rushesheka
New Member
- May 13, 2021
- 4
- 2
Fedha za fidia ya wananchi wanaopisha ujenzi wa njia ya mradi wa umeme kutoka bwawa la Mwl Nyerere za kwama Tanesco fedha hizi zilidhinishwa na bunge la bajeti la 2015/2016 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa kusimamiwa na Tanesco mpaka leo 2021hakuna taarifa yoyote rasimi kwamba fedha hizi zinalipwa lini? Ila wana kauli mbiu yao kila mara usema 'HAZINA HAWAJALETA HELA' Kingine cha kushangaza na kusikitisha hakuna mdai yeyote anayejua anadai kiasi gani cha fedha, tunadai tusichokijua. Hii ni siri inayotia mashaka makubwa sana.
Hatujui kama endapo wataamua kulipa watalipa kwa kuzingatia principal au formula hipi ? Mradi wenyewe ni kutoka Kinyerezi kupitia Chalinze kuelekea Tanga na Arusha ukiitwa North East grid KV400 ulifanyiwa tathimini mwaka 2015 na baadaye 2018 ukauhishwa na kuitwa Bwawa la Mwl Nyerere hadi Chalinze Dodoma na Dar es salaam sasa ni 2021 hapa kumbuka kisheri kuna haki ya kulipwa pamoja na riba ya miaka mitano kulingana na viwango vya Benki Kuu.
Sasa swali kwa kuwa muhathilika wa mradi hajui kiasi anchopaswa kufidiwa si nirahisi kudanganywa kuwa kiasi atakacholipwa mtu kimejumlishwa na riba ya ucheleweshaji? Hapa kunatakiwa Tanesco wawe wazi kila mtu ajue kiasi anacho stahili kulipwa na riba ni kiasi gani?
Kama matakwa ya kisheria yatatimizwa hata wakikaa miaka mingine mitano kila mtu atakuwa anajua haki yake kisheria iko wapi . Mh Waziri wa ardhi na makazi tunakutegemea sana katika hili busara zako zinaepusha migogoro mingi sana hisiyo ya lazima. Mh Mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan ametamka mwenyewe kwa kauli yake amesema hataki mtu adhulumiwe wala serikali yake isidhulumu mtu, hataki hataki kabisa.
TANESCO lini mnalipa watu fidia zao pamoja riba yao? Hilo ndio swali la msingi. Umeme kwa maendeleo yetu , lakini haki itendeke.
Hatujui kama endapo wataamua kulipa watalipa kwa kuzingatia principal au formula hipi ? Mradi wenyewe ni kutoka Kinyerezi kupitia Chalinze kuelekea Tanga na Arusha ukiitwa North East grid KV400 ulifanyiwa tathimini mwaka 2015 na baadaye 2018 ukauhishwa na kuitwa Bwawa la Mwl Nyerere hadi Chalinze Dodoma na Dar es salaam sasa ni 2021 hapa kumbuka kisheri kuna haki ya kulipwa pamoja na riba ya miaka mitano kulingana na viwango vya Benki Kuu.
Sasa swali kwa kuwa muhathilika wa mradi hajui kiasi anchopaswa kufidiwa si nirahisi kudanganywa kuwa kiasi atakacholipwa mtu kimejumlishwa na riba ya ucheleweshaji? Hapa kunatakiwa Tanesco wawe wazi kila mtu ajue kiasi anacho stahili kulipwa na riba ni kiasi gani?
Kama matakwa ya kisheria yatatimizwa hata wakikaa miaka mingine mitano kila mtu atakuwa anajua haki yake kisheria iko wapi . Mh Waziri wa ardhi na makazi tunakutegemea sana katika hili busara zako zinaepusha migogoro mingi sana hisiyo ya lazima. Mh Mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan ametamka mwenyewe kwa kauli yake amesema hataki mtu adhulumiwe wala serikali yake isidhulumu mtu, hataki hataki kabisa.
TANESCO lini mnalipa watu fidia zao pamoja riba yao? Hilo ndio swali la msingi. Umeme kwa maendeleo yetu , lakini haki itendeke.