya wanafamilia waliofariki kwenye ajali ya Noah
Hivi majuzi kuna ajali ya Noah ilisombwa na maji huko Tanga, sasa nimempata habari kuwa waliokuwa kwenye gari ni mtu na familia yake, na waliangamia kwenye hiyo ajali.
Kuna taarifa kuwa ni watu wa nyumbani na wanazikwa huko Mbeya leo.
Naomba kama kuna anayefahamu lolote kuhusu msiba huu atusaidie taarifa zaidi kama vile majina ya waliofariki nk.
Shukrani.
Watu hao 10 walipoteza maisha baada ya gari aina ya Toyota Noah yenye namba za usajili T890 CCX kutumbukia kwenye korongo lilosababishwa na kukatika daraja kipande cha barabara ya Handeni-Korogwe eneo la Sindeni kutokana na mafuriko ya maji yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe alithibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kubainisha kuwa kati ya watu hao 10, watu wazima ni nane na watoto wawili.
----
Picha: Majeneza yaliyobeba miili ya wanafamilia waliofariki kwenye ajali ya Noah