Tanga: Asilimia 33 ya Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza hawajaripoti Shule

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Zaidi ya asilimia thelathini na tatu ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza huko wilayani kilindi mkoani Tanga hawajaripoti shuleni mpaka sasa.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wilayani humo Walda Maulidi wakati akiongea na wakuu wa idara pamoja na madiwani wa halmashauri ya wilaya Kilindi.

Amesema Pamoja na wanafunzi hao wa kidato cha kwanza kutokuripoti shuleni hadi kipindi hiki cha robo ya mwaka, lakini pia hata wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya ufundi kwa ufadhili wa Mfuko wa Kaya Maskini (TASAF) nao hakuna hata mmoja aliyeripoti kwenye vyuo hivyo huku ada za wanafunzi hao zikiwa zimeshalipwa.

Naelezwa kuwa inawezekana hali hiyo ikawa ni moja kati ya sababu zinazoshusha kiwango cha elimu wilayani kilindi hivyo serikali wilayani humo imehimiza wazazi nao wakatambua umuhimu wa elimu kwa familia yao.

Chanzo: ITV
 
... halafu kesho na keshokutwa malalamiko tunaonewa, tunaonewa na majambia mikononi! Fursa hizo zitumieni hamtaki.
 
Huko si ndiko mapenzi yalikozaliwa?

Bint wa kitanga na shule wapi na wapi?

Hawana tofauti na wa ntwara.
 
Mtwara nako nimesikia asilimia 28% hawajareport.

ukisikiliza sababu zao, unaona kabisa hawako serious na kusomesha. Inasikitisha sana kuona mzazi hajui thamani ya elimu.
 
Mtwara nako nimesikia asilimia 28% hawajareport.

ukisikiliza sababu zao, unaona kabisa hawako serious na kusomesha. Inasikitisha sana kuona mzazi hajui thamani ya elimu.
Ila wanajua thamani ya demokrasia. Siunajua wapigakura wazuri wanaku vipi. Wanaongoza kwenye kupiga kura
 
Zaidi ya asilimia thelathini na tatu ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza huko wilayani kilindi mkoani Tanga hawajaripoti shuleni mpaka sasa.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wilayani humo Walda Maulidi wakati akiongea na wakuu wa idara pamoja na madiwani wa halmashauri ya wilaya Kilindi.

Amesema Pamoja na wanafunzi hao wa kidato cha kwanza kutokuripoti shuleni hadi kipindi hiki cha robo ya mwaka, lakini pia hata wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya ufundi kwa ufadhili wa Mfuko wa Kaya Maskini (TASAF) nao hakuna hata mmoja aliyeripoti kwenye vyuo hivyo huku ada za wanafunzi hao zikiwa zimeshalipwa.

Naelezwa kuwa inawezekana hali hiyo ikawa ni moja kati ya sababu zinazoshusha kiwango cha elimu wilayani kilindi hivyo serikali wilayani humo imehimiza wazazi nao wakatambua umuhimu wa elimu kwa familia yao.

Chanzo: ITV
Kwa huo mkoa wengi washaolewa na wanapelekwa Zanzibar na Pemba wanafungiwa akitoka kavaa baibui humjui
 
Zaidi ya asilimia thelathini na tatu ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza huko wilayani kilindi mkoani Tanga hawajaripoti shuleni mpaka sasa.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wilayani humo Walda Maulidi wakati akiongea na wakuu wa idara pamoja na madiwani wa halmashauri ya wilaya Kilindi.

Amesema Pamoja na wanafunzi hao wa kidato cha kwanza kutokuripoti shuleni hadi kipindi hiki cha robo ya mwaka, lakini pia hata wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya ufundi kwa ufadhili wa Mfuko wa Kaya Maskini (TASAF) nao hakuna hata mmoja aliyeripoti kwenye vyuo hivyo huku ada za wanafunzi hao zikiwa zimeshalipwa.

Naelezwa kuwa inawezekana hali hiyo ikawa ni moja kati ya sababu zinazoshusha kiwango cha elimu wilayani kilindi hivyo serikali wilayani humo imehimiza wazazi nao wakatambua umuhimu wa elimu kwa familia yao.

Chanzo: ITV


Pamoja na sababu nyingine lakini ukweli ni kwamba Shule ziko mbali sana na makazi ya watu.

Mfano sekondari za kata ni mtihani mkubwa sana.

Kutembea kwa miguu mwendo wa Dar Kubaha kwa mguu ?!

Wazazi hawana uwezo wa kuwapa wanafunzi nauli ya bodaboda na nauli ni zaidi ya shilingi 5,000/- kwenda tu bado kurudi,
Bado hela ya kula akiwa shuleni,

Huchoka na kukata tama kuendelea na masomo ama kutoanza masomo kabisa .

Mabinti huingia vishawishi vya lifti ya bodaboda na kudungwa mimba za utotoni na huo huwa mwisho wa hadithi ya Shule.
 
Yani kwa jinsi Shule zilivyo mbali ni mtihani kwa wazazi na kwa wanafunzi,

Yani mwanafunzi atembee kwa miguu mbali akifika amechoka njaa inamuuma, ame Helena maana ametoka mbali sana na ni hatari porini asubuhi atamuelewa mwalimu?

Je atayapenda masomo?

Si ataona tabu tu .

Halafu iwe hivyo kila siku, imagine
 
Yani kwa jinsi Shule zilivyo mbali ni mtihani kwa wazazi na kwa wanafunzi,

Yani mwanafunzi atembee kwa miguu mbali akifika amechoka njaa inamuuma, ame Helena maana ametoka mbali sana na ni hatari porini asubuhi atamuelewa mwalimu?

Je atayapenda masomo?

Si ataona tabu tu .

Halafu iwe hivyo kila siku, imagine
Hayo yote uliyoandika bado ni madogo ukilinganisha na umuhimu wa elimu

Kama umepata basic education utanielewa na Kama umeshawah kuishi na mtu ambaye hajasoma utanielewa zaid

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom