TANESCO yalia ukata na madeni. Yaomba serikali (walipa kodi) wawabebe deni la tril 1.39 wanalodaiwa na IPTL, Songas na TPDC

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Serikali imeombwa kubeba deni la shilingi trilioni 1.39 ambalo Shirika la Umeme nchini(Tanesco), linadaiwa na taasisi mbalimbali ikiwamo watoa huduma wake na mabenki. Katika deni hilo, shilingi bilioni 950, zinadaiwa na watoa huduma ikiwamo kampuni ya IPTL, Songas Pan Africa na TPDC, huku shilingi bilioni 442, zikiwa ni za mkopo wa benki kwa matumizi mbalimbali.

Mkurugenzi wa Tanesco, Dk.Tito Mwinuka, amesema shilingi bilioni 408 zilizokopwa kutoka benki zilitumika kununulia mafuta mazito ya kuendesha mitambo ya kufua umeme, na shilingi bilioni 34 zilitumika kulipa fidia ya ujenzi wa ilani kutoka Somangafungo hadi Kinyerezi.#KwanzaHabari
 
Mbona siku nyingi wameshaanza kukata yaani mimi nilikuwa nanunuaga umeme wa 10,000 unit 28.1 sasa hivi ukiweka 10,000 unakuja umeme unit 14 huku 5000 imeenda kusikojulikana
Screenshot_20190320-112407.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa jamaa si wanauza umeme? Inawezekana TTCL nao wana madeni yao kibao wanawasikilizia TANESCO.

Mtu huna mpinzani ila unashindwa tengeneza fedha. Mpeni mzungu Hilo shirika na mumpe Target. Hao wakugenzi mnaowapa wanatakiwa wawe chini ya mzungu.
Kisa mtu anajua V= IR Mnamkabidhi Tenesko(in Sakaya voice)
 
naombeni mwenye uelewa wa haya mambo anieleweshe jamani haswa kwenye hili deni la mafuta mazito. bilioni 408 zimetumika kununulia mafuta mazito manake umeme si ulizalishwa?ukauzwa?faida ikapatikana? inakuwaje tena hawawezi kulilipa?
 
Katika 18% ya VAT ya umeme, serikali iwachangie TANESCO 3% kwenye mfuko maalum wa kulipia madeni, serikali ibakiwe na 15%.
Pia bei za umeme zipandishwe kwa 1.5% ili hili ongezeko la 1.5% liende kwenye mfuko wa kulipia madeni ya Tanesco.
Tukifanya hivi kwa miaka miwili mitatu, tutakuwa tumefanikiwa pakubwa kuiokoa Tanesco from 'imminent collapse'...


1553093647151.png




Why the lights keep going out in South Africa
 
Mmh, 10,000/- upate 14units? Hii imeanza lini mkuu, manake jana tu nimenunua umeme na sikupata hizo units.
Kwa sisi tulioko Moshi inatupata hii maana kwenye ile tariff 4 washatutoa wote wakatuleta kwenye tariff 1.

Sasa wiki kama mbili zilizopita nilishangaa ukinunua umeme wa 10,000 unashangaa 5,000 imekatwa kwa hiyo unapata unit za 5,000. Niliamua kwenda Tanesco ya hapa Moshi ofisini kwao wakaniambia kabla ya kukuwekea LUKU kuna deni nilikuwa nalo. Ilinibidi nirudi nyumbani niangalie hizo document lakini nashangaa sikukuta deni lolote ila ndo hivyo sasa. Juzi wiki ya jana nimeenda kununua umeme wa 20,000 nikapewa umeme wa 10,000.

Tutafanyaje sasa maana tulianza kutolewa kwenye tariff 4, tukapelekwa tariff 1 maana tariff 4 nilikuwa nanunua umeme wa 8,000 napata unit 60(kama sikosei na nautumia huo umeme kwa mwezi na wiki mbili) sasa ni tariff 1 na bado ile sehemu iliyokuwa haina deni sasa tumeongezewa tufanyeje sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wapeleke pendekezo EWURA sasa wakitulilia sisi wananhi wana maana gani?
mramba felschem alipopeleka ombi la kuongeza bei alitumbulia faster.. Tusubiri tuone
Sisi wa Moshi tuulize tumelishaanza kukatwa mfano mimi nashangaa kwenye slip yangu ya luku kuna deni la sh. 36,000 sasa nashangaa limetoka wapi wakati kabla ya hapo miaka kama 10 na zaidi sikuwahi kudaiwa chochote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom