TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

we jamaa pumba sana, kwani hujui kuna mifumo mingine ipo kwenye windows? kwa hiyo serikali iandike OS kisha ifuatie na utility softwares n.k issue ni kuwa huu mfumo ungeweza kutengenezwa na watanzania kama ambavyo mingine imetengenezwa na kutika mpaka sasa bila shida, hiyo kununua nje ni ishara ya upigaji,mboba watu hawajalalamika ndege kununuliwa nje??? sababu tunajua sio uwezo wetu, ila kwa hili hapana, wataalamu wa ndani ni muhimu wapewe fursa ili waweke ujuzi wao
Wataalamu waandike basi hiyo ERP itumike kwenye mashirika ya umma na pia tuuze nje ya nchi tuingize madola. Au wewe andika yako utajirike.
 
Kwahiyo shida kubwa ya Serikali yetu haipo kwenye kutokuwa na pesa ya kutosha, hapana, shida ipo kwenye matumizi ya hovyo bila kujali wala kushirikisha wananchi

Mungu atusaidie
 
Watanzania naona tulisahau kabisa ajenda ya ufisadi wakati wa Magufuli, mpaka sasa kuna ufisadi umefanyika fasta fasta bila ya watu hata kushtuka.

Mkataba uliosainiwa baina ya Serikali ya Tanzania (kupitia TANESCO) na kampuni ya Tech Mahindra ya India wenye thamani ya dola milioni 30 ni wa kukodisha software ya Enterprise Resources Planning (ERP) - ambayo wahindi hawa wenyewe wanaiita Corporate Management System (CMS), kama inavyosomeka kwenye bango pichani chini.

Software ya aina hii huwa inaunganisha vitengo vyote vya taasisi katika software moja kwa ajili ya urahisi wa kuendesha taasisi. Hivyo basi kwa lugha nyingine ni kwamba Wahindi hawa watafunguliwa milango ya kuingia kila mahali ndani ya TANESCO, na hivyo kuwa na siri zote za mfumo wetu wa umeme.

Jambo kama hili ni hatari sana kwa usalama wa taifa. Hakuna njia rahisi ya kuiangusha nchi bila ya kufyatua hata kombora moja kama kuangusha mfumo wa nchi wa umeme.

Software kama hizi serikali inatakiwa iwawezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.

Zabuni ya kukodisha software hii ilianzaga kwenye dakika za lala salama za utawala wa Kikwete. Hivyo basi kitendo cha zabuni hii kukaa benchi kwa miaka mitano ya Magufuli kinaonesha kuwa hakuwa amekubaliana nayo. Baada ya Magufuli kufa naona wadau wa zabuni hii wameiendeleza na kuimwagia wino fasta, kama wanavyotaka kufanya kuhusu bandari ya Bagamoyo.

img-618a884f193e3.jpg
Mikataba ya namna hii, hapana kwa kweli, dah , wangewekeza kwenye miundombinu kwanza
 
Halafu wanaposema ni ya kukodi kwanza hatuelewi wanamaanisha nini hasa

Kwenye software hakuna msamiati wa kukodi bali kuna kitu kinaitwa trial au free version

Kwamba kabla hujanunua unapewa bure (trial) uijaribu kwa kipindi fulani ikiwa na limitations kadhaa ambazo huondolewa unapoamua kununua premium package

Kwahiyo hawa Tanesco kama hawapewi software kamili wapo kwenye muda wa trial (kukodi) hawapaswi kulipa hela yoyote, wanatakiwa wapewe na waijaribu bure

Hakuna software unayopaswa kulipia chochote kwenye muda wa trial (kukodi)

Labda nieleweshwe vinginevyo
 
Naamini kwa sasa nchi iko uchi, safari nyingi hizi zinawapa watu nafasi ya kufanya watakavyo sbb hakuna mwenye uwezo wa kujua hayo!

Nilikoswa imani siku aliposema mie sina uwezo wa kukagua mabati, mbao,cement ama Matofari, wakauu wa mikoa nyie ndio muwe jicho langu!

Nyie ni watu wazima hakuna haja ya kufuatiliana, tayari nikajua gari limepata pancha hakuna safari hapo.
 
Mama yangu!!
Usisahau kupitia na hapa😁👇

 
Watalaamu wetu wana uwezo mkubwa wa kutengeneza software hizi kwa gharama ndogo sana. Mahakama na taasisi nyingi tu wametengenezewa software kama hizo za uendeshaji wa ki tekohama na watalaamu wetu. Lakini tanesco chini ya January wamekodi software hiyo kwa TSh 70 bilioni kwa mwezi bila kupitia utaratibu wa bunge kupitisha bajeti hiyo.
 
Hili tatizo linaanzia kule juu kabisa, unapokuwa na kiongozi asietaka kushughulisha akili yake kwa chochote zaidi ya kusubiri kuletewa taarifa na wasaidizi wake huyo ndie chanzo.

Wasaidizi wake wanaweza kumpelekea mawazo ya hovyo yenye malengo ya "kutupiga", na kwasababu kiongozi mwenyewe hawezi kuhoji chochote anayakubali tu mawazo hayo kutokana na namna pumba anazolishwa zitakavyokuwa zimepangiliwa.

Matokeo yake ndio haya, unaona habari ya kukodi software ya $ 30 milion, baada ya kutoka kule kwenye mradi wa LNG ambao nao naamini alipigwa sound akaukubali bila kujua chochote, wala asijue hao anaowatuma ndio wajanja wenyewe, anachofanya Rais ni sawa na kumkabidhi fisi bucha sasa tunavuna tulichopanda.
jiwe ule ujuaji wake wakati mwingine ulisaidia sana Taifa maana wasaidizi walijua lolote watakalompelekea atawa challenge tu
Mama hata mimi naweza kumdanganya,yeye kila kitu hukubali tu
 
hii issue inaniuma sana, kwanini tusiwaamini wataalamu wetu wa ndani? mbona mfumo wa GePG umetengenezwa hapa bongo na unafanya kazi vyema tu, hizo hela tungewapa wataalamu wetu wa ndani zingewasaidia sana katika kujiimarisha kimifumo na ujuzi mwengine ambao ungezidi kuliheshimisha taifa letu kwa kuwaongezea CV na hatimae wangepata hata kazi zingine kimataifa. Hata kama nao wangesource baadhi ya vipengele kwa wataalamu wa nje ni sawa tu, hata kwenye sekta nyingine vingi vishafanyika kama hivyo na mambo yameenda vyema tu

kuna mtu anasema eti System haitokuwa stable wataalamu wa ndani hakuna wanachojua, kwanza, system kuzingua ni kitu cha kawaida na ndio maana hata wenye investment kubwa kama mitandao kijamii huwa kuna muda system inacheza lakini wana-troubleshoot na mambo yanakuwa sawa.
 
hii issue inaniuma sana, kwanini tusiwaamini wataalamu wetu wa ndani? mbona mfumo wa GePG umetengenezwa hapa bongo na unafanya kazi vyema tu, hizo hela tungewapa wataalamu wetu wa ndani zingewasaidia sana katika kujiimarisha kimifumo na ujuzi mwengine ambao ungezidi kuliheshimisha taifa letu kwa kuwaongezea CV na hatimae wangepata hata kazi zingine kimataifa. Hata kama nao wangesource baadhi ya vipengele kwa wataalamu wa nje ni sawa tu, hata kwenye sekta nyingine vingi vishafanyika kama hivyo na mambo yameenda vyema tu

kuna mtu anasema eti System haitokuwa stable wataalamu wa ndani hakuna wanachojua, kwanza, system kuzingua ni kitu cha kawaida na ndio maana hata wenye investment kubwa kama mitandao kijamii huwa kuna muda system inacheza lakini wana-troubleshoot na mambo yanakuwa sawa.
Halafu wabunge wenye uchungu na nchi yao kama Mh Mpina wakiibua bungeni kasoro hizi wanaandamwa sana na akina Msukuma, halafu mambo yanazimwa kirahisi na spika. Ndugai hangalikubali yazimwe.
 
Katika hili Makamba amefeli, huwezi chukua mfumo kutoka india ukauleta TZ as if TZ hakuna wataalam
 
Unaenda kukodi application ya software ya bilioni 70 kutoka India kwa pesa za umma wakati nchi hii ni maskini?Mfano mdogo tu hiyo bilioni 70 angeinvest kuboresha Tanesco umeme usikatike katike hovyo au kununua nguzo za kutosha nchi nzima?Leo hii ukienda Tanesco kujaza na kulipia kuunganishiwa umeme kama ni mahali pa nguzo wanakuambia kabisa kwamba hakuna nguzo kuna uhaba!!!
 
Tuliza puru usome uelewe!

USD 30 million ni equivalent na billion 69.5 za kitanzania! Hizo pesa ni nyingi mno kuna vichwa viko UDSM,DIT,IFM ambavyo with a fraction of that amount of money wangeweza ku develop system nzuri tu kwa msaada kidogo tu wa hao wahindi!

Haiingii akilini mtu alipe zaidi ya 70 billions kwa kukodi system mara mia angekuwa amaeinunua mazima! Hapo kuna upigaji wa kutisha sana! Hio system nauhakika haina thamani zaidi ya billion 10 kwa kuikodisha tu.
IFM wanafundisha engineering?
 
Hili tatizo linaanzia kule juu kabisa, unapokuwa na kiongozi asietaka kushughulisha akili yake kwa chochote zaidi ya kusubiri kuletewa taarifa na wasaidizi wake huyo ndie chanzo.

Wasaidizi wake wanaweza kumpelekea mawazo ya hovyo yenye malengo ya "kutupiga", na kwasababu kiongozi mwenyewe hawezi kuhoji chochote anayakubali tu mawazo hayo kutokana na namna pumba anazolishwa zitakavyokuwa zimepangiliwa.

Matokeo yake ndio haya, unaona habari ya kukodi software ya $ 30 milion, baada ya kutoka kule kwenye mradi wa LNG ambao nao naamini alipigwa sound akaukubali bila kujua chochote, wala asijue hao anaowatuma ndio wajanja wenyewe, anachofanya Rais ni sawa na kumkabidhi fisi bucha sasa tunavuna tulichopanda.
IQ ya Mama ni ndogo sana, form four failure, kaingia CCM, kafanya yake kujiendeleza vicertificate, na kupanda ngazi uko kupitia mafisi wa kiume wa uko CCM, kajikuta yuko hapo. Ni majanga kwa taifa.
 
Back
Top Bottom